Ufisadi mkubwa Wizara ya Maji

sulphadoxine

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,257
644
Wakaguzi wabaini ufujaji pesa za miradi

Mabilioni ya pesa za walipa kodi yayeyuka
Kashfa kwenye ununuzi wa mashangingi 68
Wafadhili watishia kuzuia misaada yao


SOURCE:GAZETI LA KULIKONI LA LEO 19/8/2011 -25/8/2011
 
WIZARA ya Maji na Umwagiliaji imekumbwa na kashfa kubwa baada ya ukaguzi maalumu uliofanywa kwenye miradi ya maji nchi nzima kubaini tuhuma za ufisadi, uzembe wa maofisa na matumizi mabaya ya mabilioni ya shilingi kwenye wizara hiyo.


Ukaguzi maalumu (special audit) uliofanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwenye programu ya maendeleo ya sekta ya maji (2007-2010) umebaini malipo mengi ya utata kwenye miradi ya maji nchini na matumizi mabaya ya pesa za umma.

Katika moja ya tuhuma hizo za ufisadi, Wizara ya Maji na Umwagiliaji imebainika kutumia zaidi ya dola za Marekani milioni 39 (takribani shilingi bilioni 63) kwenye mazingira ya utata bila kuzingatia miradi iliyopo kwenye mpango kazi wa mwaka wa wizara hiyo.

"Shughuli za manunuzi ndani ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji hazifanywi kuendana na mpango wa manunuzi wa kila mwaka," imesema sehemu hiyo ya ripoti mpya ya CAG kutokana na ukaguzi uliofanywa Septemba mwaka jana.
 
Pia ukaguzi huo umebaini kashfa kwenye ununuzi wa mashangingi (Toyota Land Cruiser) yapatayo 68 uliofanyika mwaka 2009 kwa Yen za Japan milioni 235.4 (zaidi ya shilingi bilioni 5) kinyume na utaratibu rasmi wa manunuzi ndani ya serikali.

Kwa mujibu wa wakaguzi wa ofisi ya CAG, ununuzi huo wa mashangingi bila kufuata taratibu za serikali umeisababishia wizara hasara ya zaidi ya shilingi milioni 218 kutokana na tofauti ya viwango vya ubadilishaji wa pesa za kigeni.

Wizara hiyo imebainika kutokuwa na ufuatiliaji wa karibu wa pesa za miradi ya maji zinazopelekwa nchi nzima kwenye mamlaka za serikali za mitaa na hivyo basi kutojua kama pesa hizo zimetumiwa kwenye matumizi sahihi ama la.

Wizara hiyo pia imekumbwa na kashfa ya matumizi makubwa ya pesa kwenye miradi mbalimbali ya maji kuliko gharama halisi za awali zilizokubaliwa kwenye miradi hiyo.

Mifano hiyo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Bwawa la Matwiga ambapo wakati mkataba wa awali ulisema kuwa mradi utagharimu dola za Marekani 284,693, wizara hiyo iliongeza malipo ya ziada kwenye mradi huo ya dola 80,615 (wastani wa shilingi milioni 129).

Kwenye mradi wa Mpwapwa na Utete, wizara ilitumia dola za Marekani 32,250 zaidi ya gharama halisi ya mradi huo kwenye mkataba wa ujenzi ambayo ilikuwa ni $39,600.
 
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Prof. Mark Mwandosya.jpg

waziri wa maji na umwagiliaji,Prof.Mark Mwandosya
 
Kazi ipo!! We needed somebody else kusafisha hii tabia chafu nchi nzima!! We can't move kama sisi wenyewe tunatoboana mifuko kwa ulafi wetu wenyewe. Its time to hang- up our boots or start afresh. Inasikitisha kuona namna ambavyo nchi hii kila mmoja alivyojaa ubinafsi, ufisadi, ujanja ujanja bila kujali kuwa mtu anahitaji pia watu wengine ili aweze kuishi kwa amani.

Nasubiri wizara ya katiba na sheria, hapo naimani ndo utakuwa mwanzo wa mabadiliko. Bila katiba mpya, tutaendelea kuchekeleana, kutishana, kuibiana na baadhi yetu kujifanya tuna haki zaidi ya wengine ilihali sote ni binadamu na twapita hapa duniani.
 
Ni kawaida yao, hasa waziri wao ndo kinara wa kuitisha mamilio yaliyopelekwa wilayani na kuyarudisha ama kuyapeleka anakokujua mwenyewe. Wakamatwe haooooooo! wezi tu
 
Wakaguzi wabaini ufujaji pesa za miradi

Mabilioni ya pesa za walipa kodi yayeyuka
Kashfa kwenye ununuzi wa mashangingi 68
Wafadhili watishia kuzuia misaada yao


SOURCE:GAZETI LA KULIKONI LA LEO 19/8/2011 -25/8/2011
Kwa utawala huu wa VASCO DA GAMA a.k.a De Lima. tutasikia mengi sana. Ndugu yangu mwana JF Sulphadoxine hata sasa tunapoongea CAG akipelekwa pale DAMPO- Tabata na akafanya ukaguzi atabaini UFISADI mkubwa sana na wakutisha. Haya ndiyo madhara ya kuwa na viongozi watokanao na CCM.
 
eeh, nchi kwishne, nukanuka, ozaoza, inapumulia mashine 99%, inahitaji madaktari bingwa kuokoa maisha la si hivyo tutaangamia nayo, Mungu sikia kilio chetu.
 
..tena ufisadi waizara hiyo haujaanza leo, kuna jamaa mmoja namfahamu yeye ni mhasibu(Though hana hata adv diploma ya accounts) yupo hapo miaka mingi alikuwa anakwiba mbaya toka miaka ya 2002 mpaka leo yupo huko!
 
eeh, nchi kwishne, nukanuka, ozaoza, inapumulia mashine 99%, inahitaji madaktari bingwa kuokoa maisha la si hivyo tutaangamia nayo, mungu sikia kilio chetu.
the best doctor is changes...hapa ukimwita mungu atakuona pungwani wa mawazo wakati akili ya kujua mema na mabaya umepewe..sasa wataka mungu aje kufanya nini..kupiga kura???? Tukubali tusikubali..mabadiliko ni lazima kwa maslahi ya taifa zima.
 
Mkuu ufisadi upo katika wizara zote .....na haya ni matunda ya mfumo mbovu uliolelewa na wenye magamba........the only way out is to overhaul
the whole system...maamuzi magumu lazima yafanyike wapende / wasipende...........Natoka kidogo
 
duh mambo yanaibuka huku bajeti ikikaribia kusomwa j3.
Nahisi kiharufu cha KIJAIRO JAIRO hivi.
 
report hii ilitoka 4 yrs ago, wizara ilisha jibu tuhuma...kulikoni inabidi wafanye homework kidogo.
 
CAG asiishie wizarani, aende huko Halmashauri za Wilaya ndiko kulikooza! Hapa jamvini tumekuwa tunafuatilia kashfa kubwa kubwa za kitaifa lakini huko mawilayani kuna mapanya buku yanakaribia kuimaliza keki ya Taifa!

The country is really sick and needs a surgeon to overhaul the entire system. Ile sheria ya uhujumu uchumi; ilsaidia sana mwaka 1983.
 
WIZARA ya Maji na Umwagiliaji imekumbwa na kashfa kubwa baada ya ukaguzi maalumu uliofanywa kwenye miradi ya maji nchi nzima kubaini tuhuma za ufisadi, uzembe wa maofisa na matumizi mabaya ya mabilioni ya shilingi kwenye wizara hiyo.


Ukaguzi maalumu (special audit) uliofanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwenye programu ya maendeleo ya sekta ya maji (2007-2010) umebaini malipo mengi ya utata kwenye miradi ya maji nchini na matumizi mabaya ya pesa za umma.

Katika moja ya tuhuma hizo za ufisadi, Wizara ya Maji na Umwagiliaji imebainika kutumia zaidi ya dola za Marekani milioni 39 (takribani shilingi bilioni 63) kwenye mazingira ya utata bila kuzingatia miradi iliyopo kwenye mpango kazi wa mwaka wa wizara hiyo.

"Shughuli za manunuzi ndani ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji hazifanywi kuendana na mpango wa manunuzi wa kila mwaka," imesema sehemu hiyo ya ripoti mpya ya CAG kutokana na ukaguzi uliofanywa Septemba mwaka jana.


Kuelekea 2015
 
billion tano 5000000000/4000000 kwa kisima tungechima visima kama 1250 wastan wa kila kijiji visima 2 ni vijiji 625 vingekuwa na maji mamasaburi bwana

Ahsante Mungu kwani unayo sababu
 
Back
Top Bottom