Mwongozo wa ufugaji wa kisasa wa Mbuzi wa nyama na maziwa

Wadau habari za humu, nipo na mpango wa kufuga mbuzi pembeni ya mji wa Dar Es Salaam. Kuna mdau yeyote mwenye clue ya hii shughuli?
Wapi naweza kupata mbegu nzuri za mbuzi wa kienyeji wa kuanzia?
 
mkuu Malila na wengine ni vyema kuwe na group la whatsapp au kama lipo ili wageni tupate kujua kinachoendelea,mi nnafuga wa kawaida ila natafuta Boer breed. #Malila
 
Talic, mbuzi wana soko kubwa Tanzania. Ukiwa na idadi yoyote jaza kwenye Fuso peleka Pugu au Vingunguti utauza wote, UTAONDOKA NA CASH YAKO MFUKONI.
 
Mkuu Aman Ng'oma,

swali langu ni hivi, je ukianza na majike 50 na kila mmoja wao akizaa, si unaweza kuanza kukamua maziwa? Na ukikusudia kufanya hivyo unaweza kupata maziwa yake kwa siku ngapi ndani ya mwaka mzima, ukizingatia muda wakati wanakuwa dry kabla ya kuzaa, kama vile kwenye ng'ombe?

Asante in advance..
 
Mkuu Aman Ng'oma,

swali langu ni hivi, je ukianza na majike 50 na kila mmoja wao akizaa, si unaweza kuanza kukamua maziwa? Na ukikusudia kufanya hivyo unaweza kupata maziwa yake kwa siku ngapi ndani ya mwaka mzima, ukizingatia muda wakati wanakuwa dry kabla ya kuzaa, kama vile kwenye ng'ombe?

Asante in advance..

Rashiditanz

Nashukuru kwa swali lako zuri.

Kimsingi, mbuzi mia wakizaa utaweza kuwakamua maziwa ingawa hutopata mengi kama yanayozalishwa na mbuzi wa kisasa wa maziwa, kwasababu mbuzi hao si pure wa maziwa ni chotara na uwezo wake wa kutoa maziwa ni mdogo. Kwa mantiki hiyo utakapowakamua maziwa, kwasababu ni mbuzi wengi waliozaa, utaweza kupata maziwa mengi ukiyachanganya pamoja na hivyo kukupatia kipato cha ziada kutokana na mauzo ya maziwa.

Maziwa ya mbuzi yana Virutubisho vingi ukilinganisha na maziwa ya ngombe na kwa msingi huo inashauriwa sana watu wazima na watoto waweze kuyatumia maziwa hayo. Pia maziwa ya mbuzi yanapunguza cholestro. Faida ni nyingi nimetaja kwa uchache tu.

Changomoto ya maziwa ya mbuzi ni kutozoeleka na watu kwa ajili ya kufanya matumizi kama ilivyo kwa maziwa ya ng'ombe

Ukamuaji wa maziwa ya mbuzi unaaza mara tu baada ya mbuzi wako kuzaa na utaendelea hadi siku 27 +/- 4 kabla ya kuzaa.

Kumkausha mbuzi kunasaidia kuyafanya yale maziwa ya mwanzo ya mbuzi kuwa bora zaidi.

Asante.
 
Na vip hii biashara ya mbuzi, mfano kuchukua huko Dom na vijijini, then kuwaleta hapa dsm, biashara inalipa? Ushauri
 
Na vip hii biashara ya mbuzi, mfano kuchukua huko Dom na vijijini, then kuwaleta hapa dsm, biashara inalipa?? Ushauri

Renyo,

Hiyo biashara inalipa tu na wengi wanaifanya ila kitu cha msingi na muhimu ujue bei ya Sokoni DSM ili ikuongoze kwenye kuwanunua Dodoma
 
Hawa mbuzi ni mbuzi bora walioboreshwa, wanapatikana dodoma. Ni matokeo ya cross breed iliyofanyika kati ya mbuzi wa kienyeji wa dodoma na exotic breed.Hivyo wengi wa uzao wao huzaa mapacha. Mbuzi hawa huuzwa tsh elfu 50, wakiwa na umri wa miezi 5.
Sasa kama wanauzwa elfu 50 huko dodoma ukiwapeleka dar utawauza bei gani kwa kila mbuzi?
 
Kwa wale wajasiriamali wanaohitaji kujiunga na group ya WhatsApp kwa masuala ya kijasiriamali nicheki 0762600100
 
Kwa mara nyingine tena, leo nimeona haja ya kuanzisha mada nyingine na tujadiliane kwa pamoja juu ya ufugaji wa mbuzi baada ya kujadili kwa muda mrefu ile mada ya ufugaji wa kuku.

Ufugaji wa mbuzi hapa Tanzania ni fursa adhimu ambayo Watanzania wengi hawajaiona. Ni ufugaji ambao wenyewe kama mfugaji atazingatia kanuni na misingi ya ufugaji Bora, ni rahisi sana mfugaji kujiondoa kutoka kwenye umasikini na kuwa tajiri. Kitu cha msingi na muhimu ni kwamba,mfugaji lazima awe na eneo pamoja na mtaji wa kuanzia.

Mbuzi wanatakiwa kufugwa shambani. Shamba ambalo mbuzi wanatakiwa wafugwe linapaswa liwe na sehemu ambayo mbuzi wanaweza kwenda kuchungwa na pia kuwe na chanzo cha maji. Mbuzi kitabia hupenda kulala juu hivyo mabanda yao yanapojengwa lazima yainuliwe juu. Mabanda ya mbuzi si ghari,kwani hujengwa simple.

Mbuzi kwa mwaka wao huzaa mara mbili na ukipata ile mbegu ya wanaozaa mapacha faida yake huwa ni kubwa zaidi, itategemea na mtaji wa mfugaji, lakini kama mfugaji ataweza kuanza na mradi wa mbuzi 50 inakuwa vizuri zaidi. Ukiwanunua mbuzi 50@ tsh.50,000/= utapata Milioni 2 na nusu, madume 2 kila moja likanunuliwa kwa tsh 75000/= kwa madume mawili itagharimu tsh laki moja na nusu. Usafirishaji wa mbuzi hauzidi laki tatu na nusu. Kwa hiyo itajikuta ukiwa na milion 5 utaweza kuanza na mradi wa ufugaji wa mbuzi majike 50 na madume mawili,pamoja na kuwajengea sehemu ya ya kulala.

Kama nilivyoainisha hapo awali, mbuzi kwa mwaka wao huzaa mara 2, hivyo kama kila mbuzi atazaa hebu chukulia kila mbuzi atazaa mbuzi mmoja tu, ingawa kuna wengine watazaa mapacha hasa ukipata ile mbegu ya mbuzi wanaozaa mapacha, mwishoni mwa mwaka utakuwa na idadi ya mbuzi 100 wapya waliozaliwa na ukujumlisha na mtaji ule wa mbuzi 50 utakuwa na jumla ya mbuzi 150, hii ni ndani ya mwaka mmoja, pata picha utakuwa na mbuzi Idadi gani baada ya miaka 3 hasa ukizingatia kuwa wale watoto wa mbuzi watakapofikia miezi 8 utaanza kuwapandisha nao watazaa nk. Ili kufikia malengo, inashauriwa kuwa mbuzi wa mtaji wanaonunuliwa lazima wawe na umri mmoja ili kusudi waweze kupata mimba kwa wakati mmoja na waweze kuzaa kwa wakati mmoja pia.

Magonjwa ya mbuzi mengi yanafahamika na ni rahisi kudhibitika,hivyo mbuzi si rahisi kufa hovyo.

Toka mbuzi anapata mimba mpaka anazaa,hutumia muda wa wiki miezi mitano yaani siku 150.

Kwa sababu hili pia ni eneo langu nilililolisomea, nawaruhusu kwa wale wote wenye Interest na uanzishaji wa Mradi huu wa ufugaji wa mbuzi kuuliza swali lolote lihusulo ufugaji bora wa mbuzi nami nitajibu.Lengo likiwa ni lile lile la kusaidiana kama Watanzania ili kuondokana na hili lindi la umasikini.

Karibu kwa majadala.
Mkuu nakuomba ujiunge nasi WhatSapp kwenye group la Biashara na Wajasiriamali Tangaza Business Solutions utatufaa nakutusaidia juu ya elimu ya ujasiriamali.

Namba yetu ya WhatSapp ni 0785-074040
Karibu sanaaaa Mkuu
 
Mkuu ningenda kujua ni majani ya aina gani ambayo mbuzi au kondoo akila yanampa afya tele? Pia kama kuna vyakula vingine ambavyo anayumia naomba unieleze ili nipate uzoefu kabisa. Maana hujaongelea chakula chao na gharama zake.
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom