Ufisadi Mwanza (Nyamagana): Walimu walioajiriwa April 01 wanyimwa mishahara kwa miezi miwili sasa

sijulikani

Member
May 15, 2014
52
89
Ajira za walimu zilitangazwa kwamba zitaanza April 01, 2014. Kweli ikawa hivyo, wengi wakaenda Halmashauri na hata wakaripoti mashuleni. Utaratibu unawataka kupeleka cheque number ambayo ikifika halmashauri basi ndiyo itakayotumika kutumia mishahara.

Baadhi wakapeleka cheque number lakini wachache tu wakapata mshahara wa April 2014. Wengi wakakosa. Ikadhaniwa kwamba tatizo la cheque namba likiisha kama walivyoelekezwa na kama walivyopewa wenzao wachache, basi mshahara wa April 2014 yaani mwezi unaoisha sasa watapa mishahara yao bila kikwazo.

Lakini ajabu ni kwamba juzi zimeanza kusambaa meseji kwenye simu kwamba walimu wanatakiwa kupeleka Halmashauri barua zao za kuomba mshahara wa mwezi huu yaani May 2014! Hakuna barua yoyote ya kufafanua au kuwaita kwa hilo bali ni hizi meseji zinazosambaa tu. Huu ndiyo utaratiibu

Hivyo ndivyo hali halisi Mwanza, wilaya ya Nyamagana. Lakini wakiulizwa walimu wa jirani yaani wa wilaya ya Ilemela, hawana tatizo hili. Wamepata mishara yao tangu mwezi walipoajiriwa April 2014.

Hiki ndicho inachokifanya uongozi wa Nyamagana bila kujali kwamba walimu hawa wanaendelea kusota bila mishahara haijulikani wanaishi vipi, wanalipia vipi pango za nyumba wanazoishi, haijulikanii wanakula kwa hela gani na ndiyo kwanza wanaanza maisha wakitokea vyuoni.

Kama kawaida habari hii hajaandikwa wala kufuatiliwa na chombo chochote cha habari ikiwemo mbunge wa Nyamagana.

Ndiyo kwanza inawaslishwa hapa JF ambacho ndiyo chombo kinachoongza sasa kwa kufumua wazi madudu kama haya.

Keep it JF, the place we dare talk openly.
 
Mwalimu punguza jazba nenda kwa ofisa elimu wako ka ulizie kero yako. Kujadili hapa mtandaoni kuna kuza tatizo kumbe jambo dogo na linaweza tatuliwa. Mbona kada zingine kama Jwt, Magereza, watendaji wa vijiji hawa lalami namna hiyo au wao hawana matatizo? Hawajui jamii forum?
 
Fuata taratibu za kiutumishi wewe acha kuropoka mitandaoni
mze wa buku saba upo...?????sasa hayo ya kuropoka unajua wewe, hayo ni baadhi ya maudhi wanayokutana nayo watumishi wengi wa serikali pindi wanpofika kwenye vituo vyao vya kazi. mimi sijui utaratibu wa nyamagana lakini kwa anayejua anaweza kumpa utaratibu mzuri zaidi na sio ku-crush tu,
Ikumbukwe tu hii hali huwa inawakuta watumishi wa ngazi za chini tu
 
kama hujapata check no huwez pata mshahara hata miaka yote ila ukipata tu check no lazima upate,shda yako una jazba sana taratibu za kiofisi haziangalii ilemela au ilala wamefanyaje,pia kumbuka nyamagana ina shule nyingi kuliko ilemela,endelea kukopa siku ukipata mshahara utarudishi shida yenu mkikopa mnaenda kula raha plasma na jembe ni jembe
 
mze wa buku saba upo...?????sasa hayo ya kuropoka unajua wewe, hayo ni baadhi ya maudhi wanayokutana nayo watumishi wengi wa serikali pindi wanpofika kwenye vituo vyao vya kazi. mimi sijui utaratibu wa nyamagana lakini kwa anayejua anaweza kumpa utaratibu mzuri zaidi na sio ku-crush tu,
Ikumbukwe tu hii hali huwa inawakuta watumishi wa ngazi za chini tu

mkuu utakuwa haupo kwenye system ww, siku ukiingia huko utajuwa tu muulize le mutuz
 
mtoa mada cheki namba au akaunt namba? mi ninavyojua ukipata cheki na mshahara tayar.
 
mtoa mada cheki namba au akaunt namba? mi ninavyojua ukipata cheki na mshahara tayar.

Mkuu,
Wewe tu ndiye umetumia akili katika thread hii na si kama watumwa wa buku saba ambao wote kwa kuwapaka mafuta kwa mgogo wachupa nimewapa LIKE.

Kama nilivyosema ni cheque number. Hivyo, hakukutakiwa kuwa na matatizo haya hata kidogo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom