Ufugaji wa Kuku aina ya Kuchi na masoko yake ndani na nje ya Tanzania

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,007
Kutokana na ongezeko la maswali ya wadau wengi juu ya ufugaji wa kuku aina hii, tumeonelea ni vema tukauweka mjadala huu vema kuweza kuwasaidia wafugaji na wanunuaji wa vifaranga/kuku wa aina hii.

Kuku aina ya KUCHI, ni wale ambao wanawauza kwa shilingi 200,000 hadi zaidi kwa kuku mmoja. Pamoja na kuwa kuku hawa wanaonekana kama wa kawaida, lakini si kama kuku wale tunaowafahamu; mbegu (breed) aina hii ya kuku huwa ni nadra sana kupatikana katika soko.

Ni kuku wakubwa kwa umbo, warefu na wenye kusimama mgongo ukiwa wima.

attachment.php


Kuchi wana manyoya machache mwilini hasa kifuani, wana mdomo mfupi na panga/vilemba vyao ni vidogo. Majogoo huwa na wastani wa uzito wa kilo 3.5 na mitetea kilo 2.

Mayai ya kuchi yana uzito wa wastani wa gramu 45. Kuku hawa wanapatikana kwa wingi maeneo ya Mwanza, Shinyanga, Tabora na Zanzibar.

Kuku hawa ni wazuri kwa nyama.

attachment.php


VIDEO toka Kenya:

KSHS 1 zidisha mara 20 kupata TSHS.
 

Attachments

  • kuchi_kuku.jpg
    kuchi_kuku.jpg
    63 KB · Views: 6,020
Last edited by a moderator:
Mkuu hii aina ya vifaranga niliiona mpwapwa kwa mkuu wa chuo cha mifugo. Ni kuku fulani wazuri sana na bei yake iko juu kiasi kwamba nilishangazwa kuambiwa kuku anauzwa laki mbili. Hawa wanapendwa sana na watu wanaopenda michezo ya kuku haswa kupigana. Bahati mbaya sikuchukua namba ya yule bwana nigekupatia uwasiliane nae.
 
Hao kuku watakuwa wanakunya Dhahabu, Ila kama ni hawa wakawaida wanao kunya mavi sidhani, Mbona kuna kuku wa Kienyeji Bora kabisa kuriko hao na hawauzwi hizo bei, Hata kuku wa Mayai ya Blue wenyewe hawauzwi hivyo,
 
Hao kuku watakuwa wanakunya Dhahabu, Ila kama ni hawa wakawaida wanao kunya mavi sidhani, Mbona kuna kuku wa Kienyeji Bora kabisa kuriko hao na hawauzwi hizo bei, Hata kuku wa Mayai ya Blue wenyewe hawauzwi hivyo,
Hauzwi laki mbili kisa ni kuku tu.. ila ile breed ndo jambo la msingi.

Pale Mpwapwa wataalamu wa mifugo wanafanya tafiti na kutengeneza breed safi sana za wanyama sio kuku pekee. Nakuhakikishia hutajutia kutoa laki mbili kwa ajili ya kuku maana utapata faida mara dufu pale wakianza kuzaliana.

Demand ya kuku hawa iko tafauti na kuku mliowazoea mtaani
 
hauzwi laki mbili kisa ni kuku tu.. ila ile breed ndo jambo la msingi. pale mpwapwa wataalamu wa mifugo wanafanya tafiti na kutengeneza breed safi sana za wanyama sio kuku pekee. nakuhakikishia hutajutia kutoa laki mbili kwa ajili ya kuku maana utapata faida mara dufu pale wakianza kuzaliana. demand ya kuku hawa iko tafauti na kuku mliowazoea mtaani

Hakuna kitu kama hicho, tuwekee sifa zake hapa, ikiwa ni pamoja na Uzito, na utagaji wake make ndo vitu vinavyo mata,
 
naiona shida mnayoipata wadau hapa ... nayo ni mazoea bahati mbaya ndio ugonjwa mkubwa umetuathiri Watanzania na shughuli zetu zote kwa kiasi kikubwa.

Tumekuwa tukilima na kufuga kwa mazoea! Ndio maana leo ukiambia mbegu ya kuku ni laki 2 unang'aka!

Tuacheni mazoea twendeni kisayansi ...chochote tunachotaraji kukifanya tukifanyie utafiti na tujiandae kugharimia.

Hapa.inaongelewa mbegu ya kuku inayoleta tija ...sasa weye benda Singida au hata hapo Sinza sokoni kaokote wake kuchi uchwara .mbegu yao imezunguka tangu ebxi ua marehemu bibi..you doomed to fail
 
naiona shida mnayoipata wadau hapa ... nayo ni mazoea bahati mbaya ndio ugonjwa mkubwa umetuathiri Watanzania na shughuli zetu zote kwa kiasi kikubwa.

Tumekuwa tukilima na kufuga kwa mazoea! Ndio maana leo ukiambia mbegu ya kuku ni laki 2 unang'aka!

Tuacheni mazoea twendeni kisayansi ...chochote tunachotaraji kukifanya tukifanyie utafiti na tujiandae kugharimia.

Hapa.inaongelewa mbegu ya kuku inayoleta tija ...sasa weye benda Singida au hata hapo Sinza sokoni kaokote wake kuchi uchwara .mbegu yao imezunguka tangu ebxi ua marehemu bibi..you doomed to fail

Mdau umeleta uzi wa maana sema wwachangiaji wengi hawajakubamba ni kwel hata mi niliwahi kufuga na jogoo wangu wa mwisho niliuza laki na 70 kwa mpemba mmoja na hapo ni baada ya kumtumia kwenye ngumi za kuku ambazo kwa kipind nlichokua nae keshaingiza zaidi ya milion moja kwa kwel kuchi ndo mpango mkuu.waliolala usiwaamshe utalala wewe

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Nadhani kuna umuhimu wa kuweka mazoea pembeni, mwenyewe nilihamaki kuambiwa kuku laki mbili ila kotkana na demand ya hiyo breed nikashawishika kuamini.

Ieleweke kwamba kuku wenyewe hawana mwili mkubwa sana, ni wa kawaida sana ila wana soko kubwa. Watu wengi wanawafuga for funny. KWa mfano huyu mkuu wa chuo mpwapwa niliyemtembelea aliniambia kuwa ana order ya kuku elfu arobaini ambapo wkt mimi ninaenda kwake alikuwa na kama elfu 18! Wateja wengi wa hawa kuku ni wazungu.

Kama unanunua kwa ajili ya kitoweo haitakuwa sawa maana kwa huyu bwana kuna kuku wana hadi kg 6 anauza kwa 25,000 tu, sasa shangaa kuchi wa kilo mbili kuuzwa laki 2!
 
hyo kitu ni kweli aisee sio mala ya kwanza kusikia kuhusu kuchi kuuzwa bei hiyo....kuna siku nilisoma makala kwenye gazeti moja la hapa kuhusu ufugaji wa kuku haswa hao kuchi nilivyoenda kwenye kipengele cha bei nilibaki mdomo wazi....kwa watu wanaojua kazi ya hao kuku wapo tayari kununua kwa hiyo bei...ni moja ya kuku ambao ni expensv sana kutokana na demand yake....sio uongo wajameni hzo bei.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom