Ufisadi Bila Majibu: Rais Kikwete na Lowassa sasa jiuzuluni ndani ya siku 90 kupisha uchunguzi huru

Rais Kikwete, uamuzi wako wa kukata DARAJA LA MAZUNGUMZO NA CHADEMA kwa kusaini 'Muswada wa Makinda' siku moja tu mgongoni mwao toka watoke kwako Ikulu, hapo kweli kuna kulaumiana tena au ndio kusema huna time na CHADEMA juu ya swala hili sio??????
 
UGENI WA 'KRIMU YA UONGOZI THABITI WA CHADEMA' IKULU MAJUZI SASA WAFICHUALIA SIRI VIKUNDI HASIMU MBIO ZA URAIS CCM JUU YA RAIS KIKWETE NA MRITHI WAKE NDANI YA 'KITCHEN CABINET' YAKE BINAFSI MAGOGONI:A S 465:

Ikulu yajitia kitanzini zaidi, ndani na nje ya CCM, kwa ukaidi Rais Kikwete kusaini muswada tata nchini kuwa sheria kwa kuegemea maamuzi binafsi ya BENARD KAMILIUS MEMBE ambaye pia ni kiongozi wa mojawapo vikundi hasimu CCM kwenye kinyang'anyiro cha kumezea mate Ikulu anayeonekana kunyanyuliwa zaidi na familia tatu za Pwani na Visiwani.

Licha ya kile kisichozuilika toka kwa upaande wa CHADEMA, Nguvu ya Umma wa Tanzania na asasi nyingi zisizo za kiserikali KUVURUMUSHA MVUA YA MAWE hivi karibuni kwa kudai nafasi zao stahiki katika mchkato mzima kuundwa kwa katiba mpyaa nchini, vita vya vikundi ndani ya CCM ambavyo tayari vinasoma lama za unafiki naa kujihisi kusalitiwa na mwenyekiti wao Ndg Jakaya Mrisho Kikwete sasa kupanda nyuzijoto za hali ya hewa zaidi ya ile Jangwani.

Kuna hatari zaidi ndani ya CCM kwamba Mapinduzi ya Ki-Chama aliyoyaahirisha Mzee Mkapa yakarudi kwa nguvu mithili ya mlipuko wa bomu la nyuklia kule Hiroshima Japan na kusababisha sura mpya ya milima na mabonde kubwa zaidi ndani ya Chama hicho kama ambavyo haikuwahi kufahamika katika historia ya uhai wake wote.

Kule kutiliwa kwa sahihi kwa mapendekezo ya kundi pekee la Membe amblo ndilo lililopata nafasi hiyo kwenda meza kuu ya maamuzi kwenye 'Kitchen Cabinet' ya Rais Kikwete, na pengine sura zingine chache za wale wanaompigia chapuo mjumbe mwingine dhaifu lakini anayeonekana kama kiraka au mchezaji wa dharura (Asha-Rose Migiro) kama mbavyo familia hizo tatu za Pwani na Visiwani vinavyojiaminisha.

Hadi hivi sasa, kuna hatari kubwa ya NDOA TATA ZISIZOTARAJIWA kufungwa ndani na au nje ya CCM kukabili huu mradi wa siri wa serikali ya Kikwete - Project Kamelius Membe / Asha-Rose Migiro endapo 'mwanetu' hatokubalika.

Wakati nikiwaahidi kuja na uchambuzi wa kina zaidi juu ya hili kosa LILILOLENGWA KULIKOMOA CHADEMA NA WANANCHI KWA UJUMLA wetu na kuishia kumuumbua mkuu wa kaya kwa kufichua siri yake ya moyoni, vile vile itakumbukwa kwamba Waziri Membe wala si Waziri wa Mambo ya Sheria na Katiba kupewa nafasi kubwa kiasi hicho kwenye meza haramu ya maamuzi Magogoni ambayo hivi sasa yaonekana watu kuikimbia kutokujitambulisha nayo kwa kwa sababu za uwekezaji wa kisiasa baada ya kiongozi huyo kwenda nyumbani.

Ndio, Membe wala si mhusika wa mambo ya Ndani, ofisi ya mwanasheria mkuu, Msajili wa vyama wala kuwa mwakilishi rasmi wa ofisi ya bunge. Achilia mbali kwanza moto mkubwa wa udhalilishaji naa usaliti wa Benchi la Kikwete kwa mazungumzo kati yake na viongozi wa CHADEMA Taifa, waunda mikakati ndani ya vikundi hasimu mbalimbali ndali ya CCM; HABARI NDIO hiyo huku nikiendelea kuwaahidi vya uvunguni zaidi baadaye kidogo.
 
UONGOZI WA JUU UNVYOTESWA NA USALITI MKUBWA MIONGONI MWA VIKUNDI HASIMU NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI

Kwa jinsi ambavyo uongozi wetu wa juu ki-taifa ilivyochangnyikiwa kufutia madai megi sana kila kona ya nchi tangu uchaguzi wa mwaka 2010 umalizike bila ya wananchi kuridhishwa nayo, siasa za Magogoni hadi hivi sasa kwao
kila kitu ni sawa na KUCHEZA KAMARI.

Yaani mambo hivi sasa ni kwamba Ikulu yetu ni wazi ime-panic kupita maelezo na sasa kuonekana wazi wakijaribisha mikono katika kila kitu na kuendelea kutekeleza kila wazo linalopita, hivyo kwa misingi ya hali hiyo hatarishi sana kwa mustakabali mzima wa taifa letu - kuna ka-mwanya kanakolilia kuzibwa na mtu yeyote
OPPORTUNIST ambaye atakua amekiona na yuko tayari kuchangamkia tenda hiyo reja reja.
 
Baada ya chenga nyingi za siasa ya makundi ndani ya CCM Rais Kikwete sasa aishia kujifunga golini kwake mwenyewe.
 
KATIBA MPYA 'INAYOWAFAA' WATANZANIA TAYARI ANAYO MFUKONI RAIS KIKWETE PAMOJA NA KUNDI LA KAMELIUS MEMBE

CHADEMA na asasi za kiraia mkifanya masihara na hili, kuna kila dalili kwa Rais Kikwete anacho mfukoni mwake kile anakionelea kuwa ndicha KATIBA MPYA itakayotufaa nchini Tanzania.

Ni swala la kuwatafuta maaskofu wawili hivi, Zitto Kabwe wawili hivi na yule aliyekua kiongozi wa upinzani bungeni CUF kupitisha hayo maoni binafsi - bure kabisa, hamna kitu mle!!!

Naam, huo ndio ukweli wa mambo kwamba katiba mpya tayari Rais Kikwete anayo mfukoni kwa msaada na faida ya kundi la Benard Kamilius Membe kati ya vikundi mbalimbali vinavyowania urais ndani ya chama hicho.

Kuna kila dalili Tanzania kupata Katiba Mpya za aina mbili tofauti ndani ya miaka 10 toka sasa; Katiba Mpya ya kwanza huenda ikaingizwa na jeshi na lingine baadaye kidogo likaandikwa na wananchi kwa kujinafasi huku wakimtupia nje Kikwete hilo la kwake akaufungie vitumbua.
 
Kumbe mheshimiwa Kigoda hakubinafsisha tu mashirika yetu, hata nayo CCM huenda kilibinafsishwa bila ya wanachama kujua only to wake up to a rude shock of the reality.

Kati ya CHADEMA na CCM Membe ambayo ndio kumbe mwenye katiba mifukoni kusubiri kushushwa kwa Wa-Tanzania wakati wowote, ni kundi gani ambalo lina OPTIONS nyingi zaidi kuliko nyingine?
 
Kama ambavyo tunatakiwa tusikubali kupata tena na tena Rais wa nchi kupitia tu kwenye mimbo ya makundi binafsi kama vile 'Kikundi cha Wanamtandao' vile vile vile kwa njia kama hiyo wala watu tusikubaliane na Katiba Mpya binafsi inayotarajiwa kuanguka chini kama manemane toka kwenye mifuko yabaadhi ya viongozi wa ngazi za juu kwenda kwa Wa-Tanzania.
 
RAIS KIKWETE ASHINDWA KULEA MWANA 'IMANI':canada: NDANI YA MASAA 24 TU MIKIKI YA ZAIDI YA MIAKA 20 KUTAFUTA UUNDWAJI WA KATIBA YA WANANCHI ATAIWEZA?

IMANI:canada: ni kila kitu katika mahusiano na mawasiliano ya aina yoyote ile kufanikiwa duniani. Lakini pindi neno hilo dogo tu IMANI inapotoweka nafasi yake siku zote huchukuliwa na MASHAKA:shetani:.

Mashaka pindi yanapopata uenyeji kati ya ndugu wa damu, huko sasa magugu huanza kouta, mawasiliano kufa, haki na uwazi kuzikwa chini ya bahari na majungu kuanza kujaza nafasi zilizoachwa wazi na mwisho jamii moja kuishi kwa utengano na wakati mwingine ha kitu uadui usioluhishika maishani hutokea.

Katika mazungumzo kati ya uongozi wa juu CHADEMA
:behindsofa: na Taasisi ya Urais:couch2: nchini, kitu mazungumzo ya mara kwa mara na mawasiliano ya karibu kati ya vyombo hivyo vyeti viwili vilitiliwa mkazo na kiongozi wa taasisi ya urais nchini Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa WINO MZITO MWEKUNDU.

Hakika hii ilikua ina maana ya kuashiria faraja yake kwa moyo huo wa ki-ndugu unaozingatia zaidi utamaduni wetu wa Ki-Tanzania kupenda amani.

Ajabu kubwa tu hadi dakika hii ni kwamba hata kabla ya ule wino mwekundu alioutumia Rais Kikwete kwa kutilia mkazo na udhabiti wake wa kutokuingiza uitikadi katika masuala ya kitaifa kama vile Katiba Mpya, kuna ripoti sehemu mbali mbali nchini zikinakili taarifa kwamba TAYAARI TAASISI HIYO YA URAIS nchini imeshakwenda kinyume na makubaliano yale hata kabla ya masaa 24 kwisha.

Sasa hadi hapo tunauliza, kwa kuwa nguzo mojawapo imara ya kutunza kitu IMANI ndio kama hivo tayari imeng'olewa na rais mwenyewe kwa mikono yake (pengine kwa ushauri wa Membe) na kuutupa baharini, je huko mbele ya safari wazee wetu waheshimiwa sana tuliobaki nao kama vile Mzee Salim Ahmed Salim, John Samwel Malecela, Joseph Butiku, Mama Maria Nyerere, Edwin Mtei, Mark Bomani, Getrude Mongela, na Bob Makani watakua na la kutulaumu tena?

Maana sasa kilichobaki ni KUTOKUSHIRIKI zoezi zima huku tukishughulikia jambo hili kwa nguvu zote kule Mahakama ya Wananchi wa Tanzania.

Hapa chini ni sehemu ndogo tu ya matokeo ya taswira mbaya iliotufikisha CHADEMA kuweka gea nyingine kabisa katika safari hii ndefu ambayo kamwe HATUTOKAA TUPUMZIKE mpaka kunakopatikana malengo kwa njia zote zinazoruhusiwa kikatiba nchini.

Tanzania ni kubwa na mashuhuri kuliko taasisi tu ya urais; utaifa mbeeeele kama tai mpaka kupata mchakato unaomweka mwananchi mahala pake shahiki KUJIUNDIA KATIBA MPYA akiwa ameshika ushukani mwenyewe!!!!
 
Chadema: Rais ametuuza
Wednesday, 30 November 2011 21:31

chadema-mnyika.jpg


Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Makao Makuu ya Chama hicho jijini Dar es Salaam, jana. Picha na Michael Jamson

YASUSIA MCHAKATO WA KATIBA ALIOSAINI JK, CUF NAO WAALIKWA IKULU

Patricia Kimelemeta

CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kuwa kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011, kimekiuka makubaliano yao, hivyo kimeamua kususia mchakato mzima wa kuratibu maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya kwa kutumia sheria hiyo.Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa hatua hiyo imefikiwa ili kuonyesha kutoridhishwa na namna kiongozi huyo wa nchi, alivyowachezea akili. "Kitendo cha Rais Kikwete kuusaini muswada huo bila ya kuupitia ni kinyume na makubaliano, jambo ambalo linatufanya tususie mchakato mzima wa kuuratibu maoni ya kwa ajili ya Katiba Mpya kupitia sheria ailiyoisaini,"alisema Mnyika na kuendelea:
"Tumeamua kujitoa kwenye mchakato mzima wa kuratibu Marekebisho ya Muswada wa Sheria ya Katiba kutokana na Rais kukiuka makubaliano yetu Ikulu yaliyomtaka aupitie kwanza kabla ya kuusaini." Mnyika aliendelea kueleza kuwa Chadema iliwasilisha waraka wa mapendekezo sita kwa Rais ikiwa ni pamoja na kumtaka asiusaini muswada huo kutokana na wananchi kutoshirikishwa ipasavyo kwenye mchakato wa ukusanyaji wa maoni.

Alisema mapendekezo mengine ni uundaji wa tume huru, upatikanaji wa uwakilishi kutoka pande zote mbili za Muungano; Zanzibar na Bara ili kutoa fursa ya kupata maoni yao katika marekebisho hayo. "Suala la tatu ni uundaji wa Bunge la Katiba na kupunguza mamlaka ya Rais na jambo la nne ni nafasi ya Zanzibar katika Muungano pamoja na mfumo mzima wa uwakilishi wa pamoja katika muundo wa Bunge la Katiba."
Mnyika alisema kutokana na hali hiyo iliyojitokeza ya Rais kutowasikiliza, watawasilisha waraka huo waliompa, kwa wananchi ili nao wausome na kutoa maoni yao.

Alisema katika kutekeleza mkakati huo, hawatafanya maandamano yeyote, isipokuwa watatoa elimu sahihi kwa wananchi juu ya Katiba wanayopaswa kuwa nayo.

"Nia yetu ni mzuri, lengo ni kuboresha upatikanaji wa Katiba iwe bora na itakayoweza kutoa nafasi ya ushiriki wa pande zote. Lakini kinachofanyika sasa ni kinyume. Tumeamua kuwarudishia wananchi wenyewe ili waweze kuamua kama tumekosea au la,"alieleza. Tamko hilo la Chadema limekuja siku moja baada ya Rais Kikwete kutia saini muswada huo hivyo kuufanya kuwa sheria.

Rais Kikwete alitia saini muswada huo ikiwa ni siku moja baada ya yeye na viongozi wa Chadema wakiongozwa na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe kukubaliana kwamba ipo haja ya kuendelea kuuboresha muswada ili ukidhi mahitaji ya kuaminiana na muafaka wa kitaifa. Pia, walikubaliana yawepo mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Serikali na wadau mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la kudumisha muafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa Katiba Mpya.

CUF nao wakubaliwa kukutana JK

Katika hatua nyingine, Chama Cha Wananchi (CUF) kimeomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili kujadili Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya Mwaka 2011, iliyotiwa saini juzi na mkuu huyo wa nchi. Taarifa ya Ikulu iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari ilieleza kuwa baada ya kupata ombi hilo, Rais Kikwete alikubali kukutana nao.

"Ofisi ya Rais, Ikulu, imepokea barua kutoka CUF kikiomba kukutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete," ilisema sehemu ya taarifa hiyo na kuongeza: " Rais amekubali ombi hilo la CUF na ameelekeza maandalizi ya mkutano huo yafanyike mara moja."

Wasomi, wanaharakati wapinga
Wakati huo huo, wasomi, wanaharakati na wanasiasa wametoa maoni tofauti kuhusu hatua ya Rais Kikwete kusaini sheria hiyo, huku Jukwaa la Katiba likieleza kuwa litafanya maandamano nchi nzima, kupinga hatua hiyo.

Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Deus Kibamba aliliambia Mwananchi jana kuwa hatua hiyo ya Rais, ni sawa na ‘maombolezo kwa taifa'."Wananchi hawana uwezo wa kwenda Ikulu kuzungumza na Rais, uwezo wao ni kufanya maandamano ya amani yasiyo na ukomo nchi nzima,"alisema Kibamba anayeongoza Jukwaa hilo lenye Asasi za Kiraia zaidi ya 180.

"Serikali hii siyo sikivu, inaandaa Katiba kwa maslahi yake. Sisi tunatoa juma moja kwa polisi kukubali madai yetu ya kufanya maandamano vinginevyo uvumilivu basi,"alisema Kibamba.

Alisema kitendo cha Rais Kikwete kusaini muswada huo muda mfupi baada ya kufanya mazungumzo na Chadema ni dharau kwa chama hicho na wananchi.

Bana asema Rais ametimiza wajibu

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Benson Bana alisema Rais ametimiza wajibu wake katika kusaini muswada huo kuwa sheria. Alisema kabla ya wananchi kuanza kulaumu, wanatakiwa kusubiri kwanza Rais aunde tume hiyo ndipo watoe maoni yao.

" Duniani kote Katiba haiwezi kutosheleza mahitaji ya kila mtu, ni lazima pande fulani zitailalamikia hata kama itakuwa inafaa kwa asilimia kubwa,"alisema Dk Bana.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alisema chama hicho kinasubiri kuiona Tume ya Katiba itakayoundwa na Rais. "Tunaunga mkono Rais kusaini muswada huo, tunachosubiri ni kuiona tume hiyo ikikusanya maoni ya wananchi, wakichakachua maoni ndipo tutakapoingilia kati,"alisema Mtatiro.
 
Kwa kawaida mtu mzima akikupa kauli yake tena kwa maandishi ustaarabu tu wa kawaida unatuambia, huna sababu ya kuwa na wasiwsi.

Lakini hili la kuruka kauli yako mwenyewe ndani ya masaa 24 tu ni rekodi ya aina yake kwa Rais Kikwete. Hivyo swali sahihi ni watu kujiuliza tu kwamba je Rais Kikwete, unatupeleka wapi kama taifa juu ya swala zima la katiba?

Na pale tunapogeuka kumuuliza tena mjeruhiwa swali kama hili basi hapo ndipo mnaposikia watu kuitwa wanafiki tena wazandiki wakubwa.

Kuna kila dalili kwamba Rais Kikwete 'Katiba Mpya tena inayotufaa Wa-Tanzania' tayari anayo mfukoni ni kiasi tu cha kufanya geresha la hapa na pale ili akauchomoe na kuuweka mezani jinsi atakavyopendezendezewa mwenyewe.

Si kweli kwamba ukiwa ni rais sasa ufanye kila kitu jinsi upendavyo tu mwenyewe; kuna mipaka ya ki-katiba!!
 
CHADEMA, ni haki ya ki-katiba kwa chama kukutana wakati wowote na kwa namna yoyote kitakachopendezewa nacho, twendeni kwa wananchi na tuanze kazi mara moja!

Juhudi zetu za kiistaarabu na za kimaelewano ndio kama hivo tumepigwa nayo usoni huku wachache wakishangilia juu ya hilo bila kujua kwamba umma unafikiri nini.
 
Mbinu kali walioitumia uongozi wa juu kabisa CHADEMA kwa kweli umekua na impact kubwa ajabu. Mbinu hiyo ulifanya kuwapumbaza Kitchen Cabinet ya kule Magogoni na hasa ule mkondo wa CCM Membe wakachanganye Simba CHADEMA kuwa ni paka.

Hivi kweli mkiona kirimu ile ya ujumbe ulioenda Magogoni ikiwa ni pamoja na Ma-Prof wawili wanaoheshimika sana kimataifa katika fani zao kweli nyinyi wenzetu akina Dr Mashilila bado mnaendeleza mbio za panya sakafuni tu!!!!!!!!!

Ile yote ilikua ni pre-emptive tactic kupima HOW GENUINE the Magogoni house is on thi Katiba processes; ndio kama hivo mmeanguka huo mtihani pwaaa!!! Lile jopo halikuenda pale kunywa kahawa, kuangalia sanamu wala kununua samaki ferry.

NEC CHADEMA, sasa ijadilini hiyo repoti ya ujumbe wa Mwenyekiti Mhe Mbowe kisha mkaitolee maamuzi huku na nyinyi wenzetu BAVICHA tukaitishe mkutano wa dharura kutathmini mwelekeo mara baada ya ujumbe wetu Magogoni kutemewa mate usoni.

Pamoja na yote hayo, CHADEMA THINK-TANK, sasa hata swala la kupanua zaidi ushirikiano na 'NEW WATERS AFAR AND LIKE-MINDED FRIENDS FROM CCM FACTIONS' nayo pia inafikirika tangu sasa
.

Ushauri mwingine ni vichekesho kweli. Hivi mtu anategemea kuwa JK atamsikiliza na kujiuzulu.
 
Ubinafsi wa viongozi na kujaribu kujihodhisha mchakato ya kuunda katiba mpya, hilo ni tatizo tena kubwa sasa.
 
ONYO KWA NGUVU YA UMMA NCHINI: TOENI ULINZI MKALI KWA VIONGOZI HAWA KESI YA KATIBA SASA INAPOHAMIA KWENYE MAHAKAMA YENU

Wananchi popote pale mlipo, TOENI ULINZI KWA VIONGOZI WA CHADEMA wa ngazi zote.

Na zaidi sana toeni ULINZI MARADUFU kwa uongozi wetu wa juu kabisa ki-Taifa bila kusaha Waheshimiwa Tundu Lissu, John Mnyika, Godbless Lema na Uongozi wa BAVICHA. Na uongozi wa juu CDM hata hapo juu jicho moja linaposinzia la pili liwe linaona.

Nao baadhi ya viongozi wa vikundi hasimu ndani ya CCM ONYO kama hilo hapo juu liwatupie jicho sana tu. And that's a FACT in the pipeline anyway!!
 
'Katiba Mpya' inayoletwa kwa nguvu ya mtutu kamwe haiwezi ikadumu na jamii yetu ya Tanzania.
 
Kichekesho:
Fungu la maneno ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kamati ndogo ya
CHADEMA iliomtembelea ikulu Magogoni mapema wiki hii: "Hata mimi naona mnazo hoja za msingi, tatizo nisipo saini wenzangu katika chama (CCM) hawatanielewa," Rais Jakaya Kikwete.

Source: TUNDU LISSU facebook page

Na ni tangu kwenye tuta hili hapa ndipo Rais Kikwete alipoanza kukosa UHALALI WA KISIASA, hata ukiachilia mbali yeye kukosa uhalali wa Ki-Katiba, kusimamia na kuratibu yeye binafsi Uundwaji wa Katiba Mpya yenye MASLAHI SAWA isioegemea kwenye ITIKADI ZA KICHAMA.

Hakika tangia hapo watu wenye busara ndani ya nchi hii hadi sasa watakubaliana na CHADEMA, Asasi za Kirais zaidi ya 180 pamoja na wanaharakati mbalimbali kwamba kiongozi huyu hawezi kuachiwa zoezi lenye maslahi kwa taifa zima akalisimamie kwa kujivalia mawani ya kudumu ya CCM kihivi.
 
Project Membe is bound to fail flat on its nose if Tanzanians ever come to relise that it is the reason why we are now being closed off the Popular Constitutional making processes. Katiba za kuchomolewa mifukoni na kuwekwa ghafla mezani, hapana!!!
 
RAIS WA TANZANIA AJAE SAFARI HII ATAPATIKANA KWA KIGEZO KIKUU CHA MWENENDO WAKE MZIMA KATIKA HISTORIA IKIPITISHWA KWENYE TANURI LA UTETEZI WA DHATI WA 'UBINADAMU, HAKI NA UTU WA MTANZANIA', KWISHA MANENO!!

Nana kakudanganya kwamba urais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania mara hii utaamuliwa na vijifamilia viwili vitatu hivi kama vile ni ma ya urithi mbele ya kikao cha wana-ukoo!! Aggghhhhhhhhhhhrrrrrr, kemea mbali fikra hizo za kipuuzi.

Safari hii ni KINYANGANYIRO HASA miti yote kuteleza na bila mtu yeyote kuvuta pumsi nyuma ya kivuli cha mwingine. Awamu hii ni awamu ya kumpata mtu bora kuwa rais KWA RIDHAA NA BARAKA ZOTE ZA WAVUJA JASHO moja kwa moja bila udalali na huku akitumia nyo katiba bora ya wananchi na wala si bora katiba ya Project Membe kule Magogoni!!

Naam, pindi niandikapo humu wengine wengi wanachukulia mzaha na utani mtupu wakati kule tayari watu wanatetemeka homa ya matumbo hata kabla sijamaliza fungu la kwanza la maneno yangu ...

Hali hii inatokana na ukweli kwamba wengi wetu pua zote zimeziba kabisa kiasi kwmba hata harufu ya petroli wala hipenyi kitu. Sasa kwa kuwa kumbe wengi hatuelewani humu, basi bora lugha ikachukua gea kubwa zaidi ya kupandia milima mithili ya Sekenke wakati wa mvua na barabara nayo changarawe.

Ndio, naona maelewano sasa ni bora kwenda kwa baadhi tu ya mi-kada; pengine ni wale wadadisi wa mambo ya siasa na hasa wana mikakakiti mipango wenye kuegemea kutetea UBINADAMU, HAKI NA UTU WA MTANZANIA leo na kesho bila kutetereka ama gizni au kwenye mwanga wa mchana.

Ngoja kwanza niende msalani nitarudi baadaye kidogo.
 
KATIKA SIASA HIZI ZA USHINDANI CHINI YA MFUMO WA VYAMA VINGI UNAOFANYA KAZI KIUKWELI, KOSA MOJA LA KIUFUNDI TAFSIRI YAKE MAGOLI MENGI MNO GOLINI KWAKO - CHADEMA WANAZO OPTIONS NYINGI SI KIFANI HAPA UWANJANI HADI SADA

Ushirikiano mpya kisiasa nchini sasa kuegemea mkondo wa kufuata kanuni za kumtafuta
A LESSER DEVIL OUT OF A BIG FOREST OF THE ili kufanya kazi nayo.

Chanzo cha watu sasa kujipanga upya kumkabili 'adui' mmoja wa kisiasa aliyefungwa mbeleko ya chuma na Rais Kikwete mgongoni hivi sasa ni kutokana na ile
GRAVE POLITICAL TACTICAL BLUNDER OF THE YEAR iliofanyika Magogoni mapema wiki hii. Kisiasa hiyo ni OPEN / BLUNK CHEQUE YA MTU YEYOTE KUJIAMULIA AANDIKA TARAKIMU GANI kabla ya kwenda benki (kwa wananchi) kujichotea fedha tani yake na kw wakati anaoona unafaa zaidi.

Kwa wale wanaoelewa mambo kiundani na kwa haraka sana, lengo la CHADEMA ilikua ni kumpunguzia Mkuu wa Kaya kile kinachoitwa KICHWA KUUMA lakini yeye akatafsiri kwamba
NI HAPA HAPA NIMEWAPATA NA KWAMBA WALA SIFANYI MAKOSA - matokeo yake ni makosa juu ya makosa.

A litle more of a dose of the Concept of 'Coperation with a Lesser Devil of them all' CAN DO after all, internal resistance to the idea notwithstanding!!.
 
Back
Top Bottom