Ufalme wa Saudi Arabia Upo Ukingoni Kuanguka

Bowie

JF-Expert Member
Sep 17, 2016
4,372
6,078
Baada ya Mfalme Salman bin Abdulaziz kutengeua nafasi ya mrithi wake Crown Prince Mohamed Bin Nayef na kumteua mtoto wake Waziri wa Ulinzi Mohamed bin Salman kuwa mrithi wake kumeleta mtafaruku mkubwa katika familia hiyo ya kifalme toka nchi hiyo iasisiwe mwaka 1932.

Mfalme wa sasa Salman bin Abdulaziz ndio mtawala wa mwisho kutoka watoto wa mwaasisi wa ufalme huo Abdualiziz bin Saud. Kuteuliwa kwa mwana mfalme huyo kuwa mrithi wa kiti cha ufalme imeonekana kama Mapinduzi dhidi ya kurithi ufalme huo kwani wakati Mfalme Salman alipochukua Kiti hicho mwaka 2015 alimteua Prince Mohamed Bin Nayef kuwa mrithi wake.

Mohamed bin Salman mwenye umri wa miaka 31 ni mtu ambaye ameleta utata mkubwa kwenye sera za nje za nchi hiyo kwani mpaka sasa anaendesha vita dhidi ya Yemen na ametishia kuanzisha vita na Iran. Pia anadaiwa ndio muhusika mkuu kwenye mgogoro wa Qatar na Saud Arabia.

Uko wa kifalme wa Saud Arabia unakisiwa kuwa idadi ya watu 15000 lakini wenye utajiri mkubwa kwenye familia hiyo inakisiwa ni watu 2000.
 
Hebu fafanua mkuu, mashia ndio makafiri gani hao?
Huyo mtoa mada kwa kusema mashia ni makafiri ni ufinyu wa kiakili na mawazo. Saud Arabia ni nchi inayoendeshwa kwa mfumo wa kifalme maana yake hakuna demokrasia familia ya kifalme ndio wanaotumia asilimia kubwa ya mapato ya Mafuta yanayopatikana hakuna msaada wowote nchi hiyo inayotoa kwenda kwa nchi nyingine duniani mbali ya kutumia mabilioni ya dola kununua silaha za maangamizi. Iran ni nchi asilimia kubwa ni mashia hawa wa Iran waliangusha utawala wa kifalme wa Shah mwaka 1979 kuanguka kwa utawala wa Mfalme Shah ilikuwa ni tishio kubwa kwa utawala wa Saudh Arabia, Iran ni nchi ya kidemokrasia wanafanya uchaguzi wa Urais. Iran wanasaidia sana wapalestina katika harakati zao dhidi ya Israel wakati wapalestina wengi ni Sunni sio Shia. Kwa kifupi utawala wa kifalme wa Saudh Arabia upo kwa maslahi ya Marekani.
 
Baada ya Mfalme Salman bin Abdulaziz kutengeua nafasi ya mrithi wake Crown Prince Mohamed Bin Nayef na kumteua mtoto wake Waziri wa Ulinzi Mohamed bin Salman kuwa mrithi wake kumeleta mtafaruku mkubwa katika familia hiyo ya kifalme toka nchi hiyo iasisiwe mwaka 1932.
Mfalme wa sasa Salman bin Abdulaziz ndio mtawala wa mwisho kutoka watoto wa mwaasisi wa ufalme huo Abdualiziz bin Saud. Kuteuliwa kwa mwana mfalme huyo kuwa mrithi wa kiti cha ufalme imeonekana kama Mapinduzi dhidi ya kurithi ufalme huo kwani wakati Mfalme Salman alipochukua Kiti hicho mwaka 2015 alimteua Prince Mohamed Bin Nayef kuwa mrithi wake...
Mkuu hebu tupe ilmu kidogo kuhusu utaratibu wa urithi wa kifalme huko Saudia.

Kwa UK kwa mfano, ma-crown wote wanafahamika na hutokana na "damu iliyoko kwenye 'line'" sio kuteuliwa na mfalme aliye madarakani. Akiondoka Her Majesty, anafuata Prince Charles ambaye naye atarithiwa na Prince William na baada yake ni Prince George (3) ambaye atarithiwa na Princess Charlotte (2). Kwa sasa ni mtoto, ila endapo George atajaliwa mtoto huko mbele ya safari, Charlotte atakuwa hana chake; and so on.

Na pia miaka michache iliyopoita UK walifuta sheria kwamba mrithi ni "mtoto wa kwanza wa kiume" ila kama mfalme hana mtoto wa kiume basi ni wa kwanza wa kike (kama ilivyo kwa Malkia Elizabeth); kwa sana ni MTOTO WA KWANZA no matter the gender.

Huko uarabuni utaratibu wao ukoje?
 
... Iran ni nchi ya kidemokrasia wanafanya uchaguzi wa Urais. Iran wanasaidia sana wapalestina katika harakati zao dhidi ya Israel wakati wapalestina wengi ni Sunni sio Shia. Kwa kifupi utawala wa kifalme wa Saudh Arabia upo kwa maslahi ya Marekani.
Somehow, japo ufalme umerudi kwa mlango wa dini. Mwenye Iran ni Ayatollah (kiongozi mkuu wa dini); huyo rais anayechaguliwa "kidemokrasia" ni maigizo tu; huwekwa pale na Ayatollah na hana say yoyote zaidi kuwa mtii kwa Ayatollah na kuzingatia maagizo yake.
 
Huyo mtoa mada kwa kusema mashia ni makafiri ni ufinyu wa kiakili na mawazo. Saud Arabia ni nchi inayoendeshwa kwa mfumo wa kifalme maana yake hakuna demokrasia familia ya kifalme ndio wanaotumia asilimia kubwa ya mapato ya Mafuta yanayopatikana hakuna msaada wowote nchi hiyo inayotoa kwenda kwa nchi nyingine duniani mbali ya kutumia mabilioni ya dola kununua silaha za maangamizi. Iran ni nchi asilimia kubwa ni mashia hawa wa Iran waliangusha utawala wa kifalme wa Shah mwaka 1979 kuanguka kwa utawala wa Mfalme Shah ilikuwa ni tishio kubwa kwa utawala wa Saudh Arabia, Iran ni nchi ya kidemokrasia wanafanya uchaguzi wa Urais. Iran wanasaidia sana wapalestina katika harakati zao dhidi ya Israel wakati wapalestina wengi ni Sunni sio Shia. Kwa kifupi utawala wa kifalme wa Saudh Arabia upo kwa maslahi ya Marekani.
Mtume akiondoka duniani, alitabiri ukhalifa kisha ufalme.
Wewe hiyo demokrasia umeitoa wapi? Au ndio kutoka kwa Abdillaah bin Sabai?

Saudia wanatoa misaada mingi sana ila hawana ria na sifa kama wairan.

Kuhusu ufinyu wa akili, kama we ni shia sina haja ya kukuthibitishia umbumbumbu wenu. Ama kama ni muislamu basi utakuwa ni mjinga sana kuhusu uislamu
 
Mtume akiondoka duniani, alitabiri ukhalifa kisha ufalme.
Wewe hiyo demokrasia umeitoa wapi? Au ndio kutoka kwa Abdillaah bin Sabai?

Saudia wanatoa misaada mingi sana ila hawana ria na sifa kama wairan.

Kuhusu ufinyu wa akili, kama we ni shia sina haja ya kukuthibitishia umbumbumbu wenu. Ama kama ni muislamu basi utakuwa ni mjinga sana kuhusu uislamu
Hizo Tende mnazopewa kila mwaka nao wasaudia naona kama zimekulewesha. Sheria gani ya kiislam inasema unaweza kuoa wake 30 unajua King Abdullah wa Saudh Arabia alikuwa na wake 30 je hiyo ni aya gani ya Quran iliyotumika. Hawa wafalme ni Playboys wakwenda kustararehe na mabilioni ya madola nje. Wananunua silaha ya dola bilioni 300 wanashindwa kutoa misaada hata ya chakula kwenye nchi masikini.
 
Mkuu hebu tupe ilmu kidogo kuhusu utaratibu wa urithi wa kifalme huko Saudia.

Kwa UK kwa mfano, ma-crown wote wanafahamika na hutokana na "damu iliyoko kwenye 'line'" sio kuteuliwa na mfalme aliye madarakani. Akiondoka Her Majesty, anafuata Prince Charles ambaye naye atarithiwa na Prince William na baada yake ni Prince George (3) ambaye atarithiwa na Princess Charlotte (2). Kwa sasa ni mtoto, ila endapo George atajaliwa mtoto huko mbele ya safari, Charlotte atakuwa hana chake; and so on.

Na pia miaka michache iliyopoita UK walifuta sheria kwamba mrithi ni "mtoto wa kwanza wa kiume" ila kama mfalme hana mtoto wa kiume basi ni wa kwanza wa kike (kama ilivyo kwa Malkia Elizabeth); kwa sana ni MTOTO WA KWANZA no matter the gender.

Huko uarabuni utaratibu wao ukoje?
Kwasasa Saudh Arabia kwa kuwa ni Kizazi cha pili ndicho kinatarajiwa kuchukua madaraka ule mfumo wa kupewa ufalme kwa seniority haupo tena Mfalme ametengua kwa Prince Nayef mwenye umri wa miaka 58 mfalme ameteua mtoto wake mwenyewe Prince Mohamed mwenye umri wa miaka 31 awe mrithi wake.
Ukoo huu wa kifalme ni mkubwa sana kuna uwezekano kwa upendeleo alliyouonesha Mfalme Salman kwa mtoto wake unaweza kuleta mgawanyiko mkubwa (power struggle ) kwenye familia hiyo.
 
Inawezekana uyo mfalme yuko sahihi,

Well said, yuko sahihi - mwanae anayemtilia shaka anaonekana sio level headed hata kidogo ni mgomvi gomvi tu na kiburi, kanzisha vita huko Yemen huu ni mwaka wa ngapi na inaonekana malengo yao ya kuvamia Yemen hayaja zaa matunda licha ya Saudia kuwa na silaha nyingi za kisasa, Saudia inahusika vile vile kwenye mgogoro wa Syria, juzi juzi hapa wamewatuma magaidi kuishambulia IRAN, mwezi jana kama sikosei kawasomba Viongozi wa nchi za kislaam waje kwenye mkutano lengo lake likiwa ni kumuonyesha Trump kwamba Saudia inakubarika sana Mashariki ya kati na Duniani - maiigizo tu ya kujenga hoja ya kuwalahumu washindani wake Mashariki ya kati notably IRAN na Qatar na kweli kwenye Mkutano Saudia ikaikandia IRAN na Qatar, Trump bila ya kutafakari malengo ya Saudia naye karudia maneno yale yale ya Saudia kuisema vibaya IRAN save Qatar, baadae Saudia ikaiwekea vikwazo vya kuichumi Qatar na kulazimisha nchi za Kiislaam Mashariki ya kati na Afrika wafuate mkumbo, Amerika nayo ikafuata mkumbo wa kuilahumu Qatar bila ya kuiwekea vikwazo - in short bila ya kumuondoa mtoto huyo wa Kifalme katika Uongozi wa Serikali ya Saudia atawaletea matatizo mengi sana possibly na the begining of the end wa utawala huo.
 
Back
Top Bottom