Dragoon
JF-Expert Member
- Nov 24, 2013
- 7,012
- 8,126
Habari za kuaminika kutoka Kampuni ya Reli Tanzania (reli ya kati) zinasema kuwa kuna ufisadi mkubwa sana umefanyika ndani ya kampuni hiyo kwenye uagizaji wa mabehewa ya treni mapya. Habari za kuaminika zinasema kuwa mabehewa yaliyoagizwa ni mabovu, na hayaendani na miundo mbinu ya reli ya kati.
Jumatatu iliyopita baadhi ya mabehewa yalifanyiwa majaribio na yalianguka kwa sababu za kiufundi. Inasemekana kwamba mabehewa yaliyoagizwa hayakupitiwa na jopo la ufundi la kampuni hiyo ili kubaini dosari zilizopo. Uongozo wa kampuni haukutaka kamati ya ufundi ichunguze mabehewa hayo.
Kutokana na hayo kuna bosi mmoja wa kampuni hiyo (jina linahifadhiwa) wiki hii yote amekuwa akifika kazini kama mgonjwa kutokana na hofu aliyonayo. Inasemekana kapuni iliyopewa tenda kutengeneza mabehewa hayo haijishughulishi na utengenezaji wa mabehewa, bali ni kampuni ya madalali tu. Mabehewa yalitengenezwa bila kufanyiwa majaribio, majaribio yakafanyika Tz.
Kuna mengine ya abiria ambayo hayajafanyiwa majaribio. Hivi karibuni Dr. Mwakembe anatarajiwa kuwasili nchini akitokea ziarani nje ya nchi. Tutegemee tamko toka kwake na kubaini mafisadi walio husika katika hili.
Jumatatu iliyopita baadhi ya mabehewa yalifanyiwa majaribio na yalianguka kwa sababu za kiufundi. Inasemekana kwamba mabehewa yaliyoagizwa hayakupitiwa na jopo la ufundi la kampuni hiyo ili kubaini dosari zilizopo. Uongozo wa kampuni haukutaka kamati ya ufundi ichunguze mabehewa hayo.
Kutokana na hayo kuna bosi mmoja wa kampuni hiyo (jina linahifadhiwa) wiki hii yote amekuwa akifika kazini kama mgonjwa kutokana na hofu aliyonayo. Inasemekana kapuni iliyopewa tenda kutengeneza mabehewa hayo haijishughulishi na utengenezaji wa mabehewa, bali ni kampuni ya madalali tu. Mabehewa yalitengenezwa bila kufanyiwa majaribio, majaribio yakafanyika Tz.
Kuna mengine ya abiria ambayo hayajafanyiwa majaribio. Hivi karibuni Dr. Mwakembe anatarajiwa kuwasili nchini akitokea ziarani nje ya nchi. Tutegemee tamko toka kwake na kubaini mafisadi walio husika katika hili.