Ufisadi Bomba la Gesi

The Fixer

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
1,365
583
Wakuu,
Hizi taarifa za kuwa kuna ufisadi wa kutisha katika mradi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi Dsm ni za kweli ?

Na ni kwanini sasa wenye data kamili wasiziweke hapa ili mpaka Januari 27 Bunge likianza tena tushuhudie uwajibikaji wa watuhumiwa ?
 
Wakuu,
Hizi taarifa za kuwa kuna ufisadi wa kutisha katika mradi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi Dsm ni za kweli ?

Na ni kwanini sasa wenye data kamili wasiziweke hapa ili mpaka Januari 27 Bunge likianza tena tushuhudie uwajibikaji wa watuhumiwa ?


Ni kweli mkuu ila hili sakata limewekwa kiporo yaani silaha ya akiba kuelekea uchaguzi mkuu 2015

Lipo hili na la sukari.....

Stay tuned........
 
Wananchi tunataka kujua ukweli kuhusu chanzo cha kifo cha mpendwa wetu aliyekuwa waziri wa fedha Mh. Dkt. William Mgimwa.

He was serving for the interest of the public..

We need to know the secret behind his death..

Nawasilisha...
 
Wakuu,
Hizi taarifa za kuwa kuna ufisadi wa kutisha katika mradi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi Dsm ni za kweli ?

Na ni kwanini sasa wenye data kamili wasiziweke hapa ili mpaka Januari 27 Bunge likianza tena tushuhudie uwajibikaji wa watuhumiwa ?

Nasikia mabomba ya gesi yanaelekea Ulaya
 
Wananchi tunataka kujua ukweli kuhusu chanzo cha kifo cha mpendwa wetu aliyekuwa waziri wa fedha Mh. Dkt. William Mgimwa.

He was serving for the interest of the public..

We need to know the secret behind his death..

Nawasilisha...

Pole, mtoto wake amekataa
 
Wananchi tunataka kujua ukweli kuhusu chanzo cha kifo cha mpendwa wetu aliyekuwa waziri wa fedha Mh. Dkt. William Mgimwa.

He was serving for the interest of the public..

We need to know the secret behind his death..

Nawasilisha...
Mwanae kadai kuwa familia yao haitaki, kifo cha mpendwa wao Dr William Mgimwa kijadiliwe in public.

Hata hivyo Mnyika akamjibu kuwa unapokuwa National figure, na inapotokea kifo ambacho kina utata, inakuwa siyo suala la familia kuamua kifo hicho kijadiliwe au laa, bali itakapoenekana kuna ulazima wa kujadili kifo hicho kwa public interest, linakuwa lishatoka kwenye maamuzi ya kifamilia.

Mfano mmojawapo ni wakati Waziri mkuu wa zamani, Edward Sokoine, alipokufa kwa ajali ya gari yenye utata huko Morogoro, suala hilo halikuachiwa familia ndiyo iamue kama inataka kifo hicho kichunguzwe au laa, bali serikali ilijitwisha jukumu la kuchunguza kifo hicho, na ndiyo maana yule kijana kutoka Afrika kusini, Dumisani Dube, ambaye gari lake ndilo lililosababisha ajali hiyo, aliburuzwa mahakanani.
 
Ati bomba la gesi na Sukari! Hii nchi wanaitaka nini Ee Mola?Ngoja tusubirie muda ufike,ukweli udhihirike.Viongozi wa nchi hii wako tayari washikiwe mtutu wa bunduki kusema ukweli.HATARI!
 
Huko Bomba la gesi kuna nini mpaka bajeti ipae namna hiyo kutoka Trillioni 1.2 naskia mpaka Trillioni 2.4 mara mbili zaidi ya ile ya mwanzo. Hivi ni kwanini pasiwe na maswali ya kujiuliza hapa ?
 
Back
Top Bottom