Ufaransa: Kwanini walinzi wa Rais Samia wanavaa Barakoa ya Zanzibar kwenye ziara ya Tanzania?

Si kweli, fungua katiba ya Zanzibar, Sura ya kwanza ibara ya 2. '' Zanzibar ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania''
Haya ni maneno ya Katiba ya Zanzibar 1984 toleo 2010.
Nchi moja ni Zanzibar , nikuulize ya pili ni ipi ikiwa Tanganyika ilishakufa mtaani?

Hoja hii ni nzuri sana. Wakati wa Mwalimu suala la G55 lilikuwa wazi na liliongelewa kwa uwazi.
Mwalimu alisema ''
Sera za CCM ni serikali 2, wanaotaka sera tofauti waondoke ndani ya chama kwanza ili wakazungumzie huko'' Hapa maana yake hakukataa hoja, alisema kuwa hoja iliyopo ni kinyume cha sera wanayo inadi. Mwalimu alikuwa na nguvu za hoja

Kumbuka kabla ya hapo kulikuwa na hoja ya Watanganyika kwenda Zanzibar kwa Passport. Tanganyika ikasema ikiwa ni hivyo, Wazanzibar waje na Passport. Mwalimu Nyerere aliitazama hoja akaona ina mantiki. Mwl akawasiliana na Jumbe na sharti liliondolewa mara moja.
Mwl hakuwalazimisha Wazanzibar bali Wazanzibar waliona hasara !

Ninachokiona sasa hivi ni tofauti kidogo. Hoja 'hoja zinapigwa rungu hazijibiwi'' kumbuka asilimia zaidi ya 80 ni ya kizazi kilichokuta muungano. Hofu iliyopo ni kuwa wajenga hoja kama Mwalimu, na wasikiliza hoja kama Mzee Warioba hawapo tena. Sasa tuna ''wasifiaji na wakujipendekeza''
Hoja ya anganyika inafukuta na siku Watanganyika wakisema enough is enough hakuna wa kuwazuia. Wao ndio wenye muungano kwa hali na mali. Kuna mahali nimesema, kwa jinsi nionavyo, na ninaweza kuwa wrong! muungano uki survive miaka 5 utadumu miaka 50. Trust me!

Hakuna tatizo la Zanzibar kustawi! kuna tatizo la ustawi wao kupatikana kwa gharama za Mtanganyika na hapo ndipo mjadala ulipo. Zanzibar waende kukopa Trilioni 100 hakuna shida, lakini wakikopa bilioni 280 na kumtupia Mtanganyika mzigo kuna tatizo.
Zanzibr hata wakiuza visiwa hata Ikulu hakuna tatizo, lakini uuzaji wao usibebeshe mzigo Mtanganyika kwa njia yoyote ile.

Katiba ya Zanzibar sura ya kwanza ibara ya 2 na katiba hiyo hiyo imetaja muungano mara 36.
Tueleze wanaJF, ni sheria ipi na ya mwaka gani imetamka kuwa ''Tanganyika imekufa?''
Lakini pia katiba ya mpito ya 1964 ilisema '' ...mambo yote ya Tanganyika yatakuwa ya JMT'' in other word Tanganyika is subsumed by URT. Since

Ndicho tunataka! Wajitegemee bila kumpa Mtanganyika gharama. Kwasasa Zanzibar inachukua sehemu kubwa sana ya bajeti ya JMT kuliko eneo lolote la Tanganyika ikiwa na mchango SIFURI, zero, Nada, Nil katika muungano

Hoja ni kuwa muungano unageuka kuwa mzigo kwa Tanganyika. Kinachotakiwa na uwajibikaji wa Zanzibar katika muungano. Kuhusu chuki hakuna kitu kama hicho bali zipo hoja kama hizi
1. Nini mchango wa Zanzibar katika JMT?
2. Ikiwa Zbar ambaye ni mshiriki wa JMT yupo, Tanganyika yupo wapi na Zbar inajadiliana na nani?
3. Katika JMT, masilahi ya Tanganyika yanalindwaje na kusimamiwa na nani?
3. Tueleze tamko lililoua nchi ya Tanganyika na ni kwa sheria ipi
4. Kero za muungao zimemalizwaje na kwanini imebaki siri kubwa
5. Tume ya Jaji Nyalali, Jaji Kisanga na Jaji Warioba na maoni ya Wananchi zinataka serikali 3, tueleze ni utafiti au tume gani nyingine yenye maoni tofauti na hizo
Hoja zenye nguvu kama hizi watu wanajifanya kama hawazioni na tunajua wanapita humu kimya kimya!! Hoja hizi tano hapo juu zinadai majibu yenye akili!! Hasa hoja namba 3 inauma sana!!
 
Zanzibar ni sehemu ya Tanzania.

Kuna ubaya gani?

Wewe ni maamuma! Point ya mleta mada ni kuwa hakuna taifa Zanzibar, kuna serikali ya Zanzibar. Kukipaswa kuwa na serikali ya Tanganyika. Ikiwa huu ni muungano wa nchi mbili, iko wapi bendera ya Tanganyika?? Kwa kinachoendelea kinachozuiliwa ni bendera na alama za serikali ya Tanganyika!! Tanganyika imefichwa katika jamhuri ya muungano wakati Zanzibar ikiruhusiwa kujitambulisha!!

Anazungumzia jambo la maana sana lakini unaleta mzaha. Hakuna ubaya kwa Serikali ya Zanzibar kutambulika, isiwe vibaya ya Tanganyika kutambulika pia na this has nothing to do with Zanzibar au Tanganyika kuwa sehemu ya Tanzania. This is “identity”!!!
 
Salaam Wakuu,

Nadhani walinzi walitakiwa kuvaa Barakoa zenye bendera ya Tanzania siyo Zanzibar, kwani hii ni ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Siku wakiambatana na Mwinyi ndio wavae hizi barakoa au ni Utalii wa Uchumi wa Bluu?

Picha zimepigwa akiwa Paris, Ufaransa, wakati huo Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa akizungumza na Mkurugenzi wa Kituo cha kuwezesha Wajasiriamali cha Station F Start Up Bi. Roxanne Varza pamoja na Meneja Mawasiliano wa Kituo hicho Bw. Grégoire Martinez kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa Kituoni hapo ikiwemo kutoa fursa kwa wajasiriamali wadogo kupata elimu ya ubunifu wa kibiashara, fursa za mitaji yenye masharti rafiki pamoja na masoko wakati alipotembelea Kituo hicho leo tarehe 12 Februari, 2022, Paris nchini Ufaransa)
View attachment 2117285View attachment 2117286
View attachment 2118155
Mcheza kao hutunzwa. Ndio maisha yetu chini ya jua. Cha muhimu atende haki tu na kukumbuka sisi sote ni wamoja
 
Nadhani walinzi walitakiwa kuvaa Barakoa zenye bendera ya Tanzania siyo Zanzibar, kwani hii ni ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Siku wakiambatana na Mwinyi ndio wavae hizi barakoa au ni Utalii wa Uchumi wa Bluu?
Kuna kila dalili watu watasema bi mkubwa kawashinikiza wenzake wavae hata kama siyo, maana huyu mama anaandamwa sijui kwanini watz tuko hivyo
 
Kuna kila dalili watu watasema bi mkubwa kawashinikiza wenzake wavae hata kama siyo, maana huyu mama anaandamwa sijui kwanini watz tuko hivyo
Hapana! kuna dhana potofu. Washauri wake walitakiwa walione hilo japo ni jambo dogo.
Rais akiwa na msaidizi nyuma yake pia angeweza kuhoji, akakaa kimya

Alikaa kimya kama ilivyokuwa Zbar kwa Rais wa Zbar kukabidhiwa bendera ya Zanzibar.
Na Rais SSH anajua kuwa yeye ni wa JMT hata kama ni Mzanzibar, hivyo uwepo wa alama nje ya za muungano ni tatizo.

Ukishaanza kuushabikia Uzanzibar lazima Utanganyika utarudi tena kwa nguvu.
Nyerere aliita Tanzania visiwani na Tanzania bara.

Kwanini kudai Tanganyika ni ''jinai'' lakini kujitambulisha kwa Uzanzibar ni halali?

Viongozi wa Zanzibar wanachagiza sana hisia, na muda si mrefu watajikuta wanashindwa kutuliza hisia wanazochochea! Ukiwa na identity ya Zabar ya Tanganyika haikwepeki

Nyalali, Kisanga na Warioba pamoja na Wananchi wote wanasema serikali 3 hazikwepeki.
 
Salaam Wakuu,

Nadhani walinzi walitakiwa kuvaa Barakoa zenye bendera ya Tanzania siyo Zanzibar, kwani hii ni ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Siku wakiambatana na Mwinyi ndio wavae hizi barakoa au ni Utalii wa Uchumi wa Bluu?

Picha zimepigwa akiwa Paris, Ufaransa, wakati huo Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa akizungumza na Mkurugenzi wa Kituo cha kuwezesha Wajasiriamali cha Station F Start Up Bi. Roxanne Varza pamoja na Meneja Mawasiliano wa Kituo hicho Bw. Grégoire Martinez kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa Kituoni hapo ikiwemo kutoa fursa kwa wajasiriamali wadogo kupata elimu ya ubunifu wa kibiashara, fursa za mitaji yenye masharti rafiki pamoja na masoko wakati alipotembelea Kituo hicho leo tarehe 12 Februari, 2022, Paris nchini Ufaransa)
View attachment 2117285View attachment 2117286
View attachment 2118155

Mwigulu hajaachana na huu ujinga wa kuvaa tai yenye rangi za bendera kumbe!?
 
He made a very good point
Yes, enzi hizo tulikuwa wamoja. Viongozi wa leo wanaendekeza sana Uzanzibar
Maana yake ni kuwa yale yenye manufaa kwa Zanzibar ni ya Wazanzibar. Mfano, ajira za SMZ, Mafuta na gesi waliyokimbiza baada ya kuambiwa kuna mapipa machache.

Yale wanayotaka kufaidika nayo wao ni Watanzania. Kwa mfano, wakitaka ardhi wanasema ni nchi moja. Wakitaka kupitisha bidhaa kwa uchochoro wanasema ni nchi moja. Wakitaka misaada na mikopo ni nchi moja, lakini madeni ni ya JMT si ya Zanzibar

Hapa ndipo hoja isiyojibiwa inakuja.
Ni yapi ya muungano yaliyoitwa kero? na yalitatuliwaje? Mbona hatuambiwi imekuwa siri?

Tanganyika iliwakilishwa na nani katika kero za Zanzibar na JMT?

Hoja inakuja, Zanzibar inachangia nini katika muungano?
Mbona tuna formula ya kugawana hatujui formula ya kuchangia au kulipa madeni?

Ukizungumzia Uzanzibar wewe ni mtu mwema, ukizungumzia Utanganyika hilo ni kosa.

Serikali 3 ni jibu la matatizo vinginevyo ipo siku atakuja Rais na sera nyingine itakuwa tabu
Wanaotaka serikali tatu ni hawa
1. Wazanzibar kupitia katiba ya 1984 toleo la 2010 sura ya kwanza ibara ya 2.
2. Tume ya Jaji Nyalali
3. Tume ya Jaji Kisanga
4. Tume ya Jaji, VP na PM J.Sinde Warioba
4. Wananchi wa Tanzania kupitia tume ya Warioba
 
Yes, enzi hizo tulikuwa wamoja. Viongozi wa leo wanaendekeza sana Uzanzibar
Maana yake ni kuwa yale yenye manufaa kwa Zanzibar ni ya Wazanzibar. Mfano, ajira za SMZ, Mafuta na gesi waliyokimbiza baada ya kuambiwa kuna mapipa machache.

Yale wanayotaka kufaidika nayo wao ni Watanzania. Kwa mfano, wakitaka ardhi wanasema ni nchi moja. Wakitaka kupitisha bidhaa kwa uchochoro wanasema ni nchi moja. Wakitaka misaada na mikopo ni nchi moja, lakini madeni ni ya JMT si ya Zanzibar

Hapa ndipo hoja isiyojibiwa inakuja.
Ni yapi ya muungano yaliyoitwa kero? na yalitatuliwaje? Mbona hatuambiwi imekuwa siri?

Tanganyika iliwakilishwa na nani katika kero za Zanzibar na JMT?

Hoja inakuja, Zanzibar inachangia nini katika muungano?
Mbona tuna formula ya kugawana hatujui formula ya kuchangia au kulipa madeni?

Ukizungumzia Uzanzibar wewe ni mtu mwema, ukizungumzia Utanganyika hilo ni kosa.

Serikali 3 ni jibu la matatizo vinginevyo ipo siku atakuja Rais na sera nyingine itakuwa tabu
Wanaotaka serikali tatu ni hawa
1. Wazanzibar kupitia katiba ya 1984 toleo la 2010 sura ya kwanza ibara ya 2.
2. Tume ya Jaji Nyalali
3. Tume ya Jaji Kisanga
4. Tume ya Jaji, VP na PM J.Sinde Warioba
4. Wananchi wa Tanzania kupitia tume ya Warioba
"Formula ya guwana ipo lakini hamna formula ya kuchangia."
Kwa mara ya kwanza kero za muungano zinatatuliwa na kufanywa siri.
 
Tanganyika ilianzishwa rasmi kama koloni la Mwingereza mwaka 1922 ikauliwa na mchonga meno mwaka 1964. Ilikuwa ni nchi huru miaka 3 tuu (1961-1964) katika historia yake. Sasa kweli hiyo ndiyo nchi mnayotaka irudishwe? Nchi bandia iliyoundwa na mkoloni? Hata ikirudi wala haiwezi kubaki kama nchi muda mrefu, itasambaratika kikabila na kiukanda.

Nyerere alijua hilo na ndiyo maana alivamia Zanzibar. Zanzibar ndiyo nchi ya kweli na yenye historia kabla ya wakoloni hawajafika hapa. Kabla ya kinyang'anyiro cha bara la Afrika, Zanzibar ilikuwepo kama nchi. Na siku huo mnaouita muungano ukivunjika Zanzibar itarudi kuwa nchi huru.
 
Tanganyika ilianzishwa rasmi kama koloni la Mwingereza mwaka 1922 ikauliwa na mchonga meno mwaka 1964. Ilikuwa ni nchi huru miaka 3 tuu (1961-1964) katika historia yake. Sasa kweli hiyo ndiyo nchi mnayotaka irudishwe? Nchi bandia iliyoundwa na mkoloni? Hata ikirudi wala haiwezi kubaki kama nchi muda mrefu, itasambaratika kikabila na kiukanda.

Nyerere alijua hilo na ndiyo maana alivamia Zanzibar. Zanzibar ndiyo nchi ya kweli na yenye historia kabla ya wakoloni hawajafika hapa. Kabla ya kinyang'anyiro cha bara la Afrika, Zanzibar ilikuwepo kama nchi. Na siku huo mnaouita muungano ukivunjika Zanzibar itarudi kuwa nchi huru.
Msije huku bara wapuuzi nyie
 
Kukosa Washauri...,

Kuna mambo usipoyafanya hupungukiwi lolote na huenda kuyafanya kwako huvunji sheria ila yanapelekea maneno ambayo yanakutoa kwenye reli au kuongeza shutuma siziso na Afya kwa Taifa
Nakubaliana na wewe kabisa. Mimi naamini katika philosophy inayosema "Just because you can do it, doesn't mean that you should".
 
Back
Top Bottom