dudus
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 22,116
- 49,357
Suala la ubadhirifu serikalini lilipofikia na kwa jinsi Serikali inavyolichukulia linahitaji sasa kuvuka mipaka ya kisiasa. Si suala la CHADEMA, NCCR, CUF, TLP, UDP peke yao - ni suala pana zaidi. Linatakiwa kuhusisha makundi mbali mbali ya kijamii na kiimani ili kuwa na nguvu za pamoja za kupigana nalo.
Ninategemea kusikia BAKWATA wakikemea kwa nguvu zote kupitia misikiti yote nchini. Ninategemea Sunni wote, Bohora wote, Shia wote, n.k. wafungulie vipaza sauti vya misikiti yao bila hofu kukemea uovu huu.
Ninategemea makanisa yote - Katoliki, Lutheran, Anglican, Walokole wote kuanzia maaskofu wao, wachungaji kwa wainjilisti wakemee na hata ikibidi kupiga mayowe kukemea wizi huu uliotamalaki.
Ninategemea asasi zote za kiraia, vyombo vya habari (of course baadhi) vikemee ushenzi huu badala ya kuviachia vyama vya siasa peke yao.
Suala la wizi (wanaofanya watendaji serikalini) sio suala la kisiasa ni jinai na inapaswa kukemewa na wote bila kujali itikadi, imani, au mlengo wa kisiasa unless unafaidika na uchafu huo. Vinginevyo ni usaliti na unafiki wa hali ya juu kukubali kutumiwa na wanasiasa nyakati za uchaguzi kwa manufaa binafsi au ya kichama badala ya maslahi ya taifa.
Kardinali Pengo, Sheikh Mkuu bin Simba, Askofu Malasusa, Askofu Mokiwa, Sheikh Ponda, Sheikh Bassaleh, Askofu Gamanywa, Askofu Mwingira, masheikh wote, maaskofu na wachungaji wote, watanzania na waumini wenu tunasubiri kauli zenu!
Ninategemea kusikia BAKWATA wakikemea kwa nguvu zote kupitia misikiti yote nchini. Ninategemea Sunni wote, Bohora wote, Shia wote, n.k. wafungulie vipaza sauti vya misikiti yao bila hofu kukemea uovu huu.
Ninategemea makanisa yote - Katoliki, Lutheran, Anglican, Walokole wote kuanzia maaskofu wao, wachungaji kwa wainjilisti wakemee na hata ikibidi kupiga mayowe kukemea wizi huu uliotamalaki.
Ninategemea asasi zote za kiraia, vyombo vya habari (of course baadhi) vikemee ushenzi huu badala ya kuviachia vyama vya siasa peke yao.
Suala la wizi (wanaofanya watendaji serikalini) sio suala la kisiasa ni jinai na inapaswa kukemewa na wote bila kujali itikadi, imani, au mlengo wa kisiasa unless unafaidika na uchafu huo. Vinginevyo ni usaliti na unafiki wa hali ya juu kukubali kutumiwa na wanasiasa nyakati za uchaguzi kwa manufaa binafsi au ya kichama badala ya maslahi ya taifa.
Kardinali Pengo, Sheikh Mkuu bin Simba, Askofu Malasusa, Askofu Mokiwa, Sheikh Ponda, Sheikh Bassaleh, Askofu Gamanywa, Askofu Mwingira, masheikh wote, maaskofu na wachungaji wote, watanzania na waumini wenu tunasubiri kauli zenu!