tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,803
- 18,227
Watanzania tumerogwa; yaani tunafurahia matokeo feki huku elimu yetu ikizidi kushuka kila mwaka. Aliyeturoga kafa. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya matokeo ya darasa la nne (SFNA), kidato cha pili (FTNA) na kidato cha nne (CSEE) kutolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) hivi karibuni na kuonyesha kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia mbili (2%) ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2020.
Baada ya kufuatilia namna mitihani inavyotungwa na kusahihishwa kwa muda mrefu nimegundua kadri miaka inavyokwenda mbele mitihani inazidi kurahisishwa ili wanafunzi wengi zaidi wafaulu. Hii ni sera ya serikali kuongeza ufaulu kwa wanafunzi kila mwaka ili wapate cha kusema mbele za wazazi (wapiga kura) kila baada ya miaka 5 ya uchaguzi.
Nikianzia kwenye suala la utunzi wa mitihani, siku hizi mitihani inatungwa kwa urahisi sana na kwa njia ya ajabu. Tangu serikali ilipoanzisha mitihani ya kubashiri (kubet) wanafunzi wengi wasiojua kusoma wala kuandika hufaulu kujiunga na shule za sekondari na wanaendelea hivyo hivyo hadi kidato cha nne.
Wanafunzi hawa wakifika kidato cha nne, serikali tena hutunga mitihani rahisi ili wengi wao wafaulu kujiunga kiadato cha tano kwa ubwete. Utafiti wangu umeonesha kwamba kadri miaka inayoenda mbele mitihani ya kitaifa kwa ngazi zote imekuwa ikirahisishwa kwa makusudi ili kuwafaulisha wanafunzi kisiasa. Tazama mtihani wa Biology wa NECTA 1996 ulinganishe na mtihani wa NECTA 2017 utapata jibu mwenyewe. Zamani kupata divisheni wani halikuwa jambo la mchezo. Lakini kwa maswali mchekea kama haya (2017) hata mkulima ambaye hakwenda shule hakosi kupata divisheni wani!
NECTA 1996
NECTA 2017
Hali ni hiyo hiyo hadi kwenye mitihani ya kidato cha sita (ACSSE) ambapo wanafunzi vilaza hupenya hadi kuingia vyuo vikuu. Na huko vyuo vikuu, mchezo ni uleule…..kazi inaendelea. Tazama mtihani wa uliotungwa kwa wanafunzi wa mwaka wa pili kutoka chuo kikuu kimoja hapa nchini Tanzania. Hali inatisha kwa kweli.
Mtihani gani wa kijinga kama huu? Unampima nini mwanafunzi wa chuo kikuu kwa mtihani wa kizembe kama huu? Tuache masikhara jamani; huu mtihani hata ukimtungia mwanafunzi wa darasa la nne atapasua pasi na shaka. Sasa iweje wanafunzi wa chuo kikuu tunaowategemea kuja kulitumikia taifa baada ya kuhitimu watungiwe mtihani wa ovyo kama huu? Inasikitisha sana, ten asana.
Jambo jengine ambalo serikali imeamua kulifanya kwa makusudi ni kuondoa penalty kwa wanafunzi wanaofeli hesabu (Mathematics) tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma. Pia somo la Bible Knowledge siku hizi linajumlishwa kwenye ufaulu ili kuwaboost wanafunzi wengi zaidi wapate divisheni wani za magumashi kisiasa. Tazama kielelezo kifuatacho:
Ndugu wadau wa elimu, sio mimi tu ninayelalamikia uchakachuaji wa elimu hapa nchini. Kila mtu ni shahidi juu ya uhuni unaoendelea katika kudidimiza kiwango cha elimu na kuwafanya watanzania wavivu wa kufikiri ili watawalike kirahisi. WanaJF wengine pia wamewahi kuguswa na jambo hili na kuliongelea kwenye nyuzi zifuatazo:
Wahadhiri vilaza huzalisha wasomi vilaza
Kwanini wahadhiri hawapelekwi tena kusoma 'postgraduate degrees' kwenye vyuo vyenye hadhi kubwa duniani kama ilivyokuwa zamani?
Nini kifanyike?
Nchi hii imefika mahali pabaya sana kielimu na endapo mchezo huu utaendelea, elimu ya nchi hii itaingia kaburini. Kumbuka kama tutakaa kimya, sisi na kizazi chetu chote tutaangamia pamwe! Je, nini kifanyike kurejesha elimu yetu kwenye reli? Karibu tujadiliane.
Baada ya kufuatilia namna mitihani inavyotungwa na kusahihishwa kwa muda mrefu nimegundua kadri miaka inavyokwenda mbele mitihani inazidi kurahisishwa ili wanafunzi wengi zaidi wafaulu. Hii ni sera ya serikali kuongeza ufaulu kwa wanafunzi kila mwaka ili wapate cha kusema mbele za wazazi (wapiga kura) kila baada ya miaka 5 ya uchaguzi.
Nikianzia kwenye suala la utunzi wa mitihani, siku hizi mitihani inatungwa kwa urahisi sana na kwa njia ya ajabu. Tangu serikali ilipoanzisha mitihani ya kubashiri (kubet) wanafunzi wengi wasiojua kusoma wala kuandika hufaulu kujiunga na shule za sekondari na wanaendelea hivyo hivyo hadi kidato cha nne.
Wanafunzi hawa wakifika kidato cha nne, serikali tena hutunga mitihani rahisi ili wengi wao wafaulu kujiunga kiadato cha tano kwa ubwete. Utafiti wangu umeonesha kwamba kadri miaka inayoenda mbele mitihani ya kitaifa kwa ngazi zote imekuwa ikirahisishwa kwa makusudi ili kuwafaulisha wanafunzi kisiasa. Tazama mtihani wa Biology wa NECTA 1996 ulinganishe na mtihani wa NECTA 2017 utapata jibu mwenyewe. Zamani kupata divisheni wani halikuwa jambo la mchezo. Lakini kwa maswali mchekea kama haya (2017) hata mkulima ambaye hakwenda shule hakosi kupata divisheni wani!
NECTA 1996
NECTA 2017
Hali ni hiyo hiyo hadi kwenye mitihani ya kidato cha sita (ACSSE) ambapo wanafunzi vilaza hupenya hadi kuingia vyuo vikuu. Na huko vyuo vikuu, mchezo ni uleule…..kazi inaendelea. Tazama mtihani wa uliotungwa kwa wanafunzi wa mwaka wa pili kutoka chuo kikuu kimoja hapa nchini Tanzania. Hali inatisha kwa kweli.
Mtihani gani wa kijinga kama huu? Unampima nini mwanafunzi wa chuo kikuu kwa mtihani wa kizembe kama huu? Tuache masikhara jamani; huu mtihani hata ukimtungia mwanafunzi wa darasa la nne atapasua pasi na shaka. Sasa iweje wanafunzi wa chuo kikuu tunaowategemea kuja kulitumikia taifa baada ya kuhitimu watungiwe mtihani wa ovyo kama huu? Inasikitisha sana, ten asana.
Jambo jengine ambalo serikali imeamua kulifanya kwa makusudi ni kuondoa penalty kwa wanafunzi wanaofeli hesabu (Mathematics) tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma. Pia somo la Bible Knowledge siku hizi linajumlishwa kwenye ufaulu ili kuwaboost wanafunzi wengi zaidi wapate divisheni wani za magumashi kisiasa. Tazama kielelezo kifuatacho:
Ndugu wadau wa elimu, sio mimi tu ninayelalamikia uchakachuaji wa elimu hapa nchini. Kila mtu ni shahidi juu ya uhuni unaoendelea katika kudidimiza kiwango cha elimu na kuwafanya watanzania wavivu wa kufikiri ili watawalike kirahisi. WanaJF wengine pia wamewahi kuguswa na jambo hili na kuliongelea kwenye nyuzi zifuatazo:
Wahadhiri vilaza huzalisha wasomi vilaza
Kwanini wahadhiri hawapelekwi tena kusoma 'postgraduate degrees' kwenye vyuo vyenye hadhi kubwa duniani kama ilivyokuwa zamani?
Nimeshangazwa na Matokeo ya Kidato cha Nne 2021
Wasalamu Wakuu Leo Baraza la Mitihani Tanzania Bara, Limetangaza matokeo ya Kidato cha Nne Na Kuonesha Ufaulu ukiongezela kwa Asilimia Chini ya 2%. Well And Good. Lakini Baada ya Kufuatilia Matokeo Ya Shule Nyingi Nimeona Division 1 zikiwa Nyingi sana na Division 4 zikipungua Sanaa. Hii...
www.jamiiforums.com
Nini kifanyike?
Nchi hii imefika mahali pabaya sana kielimu na endapo mchezo huu utaendelea, elimu ya nchi hii itaingia kaburini. Kumbuka kama tutakaa kimya, sisi na kizazi chetu chote tutaangamia pamwe! Je, nini kifanyike kurejesha elimu yetu kwenye reli? Karibu tujadiliane.