jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,989
- 22,521
Ufisadi lazima ufe
2008-07-04 09:28:38
Na Jackson Kalindimya, Dodoma
Wabunge wamewashambulia mafisadi kwamba mtandao wao umejengwa katika nguvu ya maslahi ya fedha na wametaka ung�olewe na kuuawa kabisa. Pia wamesema kuwa kuna haja ya kuuvunja mtandao huo uoze na kusahaulika.
Mbunge wa Kasulu Magharibi (CCM), Bw. Kilontsi Mporogomyi alisema lazima watawala waache kuamini katika nguvu ya fedha bali nguvu ya hoja maana fedha ni ya muda tu.
Bw. Mporogomyi alisema, mwelekeo wa sasa ni kuvunja mitandao ya ufisadi ili kukisafisha Chama Cha Mapinduzi.
Uhusiano wa wana mitandao haukujengwa juu ya imani wala uelewa au dhamira na maelewano ya dhati, bali katika maslahi yapitayo, yaozayo na kusahaulika. Tushughulikie mafisadi alisema.
Alimpongeza Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, kwamba ameonyesha uwezo mkubwa katika kuyajua masuala muhimu na makubwa ya kitaifa na kimataifa na kwamba majibu yake kwa sasa ni makini na kwa msingi huo serikali ni makini zaidi.
Naye Mbunge wa Mbozi Mashariki, Bw. Godfrey Zambi (CCM), aliwahimiza wabunge wote kupiga vita ufisadi ili iwe ajenda ya kudumu.
Alisema mabilioni ya fedha yanapotea kwa njia za ufisadi na hata kusababisha serikali kushindwa kuwahudumia vyema wananchi ili kusukuma kasi ya maendeleo.
Watanzania watatuelewaje tusipouzungumzia ufisadi. Hivi tukiulizwa kwa nini tunalala hatuzungumzii ufisadi tutakuwa na majibu gani? Tuongeze mapambano ya ufisadi bila ya kuogopa.
Na wanaotuhumiwa kwa ufisadi sheria zichukue mkondo wake,`` alisema.
Mbunge Zambi aliipongeza serikali kwa kutenga Sh. bilioni 15 kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege Songwe, Mbeya kwamba utachangia kurahisha maeneo ya ukanda wa kusini ikiwa pamoja na kufanikisha lengo la kuwa na ukanda maalum wa uchumi katika eneo hilo.
Akigusia kuhusu Mamlaka ya hali ya Hewa (TMA), alisema kwa sasa ofisi yake imepanga katika jengo la Ubungo Plaza ambapo wanalipa Sh. milioni 400 kwa mwaka na kushauri ni vyema ukaandaliwa utaratibu wa kudumu wa kujenga ofisi na hivyo kuokoa fedha za serikali.
Kuhusu bandari ya Dar es Salaam, Bw. Zambi, alisema ni muhimu ikaimarishwa, kuondoa urasimu na kupunguza msongamano kwa kuimarisha reli ya kati ili iweze kutumia kikamilifu kuinua uchumi wa nchi vinginevyo maendeleo ya nchi ni ndoto.
Mbunge Mporogomyi alisema kama serikali itaimarisha miundombinu ya Mkoa wa Kigoma ikiwemo reli, barabara na uwanja wa ndege kuna fursa kubwa kwa mkoa huo kulitosheleza taifa kwa chakula kwa sababu ardhi ya mkoa huo ni nzuri na wakazi wa mkoa huo wana nguvu na wachapakazi.
Alisema ujenzi wa daraja la Malagarasi mkoani Kigoma utafungulia neema kubwa kwa mkoa huo ambao una hadhi nzuri unaostawisha mazao mengi lakini hayafiki sokoni na wakulima kunufaika na kilimo chao.
Aidha, alishauri kuwa, kukamilika kwa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma kutafanikisha mkoa huo kuwa kituo kikuu cha biashara katika ukanda wa Maziwa Makuu.
``Mji wa Kigoma umeainishwa na Benki ya Dunia (World Bank) kuwa ukijengewa miundombinu yake vyema utaongeza utalii kwa kasi na kupunguza umasikini wa wananchi wake,`` alisema. Bi. Joyce Masunga (CCM-Viti Maalum), akichangia mjadala huo alisema kuwa ni muhimu sana barabara za mkoa wa Tabora ambazo ziko katika hali mbaya zikajengwa ili kuwapunguzia mzigo ili kuwatua na usemi usemao ``mzigo mzito mpe mnyamwezi akubebee.``
Mbunge wa Liwale, Bw. Hassan Kigwalilo (CCM), aliiomba serikali ipige marufuku biashara ya vyuma chakavu kwa sababu inasababisha hujuma ya reli na madaraja.
Alishauri ni vyema Mbunge mmoja wa kusini awe mjumbe wa
Bodi ya Mamlaka ya Bandari Mtwara ili kusukuma kasi ya maendeleo ya bandari hiyo na eneo hilo kwa ujumla.
Wabunge hao waliyasema hayo wakati wakichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Miundombinu kwa mwaka wa fedha 2008/9.
2008-07-04 09:28:38
Na Jackson Kalindimya, Dodoma
Wabunge wamewashambulia mafisadi kwamba mtandao wao umejengwa katika nguvu ya maslahi ya fedha na wametaka ung�olewe na kuuawa kabisa. Pia wamesema kuwa kuna haja ya kuuvunja mtandao huo uoze na kusahaulika.
Mbunge wa Kasulu Magharibi (CCM), Bw. Kilontsi Mporogomyi alisema lazima watawala waache kuamini katika nguvu ya fedha bali nguvu ya hoja maana fedha ni ya muda tu.
Bw. Mporogomyi alisema, mwelekeo wa sasa ni kuvunja mitandao ya ufisadi ili kukisafisha Chama Cha Mapinduzi.
Uhusiano wa wana mitandao haukujengwa juu ya imani wala uelewa au dhamira na maelewano ya dhati, bali katika maslahi yapitayo, yaozayo na kusahaulika. Tushughulikie mafisadi alisema.
Alimpongeza Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, kwamba ameonyesha uwezo mkubwa katika kuyajua masuala muhimu na makubwa ya kitaifa na kimataifa na kwamba majibu yake kwa sasa ni makini na kwa msingi huo serikali ni makini zaidi.
Naye Mbunge wa Mbozi Mashariki, Bw. Godfrey Zambi (CCM), aliwahimiza wabunge wote kupiga vita ufisadi ili iwe ajenda ya kudumu.
Alisema mabilioni ya fedha yanapotea kwa njia za ufisadi na hata kusababisha serikali kushindwa kuwahudumia vyema wananchi ili kusukuma kasi ya maendeleo.
Watanzania watatuelewaje tusipouzungumzia ufisadi. Hivi tukiulizwa kwa nini tunalala hatuzungumzii ufisadi tutakuwa na majibu gani? Tuongeze mapambano ya ufisadi bila ya kuogopa.
Na wanaotuhumiwa kwa ufisadi sheria zichukue mkondo wake,`` alisema.
Mbunge Zambi aliipongeza serikali kwa kutenga Sh. bilioni 15 kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege Songwe, Mbeya kwamba utachangia kurahisha maeneo ya ukanda wa kusini ikiwa pamoja na kufanikisha lengo la kuwa na ukanda maalum wa uchumi katika eneo hilo.
Akigusia kuhusu Mamlaka ya hali ya Hewa (TMA), alisema kwa sasa ofisi yake imepanga katika jengo la Ubungo Plaza ambapo wanalipa Sh. milioni 400 kwa mwaka na kushauri ni vyema ukaandaliwa utaratibu wa kudumu wa kujenga ofisi na hivyo kuokoa fedha za serikali.
Kuhusu bandari ya Dar es Salaam, Bw. Zambi, alisema ni muhimu ikaimarishwa, kuondoa urasimu na kupunguza msongamano kwa kuimarisha reli ya kati ili iweze kutumia kikamilifu kuinua uchumi wa nchi vinginevyo maendeleo ya nchi ni ndoto.
Mbunge Mporogomyi alisema kama serikali itaimarisha miundombinu ya Mkoa wa Kigoma ikiwemo reli, barabara na uwanja wa ndege kuna fursa kubwa kwa mkoa huo kulitosheleza taifa kwa chakula kwa sababu ardhi ya mkoa huo ni nzuri na wakazi wa mkoa huo wana nguvu na wachapakazi.
Alisema ujenzi wa daraja la Malagarasi mkoani Kigoma utafungulia neema kubwa kwa mkoa huo ambao una hadhi nzuri unaostawisha mazao mengi lakini hayafiki sokoni na wakulima kunufaika na kilimo chao.
Aidha, alishauri kuwa, kukamilika kwa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma kutafanikisha mkoa huo kuwa kituo kikuu cha biashara katika ukanda wa Maziwa Makuu.
``Mji wa Kigoma umeainishwa na Benki ya Dunia (World Bank) kuwa ukijengewa miundombinu yake vyema utaongeza utalii kwa kasi na kupunguza umasikini wa wananchi wake,`` alisema. Bi. Joyce Masunga (CCM-Viti Maalum), akichangia mjadala huo alisema kuwa ni muhimu sana barabara za mkoa wa Tabora ambazo ziko katika hali mbaya zikajengwa ili kuwapunguzia mzigo ili kuwatua na usemi usemao ``mzigo mzito mpe mnyamwezi akubebee.``
Mbunge wa Liwale, Bw. Hassan Kigwalilo (CCM), aliiomba serikali ipige marufuku biashara ya vyuma chakavu kwa sababu inasababisha hujuma ya reli na madaraja.
Alishauri ni vyema Mbunge mmoja wa kusini awe mjumbe wa
Bodi ya Mamlaka ya Bandari Mtwara ili kusukuma kasi ya maendeleo ya bandari hiyo na eneo hilo kwa ujumla.
Wabunge hao waliyasema hayo wakati wakichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Miundombinu kwa mwaka wa fedha 2008/9.
- SOURCE: Nipashe