Haya Nenda hapa mkuu:Ile thread ingine iletwe hapa basi
Wakatoliki wameingiaje kwenye mahubiri yasiyowahusu ni uchokozi
Mchungaji Gwajima amesimama na anaanza ufafanuzi
Update:
Anasema yeye anafafanua kwa habari ya washirika wake ambao wamesikia taarifa husika. Kwanza amen za na kuwauliza washirika wake ni nani amesikia taarifa hizo na kwa ujumla umati wa maelfu ya waumini wameitikia
UPDATE
Kwamba kwenye siku ya ibaada majira ya tarehe 26 mwenzi huu mwananchi mmoja alizuka kanisani, na akakutana na walinzi wa kanisa. Na wakamhoji shida yake nini, na kwa kuwa alikuwa na Shari kubwa aliwaambia lengo lake ni kumwona mchungaji kiongozi
UPDATE
mtu huyo aling'ang'ania kwa Shari kumwona mchungaji kiongozi na kwa utaratibu si rahisi kumwona yeye pasipo kujua sababu.. Kwa hasira akaanza kuropoka kwamba yeye ni mafia na kwamba yeye ndiye aliyemteka Ulimboka
Hayo ndo maswali tunayotaka majibu yake. Hivi huyo mchungaji hawezi kuongea na waandishi wa habari baada ya ibada waweze kuuliza maswali kama hayo labda anaweza kuwa na mwanga kidogo. Dr. alitekwa lini?
Kaazi kweli kweli kumbe walikiri kabisa kua ni kichaa!!!polisi wakawaambia walinzi wa kanisa wasiseme chochote kuhusu hilo maana mtu huyo alisema ni kichaa. Siku ya pili Mch akasema akashangaa Kamanda kova kutoa taarifa ya uongo kwa kilichotokea tena wiki mbili baada ya tukio. Mch akashangaa limekujaje wakati tayari polisi walishasema ni kichaa pamoja na kwamba aliziungumza maneno yaliyotoke kweli
Naomba mnikumbushe Ulimboka alitekwa tarehe ngapi?
Mtu huyo alipoulizwa mbele ya polisi kuhusu aliyoyasema alisema ni kweli. Pia alikiri alitumwa akamteke Mch Gwajima. Mch anasema kwa vile kanisa lake linaikosoa serikali inawezekana. Cha kushangaza baada ya kusema hayo Mkenya huyo akasema ni kichaa na anasikitika kwa kuropoka maneno ambayo hayapo
Mbona ni habari za uzushi?
Mmmhhh imani inanitoka mbona???
Haya hiyo point moja, Kova kashapigwa bao la kwanza dakika ya pili ya mchezo