Mwongozo wa ufugaji wa kisasa wa Mbuzi wa nyama na maziwa

TUANGAZIE UFUGAJI WA MBUZI KATIKA BIASHARA

Kwa ujumla ufugaji wa mbuzi ni biashara kubwa. Kama mfugaji atafuata na kuzingatia kanuni bora za ufugaji wa mbuzi hataweza kupata hasara.

Mara nyingi mbuzi husumbuliwa zaidi na magonjwa ya mapafu. Ugonjwa huu ikiwa mbuzi watacheleweshwa kutibiwa utawafanya wafe kwa wingi na kwa haraka. Dalili ya ugonjwa wa mapafu ni pamoja na kwamba mbuzi wanakuwa na homa kali, kukohoa, na vifo hutokea baada ya siku 1-2 tu. Ni muhimu kutambua mapema dalili za ugonjwa huo ili mbuzi wawahi kutibiwa kwa haraka.

Mbuzi ni tofauti na ng'ombe ni wastahimilivu sana dhidi ya ukame. Wanakula nyasi pia wanakula majani ya miti. Ikitokea nyesi zimekwisha au kukauka watandelea kuishi na kuzaliana kwa kula majani ya miti.Wakati wa kiangazi mmiliki wa mradi wa ufugaji wa mbuzi huwi na presha juu ya chakula cha kuwalisha mbuzi.

Thamani ya mbuzi imekuwa kubwa hasa mjini kutoka na watu wengi kuhitaji nyama choma ya mbuzi hivyo hutoa hakikisho la faida kwa mwenye mradi .Isiteshe mbuzi huzaliana haraka sana ndani ya muda mfupi na kufanya kundi lao liongezeka kwa kasi. Kwa wastani toka mbuzi ashike mimba hadi kuzaa(Gestation period) huwa inamchukua siku 150 sawa na miezi 5,ndani ya mwaka mmoja mbuzi anazaa mara 2.

Ukiwa na mbuzi 50 majike na madume 2 katika uwiano wa 1:25, ndani ya miaka 3 utakuwa na mbuzi majike jumla 200+madume 152 hawa ni wazazi na watoto wao +118 majike na 118 madume hawa ni watoto wa watoto. Kwahiyo jumla kuu utakuwa na mbuzi 588 hii idadi na ndani ya miaka 3 kati ya hao madume yatakuwa 270 na majike yatakuwa 318. Hii hesabu niliyofanya kupata hii idadi ya mbuzi jumla kwa miaka 3 ni hesabu kali sana. Unaanza na mbuzi hamsini unamaliza na mbuzi 588 ndani ya miaka 3.
 
Kaka, kwa ufupi.

Ng'ombe wanaofaa ukanda wa joto ni wale wasio na rangi nyeusi. pili uchague aina kulingana na outcome unataka nini mwisho wa siku (beef,diary, dual).

Kuna aina wanaitwa Ayrshire wanaweza kustahimili maisha ya pwani(coastal belt) na magonjwa yake. unatakuwa upate kizazi cha pili na cha tatu ikienda cha nne au pure breed uekwama kuna ugonjwa unaitwa ECF (east cost Fever) lazima ukutoe.

Uzuri wa breed hii unaweza kwenda mpaka 15Lts na butter fat content ikiwa 3.

The best ni breed inaitwa jersey kikubwa anahitaji eneo dogo,chakula kidogo pia anaweza kustawi pwani.kanuni ileile usiende kizazi cha nne.

Hawa ni maziwa yenye thamani kubwa ila volume ndogo, kwa wahuni tuna wa kross jike la ayshire na dume la jersey matokeo yake hatta kwa 2M sikuuzii ila akiwa jike.

Kuna breed nyingine wanaitwa kitukama simentor(Dual) hawa ni maziwa na nyama, wastani wa lita 8, chakula kibao ila sometimes wana ishu ya kubeba mimba baada ya mzao wa kwanza(hapo uwe mvumilivu una weza chukua mwaka kumpandisha).

Breed zingine mapambo ya kimasai, karibu shamba

Mkuu bado unafuga hao ng'ombe breed ya jersey?
 
Kama kuna wanaopenda kufuga wanyama hasa Mbuzi ( wa maziwa,nyama),njooni tuunganishe nguvu tufanye mambo.Inawezekana kabisa tukafuga kwa mafanikio sana. Kila kitu kipo ndani ya uwezo wetu.

I believe together we can go.
Hongera sana mkuu kwa maono yako kiukweli nimependa sana hillo wazo Na Niko tayari
 
UFUGAJI WA MBUZI NI UTAJIRI ULIOJIFICHA

Hawa ni mbuzi na wala si Ng'ombe. Ni mbuzi aina ya Boer wenye asili ya nchi ya Africa Kusini. Ni moja ya kosaafu bora kabisa katika mbuzi wa nyama. Sifa yao kubwa ni kuwa na miili mikubwa kama wanavyoonekana katika picha hapo chini. Dume mmoja anauzwa kwa Tsh 250,000/= na jike lake Tsh 350,000/=. Umri wao wa kuuzwa ni miezi 6. Madume ya Boer yanafaa sana kwa ajili ya kupandishia majike ya mbuzi wa asili na hivyo kusaidia kuboresha mbuzi hao na kuwafanya wawe wenye tija zaidi.

Ufugaji wa mbuzi ni utajiri uliyojificha. Kwanza huzaliana kwa haraka kwa maana kwamba kwa mwaka mmoja mbuzi mmoja ana uwezo wa kuzaa mara mbili lakini vilevile hawasumbui kwenye masoko. Wanakula majani zaidi kwa kuwa wao ni aina ya wanyama wenye matumbo manne yaani Ruminant animals ambao kwa kiasi kikubwa hutegemea zaidi majani kama chakula chao kikuu. Mbuzi si kama kuku ambao huhitaji chakula kilichotengenezwa maalum na kwamba kila siku watahitaji utoe pesa yako mfukoni kwa ajili ya kuwanunulia chakula. Mbuzi wanauwezo wa kuishi wenyewe bila kuhitaji hela yako ya mfukoni kwa ajili ya chakula kwa muda mrefu ilimradi tu wawe wazima. Ni muhimu ukawa na daktari wako maalum ukaingia nae mkataba kusudi kila baada ya muda fulani awe anakufanyia ufuatiliaji wa maendeleo ya mbuzi wako japo kwa mwezi mara moja na pale linapotoke tatizo hasa mripuko wa ugonjwa. Kutokuwa na daktari wa mifugo katika mradi wako wa ufugaji wa mbuzi ni sawa na kutembea barabarani huku ukiwa umefungwa kitambaa usoni. Daktari wa mifugo si lazima umtoe mbali, kila kijiji kuna madaktari hao au maafisa mifugo ambao unaweza ukaongea nao mmoja wapo ili awe anakupa huduma pale inapohitajika.

Mbuzi wanahitaji uwe na shamba kubwa lenye maji ya kutosha na majani. Pia kuwe na vijana wa kazi waaminifu kwa ajili kuwachunga na ulinzi. Na ni muhimu pia shambani kukawa na Mbwa kwa ajili ya kuongeza ulinzi katika mradi wako.

Tanzania tuna mapori makubwa ambayo unaweza ukafanya uendeshaji wa mradi wako wa ufugaji wa mbuzi kwa ufanisi mkubwa bila kujali ni umbali kiasi gani. Watakapokuwa tayari kuvunwa, utatafuta gari na kuwapakia mbuzi wako na kisha kuwapeleka mnadani ambako utawauza kirahisi sana. Kuna minada mingi ya mifugo hapa Tanzania. Kuna ile minada ya awali ambayo wafanyabiashara wa mifugo wanaenda kuchuuza huko na kuwapeleka kwenye minada ya upili ambayo ni minada mikubwa iliyo chini ya wizara ya mifugo. Sasa kwa mfugaji wa mbuzi, utaamua wewe mewe mwenyewe kama uwapeleke mnada wa awali au mnada wa upili. Lakini vilevile kwa sasa kuna machinjio za kisasa za mifugo mfano machinjio ya kisasa ya mifugo ya Kizota Dodoma mjini ambayo mahitaji mbuzi yamekuwa makubwa kupita maelezo kutokana na nyama yake kuhitajiwa zaidi katika nchi za kiarabu hasa Oman na Dubai. Kwahiyo mahitaji hayo ya mbuzi yametengeneza soko kubwa na la uhakika. Shughuli za kilimo katika ufugaji hazisumbuliwi sana na masoko kama zilivyo shughuli za kilimo cha mazao mfano nafaka na matunda kutokana na kwamba minada minada ya mifugo imekuwa mkombozi mkubwa kwa wafugaji.

Changamoto katika ufugaji wa mbuzi ni magonjwa ambayo kimsingi yanadhibitika kupitia wataalamu wa mifugo.

Aman Ng'oma
0767989713
Dodoma
Kaka Amani naomba nikuulize hizi aina za mbuzi ninazoziona hapa kwenye picha unazo ww!?

Pia naomba kujua bei!? Na anijulishe wanawezaje kufika mtwara kwa yule bimkubwa wetu!?
 
Kaka Amani naomba nikuulize hizi aina za mbuzi ninazoziona hapa kwenye picha unazo ww!

Pia naomba kujua bei!? Na anijulishe wanawezaje kufika mtwara kwa yule bimkubwa wetu?

Tafuta mbuzi aina ya Newala hawana utofauti na ujiji katika uzaaji wake na matunzo pia.
 
Asante kwa elimu nyumbani kwetu kijijini ni wafugaji nipo kigoma kuna maeneo makubwa sana ya kufugia mbuzi, Aman nitakutafuta ili unisaidie kupata hao mbuzi
 
Wadau, mimi nimeanza ufugaji mdogo mdogo kwa malengo ya baadae kuwa wa kibiashara. Ninatafuta mbegu ya mbuzi wanaozaa mapacha wanne. Naomba kama kuna mtu anafahamu mahali niakoweza kuwapata au ni mfugaji ajitokeze tafadhali.

Asanteni
 
Back
Top Bottom