Ufafanuzi wa Mnyika kuhusu tuhuma za CHADEMA kubadili vipengele vya Katiba...

Status
Not open for further replies.
Uchaguzi ngazi za majimbo, wilaya, mikoa na taifa haujafanyika kwa chama wala kwa jumuiya. Kikatiba, chama kinaanzia ngazi ya msingi halafu tawi, ili ngazi za mbele zifanye uchaguzi lazima ngazi ya chini si chini ya 50 ziwe zimekamilisha uchaguzi. Maeneo yaliyofanya chaguzi ni ngazi hiyo ya misingi na matawi. Tuliamua kufanya uhakiki wa uongozi na ukaguzi na kubaini kwamba tunahitaji kukamilisha chaguzi vitongoji, vijiji na mitaa kwa maana ya matawi na misingi katika maeneo mengi zaidi. Ndio maana ratiba na mkakati vikabadilishwa na sasa kwa sehemu kubwa kanda ndio zinazoratibu kazi katika maeneo yao kupitia M4C ya Kanda na program ya CHADEMA ni msingi. Kuhusu Katiba, nina nakala mango (hard copy) tu ya katiba ya 2004, ilikuwa na kipengele cha vipindi viwili vya nafasi ile ile. Hata hivyo, katiba mpya iliyoandikwa mwaka 2006 haikuwa na kipengele hicho. Hivyo, sio kwamba kimeondolewa kinyemela ila hakikuwepo kwenye katiba mpya. Juu ya uchaguzi wa ndani ya chama, kwa sasa kanda zinaendelea na kazi kwa upande wao kwa vyovyote vile mpaka tumalize kata, majimbo, wilaya na mikoa uchaguzi wa taifa hauwezi kuwa Disemba 2013; iwe ni kwa chama au mabaraza yake. Itakuwa mwaka 2014, na haya yatakuwa ni mabadiliko tu ya ratiba sio ya katiba wala hakutakuwa na kuvunja katiba. Ni kujipa muda tu wa kufanya kazi ya ujenzi wa chama ngazi ya chini kuweza kushinda chaguzi zijazo kwa kuwa na mtandao thabiti. Juu ya ruzuku, toka mwaka 2010 mara baada ya kushinda Ubunge silipwi posho yeyote ya chama, mimi ndiye ninaye kichangia chama. Hivyo, madai yako kuwa nanufaika na ruzuku ya chama hayana msingi wowote. Chama hiki kinajengwa na wengi wanaojitolea kwa hali na mali, ruzuku ni sehemu ndogo sana ya mahitaji ya ujenzi wa chama. JJ
kwanini kisiwemo kipengele cha mda wa uongozi katiba ya 2006,ndo kusema sasa mwenyekiti aweza kuwa kiongozi hata kwa miaka 50?
 
Kuhusu Katiba, nina nakala mango (hard copy) tu ya katiba ya 2004, ilikuwa na kipengele cha vipindi viwili vya nafasi ile ile. Hata hivyo, katiba mpya iliyoandikwa mwaka 2006 haikuwa na kipengele hicho. Hivyo, sio kwamba kimeondolewa kinyemela ila hakikuwepo kwenye katiba mpya. JJ

WanaJF,
Nataka kuwahakikishia wanachadema wote, kuwa nilikuwepo nimekuwa ndani ya Chadema kuanzia 1998 ambapo nilikuwa Makamu Mwenyekiti Bara, na baadaye 2003 Kaimu Katibu Mkuu, na hatimaye Katibu Mkuu. Hivyo nimeshiriki kikamilifu kuandaa Katiba ya 2004 na pia Katiba ya 2006 baada ya Rebranding ya Chama. Nataka niwahakikishie wanachadema, hakuna toleo lolote la Katiba ndani ya Chadema imeweka " muda wa Uongozi kuwa vipindi viwili tu", kuanzia Katiba aliyoiasisi Mzee Mtei na kupitishwa na Mkutano Mkuu, wala si ya 2004 au ya 2006. Kama kuna mtu anasema ilikuwepo na imeondolewa kinyemela, basi aonyeshe kifungu hicho kwenye Katiba yeyote ile, au miniti za kikao chochote kile.

Hawa ni viongozi wawili wa chama kimoja.

Kila mmoja anaongea lake juu ya uwepo wa kifungu kilichoondolewa kinyemela kwenye katiba.

Slaa anasema kifungu hicho hakijawahi kuwepo. Mnyika anasema katiba iliyoandikwa ni mpya kwa hiyo kifungu hicho hakikujadiliwa na hivyo hakikuingizwa kwenye katiba,lakini kilikuwepo.

Nani tumwamini?

Chadema ni chama kianchoendeshewa katika misingi ya kilaghai.

Kifungu muhimu kama hicho kwanini kisijadiliwe wakati wa kuandika katiba mpya? Kilisahaulika???? Na kwanini Slaa adanganye umma kuwa hakikuwepo?

Kijana kuwa macho, usilaghaike...

Cc Pasco MwanaDiwani
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, Mnyika si mru wa kumwamini hata kdogo, yeye ni kama kitambaa cha jasho cha mbowe. Asemacho mbowe ndo sahihi kwake hata kama hakina mantiki

Ukiona Mwana-Chadema anakubalika mbele ya macho ya Magamba, Ogopa sana kwani ni msaliti wa hatari...
 
Tunashukuru kwa ufafanuzi wako.

Hoja ndiyo iko hapa na ili kujidhihirisha, minutes za vikao zinaweza kutuondolea hii kadhia ambayo inaleta akisi hasi katika macho ya Watanzania.
Wala hakuna ulazima wa minutes za vikao hapa, sisi tumeandika katiba mpya mwaka 2006. Ushahidi kwamba hakuna kipengele cha ukomo wa vipindi viwili ni rasimu iliyopitishwa na wajumbe mwaka 2006. Atuletee mtu hapa kwamba katiba ilipitishwa ikiwa na ukomo wa vipindi halafu baadaye kifungu kinaondolewa kinyemela; ili madai yake yaweze kuthibitika. Katiba za chama toka 2006 zimesambaa nchini kwenye ngazi mbalimbali za chama wanazo nakala mango (hardcopies). Toka wakati huo hakujawahi kuwa na malalamiko kama haya kwenye chaguzi za ngazi za chini mpaka taifa 2009 na pia chaguzi za ngazi ya chini katika maeneo ambayo yamefanya uchaguzi 2013; jiulieze kwani sasa kuelekea uchaguzi wa ngazi ya taifa? Ambao kuna wengine walidhani bado ni Disemba 2013 kumbe sasa utakuwa mapema mwaka 2014?
 
Mkuu mtoi,
Miluzi mingi hupoteza mbwa mwambie mnyike akisaidiana na wewe mtuwekee katiba zote mbili ile ambayo ipo fresh ya mwaka 2004 na ile iliyochomolewa vipengele mhimu zote tusome zingine porojo tu mnatuchosha bure.
Unataka kugombea nafasi gani CDM?
 
Sasa mnyika kaongea nini jamaa naye siku hizi majnga kweli,ninamaswali machache kwake.

Mnyika anasema uchaguzi ndani ya chama ulianza mwaka 2013 na unaendelea utakamilika mwaka 2014 tunaomba mnyika atwambie kama uchaguzi ulishaanza ni jumuiya ipi ya chadema ambayo imeshafanya uchaguzi au wilaya ngapi au mikoa mingapi imeshafanya uchaguzi.

Tangu mnyika aanze kunufaika na matumizi mabaya ya ruzuku za wanachi sasa mnyika amekuwa bendele fuata upepo.

Halafu jambo lingine la msingi mnyika atuwekee hapa katiba ya mwaka2004 ambayo ilikuwa haijachakachuliwa ili tupime wenyewe.

Hujui na hauna chochote kichwani na bado unaleta kimbelembele.Kama unataka kujua mambo ya Chama chetu chukua kadi na uwe mwanachama,hutaki unapenda kushughulika na majungu fanya utafiti ujue kinachoendelea usije ukapoteza kazi yako Lumumba.
 
Viongozi wa Chadema wanasema uongo kiasi kwamba wanajikuta wanagongana kauli.

Nawashauri mkae chini, mkubaliane aina ya uongo mtakaosema. Kila mtu akija na uongo wake mtawachanganya watu mnaoaka kuwalaghai.

Haiwezekani kipengele muhimu kama cha ukomo wa vipindi vya uongozi kisijadiliwe kwenye mkutano wa katiba.

Huu ni uhuni wa kisiasa.

Mwigamba ana hoja ya msingi..
 
sisi tunataka copy ya hiyo katiba ambayo wao wanaificha na website yao wamefunga ili tusiisome

attachment.php
 
Hawa ni viongozi wawili wa chama kimoja.

Kila mmoja anaongea lake juu ya uwepo wa kifungu kilichoondolewa kinyemela kwenye katiba.

Slaa anasema kifungu hicho hakijawahi kuwepo. Mnyika anasema katiba iliyoandikwa ni mpya kwa hiyo kifungu hicho hakikujadiliwa na hivyo hakikuingizwa kwenye katiba,lakini kilikuwepo.

Nani tumwamini?

Chadema ni chama kianchoendeshewa katika misingi ya kilaghai.

Kifungu muhimu kama hicho kwanini kisijadiliwe wakati wa kuandika katiba mpya? Kilisahaulika???? Na kwanini Slaa adanganye umma kuwa hakikuwepo?

Kijana kuwa macho, usilaghaike...

Cc Pasco
Hili suala nilishalitolea maelezo toka mwanzo na Dr Slaa alishaelekeza marekebisho kwenye orodha kwamba katiba ya 2004 haiko kwenye orodha hiyo. Kwa hiyo kufanyia rejea kitu kilichofanyiwa marekebisho ni kutaka tu kuhamisha mjadala. Dr Slaa alizungumzia suala la rebranding ya chama, kwenye dhana hii ya kukizindua upya chama; tarehe 13 Agosti 2013 baada ya kuandika katiba mpya, tuliizindua katiba yenyewe, bendera mpya ya chama yenye rangi nne, kadi mpya za chama, mpango mkakati mpya wa chama, itikadi mpya ya chama huku tukibaki na falsafa ile ile ya nguvu ya umma. Kimsingi, tulizindua tumaini jipya, matokeo ya rebranding hiyo ndio CHADEMA kukua kwa kasi toka wakati huo mpaka sasa. Katiba hii mpya ya CHADEMA itayotuongoza katika kushiriki mchakato wa katiba mpya ya nchi, uchaguzi wa Serikali Vitongoji, Vijiji na Mitaa 2014 na uchaguzi mkuu 2015 kwa lengo la kuleta uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya nchi yetu. JJ
 
Wala hakuna ulazima wa minutes za vikao hapa, sisi tumeandika katiba mpya mwaka 2006. Ushahidi kwamba hakuna kipengele cha ukomo wa vipindi viwili ni rasimu iliyopitishwa na wajumbe mwaka 2006. Atuletee mtu hapa kwamba katiba ilipitishwa ikiwa na ukomo wa vipindi halafu baadaye kifungu kinaondolewa kinyemela; ili madai yake yaweze kuthibitika. Katiba za chama toka 2006 zimesambaa nchini kwenye ngazi mbalimbali za chama wanazo nakala mango (hardcopies). Toka wakati huo hakujawahi kuwa na malalamiko kama haya kwenye chaguzi za ngazi za chini mpaka taifa 2009 na pia chaguzi za ngazi ya chini katika maeneo ambayo yamefanya uchaguzi 2013; jiulieze kwani sasa kuelekea uchaguzi wa ngazi ya taifa? Ambao kuna wengine walidhani bado ni Disemba 2013 kumbe sasa utakuwa mapema mwaka 2014?

Kiongozi mwenzako Dr. Slaa anasema hakuna katiba iliyokuwa na ukomo wa vipindi vya uongozi.

Wewe unasema ukomo ulikuwepo ila haujaingizwa kwenye katiba mpya kwa vile haujajadiliwa kwenye vikao vya katiba.

1. Nani aaminiwe, wewe au Dr. Slaa?

2. Haiingii akilini kipengele muhimu kama ukomo wa vipindi vya uongozi kisijadiliwe kwenye vikao vya katiba. Umakini wako kama mwanasiasa kijana uko wapi? Mlijadili nini kama mmeacha kujadili jambo muhimu kama hilo?
 
Mkuu mtoi,
Miluzi mingi hupoteza mbwa mwambie mnyike akisaidiana na wewe mtuwekee katiba zote mbili ile ambayo ipo fresh ya mwaka 2004 na ile iliyochomolewa vipengele mhimu zote tusome zingine porojo tu mnatuchosha bure.

Sasa wewe kama kila kitu unataka tukufanyie pesa ya watu unachukua ya nini? Jaribu kujishughulisha ili hata wakati unaenda kwa Nape kupokea posho uonekane kazi unafanya.Nenda ofisi ya Msajili au makao makuu ya CDM utafute ukweli sio njaa yako ianze kuwaumiza wenzako nani aliyekuambia usitafute kazi ya halali ubaki na hii ya kupost majungu?
 
Viongozi wa CHADEMA kwa sasa wanalikoroga kuonyesha kuwa kuna mambo makubwa nyuma ya pazia.

kwa kudhihirisha haya, hebu someni haya maelezo ya viongozi wa juu kabisa wa CHADEMA jinsi wanavyokuja na contradictory comments kwenye maandishi yaliyo BOLDED.
Uchaguzi ngazi za majimbo, wilaya, mikoa na taifa haujafanyika kwa chama wala kwa jumuiya. Kikatiba, chama kinaanzia ngazi ya msingi halafu tawi, ili ngazi za mbele zifanye uchaguzi lazima ngazi ya chini si chini ya 50 ziwe zimekamilisha uchaguzi. Maeneo yaliyofanya chaguzi ni ngazi hiyo ya misingi na matawi. Tuliamua kufanya uhakiki wa uongozi na ukaguzi na kubaini kwamba tunahitaji kukamilisha chaguzi vitongoji, vijiji na mitaa kwa maana ya matawi na misingi katika maeneo mengi zaidi. Ndio maana ratiba na mkakati vikabadilishwa na sasa kwa sehemu kubwa kanda ndio zinazoratibu kazi katika maeneo yao kupitia M4C ya Kanda na program ya CHADEMA ni msingi. Kuhusu Katiba, nina nakala mango (hard copy) tu ya katiba ya 2004, ilikuwa na kipengele cha vipindi viwili vya nafasi ile ile. Hata hivyo, katiba mpya iliyoandikwa mwaka 2006 haikuwa na kipengele hicho. Hivyo, sio kwamba kimeondolewa kinyemela ila hakikuwepo kwenye katiba mpya. Juu ya uchaguzi wa ndani ya chama, kwa sasa kanda zinaendelea na kazi kwa upande wao kwa vyovyote vile mpaka tumalize kata, majimbo, wilaya na mikoa uchaguzi wa taifa hauwezi kuwa Disemba 2013; iwe ni kwa chama au mabaraza yake. Itakuwa mwaka 2014, na haya yatakuwa ni mabadiliko tu ya ratiba sio ya katiba wala hakutakuwa na kuvunja katiba. Ni kujipa muda tu wa kufanya kazi ya ujenzi wa chama ngazi ya chini kuweza kushinda chaguzi zijazo kwa kuwa na mtandao thabiti. Juu ya ruzuku, toka mwaka 2010 mara baada ya kushinda Ubunge silipwi posho yeyote ya chama, mimi ndiye ninaye kichangia chama. Hivyo, madai yako kuwa nanufaika na ruzuku ya chama hayana msingi wowote. Chama hiki kinajengwa na wengi wanaojitolea kwa hali na mali, ruzuku ni sehemu ndogo sana ya mahitaji ya ujenzi wa chama. JJ
HAPO KWENYE BOLD:
Maelezo ya Dr. Slaa na Mh. Mnyika yametofautiana sana . Nani hapa wa kumwamini katika hii kadhia na tukisema kuwa CHADEMA kimejengwa kwa misingi ya kilaghai tutakuwa tutakuwa hatuwaonei. Isije ikawa excuse ni kusema Verified ID ya Dr. Slaa alikuwa anatumia Josephine Mashumbusi kujibu hoja hii.

Angalia haya maelezo ya Dr. Slaa kuhusu katiba ya 2004,
WanaJF,

Pamoja na kuwa sitaki kuingilia mjadala katika hatua hii, naomba kuthibitisha kuwa:
I) Katibu Mkuu wa Chadema, kwa mujibu wa Katiba na Kanuni ya Chadema, ndiyo mhimili mkuu na mwenye jukumu la kutunza na kuhakikisha Katiba ya Chama inatunzwa.

2) Nataka kuwahakikishia wanachadema wote, kuwa nilikuwepo nimekuwa ndani ya Chadema kuanzia 1998 ambapo nilikuwa Makamu Mwenyekiti Bara, na baadaye 2003 Kaimu Katibu Mkuu, na hatimaye Katibu Mkuu. Hivyo nimeshiriki kikamilifu kuandaa Katiba ya 2004 na pia Katiba ya 2006 baada ya Rebranding ya Chama. Nataka niwahakikishie wanachadema, hakuna toleo lolote la Katiba ndani ya Chadema imeweka " muda wa Uongozi kuwa vipindi viwili tu", kuanzia Katiba aliyoiasisi Mzee Mtei na kupitishwa na Mkutano Mkuu, wala si ya 2004 au ya 2006. Kama kuna mtu anasema ilikuwepo na imeondolewa kinyemela, basi aonyeshe kifungu hicho kwenye Katiba yeyote ile, au miniti za kikao chochote kile.

3. Mimi Dr Slaa, ndiye niliyewasilisha Miniti za Mkutano Mkuu wa 2006 kwa Msajili ikiambatana na Katiba iliyopitishwa na Mkutano Mkuu. Tulichobishana Mimi na Msajili, na kwa maandishi, ni kuwa Msajili alit aka nimwasilishie nakala ya Katiba kwa Kiingereza. Nilimkatalia kwa msingi kuwa Katiba yetu ilipitishwa na Mkutano Mkuu kwa kiswahili na Mkutano Mkuu na hivyo siwezi Mimi kumpelekea kwa Kiingereza. Msajili alidai kuwa ni hitaji la kisheria. Nilimjibu kuwa sheria hiyo inapaswa kufanyiwa marekebisho. Hata hivyo, baadaye tulikubaliana kuwa nitengeneze " literal translation" lakini kwa mahitaji ya kisheria itatumika Katiba ya Kiswahili ambayo ndiyo iliyopitishwa na Mkutano Mkuu. Hivyo, ninathibitisha kuwa hakuna kipengele chochote kilichoingizwa kinyemela.

Wanachadema, wapenzi, na wananchi kwa ujumla, huo ndio ukweli. Kama mtu anadhani kuna utata aende kwa Msajili akague Katiba ya 1992, 2004 na 2006, nadhani utaratibu wa Msajili itaruhusu ukaguzi huo. Ndio njia pekee ya kuacha kabuni na kuwa watabiri kwa misingi ya waganga wa kienyeji. Tufanye kaki kisayansi, na tusiwatie hofu wananchi bila sababu.

Kama mtu Ana ajenda yake ya siri, huyo hatuwezi kumsaidia! Wananchi, tuna mambo ya muhimu zaidi kuliko hizi propaganda, tunahitaji kutumia muda wetu kwa mambo hayo, mathalan madai ya Katiba Mpya, kupigania maslahi ya Taifa na Watanzania hasa walala hoi ambao kila siku wanazidi kupigika, kupambana na manyanyaso Kama yaliyotokea Serengeti na Babati ambao wananchi wameteswa viajabu katika nchi inayojitangaza kuwa na utawala wa sheria nk.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...hwa-chadema-kinaweza-kufutwa.html#post7658224
Halafu Dr. Slaa akibanwa anakuja na excuse kuwa hizi siyo ajenda muhimu ambazo hazihitaji kujibiwa na wanaCHADEMA wakati kila siku yuko yeye mwenyewe JF kuzijibu kama alivyoijubu hii ajenda.

Ulaghai ni gharama.
 
sisi tunataka copy ya hiyo katiba ambayo wao wanaificha na website yao wamefunga ili tusiisome

attachment.php
Wavuti iko kwenye matengenezo kwa ajili ya kuzinduliwa upya kwa mwonekano tofauti, matengenezo hayo yanaendelea kwa muda mrefu sasa. Wanachama wataalamu wa IT na ubunifu wakiwasiliana nasi kupitia info@chadema.tz na nakala chademahabari@gmail.com baada ya hatua mbili tatu za uhakiki wanaweza kupewa nafasi ya kuitolea maoni kazi iliyotengenezwa mpaka hivi sasa. Ikishazinduliwa, wanachama wote na wananchi kwa ujumla wanaweza kutoa maoni kwa ajili ya kuendelea kuiboresha zaidi. Tunajiandaa kwa ajili ya kazi ya 2014 na 2015, maandalizi lazima yawe kwenye kila sehemu sio tu vijiji na mitaani kwenye misingi na matawi bali pia hata kwenye mitandao kwa maana ya kuwa na mwonekano mpya na kutumia TEHAMA katika kuwezesha mabadiliko nchini.JJ
 
Hili suala nilishalitolea maelezo toka mwanzo na Dr Slaa alishaelekeza marekebisho kwenye orodha kwamba katiba ya 2004 haiko kwenye orodha hiyo. Kwa hiyo kufanyia rejea kitu kilichofanyiwa marekebisho ni kutaka tu kuhamisha mjadala. Dr Slaa alizungumzia suala la rebranding ya chama, kwenye dhana hii ya kukizindua upya chama; tarehe 13 Agosti 2013 baada ya kuandika katiba mpya, tuliizindua katiba yenyewe, bendera mpya ya chama yenye rangi nne, kadi mpya za chama, mpango mkakati mpya wa chama, itikadi mpya ya chama huku tukibaki na falsafa ile ile ya nguvu ya umma. Kimsingi, tulizindua tumaini jipya, matokeo ya rebranding hiyo ndio CHADEMA kukua kwa kasi toka wakati huo mpaka sasa. Katiba hii mpya ya CHADEMA itayotuongoza katika kushiriki mchakato wa katiba mpya ya nchi, uchaguzi wa Serikali Vitongoji, Vijiji na Mitaa 2014 na uchaguzi mkuu 2015 kwa lengo la kuleta uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya nchi yetu. JJ

Mnyika ndugu yangu, mbona unakuwa mtu wa maneno ya kilaghai. Na wewe umeshaanza ulaghai. Kumbuka kuna watu tulikuunga mkono pamoja na kuwa uko upande uliopotoka, tukiamini kuwa pengine ungekuwa cheche ya kunyoosha upande huo.

Dr. Slaa in his own words amesema hivi:
WanaJF,
Nataka kuwahakikishia wanachadema wote, kuwa nilikuwepo nimekuwa ndani ya Chadema kuanzia 1998 ambapo nilikuwa Makamu Mwenyekiti Bara, na baadaye 2003 Kaimu Katibu Mkuu, na hatimaye Katibu Mkuu. Hivyo nimeshiriki kikamilifu kuandaa Katiba ya 2004 na pia Katiba ya 2006 baada ya Rebranding ya Chama. Nataka niwahakikishie wanachadema, hakuna toleo lolote la Katiba ndani ya Chadema imeweka " muda wa Uongozi kuwa vipindi viwili tu", kuanzia Katiba aliyoiasisi Mzee Mtei na kupitishwa na Mkutano Mkuu, wala si ya 2004 au ya 2006. Kama kuna mtu anasema ilikuwepo na imeondolewa kinyemela, basi aonyeshe kifungu hicho kwenye Katiba yeyote ile, au miniti za kikao chochote kile.

Sasa hapo Mnyika ndugu yangu porojo gani tena unaleta?

Unazidi kukuza kundi la watu uliowadisappoint kwa tabia hii ya porojo za uongo live!

Kitu gani kinafanya katiba ya 2004 isiwemo kwenye orodha hiyo? Je, Chadema kimekuwa na katiba ngapi tangu kianzishwe mpaka Slaa aamue kuiweka pembeni katiba ya 2004? Katika post yake Slaa ameitaja katiba ya 2004, wewe kwanini unasema haipo kwenye hiyo orodha?

Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai.

Cc Pasco MwanaDiwani Mwali
 
You're fighting the wrong enemy. Samson Mwigamba is not the enemy. You're enemy is democracy and accountability within the party.

Kwa sasa mnamshambulia Samson Mwigamba kwa ngumi na vijembe vya kisiasa kama mbwa mwitu wanavyoshambulia mzoga.

Samsom Mwigamba ameyasema mengi lakini kwa sasa mnajikita kwenye kipengele cha "fake" consititution ambacho hata mnashindwa kuleta vithibiti ambayo ni katiba ya 2004 na minute za vikao.

Mbona hamtoi maelezo ya matumizi ya pesa kama yalivyoainishwa na Samson Mwigamba?.

CHADEMA ni chama kilichoanzishwa kwa misingi ya kilaghai hata utendaji wake huwa niwa kilaghai.

CHADEMA Kinawalaghai wananchi kuwa ni chama cha DEMOKRASIA na maendeleo but they can't even talk the talk let alone walk the walk.

CHADEMA siyo chama cha siasa ndani ya demokrasia kwa manufaa ya demokrasia nchini bali ni private-owned enterprise through political project.

Haya maneno umeyakariri mbona kila mara ni hayahaya?
 
Wakuu, nawaaga kwa muda. Naelekea Tandika kwenye kukabidhi kadi kwa viongozi wa CCM wamemua kujivua gamba na gwanda, nimeitwa huko na M4C ya eneo lao inayofanya kazi ya ujenzi wa chama kuanzia kwenye misingi mpaka matawi. Nikimaliza jioni baada ya mkutano wa hadhara nitarejea baada ya mkutano huo kuendelea. Mjadala mwema. JJ
 
Wakuu, nawaaga kwa muda. Naelekea Tandika kwenye kukabidhi kadi kwa viongozi wa CCM wamemua kujivua gamba na gwanda, nimeitwa huko na M4C ya eneo lao inayofanya kazi ya ujenzi wa chama kuanzia kwenye misingi mpaka matawi. Nikimaliza jioni baada ya mkutano wa hadhara nitarejea baada ya mkutano huo kuendelea. Mjadala mwema. JJ

kila kheri kamanda,we chapa kazi wao maneno sisi kazi.
 
Wakuu, nawaaga kwa muda. Naelekea Tandika kwenye kukabidhi kadi kwa viongozi wa CCM wamemua kujivua gamba na gwanda, nimeitwa huko na M4C ya eneo lao inayofanya kazi ya ujenzi wa chama kuanzia kwenye misingi mpaka matawi. Nikimaliza jioni baada ya mkutano wa hadhara nitarejea baada ya mkutano huo kuendelea. Mjadala mwema. JJ
Jimboni kwako Ubungo umejwnga chama? Mbona kila kona waru wanakusonya tu kutokana na kushindwa kutekeleza kile ulichoaidi hususan suala la maji
 
Wakuu, nawaaga kwa muda. Naelekea Tandika kwenye kukabidhi kadi kwa viongozi wa CCM wamemua kujivua gamba na gwanda, nimeitwa huko na M4C ya eneo lao inayofanya kazi ya ujenzi wa chama kuanzia kwenye misingi mpaka matawi. Nikimaliza jioni baada ya mkutano wa hadhara nitarejea baada ya mkutano huo kuendelea. Mjadala mwema. JJ

Tulijua tu utakimbia.

Mnyika hufanani kabisa na ulaghai ulioanza kuufanya!

You are a disappointment to Ubungo youths!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom