Ufisadi wa kutisha serikalini: Bakwata, masheikh, makanisa, maaskofu - kauli zenu

dudus

JF-Expert Member
Feb 28, 2011
22,116
49,357
Suala la ubadhirifu serikalini lilipofikia na kwa jinsi Serikali inavyolichukulia linahitaji sasa kuvuka mipaka ya kisiasa. Si suala la CHADEMA, NCCR, CUF, TLP, UDP peke yao - ni suala pana zaidi. Linatakiwa kuhusisha makundi mbali mbali ya kijamii na kiimani ili kuwa na nguvu za pamoja za kupigana nalo.

Ninategemea kusikia BAKWATA wakikemea kwa nguvu zote kupitia misikiti yote nchini. Ninategemea Sunni wote, Bohora wote, Shia wote, n.k. wafungulie vipaza sauti vya misikiti yao bila hofu kukemea uovu huu.

Ninategemea makanisa yote - Katoliki, Lutheran, Anglican, Walokole wote kuanzia maaskofu wao, wachungaji kwa wainjilisti wakemee na hata ikibidi kupiga mayowe kukemea wizi huu uliotamalaki.

Ninategemea asasi zote za kiraia, vyombo vya habari (of course baadhi) vikemee ushenzi huu badala ya kuviachia vyama vya siasa peke yao.

Suala la wizi (wanaofanya watendaji serikalini) sio suala la kisiasa ni jinai na inapaswa kukemewa na wote bila kujali itikadi, imani, au mlengo wa kisiasa unless unafaidika na uchafu huo. Vinginevyo ni usaliti na unafiki wa hali ya juu kukubali kutumiwa na wanasiasa nyakati za uchaguzi kwa manufaa binafsi au ya kichama badala ya maslahi ya taifa.

Kardinali Pengo, Sheikh Mkuu bin Simba, Askofu Malasusa, Askofu Mokiwa, Sheikh Ponda, Sheikh Bassaleh, Askofu Gamanywa, Askofu Mwingira, masheikh wote, maaskofu na wachungaji wote, watanzania na waumini wenu tunasubiri kauli zenu!
 
Hapo usiwahesabie UDP na BAKWATA katika kukemea suala lolote la ufisadi. After all huu ni upepo tu utapita na wabongo watasahau kama epa, richmond, meremeta nk
 
Hapo usiwahesabie UDP na BAKWATA katika kukemea suala lolote la ufisadi. After all huu ni upepo tu utapita na wabongo watasahau kama epa, richmond, meremeta nk

Mkuu kosa alilowahi kufanya kiongozi mmoja ndani ya taasisi fulani isiwe kosa la wote au la taasisi nzima. Naamini UDP na BAKWATA kuna viongozi wengi sana wachukia rushwa na ufisadi kama ilivyo kwa taasisi nyingine kama makanisa n.k. Vivyo hivyo wasaliti wachache wako kila mahali mkuu na hawatakaa waishe hadi ukamilifu wa dahari. La msingi ni nguvu ya pamoja ya wenye haki ambao ndio wengi.
 
Naunga mkono hoja!!

It's either they speak now,or never!!!

Exactly! Hata mimi nitawashangaa viongozi wa dini kama hawatakemea na kulaani tena kwa sauti pana wizi na ufujaji huu wa kutisha wa mali ya umma. Hili ni muhimu kuliko kuja kuzungumza nyakati za kampeni na uchaguzi.
 
Waislamu wana swala Jangwani ijumaa wiki hii ya kulaani wabunge ambao wamekataa kusaini ishu ya kutokuwa na imani na Pinda
 
Waislamu wana swala Jangwani ijumaa wiki hii ya kulaani wabunge ambao wamekataa kusaini ishu ya kutokuwa na imani na Pinda

Great! Hayo ndio mambo ya kulaani, masula mazito yanoyoligusa taifa zima. Taasisi nyingine nazo zifanye vivyo hivyo - ibada, kwa wasomi - makongamano na mihadhara, na kwa wanasiasa - maandamano na mikutano ya umma. Kwa pamoja tunaweza kutokomeza ufisadi serikalini.
 
Ijumaa kuna dua itasomwa pale jangwani na Waislam kwa hiyo ni vyema ukajoengea hapo siku ikifika
 
mkuu kosa alilowahi kufanya kiongozi mmoja ndani ya taasisi fulani isiwe kosa la wote au la taasisi nzima. Naamini udp na bakwata kuna viongozi wengi sana wachukia rushwa na ufisadi kama ilivyo kwa taasisi nyingine kama makanisa n.k. Vivyo hivyo wasaliti wachache wako kila mahali mkuu na hawatakaa waishe hadi ukamilifu wa dahari. La msingi ni nguvu ya pamoja ya wenye haki ambao ndio wengi.

bakwata ndo walimu wa ufisadi wanauza viwanja kama hawana akili nzuri na wanalindwa na dola.hata kama watauza mara mbili kiwanja kimoja suala la bakwata kukemea ufisadi liondoeni
 
Mimi binafsi kwa kuwa nimeushuhudia uovu wa wale waliopewa dhamana ya kutuongoza dhidi ya wanyonge, sitaacha kuiomba zaburi ya 58 juu ya watawala wa taifa hili mpaka Mungu atakapoiachilia haki ya mwenye haki. Watu wote wenye mapenzi mema nao wajuao jinsi nafsi iliyodhulumiwa haki ya kuishi na kunyang'anywa fursa ya ushiriki tunu ya taifa inavyotaabika, basi naomba popote pale mlipo msiache kuiomba zaburi hii dhidi ya utawala wa Tanzania uliopoteza uhalali wa kuisimamia hazina ya nchi. Bwana ni mwema hakika kwa wakati muafaka atatujibu. Na huo wakati ni sasa; saa ya ukombozi ni sasa!
.
 
Suala la ubadhirifu serikalini lilipofikia na kwa jinsi Serikali inavyolichukulia linahitaji sasa kuvuka mipaka ya kisiasa. Si suala la CHADEMA, NCCR, CUF, TLP, UDP peke yao - ni suala pana zaidi. Linatakiwa kuhusisha makundi mbali mbali ya kijamii na kiimani ili kuwa na nguvu za pamoja za kupigana nalo.

Ninategemea kusikia BAKWATA wakikemea kwa nguvu zote kupitia misikiti yote nchini. Ninategemea Sunni wote, Bohora wote, Shia wote, n.k. wafungulie vipaza sauti vya misikiti yao bila hofu kukemea uovu huu.

Ninategemea makanisa yote - Katoliki, Lutheran, Anglican, Walokole wote kuanzia maaskofu wao, wachungaji kwa wainjilisti wakemee na hata ikibidi kupiga mayowe kukemea wizi huu uliotamalaki.

Ninategemea asasi zote za kiraia, vyombo vya habari (of course baadhi) vikemee ushenzi huu badala ya kuviachia vyama vya siasa peke yao.

Suala la wizi (wanaofanya watendaji serikalini) sio suala la kisiasa ni jinai na inapaswa kukemewa na wote bila kujali itikadi, imani, au mlengo wa kisiasa unless unafaidika na uchafu huo. Vinginevyo ni usaliti na unafiki wa hali ya juu kukubali kutumiwa na wanasiasa nyakati za uchaguzi kwa manufaa binafsi au ya kichama badala ya maslahi ya taifa.

Kardinali Pengo, Sheikh Mkuu bin Simba, Askofu Malasusa, Askofu Mokiwa, Sheikh Ponda, Sheikh Bassaleh, Askofu Gamanywa, Askofu Mwingira, masheikh wote, maaskofu na wachungaji wote, watanzania na waumini wenu tunasubiri kauli zenu!



Angalizo: Umejenga hoja vizuri mkuu. Unadhani credibility ya maneno yako ingekuwa kubwa kiasi gani kama ungetumia jina lako halisi humu, badala ya pen name? Je, unaweza kubaliana na mimi kwamba matumizi ya majina feki katika hili jamvi maarufu sana yanapunguza (au kuzimua kwa kiasi kikubwa) uzito wa hoja makini na muhimu kama hii ya kwako katika forum hii?
 
Angalizo: Umejenga hoja vizuri mkuu. Unadhani credibility ya maneno yako ingekuwa kubwa kiasi gani kama ungetumia jina lako halisi humu, badala ya pen name? Je, unaweza kubaliana na mimi kwamba matumizi ya majina feki katika hili jamvi maarufu sana yanapunguza (au kuzimua kwa kiasi kikubwa) uzito wa hoja makini na muhimu kama hii ya kwako katika forum hii?

Mkuu wangu, kwanza mimi sina na wala sitegemei kuwa na umaarufu wowote; mimi ni mwananchi wa kawaida tu nisiyefahamika katika jamii - namshukuru sana Mungu kwa ajili hiyo. Hivyo basi kama ningetumia jina langu halisi badala ya "pen name" kusingebadili au kusaidia lolote.
 
Siasa imeathiri mfumo mzima wa Dini watu wameacha kuhudhuria kwenye nyumba za ibada kwa sababu wako busy kutafuta mkate wa kila siku ambao haupatikani,,,:shut-mouth:
 
Suala la ubadhirifu serikalini lilipofikia na kwa jinsi Serikali inavyolichukulia linahitaji sasa kuvuka mipaka ya kisiasa. Si suala la CHADEMA, NCCR, CUF, TLP, UDP peke yao - ni suala pana zaidi. Linatakiwa kuhusisha makundi mbali mbali ya kijamii na kiimani ili kuwa na nguvu za pamoja za kupigana nalo.

Ninategemea kusikia BAKWATA wakikemea kwa nguvu zote kupitia misikiti yote nchini. Ninategemea Sunni wote, Bohora wote, Shia wote, n.k. wafungulie vipaza sauti vya misikiti yao bila hofu kukemea uovu huu.

Ninategemea makanisa yote - Katoliki, Lutheran, Anglican, Walokole wote kuanzia maaskofu wao, wachungaji kwa wainjilisti wakemee na hata ikibidi kupiga mayowe kukemea wizi huu uliotamalaki.

Ninategemea asasi zote za kiraia, vyombo vya habari (of course baadhi) vikemee ushenzi huu badala ya kuviachia vyama vya siasa peke yao.

Suala la wizi (wanaofanya watendaji serikalini) sio suala la kisiasa ni jinai na inapaswa kukemewa na wote bila kujali itikadi, imani, au mlengo wa kisiasa unless unafaidika na uchafu huo. Vinginevyo ni usaliti na unafiki wa hali ya juu kukubali kutumiwa na wanasiasa nyakati za uchaguzi kwa manufaa binafsi au ya kichama badala ya maslahi ya taifa.

Kardinali Pengo, Sheikh Mkuu bin Simba, Askofu Malasusa, Askofu Mokiwa, Sheikh Ponda, Sheikh Bassaleh, Askofu Gamanywa, Askofu Mwingira, masheikh wote, maaskofu na wachungaji wote, watanzania na waumini wenu tunasubiri kauli zenu!
[HILI NI JAMBO ZURI KUFANYIKA LAKINI MUASISI WA SUALA HILI KUNA KUNA MAMBO HAYAJATAFAKARI BAADHI NI HAYA;
1. AMESAHAU HAWA VIONGOZI WENGI WA DINI WANAHITAJI HIZO FEDHA ZA KIFISADI KWA AJILI YA SHUGHULI ZA UJENZI WA MISIKITI, MAKANISA NA SHUGHULI NYINGINE ZA DINI NA MADHEHEBU YAO. HAJAONA MICHANGO MIKUBWA YA MAFISADI KWENYE TAFRIJA MBALI MBALI ZA KUCHANGIA SHUGHULI ZA DINI? MICHANGO MIDOGO MIDOGO YA WAUMINI WANAAMINI HAITATOSHA. WANAWAHITAJI SANA. NANI YUKO TAYARI KUIKOSA!?
2. AMESAHAU HAWA VIONGOZI WANAMWAANGALIA KIONGOZI WA NCHI KIUDINI ZAIDI HIVYO KAMA NI WADINI YAO HATA AWE NA UFISADI WA AINA GANI ASIGUZWE WA KUSEMWA KWA SABABU NI SAWA NA KUIGUZA DINI YAO AU NI CHUKI DHIDI YA DINI YAO NA SI UFISADI. HAJAONA MARA KADHAA JAMII INAPOCHACHAMAA KUPINGA MASUALA HAYA YA UFISADI BAADHI YA MAKUNDI YENYE MTAZAMO WA KIDINI KWA KUMWANGALIA KIONGOZI WA NCHI KWA DINI YAO WANAIBUKA NA KUSEMA ANASHAMBULIWA KWA AJILI YA DINI YAKE NA WALA SI KWA AJILI YA UFISADI. SASA KIONGOZI GANI ATAKUWA MUWAZI KUKEMEA HILI? AKIFANYA HIVYO KWA WALE WENYE KUMTAZAMA KWA DINI YAO WATALETA TAFSIRI YA UDINI BADALA YA UFISADI WA MALI YA UMMA WATAMWAANDAMA NA HATA KULETA TOFAUTI ZA KIDINI BADALA YA UFISADI JAMBO LA MANUFAA KWA MALI YA UMMA
3. AMESAHAU KUWA BAADHI YA VIONGOZI WAKATI WA KAMPENI WALIMWITA MGOMBEA WA CHAMA TAWALA AMBAYE NI MKUU WA NCHI KWA SASA KUWA NI CHAGUO LA MUNGU SASA KWA UFISADI HUU WA SERIKALI YAKE WATAKUWA TAYARI KUMPINGA NA HIVYO KUONEKANA SI CHAGUO LA MUNGU, BADALA YAKE WATUELEZE KWA UFISADI HUU NI CHAGUO LA NANI?. WAPO TAYARI KUJICHANGANYA NA KUPINGANA NA IMANI YAO NA KWA WAUMINI WAO WALIOWAELEZA HILO.
KWA HAYA MACHACHE TAFAKARI KABLA YA KUWAAMBIA NAO WASHIRIKI VITA HII WA KUTETEA UMMA WA WANANCHI MASKINI WA TANZANIA WENYE KULA MLO MOJA N.K
]
 
Katika viongozi wa dini/ madhehebu yaliyotajwa usitegemee kumsikia Lusekelo, kwani yeye ni mtu anayejifanya yuko karibu na serikali ili isitambue madhambi yake. Wakati mwingine anashiriki mikutano ya JK na Wazee wa DSM.Na akiona serikali inamwelekeo fulani nae huwa anelekea hukohuko.Sijui anachofaidi zaidi ya kuwadanganya waumini na moto wa uongo.
 
HILI NI JAMBO ZURI KUFANYIKA LAKINI MUASISI WA SUALA HILI KUNA KUNA MAMBO HAYAJATAFAKARI BAADHI NI HAYA;
1. AMESAHAU HAWA VIONGOZI WENGI WA DINI WANAHITAJI HIZO FEDHA ZA KIFISADI KWA AJILI YA SHUGHULI ZA UJENZI WA MISIKITI, MAKANISA NA SHUGHULI NYINGINE ZA DINI NA MADHEHEBU YAO. HAJAONA MICHANGO MIKUBWA YA MAFISADI KWENYE TAFRIJA MBALI MBALI ZA KUCHANGIA SHUGHULI ZA DINI? MICHANGO MIDOGO MIDOGO YA WAUMINI WANAAMINI HAITATOSHA. WANAWAHITAJI SANA. NANI YUKO TAYARI KUIKOSA!?
2. AMESAHAU HAWA VIONGOZI WANAMWAANGALIA KIONGOZI WA NCHI KIUDINI ZAIDI HIVYO KAMA NI WADINI YAO HATA AWE NA UFISADI WA AINA GANI ASIGUZWE WA KUSEMWA KWA SABABU NI SAWA NA KUIGUZA DINI YAO AU NI CHUKI DHIDI YA DINI YAO NA SI UFISADI. HAJAONA MARA KADHAA JAMII INAPOCHACHAMAA KUPINGA MASUALA HAYA YA UFISADI BAADHI YA MAKUNDI YENYE MTAZAMO WA KIDINI KWA KUMWANGALIA KIONGOZI WA NCHI KWA DINI YAO WANAIBUKA NA KUSEMA ANASHAMBULIWA KWA AJILI YA DINI YAKE NA WALA SI KWA AJILI YA UFISADI. SASA KIONGOZI GANI ATAKUWA MUWAZI KUKEMEA HILI? AKIFANYA HIVYO KWA WALE WENYE KUMTAZAMA KWA DINI YAO WATALETA TAFSIRI YA UDINI BADALA YA UFISADI WA MALI YA UMMA WATAMWAANDAMA NA HATA KULETA TOFAUTI ZA KIDINI BADALA YA UFISADI JAMBO LA MANUFAA KWA MALI YA UMMA
3. AMESAHAU KUWA BAADHI YA VIONGOZI WAKATI WA KAMPENI WALIMWITA MGOMBEA WA CHAMA TAWALA AMBAYE NI MKUU WA NCHI KWA SASA KUWA NI CHAGUO LA MUNGU SASA KWA UFISADI HUU WA SERIKALI YAKE WATAKUWA TAYARI KUMPINGA NA HIVYO KUONEKANA SI CHAGUO LA MUNGU, BADALA YAKE WATUELEZE KWA UFISADI HUU NI CHAGUO LA NANI?. WAPO TAYARI KUJICHANGANYA NA KUPINGANA NA IMANI YAO NA KWA WAUMINI WAO WALIOWAELEZA HILO.
KWA HAYA MACHACHE TAFAKARI KABLA YA KUWAAMBIA NAO WASHIRIKI VITA HII WA KUTETEA UMMA WA WANANCHI MASKINI WA TANZANIA WENYE KULA MLO MOJA N.K

Mkuu umeeleza mambo mazuri na kwa uhalisia. Nafasi ya dini na taasisi zake kwa taifa letu ni ipi? Umuhimu wa dini ni nini? Nijuavyo, la kwanza na la msingi ni KUKEMEA UOVU kwa nguvu zote bila kujali aliyeutenda uovu huo ni nani au ana nafasi gani katika jamii.

Hata kama kiongozi wa dini aliwahi kula, kunywa, au kuwa na urafiki na kiongozi fulani wa kisiasa hapo kabla; bila kujali kiongozi huyo (wa kisiasa) alisaidia au kutoa msaada gani kwa taasisi; kiongozi yule wa kisiasa anapokengeuka au kugeukia UCHAFU ni wajibu wa kiongozi wa dini kuonya na kukemea. Kwenye "Job Descriptions" zao, hili ndilo namba moja!

Hata hivyo, ni kweli kwenye taasisi za kidini pia kuna mafisadi wachache ila isiwe ndio kigezo cha kwamba taasisi nzima imeoza na hakuna msafi - NO!

Ujumbe muhimu kwa viongozi wa dini: WAKISHINDWA KUKEMEA HILI WANYAMAZE MILELE NA WASITULETEE UPUUZI NYAKATI ZA UCHAGUZI.
 
tuatakukumbuka CCM ukitutoaka kwa yako uliyoyafanya japo nitaje machache
wizi wa rasilimali za nchi yetu.
kutupigavirungu tunapodai haki zetu
kutuibia kura zetu tunapochagua viongozi wetu
kututambulisha kama ombaomba nje ya nchi
 
Back
Top Bottom