Elungata
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 40,205
- 33,224
Mtangazaji wa ITV, kapigwa risasi.
Aliempiga yasemekana ni mchumb wake somebody Mushi, ambae pia kampiga risasi mamake Ufo Saro na kumuua na kisha yeye mwenyewe Mushi kujiua kwa risasi.
Ufo Sarro yuko mahututi
Cheki ITV breaknews.
--------------------------------
---------------------------------
=====================
MORE UPDATES:-
=====================
Aliempiga yasemekana ni mchumb wake somebody Mushi, ambae pia kampiga risasi mamake Ufo Saro na kumuua na kisha yeye mwenyewe Mushi kujiua kwa risasi.
Ufo Sarro yuko mahututi
Cheki ITV breaknews.
--------------------------------
---------------------------------
Alfajiri ya leo, mtangazaji wa ITV anayejulikana kwa jina la Ufoo Saro amejeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi na mchumba wake ambaye baada ya tukio hilo naye alijipiga risasi na kujiua. Akizungumza na wanahabari, Kamanda Wambura ambaye ni kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni amesema tukio hilo limetokea majira ya alfajiri ya leo.
Kamanda wambura amedai kuwa mwanaume aliyetenda mauaji hayo ni mchumba wake na alikuwa anafanya kazi katika Umoja wa Mataifa (UN) huko sudani ila bado haijafahamika kitengo alichokuwa akifanyia kazi. Kwa mujibu wa Kamanda Wambura, inasemekana kulikua kuna ugomvi kati ya wawili hao ambapo walishindwa kuelewana na ndipo walipoamua kwenda kwa mama mzazi wa Ufoo Saro(mama mkwe) ili awasuluhishe.
Baada ya usuluhishi kuanza na kuonekana kuwa tatizo liko kwa mwanaume, mwanaume huyo alimshutumu mama mkwe wake kwamba amekuwa na mazoea ya kumtetea mwanae na ndipo alipotoa bastola na kumpiga mama yake na Ufoo Saro risasi ya kichwa na kumuua papo hapo.... Alipomuua mama huyo, mwanaume huyo alimpiga Ufoo Saro risasi mbili, moja ya tumboni na nyingine ya mguuni na kudhani kwamba amemuua kumbe amemjeruhi tu kisha kujipiga mwenyewe risasi ya kidevuni na kufariki dunia hapo hapo.
sio yeye tu na mama yake mzazi ambaye ameshafariki, na muuaji amabaye anatajwa kuwa mchumba wake anayefanya kazi UN pia anadaiwa kajiua kwa risasi.
Ametoka hospital ya tumbi anapelekwa Muhìmbili. Anaendelea vizuri.
Nimesikia Breaking News ITV.Nimeshtushwa sana kusikia Taarifa hii.It's so Sad
Ufoo Saro Muda huu yupo Hospitali amejeruhiwa kwa Risasi Tumboni na Mguuni.
Mama yake amepigwa Risasi Kifuani na Huyo Mchumba wake amejipiga Risasi kidevuni na kufa papo hapo.Hali ya Ufoo Saro hadi sasa haijulikani ikoje
Jeshi la polisi limetangaza kuwa linachunguza kujua ndugu za huyo mume wake.Inasemekana ni Mfanyakazi wa UN
Tukio limetokea leo alfajiri eneo la Kimara.
=====================
MORE UPDATES:-
=====================
Mwenyekiti mtendaji wa IPP ametoka kuongea na media sasa hivi. Anasema Ufoo anaendelea vema na anazungumza.
Kapigwa risasi tumboni na mkononi na madaktari wanahangaika kuhakikisha wanaokoa maisha yake. Wameomba apumzike kwa sasa so hakuna mwandishi alieruhusiwa kuingia ndani wala ndugu zaidi ya Mzee Mengi tu.
Afande Ahmed Msangi nae amesema Ufoo anaendelea vema. Polisi wamegawanyika katika timu tatu. Moja inaongozwa na Msangi ipo Muhimbili, ya pili ipo Kibamba yalipotokea mauaji na ya tatu inashughulika mtaani kutafuta taarifa muhimu za mauaji. Soon watakutana kutoa updates.
Naweka picha za msangi na mengi wakiongea na media sasa hivi
Mengi akiongea na wanahabari nje ya kitengo cha dharula hosp ya muhimbili. Pembeni ni afande Ahmed Msangi
Afande ahmed msangi akizungumzia tukio hilo hopitalini muhimbili muda mfupi uliopita