Makindi N
JF-Expert Member
- Mar 14, 2008
- 1,066
- 173
Jamani Burka Estate, lililokua shamba la Kahawa, limegawiwa. Sitaki kuhoji kama maamuzi ya kuligawa hilo shamba na kuwa ni makazi ni sahihi. Bali Halmashauri ya Mji wa Arusha, lilitangaza watu waombe ili wapewe viwanja. Form zilitolewa na Manispaa kwa TShs. 10,000/=. Zaidi ya watu elfu 30 waliomba hivyo viwanja ambao wengi wao ni wa kipato cha kati, cha chini na wasio na viwanja kama maelekezo yalivyohitaji. Majina yamebandikwa notice board ya Wilaya ya Arusha, haya ni majina ya baadhi ya vigogo waliopo katika list ya waliopata viwanja; Lowassa, Ridhiwani Kikwete, Karamagi, Nagu, Mwanri, Ruth Mollel, Ritha Mlaki, Ole Nangole, Warioba, Iddi Simba, Tarishi, Ole Medei etc.
Pamoja na pesa nyingi zilizokusanywa kwa walalahoi kupitia application forms, majina yao yametupwa kapuni.
MY TAKE
1. This is a prime area, na wametangaza, walioomba wengi ni watu wa chini na wasio na viwanja inamaana vigezo vilikuwa ni majina makubwa? Kwanini hawakusema watu wa chini wasiombe?
2. Vigezo gani vilitumika kugawa viwanja? Halmashauri inabidi itoe majibu
3. Ukila na kipofu usimguse mkono, hawa wakulu wamefika mbali kutunganinia mkono kabisa
4. Hivi ni kweli hawa wakubwa hawana sehemu ya kuishi? Au ndo vile mwenye nacho ataongezewa?
KWA OLE MEDEI (MBUNGE MTEULE) NA GODBLESS LEMA (MBUNGE MTEULE) NA FULL COUNCIL YA ARUSHA
Ole Medei kama Mbunge mteule wa hilo jimbo na uliepata kiwanja, tupe majibu ya utaratibu uliotumika maana ni tofauti na uliotangazwa. Please NULLIFY this stupid decision at its worst.
Kazi ya kwanza kwa Mheshimiwa Mbunge mteule (Godbless Lema) na ukweli kwamba CHADEMA ndio inaunda Full Council kufuatia kuwa na madiwani wengi, pitieni maamuzi kama haya hapo Arusha Mjini na mfanye maamuzi mapya ya busara.
Wapenda Arusha na Tanzania yote, kwa mlio Arusha piteni hapo Halmashauri Arusha mjionee.
Pamoja na pesa nyingi zilizokusanywa kwa walalahoi kupitia application forms, majina yao yametupwa kapuni.
MY TAKE
1. This is a prime area, na wametangaza, walioomba wengi ni watu wa chini na wasio na viwanja inamaana vigezo vilikuwa ni majina makubwa? Kwanini hawakusema watu wa chini wasiombe?
2. Vigezo gani vilitumika kugawa viwanja? Halmashauri inabidi itoe majibu
3. Ukila na kipofu usimguse mkono, hawa wakulu wamefika mbali kutunganinia mkono kabisa
4. Hivi ni kweli hawa wakubwa hawana sehemu ya kuishi? Au ndo vile mwenye nacho ataongezewa?
KWA OLE MEDEI (MBUNGE MTEULE) NA GODBLESS LEMA (MBUNGE MTEULE) NA FULL COUNCIL YA ARUSHA
Ole Medei kama Mbunge mteule wa hilo jimbo na uliepata kiwanja, tupe majibu ya utaratibu uliotumika maana ni tofauti na uliotangazwa. Please NULLIFY this stupid decision at its worst.
Kazi ya kwanza kwa Mheshimiwa Mbunge mteule (Godbless Lema) na ukweli kwamba CHADEMA ndio inaunda Full Council kufuatia kuwa na madiwani wengi, pitieni maamuzi kama haya hapo Arusha Mjini na mfanye maamuzi mapya ya busara.
Wapenda Arusha na Tanzania yote, kwa mlio Arusha piteni hapo Halmashauri Arusha mjionee.