Ufafanuzi wa kilichotokea Uchaguzi Meya Mwanza...

Tatizo nini?je ni kutoeleweka sawasawa kwa vugu vugu la M4C -chadema kwa upande mmoja na V4C- cuf na kueleweka sawasawa kwa vuvuzela la NAPE la vua gwanda vaa uzalendo????tafakari kisha toa maoni yatakayoisaida chadema na upinzani kwa ujumla mbele ya safari,waswahili wanasema inakua ni rahisi sana kusimama kama utaanguka na kukubali umeanguka kuliko ukiwa umeanguka lakini hukubali kwamba umeanguka,maana yake utaendelea kubali hapo hapo chini ukiamini bado umesimama kumbe upo chini unagalagala sakafuni.

Kama hata wewe hujaelewa kuwa katika uchaguzi huu unaouzungumzia wanaopiga kura ni madiwani, na sio wananchi wapiga kura, basi TZ kuna kazi kweli !!
Hii umeandika tu ili kutaka kuonyesha kuwa wananchi ndio waliopiga kura, na kuwa wananchi hawajaikubali M4C.
Haya, kwa ufafanuzi wa nini kilichotokea, kuna thread inayofafanua kila kitu.
Angalia thread hiyo utaelewa (kama kweli huelewi !!).
 
kufukuzana noma,wangekua wamefanya kosa lawazi na kubwa sawa,kuvumiliana kupo,shibuda mbona anavumiliwa,hayo mambo yapo,zama zasasa kupishana mawazo kupo,siamini kama wasaliti kwasababu mipango yao iliungwa mkono na madiwani wengine wa cdm.
 
kufukuzana noma,wangekua wamefanya kosa lawazi na kubwa sawa,kuvumiliana kupo,shibuda mbona anavumiliwa,hayo mambo yapo,zama zasasa kupishana mawazo kupo,siamini kama wasaliti kwasababu mipango yao iliungwa mkono na madiwani wengine wa cdm.
Nduguyangu chadema si pango la walarushwa Uadilifu na uajibikaji Ni zaidi ya Umea
 
Kura zikapigwa. Matokeo nidyo kama hayo ambayo watu wengi hapa tayari mnayajua, 11-8. Kuwa honestly, hata kama " kura ni siri, haitarajiwi kuwa Chagulani ambaye anapita barabarani akibeza uamuzi wa Kamati Kuu ya CHADEMA na viongozi wa chama, hivyo ana hasira, angeipigia kura CHADEMA. Never. So unaweza kupiga hesabu zako kichwani.

Kwenye nafasi ya Unaibu Meya, ambayo walipambana mgombea wa CCM na CUF, kura zikabadilika kidogo. Ikawa 10 (CCM)-9 (CUF). Hapa unaweza kuona kuwa madiwani karibu wote wa CHADEMA walimpatia mgombea wa CUF hivyo plus kura yake na ile ya diwani mwenzake, zikawa tisa. CCM waka-maintain kura zao na washirika wao "

My Take:
Uchaguzi wa Meya, ni 11 kwa 8, naaamini ni CCM 8 + CUF 2 + Chagulani 1, kwa CDM 8.

Naibu Meya, Ni 10 kwa 9, Naamini ni CCM 8 + Chagulani 1 + CUF 1, kwa CDM 8 + CUF 1.

Kwa Vyovyote haiwezekani CUF akamtosa CUF mwenzie na Kumpiga CCM kwenye naibu Meya , Maanake ni kuwa hata hizo kura za CMD 8 zina walakini , kuna mamluki mmoja ua wawili at most wapo humo.
 
Huu uhuni kumbe ndivyo ulivyokuwa??

Naona hapa Musoma walijaribu sana kuvuruga ikashindikana!

Leo tunakinukisha Nyasho Stand!

Karibuni wote mlioko huku!
 
Hapo umenena hizi siasa za umeya wa majiji zihusishe wananchi!

Mbaya zaidi chama ili ifanikiwe kushinda umeya inakwenda kuazima kura za madiwani wa chama kingine! Ingelikuwa ni wananchi tusingejua kuwa madiwani wa cuf wamewapigia kura ccm!

wakuu sijui ni watanzania wangapi huwa wanakumbuka kutoa maoni ya utaratibu wa kuwapata mameya na wenyeviti wa halmashauri kwa tume ya katiba kwasababu tumeshaona matajiri wakisponsor madiwani wakati wa kampeni na baadae kumwaga fedha kwa madiwani haohao kumuweka meya wanayemtaka ili iwe rahisi kwao kupata tenda za upendeleo. Naona hata mchambuzi wetu hapo juu na wengi waliochangia wameweka hali ya kusalitiana wakati wa kupiga kura na kujisahaulisha kuwa kuna kitu kinaitwa demokrasia.

chadema nacho kinaanza yaleyale ya ccm na cuf kutafuta madaraka kwa njia yoyote kama hii ya kufunga ndoa na cuf kumpata meya wa cdm na naibu kutoka cuf bila kuangalia uwezo wake.. hii kwangu mimi ni rushwa ya madaraka kama nilivyowahi kusema hapo nyuma, leo ndoa ya madiwani.. 2015 si ajabu cdm kikafunga ndoa na ccm kuunda serikali ya mseto.
 
Nifafanulie hapa mkuu,
Ilemela na Nyamagana zote ziko ndani ya Mwanza,
So any movement within these districts will not affect the entire total number of madiwani within Mwanza, au ikoje hii?
Mtu akitoka ilemela akahamia Nyamagana itaathiri vipi jumla ya madiwani wa Mwanza?
Ufafanuzi please!!
Nikweli Ilemela na Nyamagana zote ziko Mwanza ila kwa sasa Ilemela ni Manispaa inayojitegemea, hivyo itakuwa na baraza lake la madiwani likiongwa na Meya kama ilivyo kwa Ilala, Kinondoni na Temeke hapa Dar es Salaam...Na Nyamagana imepewa hadhi ya jiji kama ilivyo kwa Jiji la dar es Salaam japo hazifanani sana maana jiji la Dar linajumuisha madiwani toka manispaa zote tatu za Dar....Kwa Nyamagana baraza lake la madiwani litaundwa na madiwani ndani ya mipaka (kata zilizo ndani ya wilaya ya Nyamagana) ya Nyamagana.....Sasa kwakuwa madiwani wa CCM ni wachache, na kwakuwa inataka ishinde, ilibidi ikodimajeshi toka Manispaa ya Ilemela ambao ni diwani viti maalumu na mbunge viti maalumu wa Mkoa wa Mwanza, kwa mbunge kunaweza kusiwe na tatizo coz yeye anafanya kazi za mkoa mzima ila kwa diwani huyu ambaye umaalum wake unatokana na kura za udiwani wa kata (bila shaka) kunaweza kukawa na mushkel...Sasa sina hakika kisheria kama inaruhusiwa kuamisha diwani wa kata nyingine na si tu kata nyingine bali kutoka halmashauri nyingine....Bila shaka hapa tutahitaji wanasheria kutusadia hapa...Na je uchaguzi wa Ilemela utakapofanyika, CCM itawarudisha tena hao madiwani waliokuwa wameamishiwa Nyamagana! Kesi hii inataka kufanana na ile ya Arusha...So hapa hapazungumzii madiwani wa Mwanza kwa maana ya jiji la zamani la Mwanza ila inazungumzia madiwani wa Halmashauri mbili yaani Manispaa ya Ilemela na Jiji...Ni sawa ukamchukua diwani wa viti maalumu toka Temeke na kumuhamishia Ilala au Kinondoni....Hapa ndo tunataka watu wa sheria watusaidie....

 
CCM wameshindishwa na mbinu za kisiasa amabzo uhalali wake kisheria linabaki kuwa suala la wanasheria wanaojua taratiu zikoje.

Baada ya mgawanyo wa h/shauri ya jiji na kuwa na h/shauri ya jiji inayoundwa na jimbo la Nyamagana na halmashauri ya ilemela inayondwa na jimbo la ilemela mwezi Julai mwaka huu mgawanyo wa madiwai ulikuwa hivi kwa nyamagana

Chadema -wa kata 5, viti ,maalum 2. mbunge mmoja, jumla wanakuwa 8
CCM - wa kata 6, viti maalum 1 jumla wanakuwa 7
Cuf - wa kata 1, viti maalum 1

Ilemela

Chadema -- wak kata 6, viti maalum 2 mbunge 1 jumla wanakuwa 9
CCM - wa kata 3, viti maalum 2 na mbunge 1 (wa viti maalum) jumla wanakuwa 6
CUF - MBUNGE WA viti maalum 1

Kilchotokea kwenye uchaguzi ni CCM kuhamisha diwani mmoja wa viti maalum (kwa barua ya CCM kwenda kwa mkurugenzi wa jiji ya tarehe 14, Septemba, 2012) na mbunge wa viti maalum toka Ilemela kuja nyamagana na hivyo kuongeza idadi ya kura zao kuwa 9, wakati huo huo Chadema walishakuwa hawaihehabu kura ya Diwani wa Igoma Chagulani ambaye wamemfukuza uanachama akalejeshewa na mahakama wao wanapugukiwa na kura 1 zao zinabaki 7 , aliyepungua Chadema akiwapigia CCM wanakuwa na kura 10 dhid ya 7 za Chadema.

Lakini pia CUF walishakubaliana na chadema kuungana mkono, kwa hiyo kwa kura 2 za CUF Chadema wangekuwa na kura 9, lakini inaonekana ama mwana Chadema mmoja kapigia CCM au CUF mmoja kapigia CCM na kufanya matokeo ya kuwa kuwa 11 kwa CCM dhidi ya nane za Chadema.

Hiyo ndiyo hali halisi ya jinsi mahesau ya kura yalivyochezwa, kama kuna uhalali katika mchakato huo au la ni suala la wataalamu wa masuala haya kutujuza.

Hayo yakiendelea uchaguzi wa Meya wa Ilemela meahirshwa katika mazingira tata, baada ya Mkurugeni kusoma Amri ya Mahakama iliyopewa tafsiri na mwanasheria wa jiji kuwa inakifanya kikao hicho kuahirishwa kwa kuwa Diwani wa Chadema Matata (pia alifukuzwa uanachama pamoja na wa igoma na anaendelea na udiwani kwa amri ya makahama) kuleta pia barua ya kutaka atambuliwe kaa mgombea.

Ukazuka ubishi kidogo juu ya hoja ya mgombea kuteuliwa na chama, mkurugenzi wa jiji akasema hiyo siyo sheria ni mwogozo, na kwa kuwa sheria na mwongozo zikigongana sheria ndiyo inatamalaki hatakia aingie katka mgogoro wa tafsiri ya sheria, akaahirisha kikao bila hata madiwani kujadili hoja hiyo.

Kwa mujibu wa mwanasheria wa wa Chadema, pingamizi hilo lilikuwa linawarejeshea haki yao ya uanachama na hivyo kuendelea na udiwani wao, na kutaka matata asizuiliwe kuendelea na mchakato wa kuomba umeya, Kwa hiyo matata ameomba lakini hakuteuliwa na chama na mahakama haiwezi kuwalazmisha chama wateue mgombea kwa amri ya mahakama, anadhani ni uhuni tu na njama za kisiasa zimefanyika kuahirisha uchaguzi huo.
Nadhani kidogo piacha itaeleweka kwa wanjamvi juu ya nini hasa kimetokea.

SOURCE: Kamnada Deus Bugaywa-Mchambuzi Raia Mwema

Ushuhuda wa aliyekuwa eneo la tukio:


TATIZO LAKO DICK kavu za mwanza na hasa kule Malimbe na maeneo ya Beach kule zimekuharibu kichwa

Haya nambie jumapili kavu wapi??????????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
TATIZO LAKO DICK kavu za mwanza na hasa kule Malimbe na maeneo ya Beach kule zimekuharibu kichwa

Haya nambie jumapili kavu wapi??????????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Hahahahaha....Hahahahaha....Duh! Ila wewe kiboko...Basi nitextie kwa 0716030030 coz am totally BLIND....Hahahahahaha....WABHEJASANA
 
Back
Top Bottom