Ufafanuzi wa hotuba ya "upotoshaji" ya Zitto kwa watanzania waishio Marekani

Nape hivi unapata muda wa kumuudumia mke kamaunavyo poteza muda kuhiudumia ccm nape Ccm imekufa da nakuonea huruma ijenge familaya yako nape
 
nape na ccm yako hizo mbwembwe hapo juu hazina jipya , zito zuber kabwe z.z.k sio kichaa aanze kukurupuka na kuwaongopea watanzania walioko u.s.a, alichokisema kipo kwenye ilan ya chadema na sio kwenu ilan yenu 2nayo 2meipitia haina jipya na tafadhalin sana ccm 2mawaheshm msi2tibue
 
kwa sasa taifa halihitaji katiba mpya-waziri wa katiba selina kombani-2010 .katiba ya sasa ni nzuri,hatuitaj kutunga katiba-mwanasheria mkuu wa serikali mwaka 2010.
 
Nape anapompinga Zitto kuhusu hali ya mfumuko wa bei na anathubutu kusema Mh Zitto hajafanya utafiti juu ya aliyoyaongea hivi mtu unahtaji kufanya research kwa hali ambayo inajionyesha kabisa!!?Mfano sehemu kama Mbeya haijawahi kushuhudia mfumuko wa bei ya mchele kwa asilimia zaidi ya 150 mahindi asilimia 100 na Mbeya ndo Wakulima walipo.
Hivi Nape lini amewahi kwenda huko anakosema (
watanzania wa vijijini
chakula chao
hakitokani na pesa,
wanakula vitu vingi
ambavyo haviingii
kwenye takwimu za
uchumi mfano, kuku,
mayai, maziwa,
mihogo, viazi vitamu,
nyama n.k. Hivyo
vinaliwa bila kuingia
kwenye mzunguko
wa soko ndio maana
hakuna mtanzania
anayekufa njaa.)Daah kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa uliza bei ya hivyo vitu mbozi, rungwe na Mbeya .Tuwe na umakini kuchambua mambo watz wenzangu. habari zilizonfkia kutoka Ileje zinsema baadhi wananchi wa wilaya hiyo wanafuata huduma za afya Malawi inamaana Nape haoni yote hayo!? CCM isitafute visingizio kwa kuwa wamekua wakiwadanganya watz waishio nje kuwa hali ni nzuri wakati si kweli.
 
Si unajua tatizo la siasa za wabongo ni kupinga kila kitu, ipo siku watapinga hata tahadhari ya kuwanusuru.

Huoni hata hii ya kifo cha ccm wanapinga kwakujidai wana wanachama hai wengi kuliko cdm kwani hao wanachama hawajui kuhama na hawaoni haya madudu ya ccm na ugumu wa maisha kwa ujumla?
 
anachotaka kufanya nape ni kuendelea kujihuisha yeye na chama chake kwa wakati ambao ulishapita na mara nyingi kwenye hotuba zake anashindwa kuwa mhalisia kwa kusoma alama za nyakati na matukio,nafikiri ni mda wa yeye kujipima vinginevyo atakuwa na mchango mkubwa wa kuipeleka ccm kaburini
 
Nape ni kauzu zaidi ya dagaa maana kama yote hayo anayakataa inaonyesha ni jinsi gani serikali ya ccm ilivyo mbali na wananchi wake kama hataki kukubaliana kwamba hakuna watz wanaoshindwa kupata mlo mmoja kwa siku na kujaribu kung'ang'ania takwimu gansi zinazotengenezwa na ccm ili kuwahadaa wananchi, abishe tena kama siyo cdm mawaziri waliohuwa na kashfa wasingeondolewa kwani huyo wanaedai ni mwenyekiti wao alishachukulia ni upepo wa kisiasa na hakuwa na uchungu na Tz inayoibiwa kila kukicha
 
Kwa kweli ccm imechoka sana! mpaka inatia huruma. Eti nao wanatoa mapendekezo kwenye katiba mpya! baada ya kuliangusha gari, dereva anawashauri majeruhi kuwa apunguze mwendo, wakati gari matairi yameangalia juu!!!!!
 
Najua tatizo linalomuandama Bw Nap katika kipindi kigumu kama hiki.
1. anajaribu kujustfy mafao anayoyapata... isije ikaonekana yuko idle
2. Sheria ya maumbile(evolution) inailazimisha ccm ife kwa lazima kwa vile chama kimeshindwa kwa muda mwingi wa uhai wake kuteea wanyonge.
3 kizazi kipya cha sasa na kijacho hakiitaji ngojera za nape,
4. Harakati za kudai katiba mpya zimetokana na juhudi za CDM, vyama vya upinzani na wanaharakati mahili.


Kwa hiyo, ww endelea kupuliza vuvuzela lako lakini ccm lazima iende na maji. imewafanyia maovu mengi watanzania kuliko mazuri.

you better start counting some days to be kept in museum.....

miaka michache ijayo wajukuu wetu watasoma uraia kwamba kilikuwepo chama kilichwekwa kwapani na mafisadi, wezi, na wababaishaji wa kila aina na hatimaye kilikufa kifa cha lazima..........pmbafu
 
Nape ni kasha, hajui uhusiano kati ya 'CAUSE NA EFFECT' ****** aliongea kwenye hotuba baada ya nini? nadhani hafanyi kusudi ila uelewa mdogo.
 
Katika hotuba yake anadai kwamba mchakato wa Katiba Mpya unaoendelea hivi sasa unatokana na shinikizo la CHADEMA, Asasi za kiraia na viongozi wa dini.

UFAFANUZI
Huo ni upotoshaji mkubwa na wa wazi kabisa unaolenga kufuta historia sahihi ya mchakato wa uandikaji au upatikanaji wa Katiba Mpya unaoendelea hivi sasa.

Ni jambo lililo dhahiri kabisa kwamba mchakato wa Katiba Mpya ni utekelezaji wa hotuba ya Mhe. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyoitoa katika salamu za kuaga mwaka 2010 kukaribisha mwaka 2011 na baadaye katika sherehe za Chama Cha Mapinduzi kutimiza miaka 34 Mjini Dodoma. Hili ndilo chimbuko halisi la hoja ya Katiba Mpya.

Akitoa maamuzi hayo alisema Katiba iliyopo sasa ni nzuri, imetuvusha salama miaka hamsini iliyopita, tukiwa wamoja, imetujengea umoja wa Kitaifa. Lakini katika kipindi hicho hicho kumetokea mabadiliko mengi duniani na hapa nchini ya kisayansi, kiteknolojia, kitamaduni, kisiasa n.k. Hakuna shaka kwamba sasa tunahitaji Katiba Mpya itakayotuvusha miaka mingine 50 ijayo. Jambo hili Zitto Kabwe kalinukuu kwenye hotuba yake anaposema kuwa:-

“Tanzania tunayoitaka kwa miaka mingine hamsini ….” Mantiki hii ya miaka mingine 50 inatokana na hotuba ya Mhe. Dr. Jakaya M. Kikwete sio yeye.


KAMA KWELI HAIKUWA HOJA YA CHADEMA NA SHINIKIZO LA ASASI ZA KIRAIA KWANINI HAIKUWEKWA KWENYE ILANI YENU? MBILI KWANINI UTEKELEZAJI WAKE UMEKUWA WA KUSHINIKIZWA HUKU BAADHI YA VIONGOZI NA MAWAZIRI WAKISEMA HAKUNA HAJA YA KUWA NA KATIBA MPYA? KAMA KWELI ILIKUWA NI AJENDA YA CHAMA KWANINI WENGINE WANAPINGA SUALA AMBALO LIMEPENDEKEZWA AU AMBALO LIMESHAKUWA AJENDA YA CHAMA?


Katika hotuba yake amedai kuwa CHADEMA ndio viongozi waliobeba dhamana ya mpito huu, kutoka Serikali ya kibadhirifu isiyojali watu mpaka Taifa lenye demokrasia iliyokomaa na lenye maendeleo na ustawi wa watu wake. (Developmental Democratic State).

UFAFANUZI
Kwanza CHADEMA haina “dhamana” ya uongozi wa nchi, mwenye dhamana ya uongozi wa nchi ni Chama Cha Mapinduzi ambacho kina Rais ambaye ni Mkuu wa nchi, Mkuu wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu. CHADEMA wanachokitafuta ni Mob leadership ambayo ni fujo “Anarchy or law lessness” kitu ambacho huwezi kukidhibiti hata ukishika madaraka (mfano ni Libya, Mali, Algeria n.k.).

Mob leadership ni fujo kwa sababu ina watu ambao hawana sera ya pamoja hawana wajibu wa kisheria, hawana maslahi ya kijamii na kidini, wanadai haki bila wajibu.

Dhamana ya kuwafikisha watu katika Serikali ya kidemokrasia imo mikononi mwa Serikali iliyopo madarakani. Matamshi yanayotolewa na baadhi ya viongozi wa CHADEMA yanaonyesha dhahiri kuwa hawathamini demokrasia ya nchi, umoja wa kitaifa wala amani na utulivu.

NAFIKIRI CCM WAMESAHAU CHAMA KILICHOKUWA KINASHIKILIA CCM KUNA MAFISADI NI CHADEMA PEKE YAKE AU AMESAHAU LIST OF SHAME ILIYOTOLEWA MWEMBE YANGA NA DR SLAA HUKU VIONGOZI WENU WAKIKANUSHA NA KUSEMA HUO NI UZUSHI,LAKINI WAMEKUJA KUPORA HOJA BAADA YA MATOKEO YA UCHAGUZI MKUU YA MWAKA 2010 AMBAPO CHAMA CHENU KWA MARA YA KWANZA KILIKUBALI KWAMBA NDANI YA CHAMA KUNA MAFISADI LAKINI MMESHINDWA KUWACHUKULIA HATU BADALA YAKE MNAKUJA NA SERA NA AJENDA NYINGI AMBAZO HAZIONESHI KAMA KWELI MNA NIA YA DHATI YA KUSHUGHURIKA NA MAFISADI KUONESHA NI KWA JINSI GANI SERIKALI YENU ILIVO DHAIFU IMESHINDWA KUWAFIKISHA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA WATU WANAOTUHUMIWA KWA UFISADI BADALA YAKE MNAWABADILISHA VITENGO AU KUWAPUMZISHA BILA KUTOA HATUA ZIPI ZITACHUKULIWA KUHAKIKISHA HIYO HELA YA UMMA INARUDISHWA.

Katika hotuba yake amedai kuwa Tanzania haina sera ya Gesi asili na kwamba, sheria ya madini ya mwaka 2010 imetokana na shinikizo la CHADEMA na Asasi za kiraia.

UFAFANUZI
Chama Cha Mapinduzi katika ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2010 ambayo inapatikana katika website ya CCM
www.ccm.or.tz katika ibara ya 55 ya ilani imeeleza mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya madini kwa kipindi cha 2005/2010, ambayo ni pamoja na kukamilika kwa sera ya madini ya 2009 na kupitishwa kwa sheria ya madini ya mwaka 2010.

Mhe. Kabwe mwaka 2009 alikuwa wapi kutoa mchango wake?

Hoja hii ni ya CCM yeye na Chama chake wameidandia kwa malengo ya kibinafsi na sio maslahi ya nchi.

NAFIKIRI HIKI HAPA NDO KIPIMO CHA UONGOZI KWA CHAMA CHA MAPINDUZI ALICHOSEMA MWESHIMIWA ZITTO NI KWAMBA SERA ILE ILITOKANA NA SHINIKIZO LA CHADEMA NA ASASI ZA KIRAIA LAKINI NYIE AMBACHO MMEWEKA KWENYE ILANI NI MAFANIKIO YA SERA ILIYOTOKANA NA SHINIKIZO LA CHADEMA NA ASASI ZA KIRAIA KWA HIYO UNATHIBITISHA NI KWA JINSI GANI CHADEMA IMEKUWA BORA MAANA HOJA NA SERA ZAKE ZINATEKELEZEKA.

6. HALI YA UCHUMI WA NCHI
Amedai kuwa uchumi unaokuwa hivi sasa sio uchumi wa watanzania bali ni uchumi wa watu wachache kwenye sekta chache kama madini, mawasiliano na ujenzi; hivyo kupelekea watanzania wengi zaidi ya 15m kuishi chini ya Tshs. 500 kwa siku, kutokuwa na uhakika wa kula na kukabiliwa na mfumuko wa bei.

UFAFANUZI
Kwanza, takwimu zake sio za kitafiti kwani hazionyeshi chanzo. Pili hazina ulinganisho wa hali ya maisha ya wananchi wa nchi zinazotuzunguka ili uchungu alionao moyoni uonekane waziwazi kama ni kweli au ni uzushi.

Mhe. Kabwe amepotosha kwa makusudi ya kulinda maslahi binafsi ya Urais wa 2015 kwa kuwa haiingii akilini kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama takwimu hizo yeye hajazisoma.

Kwa mujibu wa kitabu cha Hali ya Uchumi wa Taifa katika mwaka 2010 kilichotolewa na Wizara ya Fedha kukuwa kwa sekta ya kilimo kumeongezeka kwa 4.2% mwaka 2010 tofauti na asilimia 3.2% mwaka 2009. Lakini katika taarifa yake anadai kuwa uchumi wa vijijini ambako ndiko kwenye kilimo umekuwa kwa asilimia moja tu (flat lining).

Katika uchambuzi wake wa hali ngumu ya uchumi na mfumuko wa bei kama angelinganisha na nchi jirani angegundua kuwa mfumuko wa bei kwa Tanzania upo chini zaidi kwa asilimia 19 ukilinganisha na nchi zinazotuzunguka ambao mfumuko ni mkubwa zaidi mfano Ethiopia ni 30%.

Katika hali halisi ya maisha ya watanzania wa vijijini chakula chao hakitokani na pesa, wanakula vitu vingi ambavyo haviingii kwenye takwimu za uchumi mfano, kuku, mayai, maziwa, mihogo, viazi vitamu, nyama n.k. Hivyo vinaliwa bila kuingia kwenye mzunguko wa soko ndio maana hakuna mtanzania anayekufa njaa. Lakini nchi jirani wanakufa njaa na wanakimbia nchi zao kwa njaa. Mfumuko wa bei ni tatizo la Dunia nzima sio Tanzania peke yake.

Huyu ni mgombea Urais wa aina gani ambaye si mkweli kwa nchi yake, hasomi takwimu na anaropoka mambo ya ndani ya nchi hovyo hovyo duniani.

NAFIKIRI CCM WALIKUWA WANAJIBU KITU AMBACHO HAWANA UHAKIKA NACHO KWANI SIYO KWELI KWAMBA UCHUMI UNAKUWA KWA WALIONAZO NA MAFISADI AMBAO NI WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI? HIZO KUKU,NYAMA NA MAYAI WANAKULA WATANZANIA HAWA HAWA WASIO NA AJIRA AU WANAKULA VIGOGO WA SERIKALI NA WAFANYABIASHARA WAKUBWA HAINGII AKILINI UNIAMBIE MTU ASHINDWE KUNUNUA KILO YA MCHELE AWEZE KUNUNUA KILO YA NYAMA,NAJUA NI KWA JINSI GANI HIKI MNACHOKIONGEA MNA UHAKIKA NACHO MAANA MMEKUWA MKITUMIA UMASIKINI WAO KWA KUWAHONGA TSHIRT NA KHANGA PAMOJA NA MAFUTA YA KULA,KWANINI UNAONGELEA TABAKA LA JUU KWANINI USIONGELEE TABAKA LA CHINI AMBAO NDO WAPO WENGI, KWA HIYO MWENZIO AKIFANYA VIBAYA KWAKO LINAKUWA JEMA ETI ETHIOPIA MFUMUKO WA BEI UNAFIKA 30% KWANI ZITTO KAONGELEA ETHIOPIA AU TANZANIA? KWANI NI UONGO MFUMUKO WA BEI HAUJAKUWA KWA KASI? KWANI NI UONGO HALI YA MAISHA KWA MTAZANIA WA HALI YA CHINI SIYO MBAYA?




 
Swala la katiba ni CDM ndiyo waliolishikilia bango kabla ya uchaguzi na baada ya ya uchaguzi, leo hii wanadai ni wao ? kama ni wao mbona hawakuiweka katika ilani yao ya uchagu?Kuhusu elimu hapa dar tu wanafunzi bado wanakaa chini mikoani ndiyo kabisaa shule ina mwalimu mmoja,tukiingia shule za kata ndiyo zimkuwa vijiwe vyakupotezea muda hakuna walimu.Hivi hawajui hata kusoma alama za nyakati?
 
Acheni uongo na ndoto za mchana,hvi ilani ya ccm ilizungumzia katiba mpya?kama co cdm?
 
Wahenga wanasema:"USIMWAMSHE ALIYELALA" CCM imekwisha kulala tulifunike kabisa lisiamke!
 
Ngumi za CHADEMA balaa yaani ndani na nje ya nchi, hotuba ya Marekani wanahangaika kuijibu bado ya CHADEMA SQUARE,Mtwara na penginepo. Kwa kifupi wamechanganyikiwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom