Ufugaji wa Bata Mzinga, Bata Bukini na Kanga: Maoni, Ushauri, Utaalamu na Masoko

Nataka kufuga bata mzinga ila naomba mnifahamishe changamoto zao pia naomba kujua upatkanaji Wa masoko ya kuwauza pia ni wap nitapata vifaranga vya bata mzinga?

Naomba msaada wenu wakuu

Sent using Jamii Forums mobile app
karibu mkuu kwenye fursa ya ufugaji wa bata mzinga. bata mzinga wanafugika kirahisi kuliko kuku kwa maana kwamba hawana changamoto nyingi kama kuku, ninawafuga bata mzinga pia nafuga kuku nimeona nakuthibitisha mwenyewe kauli hii niliyotoa. uzuri wao wana uwezo mkubwa wakustahimili magonjwa labda tuseme baadhi tu ya magonjwa ya kuku kama ndui ndio inaweza kuwasumbua ila si kwamba yaweza kuwaua kirahisi. ukiwa makini kuwapa chanjo na kua makini kufanya usafi bandani kwao. nikiwa na maana ya mazingira ya banda na vyombo vyakuwalishia chakula na maji, hutaona batamzinga akifa ovyo. jambo jingine ni umakini wa mazingira unapowafugia kwani hua wanapenda kudonoadonoa vitu mbalimbali na kumeza wakati mwingine vitu vikubwa ambavyo vyaweza kuwashinda kumeza jambo linaloweza kuwasababishia kifo endapo kitawakaba na kukosa mtu wakuwasaidia kutoa vilivyowakaba kooni. kuepuka changamoto hii ni kuhakikisha unawafugia bandani kwani humo bandandi utakua na uhakika na wanachokula hivyo kuepuka hasara inayoweza kutokana na changamoto hiyo. kwa anaehitaji vifaranga waweza kunitafuta kwa namba 0714756625 :::: 0623460298: napatikana dar es salaam
 
Changamoto kubwa kwa kanga ni vifo vya ghafla kwa vifaranga. Mwanzoni nilichanganyikiwa unakuta kifaranga mzima kabisa akilowa kidogo tu na hata ukimgusa mikono ikiwa na vimajimaji ghafla anaanza kutetemeka na ndani ya nusu saa amekufa. Akipata stress kidogo amekufa.

Tatizo lingine ni udhaifu wa miguu yaani anatambalia tumbo miguu ime paralyze kabisaa na baada ya muda anakufa

Nilikuwa na vifaranga 200 kila siku wanakufa 10-20 mpaka wakabaki 92

Suluhisho:
Nilikwenda kwa mzee daktari dukani nikamueleza nahitaji chanjo ya kanga na nikampa sababu, akaniambia kanga huwa hashambuliwi na magonjwa Kama kuku na hivyo chanjo haina maana ila vifo kwa vifaranga ni kutokana na upungufu mkubwa wa vitamin A. Alinipa aminovet ya kuwachanganyia kwenye maji (bei 6000) niliwapa mchana ule ule siku ya pili walikufa 2 ambao walikuwa dhaifu na siku ya 3 hakuna kifo na ndiyo ukawa mwisho wa vifo.

Hii iminovet unawapa kila siku na wanaipenda sana, ukiwawekea maji pure hawanywi

Asante sana mzee wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Vipi dawa ya minyoo huwapi?
 
karibu mkuu kwenye fursa ya ufugaji wa bata mzinga. bata mzinga wanafugika kirahisi kuliko kuku kwa maana kwamba hawana changamoto nyingi kama kuku, ninawafuga bata mzinga pia nafuga kuku nimeona nakuthibitisha mwenyewe kauli hii niliyotoa. uzuri wao wana uwezo mkubwa wakustahimili magonjwa labda tuseme baadhi tu ya magonjwa ya kuku kama ndui ndio inaweza kuwasumbua ila si kwamba yaweza kuwaua kirahisi. ukiwa makini kuwapa chanjo na kua makini kufanya usafi bandani kwao. nikiwa na maana ya mazingira ya banda na vyombo vyakuwalishia chakula na maji, hutaona batamzinga akifa ovyo. jambo jingine ni umakini wa mazingira unapowafugia kwani hua wanapenda kudonoadonoa vitu mbalimbali na kumeza wakati mwingine vitu vikubwa ambavyo vyaweza kuwashinda kumeza jambo linaloweza kuwasababishia kifo endapo kitawakaba na kukosa mtu wakuwasaidia kutoa vilivyowakaba kooni. kuepuka changamoto hii ni kuhakikisha unawafugia bandani kwani humo bandandi utakua na uhakika na wanachokula hivyo kuepuka hasara inayoweza kutokana na changamoto hiyo. kwa anaehitaji vifaranga waweza kunitafuta kwa namba 0714756625 :::: 0623460298: napatikana dar es salaam
Vipi kuhusu upatikanaji wa masoko kuhusu hii biashara ya bata mzinga ikoje?
 
Mkuu katika hao ndege hapo juu mimi ninawafuga kanga kiukweli kanga ni wazuri sana kufuga kwasababu kanga siku akitotolewa vifaranga vyake huwa ni mchaka mchaka havitulii na haviitaji dawa ya aina yoyote zaidi ya maji na chakula na huwa inakuwa vizuri ukinunua mayai yake ukaatamisha kwa kuku ili avilee vizuri vifaranga,vifaranga vya kanga huwa vinakuwa haraka kuliko vya kuku na wakisha kuwa wakubwa watakusumbua tu kwenye kelele vile vile huwa wanataga kwa msimu wako tofauti na ndege wengine na huwa wanapenda kutagia nje au kwenye pori sasa ukishaona wanataka kuanza kutanga inatakiwa unaweka kiota ndani harafu unakuwa unawafungia bandani hadi saa 7 mchana unawatoa hapo wanakuwa wamesha taga kabisa ndio unawatoa nje baada ya hapo unachagua hayo mayai umwachie kanga alalie mwenyewe au uchukue mayai umwekee kuku maana huwa yanakuwa mengi na kanga huwa anataga tu mfululizo.

Kuhusu soko,wewe anza kuwafuga wakishakuwa wengi utaona watu watakavyo kuwa wanakujalia kuulizia mayai na vifaranga hadi utashangaa mwenyewe hao hunaaja ya kujitangaza kelele zao tu zinakuletea wateja nyumbani,mayai moja(2000)
Kifaranga 5000
Kanga wakubwa 30000
Na haina kulemba wanauzika sana baadaye ndakuwekea picha

Kuhusu hao bukini na bata mzinga bado sijajua vizuri ngoja tusubiri wadau

-Ndumilakuwili-
Mkuu samahani hebu share nasi experience yako katika uleaji wa vifaranga vya kanga wengine tunakutana na changamoto vinakufa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Changamoto kubwa kwa kanga ni vifo vya ghafla kwa vifaranga. Mwanzoni nilichanganyikiwa unakuta kifaranga mzima kabisa akilowa kidogo tu na hata ukimgusa mikono ikiwa na vimajimaji ghafla anaanza kutetemeka na ndani ya nusu saa amekufa. Akipata stress kidogo amekufa.

Tatizo lingine ni udhaifu wa miguu yaani anatambalia tumbo miguu ime paralyze kabisaa na baada ya muda anakufa

Nilikuwa na vifaranga 200 kila siku wanakufa 10-20 mpaka wakabaki 92

Suluhisho:
Nilikwenda kwa mzee daktari dukani nikamueleza nahitaji chanjo ya kanga na nikampa sababu, akaniambia kanga huwa hashambuliwi na magonjwa Kama kuku na hivyo chanjo haina maana ila vifo kwa vifaranga ni kutokana na upungufu mkubwa wa vitamin A. Alinipa aminovet ya kuwachanganyia kwenye maji (bei 6000) niliwapa mchana ule ule siku ya pili walikufa 2 ambao walikuwa dhaifu na siku ya 3 hakuna kifo na ndiyo ukawa mwisho wa vifo.

Hii iminovet unawapa kila siku na wanaipenda sana, ukiwawekea maji pure hawanywi

Asante sana mzee wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
Nashukuru sana mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu sijajua kama sehemu zote msimu wa kutaga huwa ni mmoja ila kwa sehemu nilipo Kanga hutaga kuanzia mwezi wa 11 na dalili za kanga kutaga mara nyingi huwa naona dume kunamlio fulani huwa analia na huwa anafatana sana jike hadi kwenye kutaga dume linamfuata jike.
Profesa vipi ufugaji bado unaendelea naoo/ maana naona ulitaka kufuga vitu vingi hebu ukuje utupe mrejesho
 
Wana forum naombeni msaada wa maelekezo ya kufuga Kanga. Nataka kufuga nyumbani ambapo nina uwanja wa kutosha na nyumba ina fence ya ukuta.
Pamoja na faida nyingine, lengo kubwa ni kufuga Kanga kama mapambo ya nyumba, sababu nawapenda kimwonekano.
Kwa sababu hiyo ninalenga kufuga wachache, kama 6 nafikiri wanatosha.
Naomba maelezo kama yupo mwenye uzoefu au ujuzi wa ufugaji wa Kanga, kuanzia ujenzi wa banda, vyakula na ulishaji, magonjwa na matibabu yake, uzalishaji na utunzaji wa vifaranga na mambo mengine muhimu.
Tafadharini, mwenye maelezo anaombwakuyatoa hapa.
Njoo inbox nikupe maujanja then nikuizie kanga ninao wamadoa
 
Wana JF Habari za mapumziko ya sikukuu ya X-mas.

Leo nina jambo nataka uliza. Nimepata fununu kuwa katika kipindi cha hivi karibuni biashara ya mayai ya Kanga imekuwa nzuri sana kwani yai linafika hadi Tsh 1000 hasa kwa Jijiji Dsm.

Mimi huwa najishughulisha sana na ufugaji wa kuku wa kienyeji na niliposikia hii biashara mpya inayolandana na nifanyayo nikavuitwa, ila sina taarifa za kutosha kuanza kulifanyia kazi. Hivyo nimeona nililete hapa jukwaani ambapo kuna utaalam wa kila aina ili kunifungua macho.

Kwa kuanzia tu,
(1) Je ufungaji wa Kanga unakuwaje ukiliganisha na wa Kuku?
(2) Kuna sehemu maalum ambapo naweza pata hawa Kanga (vifaranga) wa kuanzia?
(3) Hivi Kanga sio maliasili ya Taifa? nikimaanisha sitasumbuliwa na Afisa wanyama pori pindi wakigundua nafuga Kanga?

Ni hayo tu kwa leo na asanteni
Mayai ya kwale au Kanga kwanini Yana thamani kiasi hiki au Yana matumizi gani?
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom