UFAFANUZI WA KINACHOSAMBAZWA MITANDAONI KUHUSU DC MURO
Mimi mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ikungi Ndugu Mika Lucas likapakapa naomba kuweka wazi ukweli wa tukio linalotajwa katika mitandao ya kijamii kuhusu Dc Muro
Salamu nimeona niseme kidogo kuondoa upotoshaji umaofanywa kwenye mitandao
1. Tarehe 14/07/2021 Nilifanya ziara ya dharura ya kichama CCM katika kijiji cha Minyinga kata ya Makiungu jimbo la singida mashariki, nikiwa na baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya ikungi nililazimika kufanya ziara ya dharura kufuatia baadhi ya wananchi kuchoma moto nyumba ya mkazi kutokana na mgogoro wa ardhi ambapo kwa mujibu wa taarifa zinazoendelea kuchunguzwa zinataja kuwa baadhi ya viongozi wa siasa walihamasisha wananchi kwenda kuchoma nyumba ya mkazi mwenzo kwa kusingizio cha mgogoro wa Ardhi
Ofisi yetu ya chama ilipokea taarifa kutoka kwa Diwani na mwenyekiti wa CCM kata kuwa kuna machafuko, nikalazimika kuitisha kikao cha ndani cha chama na baadhi ya wananchi na wazee maarufu na viongozi wa dini kujadili changamoto hiyo mana kuna viongozi wetu wa chama pia wanatajwa kuhusika katika mgogoro
Katika jitihada za chama kutatua changamoto hii nililazimika kumuomba Mhe Mkuu wa wilaya ya Ikungi tuambatane wote katika kata ya Makiungu japo Dc Muro alisema jambo hilo linashughulikiwa na vyombo vya kiusalama na hakupenda kuwa sehemu ya mchakato wa hatua za kisheria, ila kwa kuwa yeye ni mjumbe wa kamati ya siasa ya chama ilitulazimu kwenda nae
Mimi mwenyekiti wa CCM wa wilaya ndie niliekuwa mwenyekiti wa kikao hicho ambacho kilikuwa cha ndani nilitoa nafasi kwa wajumbe kuongea kisha nikamkaribisha Dc Muro kutoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja zilizoibuliwa na wananchi haswa wa chama chama mapinduzi na baadhi ya wazee mashuhuri
Dc Muro alitoa ufafanuzi wa kutosha wa hoja zilizoibuliwa na kubwa alilosema ni kuwapiga marufu wanasiasa wanaotengeneza Migogoro ya ardhi kwa ajili ya kujipatia umaarufu wa kisiasa kauli ambayo hata sisi chama tumeiunga mkono mana amani ni jambo la muhimu kwa ccm
UPOTOSHAJI
Wako watu wanasambaza taarifa kuwa Dc Muro amepiga marufuku watu kuongelea katiba mpya
1. Hii ni hoja dhaifu maana kwa Ikungi hakuna mkutano au watu wanaozungumza au kuongelea katiba mpya na hata ofisi ya Dc Muro haina maombi ya watu kuomba kufanya mikutano au makongamano ya katiba mpya hakuna uku Ikungi sisi tuko busy na kilimo na biashara, hivyo Dc Muro hakuwa na haja ya kupiga marufuku mana hatuna mambo hayo sisi wa ccm wala wa vyama vingine na ndio mana hawajafanya mikutano wala sidhani kama wana nia ya kufanya hivyo
Katika hii hoja nachokumbuka ni Dc Muro alikuwa anaongea na kina mama wa pale ndani na Dc Muro aliunga mkono kauli ya mama Martha ambae alisema kwa Ikungi hata wao hawaoni haja ya katiba mpya kwa sasa zaidi wanataka shule na maji na huduma bora za afya jambo ambalo Dc Muro katika hali ya mazungumzo alisema na yeye kwa mtazamo wake anaona aweke kipaumbele katika kuharakisha mchakato wa utoaji wa huduma bora za afya elimu pamoja na miundombinu ya barabara
2. Kuna kipande cha sauti ambacho kinasambazwa mitandaoni
- Hapa naomba niseme kwanza katika kikao cha ndani hakuna alierekodi, na hata ukisikiliza kwa makini utaona mwanzoni kabisa watu wanaongea wenyewe kwa sauti kubwa kuonyesha wanatengeneza kitu, kisha baadae inasikika sauti kwa mbali sana ya mtu kama Dc Muro akiongea
- Udhaifu wa sauti hiyo ni kwamba kuna sehemu zinakatwa katwa kabisa kisha kinaanza kitu kingine kwa mbali ili ukisikiliza vizuri utasikia maneno ambayo pia Muongeaji pia akiomba wanasiasa kuacha kutengeneza migogoro ya ardhi kwa ajili ya kujipatia umaarufu
- Katika clip hiyo pia yanasikia maneno ambayo wanasiasa wa vyama vyote wanaombwa kushirikiana kuijenga ikungi na kufanya siasa za Maendeleo
- Katika clip hiyo pia inasikika sauti ambayo wajumbe walicheka pale ambapo sauti inasema mimi nawabatiza kwa maji na mama samia atawabatiza kwa moto kauli ambayo iliwafanya wajumbe wacheke kwa utani
HITIMISHO
Nataka kusema kuwa ule ulikuwa mkutano wetu wa chama wa ndani na ulifanyika katika ofisi za chama tawi la CCM Minyinga na sisi tulialika wazee maarufu na viongozi wa dini, tunaomba sana mambo yetu katika chama yasiingiliwe na wasio wa kwetu
Kama mna jambo na Dc Muro mumsubiri akiwa kwenye mikutano yake na Wananchi au katika ziara zake za kata na sio uku kwenye mambo yetu ya kichama
Tunamshukuru Dc Muro maana katika kikao kile cha ndani alitolea suluhu mgogoro wetu wa ardhi na muafaka ulipatikana, sisi kama chama tunaunga mkono jitihada za Dc Muro katika kutatua kero na kuwaletea wananchi Maendeleo
Dc Muro ameanza vizuri Ikungi, tunaendelea kumuunga mkono
Wenu katika utumishi,
Mika Lucas likapakapa
Mwenyekiti wa ccm Ikungi
16/07/2021
Mimi mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ikungi Ndugu Mika Lucas likapakapa naomba kuweka wazi ukweli wa tukio linalotajwa katika mitandao ya kijamii kuhusu Dc Muro
Salamu nimeona niseme kidogo kuondoa upotoshaji umaofanywa kwenye mitandao
1. Tarehe 14/07/2021 Nilifanya ziara ya dharura ya kichama CCM katika kijiji cha Minyinga kata ya Makiungu jimbo la singida mashariki, nikiwa na baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya ikungi nililazimika kufanya ziara ya dharura kufuatia baadhi ya wananchi kuchoma moto nyumba ya mkazi kutokana na mgogoro wa ardhi ambapo kwa mujibu wa taarifa zinazoendelea kuchunguzwa zinataja kuwa baadhi ya viongozi wa siasa walihamasisha wananchi kwenda kuchoma nyumba ya mkazi mwenzo kwa kusingizio cha mgogoro wa Ardhi
Ofisi yetu ya chama ilipokea taarifa kutoka kwa Diwani na mwenyekiti wa CCM kata kuwa kuna machafuko, nikalazimika kuitisha kikao cha ndani cha chama na baadhi ya wananchi na wazee maarufu na viongozi wa dini kujadili changamoto hiyo mana kuna viongozi wetu wa chama pia wanatajwa kuhusika katika mgogoro
Katika jitihada za chama kutatua changamoto hii nililazimika kumuomba Mhe Mkuu wa wilaya ya Ikungi tuambatane wote katika kata ya Makiungu japo Dc Muro alisema jambo hilo linashughulikiwa na vyombo vya kiusalama na hakupenda kuwa sehemu ya mchakato wa hatua za kisheria, ila kwa kuwa yeye ni mjumbe wa kamati ya siasa ya chama ilitulazimu kwenda nae
Mimi mwenyekiti wa CCM wa wilaya ndie niliekuwa mwenyekiti wa kikao hicho ambacho kilikuwa cha ndani nilitoa nafasi kwa wajumbe kuongea kisha nikamkaribisha Dc Muro kutoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja zilizoibuliwa na wananchi haswa wa chama chama mapinduzi na baadhi ya wazee mashuhuri
Dc Muro alitoa ufafanuzi wa kutosha wa hoja zilizoibuliwa na kubwa alilosema ni kuwapiga marufu wanasiasa wanaotengeneza Migogoro ya ardhi kwa ajili ya kujipatia umaarufu wa kisiasa kauli ambayo hata sisi chama tumeiunga mkono mana amani ni jambo la muhimu kwa ccm
UPOTOSHAJI
Wako watu wanasambaza taarifa kuwa Dc Muro amepiga marufuku watu kuongelea katiba mpya
1. Hii ni hoja dhaifu maana kwa Ikungi hakuna mkutano au watu wanaozungumza au kuongelea katiba mpya na hata ofisi ya Dc Muro haina maombi ya watu kuomba kufanya mikutano au makongamano ya katiba mpya hakuna uku Ikungi sisi tuko busy na kilimo na biashara, hivyo Dc Muro hakuwa na haja ya kupiga marufuku mana hatuna mambo hayo sisi wa ccm wala wa vyama vingine na ndio mana hawajafanya mikutano wala sidhani kama wana nia ya kufanya hivyo
Katika hii hoja nachokumbuka ni Dc Muro alikuwa anaongea na kina mama wa pale ndani na Dc Muro aliunga mkono kauli ya mama Martha ambae alisema kwa Ikungi hata wao hawaoni haja ya katiba mpya kwa sasa zaidi wanataka shule na maji na huduma bora za afya jambo ambalo Dc Muro katika hali ya mazungumzo alisema na yeye kwa mtazamo wake anaona aweke kipaumbele katika kuharakisha mchakato wa utoaji wa huduma bora za afya elimu pamoja na miundombinu ya barabara
2. Kuna kipande cha sauti ambacho kinasambazwa mitandaoni
- Hapa naomba niseme kwanza katika kikao cha ndani hakuna alierekodi, na hata ukisikiliza kwa makini utaona mwanzoni kabisa watu wanaongea wenyewe kwa sauti kubwa kuonyesha wanatengeneza kitu, kisha baadae inasikika sauti kwa mbali sana ya mtu kama Dc Muro akiongea
- Udhaifu wa sauti hiyo ni kwamba kuna sehemu zinakatwa katwa kabisa kisha kinaanza kitu kingine kwa mbali ili ukisikiliza vizuri utasikia maneno ambayo pia Muongeaji pia akiomba wanasiasa kuacha kutengeneza migogoro ya ardhi kwa ajili ya kujipatia umaarufu
- Katika clip hiyo pia yanasikia maneno ambayo wanasiasa wa vyama vyote wanaombwa kushirikiana kuijenga ikungi na kufanya siasa za Maendeleo
- Katika clip hiyo pia inasikika sauti ambayo wajumbe walicheka pale ambapo sauti inasema mimi nawabatiza kwa maji na mama samia atawabatiza kwa moto kauli ambayo iliwafanya wajumbe wacheke kwa utani
HITIMISHO
Nataka kusema kuwa ule ulikuwa mkutano wetu wa chama wa ndani na ulifanyika katika ofisi za chama tawi la CCM Minyinga na sisi tulialika wazee maarufu na viongozi wa dini, tunaomba sana mambo yetu katika chama yasiingiliwe na wasio wa kwetu
Kama mna jambo na Dc Muro mumsubiri akiwa kwenye mikutano yake na Wananchi au katika ziara zake za kata na sio uku kwenye mambo yetu ya kichama
Tunamshukuru Dc Muro maana katika kikao kile cha ndani alitolea suluhu mgogoro wetu wa ardhi na muafaka ulipatikana, sisi kama chama tunaunga mkono jitihada za Dc Muro katika kutatua kero na kuwaletea wananchi Maendeleo
Dc Muro ameanza vizuri Ikungi, tunaendelea kumuunga mkono
Wenu katika utumishi,
Mika Lucas likapakapa
Mwenyekiti wa ccm Ikungi
16/07/2021