Ufisadi ulirasimishwa na kuwa mfumo wa maisha ya watanzania!

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,668
40,916
Kwakweli hali ilikua mbaya sana ilipofikia. Kila mtu aliyelipenda hili Taifa, alitaka apatikane kiongozi atakayeiondoa nchi kwenye uoza wa ufisadi uliopindukia, kukubalika na jamii na kufanywa kuwa mfumo halali wa maisha ya watanzania.

Sio mimi peke yangu niliyekua nikisubiri hilo kufanyika, bali kuna wengine wengi ambao watakubaliana na mimi kuwa kulikuwa na umuhimu wa hatua stahiki kuchukuliwa ili kulimaliza tatizo.

Unakuta kijana anamaliza chuo, anaajiriwa kwenye taasisi ya serikali, baada ya mwaka, anakuwa na nyumba kadhaa, magari kadhaa, biashara kadhaa na mabibi kadhaa, lakini kwa uhalisia wa mshahara wake hakukuwa na uwezekano wa hayo yote kufanyika kwa muda mfupi sana. Ulihitajika muda.

Utaratibu halali wa maisha ya binadamu, mambo hufanyika kwa hatua na sio kwa mkupuo na kasi ya aina yake kama mfano nilioutaja hapo juu.

Ukifuatilia kiini cha fedha anazotumia kijana niliyemtaja hapo juu katika mfano nilioutoa, utakuta ni fedha za serikali ambazo zilikua ziende kwenye miradi ya maendeleo , ila zimekua diverted kwenye mifuko ya wachache.

Mfumo wa matumizi na wizi wa fedha za serikali, ulirasimishwa na kua halali, kiasi kwamba jamii ilimshangaa kabisa mtu mwenye ajira serikalini na kushindwa kupata maendeleo kwa kasi.

Baada ya awamu ya tano kuja na kuziba mianya yote ya ufujaji, kwa namna yoyote ile beneficiaries wa hiyo mirija iliyozibwa lazima wayasikie maumivu. Kwa kua fedha hizo zilikua rasmi na zilikuwa zikiingizwa kwenye mzunguko wa fedha, hakuna ubishi kwamba uchumi uliotegemea fedha hizo kwa namna moja ama nyingine utaathirika.

Baada ya uchumi uliotegemea ufisadi uliorasimishwa kutolewa upepo, uliobaki ni uchumi halisi na ndio uwezo wetu halisi wa kifedha.

Kama tunalengo la kujenga Taifa letu, tunaweza kutengeneza mifumo bora ya utafutaji wa kipato na kujenga Taifa lenye kufuata utaratibu kwa raia wake katika kufikia malengo ya kila mmoja kimaendeleo.

Tunayo nafasi ya kufanya hivyo, na tunaweza kufanikiwa kama tukitaka.
 
Mmeshindwa kumpa CAG budget ya kutosha, halafu unakuja kutapika hizo pumba zako bila evidence.
 
Kwaiyo baada ya kuzuia ufisadi na ubadhilifu nyie wenyewe kwenye chama na serikali ndio mmegeuka kuwa wapigaji kwa kula michango yote ya wana Kagera...?!!!

Shame Kabisa!!

Pelekeni pesa kwenye Halmashauri zinakufa huko...

Hopeless!!
 
wapo watakao kupinga na kukukejel, ila umeongea ukwel, wantanza nia tuyakubali mabadiliko ya kweli hata kama yanamaumiv.
 
Kwaiyo baada ya kuzuia ufisadi na ubadhilifu nyie wenyewe kwenye chama na serikali ndio mmegeuka kuwa wapigaji kwa kula michango yote ya wana Kagera...?!!!

Shame Kabisa!!

Pelekeni pesa kwenye Halmashauri zinakufa huko...

Hopeless!!
Kufanya hivyo itakua ni kutupa dhahabu kwenye zizi la nguruwe, watazichafua tu. Sasa tusafishe na kuua chembe chembe zote za kifisadi halafu tupeleke fedha tukiwa na kiasi flani cha imani kua zitatumika kutokana na malengo tuliyojiwekea.
 
Kwa hiyo hupendi mtu awe na majumba awe na magari awe na mabibi! Ila unapenda ashinde njaa! Ww kweli akili zako kama za pumba!
 
Kwa hiyo hupendi mtu awe na majumba awe na magari awe na mabibi! Ila unapenda ashinde njaa! Ww kweli akili zako kama za pumba!
Kama sio fedha za wizi kwanini usiwe nazo? Kama sio fedha za dili haramu na kujibinafsishia fedha za umma, kwanini usiwe nazo, kuwa nazo nyingi tu, ila usituibie!
 
Kama sio fedha za wizi kwanini usiwe nazo? Kama sio fedha za dili haramu na kujibinafsishia fedha za umma, kwanini usiwe nazo, kuwa nazo nyingi tu, ila usituibie!
Ntakupa mfano mdogo, kuna leseni ya kukata mkurungu nimelipia serikalini 8,835,000 sheria inasema nikilipa ndani ya siku 30 niwe nimetoa hiyo idadi ya miti nayoruhusiwa, akaja maghembe na siasa zake akasema hakuna kukata miti ya mkurungu! Ukumbuke serikali imechukua hela yangu halaf inasema siruhusiwi kukata miti! Hebu imagine hiyo hela nimewekeza nyumba yangu bank wamenipa credit, sasa si watauza hii nyumba yangu? Huoni hii serikali imenitia umaskini? Na ukumbuke miaka yote serikali huruhusu ukataji miti kihalali na kwenye budget ya mwezi wa saba tumepewa leseni tukate miti inayoruhusiwa!
 
Kwakweli hali ilikua mbaya sana ilipofikia. Kila mtu aliyelipenda hili Taifa, alitaka apatikane kiongozi atakayeiondoa nchi kwenye uoza wa ufisadi uliopindukia, kukubalika na jamii na kufanywa kuwa mfumo halali wa maisha ya watanzania.

Sio mimi peke yangu niliyekua nikisubiri hilo kufanyika, bali kuna wengine wengi ambao watakubaliana na mimi kuwa kulikuwa na umuhimu wa hatua stahiki kuchukuliwa ili kulimaliza tatizo.

Unakuta kijana anamaliza chuo, anaajiriwa kwenye taasisi ya serikali, baada ya mwaka, anakuwa na nyumba kadhaa, magari kadhaa, biashara kadhaa na mabibi kadhaa, lakini kwa uhalisia wa mshahara wake hakukuwa na uwezekano wa hayo yote kufanyika kwa muda mfupi sana. Ulihitajika muda.

Utaratibu halali wa maisha ya binadamu, mambo hufanyika kwa hatua na sio kwa mkupuo na kasi ya aina yake kama mfano nilioutaja hapo juu.

Ukifuatilia kiini cha fedha anazotumia kijana niliyemtaja hapo juu katika mfano nilioutoa, utakuta ni fedha za serikali ambazo zilikua ziende kwenye miradi ya maendeleo , ila zimekua diverted kwenye mifuko ya wachache.

Mfumo wa matumizi na wizi wa fedha za serikali, ulirasimishwa na kua halali, kiasi kwamba jamii ilimshangaa kabisa mtu mwenye ajira serikalini na kushindwa kupata maendeleo kwa kasi.

Baada ya awamu ya tano kuja na kuziba mianya yote ya ufujaji, kwa namna yoyote ile beneficiaries wa hiyo mirija iliyozibwa lazima wayasikie maumivu. Kwa kua fedha hizo zilikua rasmi na zilikuwa zikiingizwa kwenye mzunguko wa fedha, hakuna ubishi kwamba uchumi uliotegemea fedha hizo kwa namna moja ama nyingine utaathirika.

Baada ya uchumi uliotegemea ufisadi uliorasimishwa kutolewa upepo, uliobaki ni uchumi halisi na ndio uwezo wetu halisi wa kifedha.

Kama tunalengo la kujenga Taifa letu, tunaweza kutengeneza mifumo bora ya utafutaji wa kipato na kujenga Taifa lenye kufuata utaratibu kwa raia wake katika kufikia malengo ya kila mmoja kimaendeleo.

Tunayo nafasi ya kufanya hivyo, na tunaweza kufanikiwa kama tukitaka.
Huu ndio ukweli ambao naamini kuna watu wataupinga
 
Ni mfumo wa maisha ya CCM! (kuhonga wabunge milioni kumi). Siyo watanzania.!Jifunze kuwa na heshima kwa watanzania.! Heshima ni kitu cha bure! Wewe unakikosaje?!
 
Kwakweli hali ilikua mbaya sana ilipofikia. Kila mtu aliyelipenda hili Taifa, alitaka apatikane kiongozi atakayeiondoa nchi kwenye uoza wa ufisadi uliopindukia, kukubalika na jamii na kufanywa kuwa mfumo halali wa maisha ya watanzania.

Sio mimi peke yangu niliyekua nikisubiri hilo kufanyika, bali kuna wengine wengi ambao watakubaliana na mimi kuwa kulikuwa na umuhimu wa hatua stahiki kuchukuliwa ili kulimaliza tatizo.

Unakuta kijana anamaliza chuo, anaajiriwa kwenye taasisi ya serikali, baada ya mwaka, anakuwa na nyumba kadhaa, magari kadhaa, biashara kadhaa na mabibi kadhaa, lakini kwa uhalisia wa mshahara wake hakukuwa na uwezekano wa hayo yote kufanyika kwa muda mfupi sana. Ulihitajika muda.

Utaratibu halali wa maisha ya binadamu, mambo hufanyika kwa hatua na sio kwa mkupuo na kasi ya aina yake kama mfano nilioutaja hapo juu.

Ukifuatilia kiini cha fedha anazotumia kijana niliyemtaja hapo juu katika mfano nilioutoa, utakuta ni fedha za serikali ambazo zilikua ziende kwenye miradi ya maendeleo , ila zimekua diverted kwenye mifuko ya wachache.

Mfumo wa matumizi na wizi wa fedha za serikali, ulirasimishwa na kua halali, kiasi kwamba jamii ilimshangaa kabisa mtu mwenye ajira serikalini na kushindwa kupata maendeleo kwa kasi.

Baada ya awamu ya tano kuja na kuziba mianya yote ya ufujaji, kwa namna yoyote ile beneficiaries wa hiyo mirija iliyozibwa lazima wayasikie maumivu. Kwa kua fedha hizo zilikua rasmi na zilikuwa zikiingizwa kwenye mzunguko wa fedha, hakuna ubishi kwamba uchumi uliotegemea fedha hizo kwa namna moja ama nyingine utaathirika.

Baada ya uchumi uliotegemea ufisadi uliorasimishwa kutolewa upepo, uliobaki ni uchumi halisi na ndio uwezo wetu halisi wa kifedha.

Kama tunalengo la kujenga Taifa letu, tunaweza kutengeneza mifumo bora ya utafutaji wa kipato na kujenga Taifa lenye kufuata utaratibu kwa raia wake katika kufikia malengo ya kila mmoja kimaendeleo.

Tunayo nafasi ya kufanya hivyo, na tunaweza kufanikiwa kama tukitaka.
Ukweli mchungu sana huo!! Pesa za Ufisadi zilizagaa mitaani bila mipangilio. Watu wachachr wakawa wanajitajirisha na kufanya anasa!! Sasa wamebanwa!! Hakuna longolongo tena!!
 
Ukweli mchungu sana huo!! Pesa za Ufisadi zilizagaa mitaani bila mipangilio. Watu wachachr wakawa wanajitajirisha na kufanya anasa!! Sasa wamebanwa!! Hakuna longolongo tena!!
Ukisikia vilio jua kuna watu wamebanwa! na wabanwe kwa maslahi mapana ya walio wengi!
 
Ni ukweli ulichokiandika kwamba ufisadi ulikuwa tayari ni mfumo kwenye maisha yetu, serikali iendelee kuupiga marufuku na sisi wananchi tutakuwa nyuma yake ila na hela inayookolewa ionekane.
 
Ukisikia vilio jua kuna watu wamebanwa! na wabanwe kwa maslahi mapana ya walio wengi!

Labda kama mm ndio sielewi, mpaka sasa japo kuna kubanwa kwa njia hizo, lakini walio wengi ndio bado wanalia na wachche ndio wanapeta. Angalia mkuu wa nchi, mawaziri, na viongozi wa taasisi mbalimbali za umma wanapata mishahara mikubwa, wanatumia magari ya bei mbaya, huduma karibia zote ni bure kama maji, nishati nk. Kwanini ni wao wasilipwe kidogo kuendana na uchumi wa nchi na huduma zote wajilipie ikiwa ni pamoja na kutotumua ma VX mpaka uchumi ukue? Ama wao wafarisayo kuwabebesha wengine mizigo wasiyoweza kuibeba? Hapa ndio unakuta kiongozi anahimiza watu wajiajiri, ila yeye hayuko tayari kujiajiri na yuko radhi kushinda kwa sangoma ama hata kuharibu amani ili abaki kwenye mrija.
 
Back
Top Bottom