Tina
JF-Expert Member
- Jul 9, 2007
- 572
- 579
NIKIWA HAPA DAR nakutana na Habari ya UONGO katika Gazeti la ALASIRI.
Nililibahatika kuwa Moshi mkoani Kilimanjaro na kwa bahati mbaya sana hakuna aliyejua kama mimi ni mwana JF ambaye ninafahamu mambo mengi ya nchi hii na kwa urembo wangu ndio kabisaa nilipokuwa katika hoteli moja pale mjini Moshi kabla ya kwenda Arusha, nimeshuhudia mambo ya aibu kwa waandishi wetu wa habari wa Tanzania ila sikuwa nikiamini kinachojadiliwa kabla ya kuthibitisha katika habari hii hapa chini. Kwa muhtasari hii habari ya Alasiri ya leo ni ya uzushi na kupandikizwa kwa malengo ya kisiasa na aliyekuwa akifadhili mkakati huu ni mmoja wa watu anayewania kuingia katika siasa katika jimbo la Moshi Vijijini. Mtu huyo ndiye aliyehusika pia katika ugawaji wa kadi bandia zenye malengo ya kuwang'oa wanasiasa kadhaa mkoani Kilimanjaro akiwamo Dk. Chami na Aloyce Kimaro.
Jambo la kusikitisha ni jinsi waandishi wa habari kabla hata ya 2010 wanavyokubali kutunga habari kama hii. Kwanza Chami hakuwapo msibani. Pili fedha za rambirambi zilienda kufuatwa na mwandishi mmoja katika hoteli moja ya mjini Moshi na huyo mwandishi ndiye aliyekuwa akimsema vibaya Marehemu Ali Sonda (Mungu aiweke roho yake pepoeni) na kuwasema pia waandishi wenzake wa Moshi mbele ya Dk. Chami na alichofanya Chami ni kukiri baadhi ya mambo yanayomhusu kama vile marehemu kuandika habari nyingi mbaya bila kuwa na ushahidi nazo. Hii ni hatari sana na wahusika wa IPP Media na vyombo vingine waangalie, kabla vyombo vyao havijachafuliwa na UFISADI.
Jambo la kujiuliza ni kwanini mwandishi afuate mchango kwa Dk, Chami hotelini na akae kuanzia saa moja usiku hadi saa nne? Kwanini waandishi badala ya kuchanga wao waende kwa wanasiasa na wagombea wapya? Kwanini waandishi waingilie matatizo ya kifamilia nyumbani kwa marehemu Sonda kwa kuanza kuingilia hadi ugawaji wa mali za marehemu? huu ni UFISADI mwingine katika media UMULIKWE.
HABARI HUSIKA HII HAPA.
..
Waziri akwaa kashfa msibani
Na Jackson Kimambo
25th September 2009
Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Bw. Cyril Chami, amekwaa kashfa nzito baada ya kudaiwa kumsimanga marehemu kwenye msiba mmoja na hivyo wafiwa kudaiwa kumrejeshea pesa zake zote alizotoa kama rambirambi ya mpendwa wao.
Tukio hilo, limetokana na msiba wa mwandishi wa habari, Ali Sonda (47) wa gazeti la Mwananchi mjini hapa, ambaye alifariki dunia Septemba 14 mwaka huu.
Inadaiwa kuwa Naibu Waziri Chami, alitoa pesa za rambirambi kiasi cha shilingi 50,000 kwa mazishi ya mwandishi huyo aliyefia katika Hospitali ya KCMC mjini Moshi, huku pia akitoa maneno ya masimango yaliyowakera waandishi wenzie wa habari na mwishowe kuamua kumrejeshea pesa zake kwa njia ya simu ya mkononi.
Inadaiwa kuwa Chami alisema anatoa pesa kwa marehemu Sonda basi tu, kwani enzi za uhai wake alikuwa akimchafua sana, kauli ambayo iliwafanya waandishi ambao ni sehemu ya wafiwa kuamua kumrejeshea rambirambi yake, kwani walidai kuwa Sonda (marehemu) ametuhumiwa na Naibu Waziri Chami ilhali ikijulikana fika kuwa hawezi kufufuka na kujitetea.
Uamuzi wa kususia rambirambi ya Chami kutokana na msiba wa marehemu Sonda, umetolewa na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Kilimanjaro, ikiwa ni baada ya Kamati ya mazishi kutamka kwenye majumuisho yaliyofanyika hoteli ya Kilimanjaro Cren kuwa haikuridhishwa na kauli alizotoa Chami ambaye pia ni Mbunge wa Moshi Vijijini (CCM), wakati akitoa rambirambi yake kwa marehemu (Sonda).
Kaimu Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Lini Kamafa, alisema wao na kamati hiyo ya mazishi haikufurahishwa na kauli za Chami wakati akitoa rambirambi yake kuhusiana na kifo cha mwenzao, hivyo wanasusia rambirambi hiyo kwa kumrejeshea fedha yake yote.
Kamafa akasema hawakufurahishwa na kauli iliyotolewa na Naibu Waziri huyo kuhusu uhusiano wake na Sonda wakati wa uhai wake na waandishi wengine wa habari mkoani Kilimanjaro kwa jumla.
Akadai kuwa pamoja na mambo mengine, Mbunge huyo (Chami), anadaiwa kumtupia lawama marehemu huyo kwa kile alichodai kuwa alikuwa akimwandika vibaya katika magazeti.
"Kwanza namchangia Sonda basi tu .... kwani alikuwa akinichafua... na nimeshawasaidia sana waandishi... nakutuma nenda kawaambie na ujumbe umefika, mmoja wa waandishi hao akasema kwa kukariri maneno ya Chami.
Kamafa akasema wamelazimika kurejesha Sh. 50,000 na kwamba kama Chami ataona hajatendewa haki, anayo nafasi ya kuomba kukutana na waandishi hao ili kuelezea malalamiko yao.
Kwanza Sh 50,000 tayari tumeshazirejesha kwake kwa kutumia simu yake ya mkononi... huko alipo tayari zitakuwa zimeshamfikia, akasema Kamafa na kushangiliwa na waandishi wenzie wa mkoani Kilimanjaro.
Sonda ambaye alikuwa miongoni wa waandishi wa Mwananchi Mkoa wa Kilimanjaro, alizaliwa mwaka 1962 na kufariki dunia baada ya kuugua kifua kwa muda mrefu na kuzikwa nyumbani kwao katika Kijiji cha Chekereni.
Alasiri ilipomsaka Chami kwa njia ya simu leo asubuhi ili kuweza kupata maelezo yake, haikuweza kufanikiwa kwani simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita hadi kukatika bila kupokelewa.
CHANZO: ALASIRI
Nililibahatika kuwa Moshi mkoani Kilimanjaro na kwa bahati mbaya sana hakuna aliyejua kama mimi ni mwana JF ambaye ninafahamu mambo mengi ya nchi hii na kwa urembo wangu ndio kabisaa nilipokuwa katika hoteli moja pale mjini Moshi kabla ya kwenda Arusha, nimeshuhudia mambo ya aibu kwa waandishi wetu wa habari wa Tanzania ila sikuwa nikiamini kinachojadiliwa kabla ya kuthibitisha katika habari hii hapa chini. Kwa muhtasari hii habari ya Alasiri ya leo ni ya uzushi na kupandikizwa kwa malengo ya kisiasa na aliyekuwa akifadhili mkakati huu ni mmoja wa watu anayewania kuingia katika siasa katika jimbo la Moshi Vijijini. Mtu huyo ndiye aliyehusika pia katika ugawaji wa kadi bandia zenye malengo ya kuwang'oa wanasiasa kadhaa mkoani Kilimanjaro akiwamo Dk. Chami na Aloyce Kimaro.
Jambo la kusikitisha ni jinsi waandishi wa habari kabla hata ya 2010 wanavyokubali kutunga habari kama hii. Kwanza Chami hakuwapo msibani. Pili fedha za rambirambi zilienda kufuatwa na mwandishi mmoja katika hoteli moja ya mjini Moshi na huyo mwandishi ndiye aliyekuwa akimsema vibaya Marehemu Ali Sonda (Mungu aiweke roho yake pepoeni) na kuwasema pia waandishi wenzake wa Moshi mbele ya Dk. Chami na alichofanya Chami ni kukiri baadhi ya mambo yanayomhusu kama vile marehemu kuandika habari nyingi mbaya bila kuwa na ushahidi nazo. Hii ni hatari sana na wahusika wa IPP Media na vyombo vingine waangalie, kabla vyombo vyao havijachafuliwa na UFISADI.
Jambo la kujiuliza ni kwanini mwandishi afuate mchango kwa Dk, Chami hotelini na akae kuanzia saa moja usiku hadi saa nne? Kwanini waandishi badala ya kuchanga wao waende kwa wanasiasa na wagombea wapya? Kwanini waandishi waingilie matatizo ya kifamilia nyumbani kwa marehemu Sonda kwa kuanza kuingilia hadi ugawaji wa mali za marehemu? huu ni UFISADI mwingine katika media UMULIKWE.
HABARI HUSIKA HII HAPA.
..
Waziri akwaa kashfa msibani
Na Jackson Kimambo
25th September 2009
Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Bw. Cyril Chami, amekwaa kashfa nzito baada ya kudaiwa kumsimanga marehemu kwenye msiba mmoja na hivyo wafiwa kudaiwa kumrejeshea pesa zake zote alizotoa kama rambirambi ya mpendwa wao.
Tukio hilo, limetokana na msiba wa mwandishi wa habari, Ali Sonda (47) wa gazeti la Mwananchi mjini hapa, ambaye alifariki dunia Septemba 14 mwaka huu.
Inadaiwa kuwa Naibu Waziri Chami, alitoa pesa za rambirambi kiasi cha shilingi 50,000 kwa mazishi ya mwandishi huyo aliyefia katika Hospitali ya KCMC mjini Moshi, huku pia akitoa maneno ya masimango yaliyowakera waandishi wenzie wa habari na mwishowe kuamua kumrejeshea pesa zake kwa njia ya simu ya mkononi.
Inadaiwa kuwa Chami alisema anatoa pesa kwa marehemu Sonda basi tu, kwani enzi za uhai wake alikuwa akimchafua sana, kauli ambayo iliwafanya waandishi ambao ni sehemu ya wafiwa kuamua kumrejeshea rambirambi yake, kwani walidai kuwa Sonda (marehemu) ametuhumiwa na Naibu Waziri Chami ilhali ikijulikana fika kuwa hawezi kufufuka na kujitetea.
Uamuzi wa kususia rambirambi ya Chami kutokana na msiba wa marehemu Sonda, umetolewa na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Kilimanjaro, ikiwa ni baada ya Kamati ya mazishi kutamka kwenye majumuisho yaliyofanyika hoteli ya Kilimanjaro Cren kuwa haikuridhishwa na kauli alizotoa Chami ambaye pia ni Mbunge wa Moshi Vijijini (CCM), wakati akitoa rambirambi yake kwa marehemu (Sonda).
Kaimu Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Lini Kamafa, alisema wao na kamati hiyo ya mazishi haikufurahishwa na kauli za Chami wakati akitoa rambirambi yake kuhusiana na kifo cha mwenzao, hivyo wanasusia rambirambi hiyo kwa kumrejeshea fedha yake yote.
Kamafa akasema hawakufurahishwa na kauli iliyotolewa na Naibu Waziri huyo kuhusu uhusiano wake na Sonda wakati wa uhai wake na waandishi wengine wa habari mkoani Kilimanjaro kwa jumla.
Akadai kuwa pamoja na mambo mengine, Mbunge huyo (Chami), anadaiwa kumtupia lawama marehemu huyo kwa kile alichodai kuwa alikuwa akimwandika vibaya katika magazeti.
"Kwanza namchangia Sonda basi tu .... kwani alikuwa akinichafua... na nimeshawasaidia sana waandishi... nakutuma nenda kawaambie na ujumbe umefika, mmoja wa waandishi hao akasema kwa kukariri maneno ya Chami.
Kamafa akasema wamelazimika kurejesha Sh. 50,000 na kwamba kama Chami ataona hajatendewa haki, anayo nafasi ya kuomba kukutana na waandishi hao ili kuelezea malalamiko yao.
Kwanza Sh 50,000 tayari tumeshazirejesha kwake kwa kutumia simu yake ya mkononi... huko alipo tayari zitakuwa zimeshamfikia, akasema Kamafa na kushangiliwa na waandishi wenzie wa mkoani Kilimanjaro.
Sonda ambaye alikuwa miongoni wa waandishi wa Mwananchi Mkoa wa Kilimanjaro, alizaliwa mwaka 1962 na kufariki dunia baada ya kuugua kifua kwa muda mrefu na kuzikwa nyumbani kwao katika Kijiji cha Chekereni.
Alasiri ilipomsaka Chami kwa njia ya simu leo asubuhi ili kuweza kupata maelezo yake, haikuweza kufanikiwa kwani simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita hadi kukatika bila kupokelewa.
CHANZO: ALASIRI