Ufisadi: Taarifa zaidi

yesekaguta

New Member
Jan 21, 2008
1
0
Wana JF,

Hapa kuna kipande cha habari zingine, zimepatikana kwa mdau mmoja hapa. Sina uhakika sana na habari hizi. Naomba senior JF members and experts angalieni ukweli wake.

Ndugu JK, Watu wananchi wanasema hivi:

(1) Tanzania ni nchi yenye rasimali na utajiri wa hali ya juu Afrrica na ulimwenguni, lakini ni masikini ya kutupwa kwa kiwango cha nafasi ya tatu kwa umasikini duniani kwani nyie viongozi wa ngazi za juu mnalea na kukumbatia ufisadi na mafisadi mufilisi ambayo nitayataja leo kwa ufisadi wake.

(2) Utajiri wa rasilimali zinazoporwa na mafisadi ulionao zingeweza kufanya mambo makubwa na mazuri yafuatayo:

(i) Kusomesha Watanzania wote bure kuanzia Chekechea hadi kiwango cha PhD

(ii) Kuwalipa posho Watanzania wasio na ajira kila mwezi kama yanavyofanya mataifa yenye utajiri kama wetu

(iii) Kuwa na kilimo na mifugo bora na endelevu yenye kuingiza zaidi ya 60% ya pato la taifa kuliko sasa ambapo sekta hiyo inachangia 12% tu ya pato la taifa kutokana na kuhujumiwa na mafisadi wafanyabiashara kwa manufaa binafisi kma Wasira na Diallo.

(iv) Kuwa na matibabu bure kwa kila mtanznia kwani kodi wanazotozwa wafanyakazi, wafanyabiashara na wakulima ni kubwa mno. Pia zaidi ya 90% ya pato la taifa inaporwa na mafisadi uliowaweka katika ngazi ya uwaziri, makatibu wakuu na kurugenzi mbalimbali kote nchini zikiwamo halimashauri.

(v) Kuwa na viwanda vikubwa, vya kisasa vyenye kuingizia taifa zaidi ya 46% ya pato la taifa. Lakini cha kushangaza serikali imefunga ndoa na kunguruwaporaji wa uchumi wa kihindi na Kiarabu kama Jeetu P, Chavda na R. Aziz

(vi) Tanzania ingekuwa ni kisiwa cha uzuri na mandhari murua ya maendeleo ya kuja kujifunizia matifa mbalimbali ulimwenguni lakini cha ajabu ndiyo imekuwa jalala la kila nyanja ya umasikini

Ndugu Kikwete, pamoja na kwamba Mafisadi Lowassa, Karamagi na Msabaha waneshaachia ngazi, bado kuna mafisadi wengine uliowakumbatia na kuwaweka karibu na wewe huku wakiifilisi nchi kama mafisi ya kienyeji ni hawa wafuatao:

Zakhia Meghji:
-
(A) Aligawa holela vitalu vya uwindaji akaipotezea Tanzania Tsh 3,304, 903,050/- akiwa waziri wa Mali Asili na Utalii. Ovyo zaidi hata wanafamilia wake walijiingiza katika ufisadi huo kwa kumiliki baadhi ya vitalu kibadhilifu.

(B) Alipotosha ripoti ya mkaguzi wa BOT mwaka 2005/2006

(C) Kuchonga bajeti angamizi ya mwaka 2007/2008

(D) Kuidhinisha matumizi mabovu zaidi ya millioni 143 kwa mawaziri mafisadi kwenda kuifagilia bajeti ya kihuni ya 2007/2008 mikoani. Mafisadi hao hawakusita kukomba millioni 143 Tsh kwenda kuzomewa mikoani.

(E) Kufumbia macho shughuli fisadi na za kitapeli za BOT ambayo iliipatia Tangold ltd Kampuni feki kiasi zaidi ya Sh 37.7 billioni ambayo haikuwa na usajili wowote, akidanganya kuwa ni matumizi nyeti ya serikali kumbe ni ulaji wake na vigogo wenzake

(F) Kubarikli uporaji wa fedha BOT tsh 18,465,755,495. 39/- zilizopelekwa kwenye makampuni mbalimbali feki kuanzia decemba 2005 hadi 2007.

Benjamini Mkapa:

(A) Kufanya biashara akiwa ikulu ambacho ni kinyume kabisa na katiba ya nchi yetu.

(B) Kuanzisha makampuni mufilisi akiwa ikulu ambayo yamelipora taifa zaidi ya Tsh 908,798,045, 050/- akiwa ikulu hadi leo kwa makampuni ya kihuni kama ANBEN ltd, Fosnik ltd na Tanpower.

(C) Wizi wa zaidi ya Tsh Trillioni 8,86 BOT kwenye kampeini za uraisi na ubunge zilizotuwekea rais mufilisi. Mkapa anatakiwa asimame kuelekea kizimbani na kujibu wizi huo ulioifilisi nchi ikawa kama dampo la umasikini.

(D) Uporaji fedha za taia hili kupitia ununuzi wa rada feki Tsh 50 billioni ambayo aliishupalia kama ruba.

(E) Uuzwaji angamizi wa mashirika ya umma na viwanda kwa hila zote, kwani hata yale yaliyokuwa yakijiendesha kwa faida kubwa yaliuzwa kwa bei ya tupatupa (throw away prices).

(F) Kushiriki mikataba mibovu ya madini alilipotezea taifa zaidi ya Tsh 959,588,789, 005/- kwa kipindi chote Hivyo huyu ni fisadi lililokubuhu.

Edward Lowassa

(A) Anahusika moja kwa moja na ufisadi kupitia kampuni haramu ya RICHMOND na shoga wake DOWANS ambao wamelipora taifa zaidi y ash billioni 273/- kwa umeme hewa.

(B) Upotevu wa sh millioni 12.5 /- kupitia kampuni feki ya Water City ambayo aliibariki licha ya kuambiwa kuwa ilikuwa haifai, lakini E.L. aliing'ang'ania kama alimasi.

(C) Kuliingiza taif kwenye mkataba mufilisi ,fisadi na angamizi wa Buzwagi. E.L. alikuwa pamoja na fisadi kuu Karamagi kusaini mkataba angamizi na filisi hotelini uingereza. Hivyo analipotezea taifa zaidi ya billioni 3,895/- kila mwaka kwa muda wa miaka 25 kama ulivyo mkataba.

(D) Kujiingiza kwenye uporaji kwa kutumia ujenzi wa mahekalu ya hoteli ambayo hayalingani na kipato chake, akibisha data halisi tutazianika hadharani.

David Ballali

(A) Amelipotezea taifa kifisadi zaidi ya sh 693,795,398, 805.39/- kupitia BOT kwa malipo hewa kwa makampuni hewa ya kitapeli ya EPA, Jeetu P.ltd, Alex Stewart, Tangold ltd, Mwananchi gold co.ltd, Green F. Co.ltd na mengine mengi.

(B) Kulipotezea taifa matrillioni ya fedha kwa kukwamisha ukaguzi halisi wa BOT (C) Trillioni 5.3 alizochota kwa ajiri ya kampeini haramu za urais za mwaka 2005 zilizozaa rais mlea mafisadi – The breeder of corrupt leaders at all level

Basil Pesambili Mramba
(A) Alibariki na kuhusika na uporaji wa Sh 17,697,556,594. 85/- kutoka BOT akiwa waziri wa fedha kwenda kwa makampuni mbalimbali feki na watu binafsi hasa magabacholi wa kihindi na kiarabu.

(B) Ununuzi wa ndege feki ya rais, rada feki ya rais. Alitangaza Watanzania hata wakila majani ndege feki ya rais lazima ingenunuliwa. Je, mr. Mramba, uliona Watanzania ni mbuzi hata wale majani?

(C) Uuzaji feki wa Air Tanzania kwa makaburu. Asingeiingilia Kikwete Hapa Mrambaji angetajirika ukomo.

(D) Ubinafsishaji holela na kwa kiburi na uhujumu wa rasilimali za taifa kwa masilahi yake akiwa waziri wa fedha , walishirikiana na fisadi ambaye ni rafiki wake wa damu, Abdallah Kigoda.

Andrew Chenge

(A) Kalipotezea taifa zaidi ya sh 17,857,616,400/ - zilizoporwa na Tangold ltd kutoka BOT . Chenge hili hawezi kukwepa kwani alikuwa mkurugenzi wa Tangold ltd at the same time akiwa mkurugenzi wa BOT.

(B) Kulipotezea taifa mabillioni ya fedha kwa kuridhia mikataba mibovu/feki/ angamizi ya madini akiwa mwanasheria mkuu wa serikali. Takribani zilipotea zaidi ya sh 2,890,687,084, 573/- kwa kipindi chake chote. Kama anabisha tutazitoa kwa unyambulisho wake.

(C) Zaidi ya billioni 800 zinapotea kwa mwaka kwa mikataba mibovu ya ujenzi wa barabara ama kwa kuweka makampuni feki ambayo huishia kuchota fedha na kutoroaka nchini na vitita vya fedha. Ana kurugenzi wezi wizarani kwake lakini amefumbia macho kwa manufaa yake binafisi. Chenge unasubiri nini kung'atuka?

Gray Mgonja
(A) Alibariki na kuhusika na uporaji wa sh 17,857,616,400/ - BOT kwenda kampuni yao ya tangold ltd akiwa mkurugenzi wa BOT pia hapo hapo akiwa mkurugenzi wa Tangold ltd kampuni ambayo haikuwa na usajili.
(B) Kunyamazia ufisadi wa uporaji wa trillioni za fedha BOT kwenda kwenye makampuni hewa akiwa mkurugenzi BOT

Peter Msolla
(A) Uporaji wa sh millioni 5000 zilizokuwa zimetolewa na EUROPEAN OVERSEAS ANGENTS miaka ya 90 akiwa makamu mkuu wa SUA. Fedha hiyo ilikuwa imetolewa kukiendeleza chuo (SUA) kitaaluma, miundo mbinu kama barabara za ndani, tafiti mbalimbali na kuwa dila ya maendeleo ya kanda ya mashariki mwa Tanzania (Morogoro, Pwani, Tanga, Dar-es salaam).

Cha ajabu fedha hiyo iliishia kwenye midomo ya mamba mafisadi (Prof Msolla, Prof Ishengoma, Mr A. Magoma (mhasibu wa kufoji), keshia Prof Mgongo na maswahiba wao.. Planner mkuu wa wizi huo alikuwa Magoma wakisaidiana na Msolla. Wakaamua kununua magari ya kifahali na kujenga majumba ya kifahali yakiwapo magesti house kwa siri.

(B) Uporaji wa fedha za DANIDA millioni 490 zilizokuwa zimetolewa kwa ajili ya mradi wa OTAITISI (OTITIS). Fedha hiyo iligawanywa hapo vet –SUA na kunguru mafisadi wachache. Msolaa akachukua 80% ya fedha hiyo na kujenga majumba makubwa ya kifahali . Ng'ombe wa Mradi huo wakaishia kulala kwenye matope yafikapo kwenye kimo cha tumbo lao wakiwa wamesimama.. Wafadhili walikasirika kupita upeo, wakajitoa. Ukweli huu hauhitaji hata kupeleleza pale VET-SUA.

(C) Hujuma ya fedha ya punguzo la wafanyakazi SUA Tsh 2,245,045,000/ - ilyotolewa na benki ya dunia 30/6/1996. Ilipangwa kwamba mtu mwenye mshahara mdogo kabisa apewe Tsh millioni 8. Jambo la kushangaza ni kwamba kila mtu aliyepunguzwa kazi alipewa asilimia kumi tu (10%) ya malipo yake. Hivyo mwenye mshahara mdogo alipewa sh 300,000/- tu. Aliyekuwa anatakiwa kulipwa millioni 20/- alipewa millioni tatu tu.

Yeye Msolla na mafisadi wenzie (A. Magoma, Prof Luoga akiwa VC-SUA, Prof Mgongo, keshia na maswahiba wao waligawana 90% ya fedha yote iliyotolewa na benki ya dunia. Mafisadi hawa wakawa wanaishi kama wapo peponi. Wakanunua magari ya kifahali na kujenga majumba ya KUFURU yakiwamo magesti house bubu (kwa siri) na kununua mashamba kila kona Mkoani Morogoro.

(D) Wizi wa millioni 442/0 SUA kuamkia tarehe 22/4/2006.Yaani, Kati ya shs 442, shs millioni 400/- zilikuwa peti keshi zilizokusanywa kwa miaka miwili . Hivyo Msolla, Keshia, Prof Luoga na Magoma waliziiba zile millioni 400/- mchana kweupe tarehe 21/4/2006 kutoka kwenye sefu, baadaye wakaingiza sh millioni 42/- za malipo ya wafanya kazi SUA, ndipo kesho yake tarehe 22/4/2006 wakatangaza kuwa sh millioni 42/- za malipo ya wafanyakazi SUA zaibiwa Kwa uhakika zilizohamishwa kiporaji zilikuwa sh millioni 442(millioni 42 zikiwa malipo ya wafanyakazi SUA na millioni 400 zikiwa peti kesh).

Sababu ya uporaji huo wa kifisadi ni:

(i) Kujiandaa kwa kustaafu kwa Prof. Luoga, Mr Magoma na Msolla
(ii) Kutokuwa na imani na Kikwete kwani SUA walitegemea Sumaye ndiye angekuwa rais ambaye ni fisadi mwenzao. Hata hivyo hawakujua kuwa hata Kikwete ni mama na mlezi wa mafisadi
(iii) Kupata fedha lukuki za kufanyia kampeini za ubunge kwa Msolla na hatimaye uwaziri. Hivyo kesi hiyo aliisimamia Prof Monera kwa ahadi kwamba kama angefanikiwa kuivunja kesi hiyo angekuwa VC. Monera alifanikiwa kuizima kesi hiyo, Prof Luoga na Msolla wakampendekeza kwa rais awe VC ili siri hii isifichuke. Kikwete akaingia kwa jeuri yake kichwa kichwa akaweka fisadi pandikizi kuwa VC la SUA ambalo linakomba fedha ya SUA na ya wafadhili likishirikiana na Mufilisi mwenzie Prof Msolla kiasi kwamba, fedha ya wafadhili inayopitia Wizarani (Sayansi na Elimu ya juu) kwenda SUA igawanwe na kukombwa vizuri.

Joseph Mungai

(A) Aliingiza silabasi feki kuanzia chekechea hadi elimu ya sekondari kwa Watanzania wa kawaida huku watoto wao wanasoma nje ya nchi. Watoto hapa nchini hawakujua walichokuwa wanasoma, si jogg ama mchemsho. Akaua elimu kupindukia. Alifanya hivyo ili fedha nyingi zibaki wizarani ili azitumie na mafisadi wenzie kwa masilahi binafsi. Zaidi ya billioni 300 zilikuwa zinaliwa wizarani kwa ufisadi huu.

(B) Alikula takribani sh millioni 8/- za bima na Likizo za waalimu na mapunjo mbalimbali ya waalimu yakiwamo ya mishahara ya walimu wa shule za msingi na sekondari. Waalimu wakapiga kelele kudai haki zao wakaonekana kutimiza usemi kwamba KELELE ZA MLANGO HAZIMKOSESHI USINGIZI MWENYE NYUMBA.

(C) Kupora fedha inayobaki wizarani mwisho mwa mwaka. Kapuya alichagua baadhi ya maofisa wa elimu wa mikoa/wilaya na maedimasta wa shule za sekondari ambako alikuwa akituma fedha mwishoni mwa mwaka (mwezi wa 5) na baadaye kutuma wahasibu mafisadi kuifuata fedha hiyo. Alikuwa akipora kati y ash billioni 3-4 kwa mtindo huo kila mwaka alitafuna na maswahiba wake

Juma Ngasongwa

(A) Kalipotezea taifa zaidi ya sh Billioni 9,845/- kwa kipindi akiwa waziri wa Mali Asili na Utarii kwa kupewa pipi kidogo na kuachia uwindaji haramu na angamizi kwa rasilimali na uchumi wan chi. Ufisadi huu ulimfanya afukuzwe uwaziri wakati wa MZEE RUKSA kwani mzee ruksa alikuwa makini. Hakuwa kama kikwete ambaye amefunga ndoa na mafisadi kama Kapuya, Ngasongwa, Meghji, Ballali, Msolla, Diallo, Benno Ndullu nk.

(B) Kuchochea vurugu SUA. Yeye alipoona kuwa wanafunzi wa SUA wamemkataa kwa kuwa alikuwa haeleweki anachofundisha, si DS ama DESKI CHAFU, alianza vurugu zilizomfanya afukuzwe kazi SUA katika miaka ya 90. akakimbilia siasa. Vilevile mzee ruksa akamfukuza kazi Mali asili na utalii katika miaka ya 90. ----- Mkapa akamrudisha kuhujumu, pia Kikwete akameza matapishi hayo hayo.

Stephano P. Wasira

(A) Mamillioni ya fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya kupunguza makali ya mbolea ameyakomba. Yaani, fedha ya sabusidi ya mbolea zaidi ya sh billioni 12,5 ameifagia na kufanya bei ya mbolea kuanza kupaa juu kama kunguru kila kukicha katika mikoa ya nyanda za juu kusini – The big four (Mbeya, Iringa, Ruvuma na Rukwa).

Kilimo katika mikoa hiyo hutegemea mbolea asilimia mia moja (100%). Sasa mbolea haishikiki kwa wakulima wengi (90%) kwani ni kati ya sh 40000/- sh 55000/- kwenye mfuko wa kilo 50. Kwa eka moja inahitajika mifuko 4-5 kutegemea na hali ya udongo husika. Mbaya zaidi , si kikwete wala wasira anayetembelea mikoa ya Mbeya, Iringa ama Rukwa tangu wawahadae wananchi kuwaletea maisha mazuri. Huu ni utapeli wa unaotakiwa ulaaniwe na kila mpenda haki. Kila leo utamwona Kikwete akitembelea KWA WASUKUMA (MWANZA NA SHINYANGA), BUKOBA NA MUSOMA, PWANI NA MOROGORO MAANA AMEYAONA MAJITU HAYO ZUMBUKUKU.

Nazir Karamagi

(A) Kufanya ufisadi wa kusaini mikataba angamizi ya madini kama ya Buzwagi nje ya nchi hotelini! Uliolikosesha taifa sh 9,239,389,394. 25/- kwa kipindi chote

(B)Kuligharimu taifa zaidi ya billioni 173 kutokana na uroho wa kujitumbukiza kwenye sakata la kampuni tapeli ya RICHMOND na binti ya DOWANS

(C) Kunyamazia kupanda kwa umeme kwa mlipa kodi maskini ili kufidia gharama angamizi za TANESCO zinazotokana na mafisadi vigogo kutolipa gharama za umeme.

Ibrahim Msabaha

(A) Kulipotezea taifa zaidi ya sh billioni 174 kutokana na kufunga ndoa na kampuni mufilisi , feki na tapeli ya RICHMOND. Anatakiwa akamatwe atiwe ndani na alipe deni hilo .

Benno Ndullu

(A) Kabariki ufisadi na uharamia wa sh 693,795,398, 800/- zilizohamishwa kijambazi na kaka zake (Ballali, Mramba, Zaakhi M) akiwa naibu gavana wa BOT. Hili halikwepi. Tunajua amewekwa pale na kikwete ili kuficha ushahidi wa mafisadi wenzie wakiwemo watoto wa vigogo. Hapa tayari anaingia kwenye kundi la mafisadi.

(B) Kutomshauri Kikwete avunje bodi inayoshughulikia kutafuta kiini cha ufisadi BOT, kwani bodi hiyo imejaa mafisadi kama G. Mgonja, Zakhia Meghji nk Hivyo hakuna chochote kitakachofanyika zaidi ya kwenda kuficha ushahidi.

Edward Hosea

(A): Amekomba zaidi ya billioni 65 kwa kupokea rushwa nene na kutoa taarifa feki kwenye uchunguzi wa RICHMOND, sakata la Buzwagi, mikataba mibovu ya madini, sakata na hujuma za wahindi kupanga kwenye nyumba nzuri za National Housing kuliko wazawa, Sakata la DOWANS na hujuma nyingine nyingi. Ni fisadi anayetakiwa ajiuzuru mara moja.

USHAURI KWA WAPINZANI
(1) Shinikizeni kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi itakayochaguliwa na wabunge mseto. Yaani wabunge 2 CCM, 2 CHADEMA, 2 CUF, I TLP, I UDP na isiwajibike kwa kingunge yoyote bali kwa masilahi ya kitaifa. Msipofanya hivyo, mtakuwa wasindikizaji watindikiwa katika uchaguzi wa mwaka 2010. Hata tahahir huwa hashiki moto.

(2) Tembeleeni vijijini mkawaelimishe watu wanaodanganywa na CCM kila kukicha, kwani huko ndiko kuna zaidi ya 85% ya wapiga kura nchini. Wanaishi maisha magumu kama wako mahabusu ya uhaini ndani ya nchi yao lakini hakuna wa kuwaelimisha Kikwete ndio amewasusa watu wa Mbeya, Iringa, Rukwa na Ruvuma huku akiita mikoa hiyo THE BIG FOUR na kunadi kuwa kilimo ni uti wa mgongo na kuwasuta akisema kuwa mbolea ya ruzuku haipo , wasibweteke, watainunua tu hata kama bei yake inapaa kama tai kila kukicha.. Kwa akili finyu ya watanzania, mwaka 2010 atajipitisha kwao na kuwafanya wasahau kuwa aliwahi kudondoka chini akiwahadaa maisha bora katika kura za mwaka 2005. Hivyo wapinzani tembeleeni vijijini maana mjini watu wanawaelewa.

(3) Piteni mkiwaambia watanzania kuwa MAFIGA MATATU YA KIKWETE ni kurudisha utawala wa chama kimoja wenye kubariki kila ufisadi na mafisadi wa uchumi wetu na rasilimali za taifa. Utawala wa kidikiteta na mufilisi bila kuhojiwa na mtu yeyote kwani bunge linakuwa na mafisadi wanaotetea mafisadi , ufisadi na hujuma ya kila aina kwa Watanzania ili mradi tu yapore utajiri wa taifa hili.

USHAURI KWA JK

(1) Wale wote wanaohusika na ufisadi usiwarudishe madarakani (Uwaziri ama ukatibu mkuu ama ukurugenzi.

Kwa mfano;

(a) Wizara ya mifugo imeoza tangu waziri wake, makatibu wakuu na kurugenzi zake ndiyo maana haipafomu chochote. Fedha zaidi ya millioni 600 zimekuwa zikitumwa kwenye ranchi za kuzalisha mitamba na kwenda kuchukuliwa bila kufanya kazi iliyokusudiwa.


(b) Wizara ya kilimo ovyo kwani mbolea zimepanda na zinapanda kila kukicha, Wasira amekomba fungu la mbolea za ruzuku takribani billioni 12.5. Data tunazo.

(2) Achana na kuchagua watu kwa kufuata urafiki, ukoo, nafikiri umeyaona mwenyewe..
 
Dah!! sikujua kama prof Msola nae aliiba kiasi hicho kingi cha pesa..inaonekana serikali ya JK inamafisadi wengi sana nso alikuwa analipafadhila kwa wale walionesha juhudi zao kuelekea kwenye kiti cha enzi...nimesoma mpka macho yakawa yanatoa machozi:(

habari nzito hii kama imetoka kwenye reliable source na data ziwepo
 
Aisee!Hivi hizi kanuni na miiko ya viongozi imefichwa wapi?au Nyerere alizikwa nazo??

Kila mwenye mapenzi mema na nchi yetu aanike haya peupe kwa wananchi kwa njia ambayo ni rahisi kwake ,ili wasioweza kuyapata hasa vijiji hawana hii njia tando ya kupata jumbe ,Tusiwaachie wapinzani tu kuzunguka vijijini,sote tuna ndugu na jamaa vijijini,kwa nini tusitumie muda wa miezi 30 iliyobaki kuwaelimisha hamna maisha bora bila kumkoma nyani giladi??

TOGETHER WE STAND DIVIDED WE FALL
 
Mkuu nimesoma kwa makini sana hii kitu!! Wengi hawa jamaa tulikuwa tunawashtukia, lkn tulikuwa hatuna facts zozote! Asante kwa thread hii!! Tutawachmbua kama karanga mafisadi wote!
 
Mkuu nimesoma kwa makini sana hii kitu!! Wengi hawa jamaa tulikuwa tunawashtukia, lkn tulikuwa hatuna facts zozote! Asante kwa thread hii!! Tutawachmbua kama karanga mafisadi wote!
jamani mi sidhani kama hii yote ni kwelii mtu mmoja unawezaje kuchukua kiasi kikubwa hivyo??billions ??jamani acheni kupakana matope wakati mwingine tuongeee mambo yenye msingi si kila siki tuuuu kutoa shutuma za uongooo......sidhani kama inawezekana.....acheni hizoo jamani......
 
ukisoma kwa makini utagundua kuna mambo si ya kweli na kuna mambo yanahitaji kuangaliwa kwa undani zaidi.............thanks for the lead anyway
 
Pia tukumbuke kuwa Tanzania kuna kitu kinaitwa "kuongeza chumvi". Hata hivyo katika mwanga wa yaliyotokea EPA na pesa nyingine kuchotwa naamini katika Tanzania mtu anaweza kuchota milioni 400 kama kuibua kata mtungini!

Binafsi sijashtuka na kiasi cha fedha kilichoibwa (hata kama ingekuwa ni shilingi milioni moja) ninashtuka kwamba inawezekana. For now, I lean towards believing it unless proven otherwise.

Mtoa hoja kama unadata mwaga kwa 'mchunguzi(at)klhnews.com

Kwa sababu ni lazima ujiulize kwanini Msolla karudi? lazima at the end kuna pesa...
 
Benjamini Mkapa: (A) Kufanya biashara akiwa ikulu ambacho ni kinyume kabisa na katiba ya nchi yetu (B) Kuanzisha makampuni mufilisi akiwa ikulu ambayo yamelipora taifa zaidi ya Tsh 908,798,045, 050/- akiwa ikulu hadi leo kwa makampuni ya kihuni kama ANBEN ltd, Fosnik ltd na Tanpower (C) Wizi wa zaidi ya Tsh Trillioni 8,86 BOT kwenye kampeini za uraisi na ubunge zilizotuwekea rais mufilisi. Mkapa anatakiwa asimame kuelekea kizimbani na kujibu wizi huo ulioifilisi nchi ikawa kama dampo la umasikini

jamani data nyingine wala haziingii akilini, wewe just imagine Trillion 886, Tanzania zitoke wapi!, bajeti yetu yenyewe haifiki hata shillingi Trilion kumi, hizo Trillioni 886 za kuibwa zitatoka wapi?
 
yeah.. nadhani hayo manamba mengi siyo tu kutia chumvi, na mtu katia limau, vitunguu saumu, pilipili hoho na mdalasini!
 
Wanaume TMK last year waliimba ni mwaka wa shetani lakini mie nadhani huu ndio mwaka wa shetwani kwao mafisadi...
Mpaka wapandishwe kizimbani wajimini nasi ndio tupumzike na sio tuu kwaipumzishana tuu kama wajawazito huku wakiendelea kutumia fweza zetu watz....
 
Juma Ngasongwa (A) Kalipotezea taifa zaidi y ash Billioni 9,845/- kwa kipindi akiwa waziri wa Mali Asili na Utarii kwa kupewa pipi kidogo na kuachia uwindaji haramu na angamizi kwa rasilimali na uchumi wan chi. Ufisadi huu ulimfanya afukuzwe uwaziri wakati wa MZEE RUKSA kwani mzee ruksa alikuwa makini. Hakuwa kama kikwete ambaye amefunga ndoa na mafisadi kama Kapuya, Ngasongwa, Meghji, Ballali, Msolla, Diallo,Benno Ndullu nk. (B) Kuchochea vurugu SUA. Yeye alipoona kuwa wanafunzi wa SUA wamemkataa kwa kuwa alikuwa haeleweki anachofundisha , si DS ama DESKI CHAFU, alianza vurugu zilizomfanya afukuzwe kazi SUA katika miaka ya 90. akakimbilia siasa. Vilevile mzee ruksa akamfukuza kazi Mali asili na utalii katika miaka ya 90. ----- Mkapa akamrudisha kuhujumu, pia Kikwete akameza matapishi hayo hayo.

Hili nalo pia si kweli, Mh Ngasongwa hakuwahi kuwa Waziri wakati wa utawala wa Mwinyi. Aliingia kwa mara ya kwanza kwenye cabinet mwaka 1995 awamu ya Mkapa akiwa waziri wa Utalii, alijiuzuru kufuatia kashfa ya minofu na vitalu vya uwindaji.Tume iliundwa kuchunguza ilimsafisha na hatimae akarejeshwa kwenye baraza...

The rest is history....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom