Ufugaji wa Bata Mzinga, Bata Bukini na Kanga: Maoni, Ushauri, Utaalamu na Masoko

Namba yako please inbox. Nahitaji sana vifaranga
Za muda huu wadau wa humu ndani. Kwa ishu ya bata mzinga ninao. kwa anaehitaji tunaweza kuwasiliana. Ninao wenye umri kuanzia mwezi mmoja, miwili na mitatu na bei ni nzuri ukilinganisha na umri wao. Karibu upate bata mzinga kwa manufaa yako ya ufugaji.
 
mkuu umeongelea yooote na ukasahau masoko...karibu kutupa fursa za masoko
View attachment 602460Ili kuzaliana na kumpatia mfugaji faida, bata mzinga wanahitaji matunzo ya hali ya juu. Kwa kawaida bata mzinga hula chakula kingi kuliko kuku. Bei yake ni ghali zaidi. Kabla ya kuanza ufugaji wa bata mzinga ni lazima kuhakikisha una chakula cha kutosha kwa sababu ulishaji wa ndege hawa kadri wanavyokua huwa na gharama kubwa zaidi. Ni muhimu pia kujifunza kwa undani na kufahamu namna ya kutunza vifaranga wa bata mzinga kwa kuwa hufa kwa urahisi sana. Pia, unapaswa kujikita kutafuta soko kwa sababu wanapokuwa ni vigumu kuwatunza kwa muda mrefu kutokana na ukubwa wa gharama ya chakula.
Wafugaji wachache kati ya wengi waliojaribu kuwafuga ndege hawa na kufanikiwa hata kufikia malengo yao ni kutokana na kuzingatia lishe kamili. Pamoja na hayo, wapo wafugaji ambao walishindwa kutokana na magonjwa pamoja na gharama ya utunzaji.
Chakula
Chakula cha bata mzinga hakina tofauti na cha kuku. Vifaranga wanahitaji kupata lishe kamili yenye protini kwa wingi ili waweze kukua vizuri. Vifaranga kwa siku za awali wanahitaji kiasi cha asilimia 27 ya protini mpaka wanapofikia umri wa wiki sita. Baada ya hapo mfugaji anaweza kupunguza hadi kufikia asilimia 18, na kuendelea hivyo hadi wanapokomaa. Kutokana na gharama ya kununua chakula kuwa kubwa, unaweza kutumia reseheni ifuatayo kwa ajili ya kutengeneza chakula cha bata mzinga wewe mwenyewe.

Mahitaji
• Mahindi 5kg (yasiyokuwa na dawa)
• Karanga 5kg
• Dagaa 5kg
• Mashudu 10kg
• Chokaa 5kg (chokaa inayotumika kwa lishe ya mifugo)
Namna ya kutengeneza chakula
Twanga au saga pamoja kiasi cha kulainika kisha walishe vifaranga. Mchanganyiko huu hutegemeana na wingi wa bata mzinga unaowafuga. Hakikisha kila bata anapata chakula cha kutosha na chenye uwiano ulioelekezwa. Pia waangalie mara kwa mara kuhakikisha wana chakula cha kutosha.
Uhifadhi: Hifadhi chakula cha ziada kwenye mifuko au debe kisha weka sehemu isiyo na unyevu.
Kutaga
Bata mzinga huanza kutaga anapofikisha umri wa mwaka mmoja. Ndege hawa wana uwezo wa kutaga kati ya mayai 15 hadi 20 kwa mara ya kwanza na kisha kuhatamia. Anapoendelea kukua huweza kutaga hadi mayai 30. Hii ni kulingana na lishe nzuri atakayopatiwa.
Kuhatamia
Bata mzinga anaweza kuhatamia mayai 17 hadi 20. Mayai hayo huhatamiwa kwa siku 28 na huanza kuanguliwa vifaranga kwa muda wa siku 3, kuanzia siku ya 28 hadi 31. Baada ya hapo mayai yaliyosalia bila kuanguliwa hutakiwa kutupwa kwa kuwa hayatoanguliwa tena na hayafai kwa matumizi mengine.
Utunzaji wa vifaranga
Baada ya vifaranga kuanguliwa, watenge na mama yao kwa kuwaweka kwenye banda safi lisilopitisha baridi. Unaweza kuwawekea taa ya kandili au ya umeme endapo upo kwenye sehemu unakopatikana.
Banda
Ni vyema banda liwe limesakafiwa au banda la asili la udongo usiotuhamisha maji. Pia, unaweza kutumia banda lenye mbao au mabanzi kwa chini. Unaweza pia kutandaza maranda kwenye mabanda. Hakikisha kuta za banda zimefunikwa vizuri ili kuwakinga dhidi ya baridi.
Maji
Kama ilivyo ndege wengine, bata mzinga pia wanahitaji kupatiwa maji masafi na ya kutosha wakati wote. Wawekee maji katika chombo ambacho hawatamwaga na wanakifikia vizuri. Hakikisha maji hayamwagiki bandani kwani kwa kufanya hivyo banda litachafuka na kukaribisha magonjwa kwa urahisi. Ni vizuri kuwalisha bata mzinga vyakula vingine kama majani. Majani husaidia kuwapatia protini: mfano; kunde, fiwi na aina nyingine za majani jamii ya mikunde huhitajika zaidi kwa kiasi cha 25% hadi 30%.
Magonjwa
Bata mzinga hushambuliwa na magonjwa kama taifodi, mafua na kuharisha damu. Wanapougua ni rahisi kuambukiza kuku, bata na ndege wengine wanaofugwa kwa haraka sana. Pia, ndege hawa husumbuliwa na viroboto wanaosababishwa na uchafu wa banda hasa linapokuwa na vumbi.
Chanjo
Bata mzinga wanatakiwa kupatiwa chanjo ya ndui (mara moja kila mwaka), kideri (kila baada ya miezi mitatu), gumboro (kwa muda wa wiki tano - ukiwapa jumatatu, basi unawapatia kila jumatatu ya wiki), na vitamini A mara baada ya kuanguliwa.

Kwa mafunzo zaid tembelea www.lengisho.blogspot.com[/QUOTE
 
Nina fuga bata nina muda mrefu sijala nyama ya kuku kabisa nyumbani labda nje ya nyumbani kitu ambacho kina nifanya nipende nyama ya Bata bata hatibiwi tibiwi kama kuku kuku kila mara chanjo!
Bata huwa nina Tafuna na mifupa kabisa bila hofu!
Kuku ma antibiotics kila mwezi wana pewa sio wa kisasa sio wa kienyeji labda kidogo kuku wa huko mikoani Ila pia dawa hawakwepi!
 
Nina fuga bata nina muda mrefu sijala nyama ya kuku kabisa nyumbani labda nje ya nyumbani kitu ambacho kina nifanya nipende nyama ya Bata bata hatibiwi tibiwi kama kuku kuku kila mara chanjo!
Bata huwa nina Tafuna na mifupa kabisa bila hofu!
Kuku ma antibiotics kila mwezi wana pewa sio wa kisasa sio wa kienyeji labda kidogo kuku wa huko mikoani Ila pia dawa hawakwepi!
nataka bata perkin na bukin kama unao boss wangu
 
yes wanaliwa na ni watamu sana. sema tu bei yake huwa iko juu kiasi ndio maana watu wengine wanaogopa kununua
Duuh me sidhani kama nitaweza kuwala labda nipewe nyama yao bila kujua... bata wa kawaida tu nimeanza kuwazoea juzi kati tu.
 
hapa ndo huwa napenda yaani kama hujuikitu we uliza kisha utapata majibu yanayo stahili bila taabu na kuwaelewesha wengine maana hatamimi nilikuwa naitaji sana nshu hii
Nimeifurahia hii,nilikuwa sijui kanga anaatamia muda gani sasa nimeelewa.
 
Pia kanga anapiga kelele akiona kitu hatari mfano nyoka, vicheche na hivyo kuwakurupusha maadui Hawa waingiapo himaya ya mfugaji
 
nataka bata perkin na bukin kama unao boss wangu
IMG_20181231_134459.jpg

Ninao mkuu Ila sijawaza kuwauza maana nina penda sana kuwaona upo wapi mkuu unataka wangapi?
 
Changamoto kubwa kwa kanga ni vifo vya ghafla kwa vifaranga. Mwanzoni nilichanganyikiwa unakuta kifaranga mzima kabisa akilowa kidogo tu na hata ukimgusa mikono ikiwa na vimajimaji ghafla anaanza kutetemeka na ndani ya nusu saa amekufa. Akipata stress kidogo amekufa.

Tatizo lingine ni udhaifu wa miguu yaani anatambalia tumbo miguu ime paralyze kabisaa na baada ya muda anakufa

Nilikuwa na vifaranga 200 kila siku wanakufa 10-20 mpaka wakabaki 92

Suluhisho:
Nilikwenda kwa mzee daktari dukani nikamueleza nahitaji chanjo ya kanga na nikampa sababu, akaniambia kanga huwa hashambuliwi na magonjwa Kama kuku na hivyo chanjo haina maana ila vifo kwa vifaranga ni kutokana na upungufu mkubwa wa vitamin A. Alinipa aminovet ya kuwachanganyia kwenye maji (bei 6000) niliwapa mchana ule ule siku ya pili walikufa 2 ambao walikuwa dhaifu na siku ya 3 hakuna kifo na ndiyo ukawa mwisho wa vifo.

Hii iminovet unawapa kila siku na wanaipenda sana, ukiwawekea maji pure hawanywi

Asante sana mzee wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom