Wanaokula kwa kutumia akili na kina Lema, Mbowe, Slaa, wote kutoka Kaskazini ebu fungua akili yako halafu jiulize kwa nini kwenye hiyo michango ya M4C, hawa wabunge hawaruhusiwi kufika Zitto Kabwe Kigoma Kaskazini, Silverster Mhoja Maswa Magharibi, Meshack Opulukwa Meatu, Said Afri Mpanda mjini, Salvatory Machemuli Ukerewe.
Wanabodi.
Baadhi ya wabunge wa Chadema pamoja na viongozi wao wameonyesha ubabaishaji mkubwa kwenye maswala ya siasa.
John Myinka, aachane na siasa za vijiweni na zile za kwenye mitandao ya kijamii zinazomtukuza na kumuona shujaa akavimba kichwa, nchi yetu ina watu wenye upeo mkubwa wa maswala mbalimbali na kukaa kwao kimya anaporopoka, ni kwamba wanampuuza Mnyika amekuwa mtu wa kuropoka tu.
Tundu Lissu, huyu mwanasheria aliingia katika siasa akitokea kwenye NGO moja wa Wanasheria wa Mazingira, Lissu alidai ana mkanda wa video ambao unaonyesha wachimbaji wadogo wakifukiwa huko Bulyankulu alidandia hoja ya Augustine Lyatonga Mrema, kufanya mropanganda hiyo ambayo aliamini kuitumia kujipatia umaarufu kisiasa zaidi kuliko fani yake, leo hii ukumuuliza vipi ule mkanda video hana tena na ameishasahau.
Godbless Lema, sihitaji kuyasema sana kuyasema mambo yake nadhani wote mnafahamu na siasa zake za kusukumwa na jazba, jana nimebahatika kumuona kwenye Star Tv katika kuchangia Chadema, kauli ya Lema anayashambulia makampuni ya simu ambayo ni wawekezaji, Lema kwa akili yake anadhani hizo kamapuni ni wapinzani wa Chadema, Lema anaongea kwa jazba bila ushahidi wala ufahamu wa maswala ya mawasiliano, Lema anatoa amri mbele ya TV nyie makampani ya simu tafadhali nawaamuru wachieni line watu wachangie la sivyo kesho asubuhi nitaamuru wananchi wote watupe line zenu chooni, sababu Chadema ni chama cha wananchi.
Mbali na maudhui hafifu,maneno uliyoandika kuwahusu Lissu & Mnyika umeyachukua,pasipo kuhariri, kutoka makala mojawapo ya gazeti la Tazama Tanzania la wiki iliyopita...Kuna jamaa aliliacha mezani nami nikapata fursa ya kulipitia...(sina kawaida ya kununua na kusoma jarida hilo).
Sasa tueleze kama wewe ndiye mwandishi wa ile makala...kama sivyo kwa nini uchukue kazi ya mtu mwingine na kujifanya ya kwako bila ku-acknowledge source?katika lugha za wanataaluma umefanya plagiarism ya wazi.
Aibu!
Na wewe kweli una mapungufu ya uelewa ebu niambie Lema kayafokea lini makampuni ya simu? Mnyinka na mwongozo wa spika nani afahamu, Lissu kufyatuka hovyo nani hajui?
Magwanda yanakuwasha nini mie ni Ritz wa JF...soma Zaburi ya 17.
Mbona unamsakama sana mnyika kosa kumuita JK DHAIFU, kwa maendeleo ya Ubungo kama yapo chini wa kwanza kulaumiwa ni serikali kwa kuwa na ubaguzi wa kuleta maendeleo kwa yale majimbo yaliyochukuliwa na upinzani pia ikumbukwe JJ Mnyika kachukua jimbo lililokuwa na Mbunge wa CCM kwa hiyo moja kwa moja mbunge aliyekuwepo anabeba lawama pia kwani hakuweza kuliongoza Jimbo kimaendeleo na inawezekana hakukuwa na hata vipaumbele vinavyoonyesha mipango ya maendeleo kwa awamu kwa muendelezo kwa kila mwaka.Hii ndio hatari ya kujiingiza katika siasa bila kujua unachokitaka kukifanya ndio kunakosababisha udandiaji wa hoja, uzushi, madai yasiyo mashiko, Mnyika amekuwa mbunge wa mwogozo spika hivi kweli Mnyika anajua upungufu wake umelifikisha wapi Jimbo la Ubungo? Ni vyema Mnyika kabla ya kuwahukumu wenzake kwa kutoa kauli za kitoto angejipima kwanza je, amelifikisha wapi Jimbo lake.
Swali langu lilikuwa moja tu; Je,wewe ndiye mwandishi wa ile makala ya ''Tazama Tanzania'' ya wiki iliyopita?
Ikiwa jawabu lako ni ndio,basi, hakika hilo ndilo gaazeti mwafaka kuendesha mazungumzo yako ya kizandiki .Na kama jibu lako ni hapana,kwa nini umefanya plagiarism ya wazi wazi,tena ya kazi dhaifu na isiyo na mvuto?
Sikukusudia na wala sitegemei kuendesha majadiliano ya kihoja na wewe..uwezo wako kiufahamu upo chini sana.
Right?
Mbona unamsakama sana mnyika kosa kumuita JK DHAIFU, kwa maendeleo ya Ubungo kama yapo chini wa kwanza kulaumiwa ni serikali kwa kuwa na ubaguzi wa kuleta maendeleo kwa yale majimbo yaliyochukuliwa na upinzani pia ikumbukwe JJ Mnyika kachukua jimbo lililokuwa na Mbunge wa CCM kwa hiyo moja kwa moja mbunge aliyekuwepo anabeba lawama pia kwani hakuweza kuliongoza Jimbo kimaendeleo na inawezekana hakukuwa na hata vipaumbele vinavyoonyesha mipango ya maendeleo kwa awamu kwa muendelezo kwa kila mwaka.
Ndio mimi una swali lingine?
Kumsakama kivipi mkuu si mwenyewe kaamua kuwa mwanasiasa kuwatumikia wananchi lazima watu wahoji utendaji wake katika jimbo la ubungo.
John Mnyika, nakushauri jikite kwenye kutatua kero za jimbo lako wana Ubungo hawana maji hawana barabara wakazi wa Kimara Bonyokwa, Kimara Temboni hawajawai kukuona wanakuona kupitia bungeni ukiomba mwongozo spika na kutoka bungeni baada ya amri ya Tundu Lissu.
Wanaokula kwa kutumia akili ni kina Lema, Mbowe, Slaa, wote kutoka Kaskazini wewe na Pro-Chadema wenzako mnafuata mkumbo tu ebu fungua akili yako halafu jiulize kwa nini kwenye hiyo michango ya M4C, hawa wabunge hawaruhusiwi kufika Zitto Kabwe Kigoma Kaskazini, Silverster Mhoja Maswa Magharibi, Meshack Opulukwa Meatu, Said Afri Mpanda mjini, Salvatory Machemuli Ukerewe.
Kuna kitu sitakisahau maishani kuhusu hili jembe la CCM. Nimewahi kuhudhuria mkutanao uliohutubiwa kwa mbwembwe na bwana Lusinde. Kama kawaida yake, alitukana sana viongozi wa CDM kwa maneno yake yaleyale ambayo hayawezi kuandikwa hapa. Lakini kinachofanya nisimsahau huyu bwana, ni pale alipohitimisha kwa kujaribu kuuelimisha umma juu ya umuhimu wa kuandikwa katiba mpya ya nchi.Ritz inaelekea unajuwa wasifu wa wabunge, tafadhali naomba wasifu na uwajibikaji bungeni wa wabunge hawa majembe ya CCM: Lusinde ( Mtera); Mwigulu Nchemba (Iramba sikumbuki vizuri); John Komba, Steve Wassira; Jenista Muhangama na Job Ndugai