Ufafanuzi mdogo juu ya mamlaka ya kamati kuu ya NEC kuteua wagombea ubunge bila mchakato wa kura ya maoni

Tatizo Vijana wa ccm waoga, tukatae huu ujinga haiwezekani mtu mmoja aendeshe chama bila vikao huu upuuzi,

kwa taarifa yako ccm mpya haitegemei wanachama wala nguvu ya hoja. Ccm mpya inategemea kofia ya mwenyekiti ya amiri jeshi mkuu. Na mwenyekiti wenu kwa kujua yeye au nyie wanachama wa ccm hamna uwezo wa kujenga hoja za kisiasa, ameamua kutunga sheria ya mfukoni ya kudhibiti vyama vya siasa. Na soon akina Kafulila, Katambi nk, watapata vyeo. Ww na wenzako mliokulia na kuzeekea ccm mtabaki kubeba mapanga kukata wapinzani, kupeleka viongozi kwa waganga nk.
 
Wadau tafadhali pitieni ufafanuzi kutoka CCM

*Kumekuwapo malumbano kwa baadhi ya watu kuhusu Mamlaka iliyotumia Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kufanya uteuzi wa Wagombea Ubunge katika Majimbo ya Kinondoni na Siha pasina kupitia mchakato wa Kura wa Kura ya Maoni.

Chama kinapenda kutoa ufafanuzi mdogo, kwamba uamuzi wa Kamati Kuu iliyoketi Mwezi Desemba 2017, Mjini Dodoma, umefanyika kwa mujibu wa Katiba, Kanuni ya Uchaguzi na Kanuni za Uteuzi wa Wagombea wa CCM katika Vyombo vya Dola.

Kanuni Za Uteuzi Wa Wagombea Wa CCM Kuingia Katika Vyombo Vya Dola (2010), Fungu la Tatu, Ibara ya 16 (2) Kanuni inasema, "Endapo, kwa sababu maalum, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa itaona kuwa hakuna haja ya kuitisha kura za maoni, hususan katika uchaguzi mdogo, itakuwa na uwezo wa kuelekeza kwamba zoezi la kura za maoni lisifanyike."

Kanuni hii haina mabadiliko na inasomeka hivyo hivyo katika Kanuni hii toleo la 2005 Fungu la Pili Ibara ya 10(2)*

Imetolewa na,

*IDARA YA ITIKADI NA UENEZI*
*CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)*
We mwandishi wa lumumba feki Nna maswali Naomba majibu?
1)Hivi ni Lini mlifanya mchakato wa kuchukua form na zilirudishwa lini?
2)maini ya kupiga kura za majimbo mlifanya lini?
3)lini huyo polepole alikaa na kamati kuu ya ccm ili kuwapitisha hao mliyowachagua...

Nasubiria majibu gamba

Ova
 
kwa taarifa yako ccm mpya haitegemei wanachama wala nguvu ya hoja. Ccm mpya inategemea kofia ya mwenyekiti ya amiri jeshi mkuu. Na mwenyekiti wenu kwa kujua yeye au nyie wanachama wa ccm hamna uwezo wa kujenga hoja za kisiasa, ameamua kutunga sheria ya mfukoni ya kudhibiti vyama vya siasa. Na soon akina Kafulila, Katambi nk, watapata vyeo. Ww na wenzako mliokulia na kuzeekea ccm mtabaki kubeba mapanga kukata wapinzani, kupeleka viongozi kwa waganga nk.
Huyó akipiga sim akisema tu wanafata tena bila kufata protokali

Ova
 
Wadau tafadhali pitieni ufafanuzi kutoka CCM

*Kumekuwapo malumbano kwa baadhi ya watu kuhusu Mamlaka iliyotumia Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kufanya uteuzi wa Wagombea Ubunge katika Majimbo ya Kinondoni na Siha pasina kupitia mchakato wa Kura wa Kura ya Maoni.

Chama kinapenda kutoa ufafanuzi mdogo, kwamba uamuzi wa Kamati Kuu iliyoketi Mwezi Desemba 2017, Mjini Dodoma, umefanyika kwa mujibu wa Katiba, Kanuni ya Uchaguzi na Kanuni za Uteuzi wa Wagombea wa CCM katika Vyombo vya Dola.

Kanuni Za Uteuzi Wa Wagombea Wa CCM Kuingia Katika Vyombo Vya Dola (2010), Fungu la Tatu, Ibara ya 16 (2) Kanuni inasema, "Endapo, kwa sababu maalum, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa itaona kuwa hakuna haja ya kuitisha kura za maoni, hususan katika uchaguzi mdogo, itakuwa na uwezo wa kuelekeza kwamba zoezi la kura za maoni lisifanyike."

Kanuni hii haina mabadiliko na inasomeka hivyo hivyo katika Kanuni hii toleo la 2005 Fungu la Pili Ibara ya 10(2)*

Imetolewa na,

*IDARA YA ITIKADI NA UENEZI*
*CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)*
Sasa hiyo sababu maalumu ni ipi zaidi ya kutekeleza makubalino mliyofikia na wahamiaji? Wanachama wa kupiga kura hawapo? Maana mngepeleka kwenye kura za maoni si ajabu wangekataliwa kama wale madiwani wahamiaji. Mkisema sababu maalumu muwaambie basi wanachama wajue au ndiyo sababu mlijitoa katika mpango wa kuendesha mambo kwa uwazi? You can not be trusted with your sababu maalumu. Kwanini wasi shindanishwe na wagombea wengine katika chama kama kweli wanakubalika?!
 
Wadau tafadhali pitieni ufafanuzi kutoka CCM

*Kumekuwapo malumbano kwa baadhi ya watu kuhusu Mamlaka iliyotumia Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM


Hivi wewe bwana ndiyo nilikuona kwenye mkutano wa CCM, sikumbuki wa Ikulu au Dodoma hivi karibuni?
 
Ww uko sahihi kabisa, wanaccm wote ni wajinga hakuna mwenye uwezo wa kuhoji chochote ili mradi ccm ipo madarakani basi. Chochote kifanywacho na uongozi ni kutii tu!!
Huyo ni mmoja wa yale majinga ambayo na yenyewe siyo CDM lakini kila siku kulalamika Mbowe kuwa mwenyekiti
 
Huyo ni mmoja wa yale majinga ambayo na yenyewe siyo CDM lakini kila siku kulalamika Mbowe kuwa mwenyekiti

Mkuu hebu rudia hii post yako kwa kiswahili chepesi maana kama ni ujumbe ndani ya box. Iweke vizuri ipate mchango mujarabu.
 
MAZWAZWA wanataka kutuzuga wakati ukweli unajulikana udikteta uchwara hadi kwenye chama ule utaratibu wa katiba kupata wagombea tupa kule!!!

Rushwa ni adui wa haki sitapokea wala kutoa rushwa! Wakati uchwara ndiye mgawa rushwa nchini nambari one.

Semeni mnatekeleza mlichowaahidi, kwani kuna shida gani kusema ukweli?
 
Hao wamenunuliwa na pamoja na malipo waliyopewa waliahidiwa kurudi tena na kupewa ubunge wao.
 
Nacheka sana yale yaliyokuwa yanasemwa juu ya upinzani juu ya mchakato wa kura za maoni leo ndio ccm wanayafanya vilevile....eti lowasa kahamia leo mmempa tiketi ya kuwania uraisi mara ohh chadema wanateua watu bila kura za maoni... leo ccm mnafanya nini sasa.. msitufanye wananchi mazuzu..
Si umeandikiwa vifungu vilivyotumika?
 
kwenye mradi wa pombe mngetoa maoni gani ?
fumbieni macho anayowatendea mtashtuka mmeshachafuka..
*mwenyekiti wa chama yeye
*mwenyekiti uvccm mpwa, heri
*katibu wa minoti wizara ya minoti, mpwa
*mkuu wa mkoa mwenye nguvu mukabila
*mkuu wa majeshi mukabila
*mkuu idara ya polisi mukanda
*mkuu idara ya uhamiaji mukanda
*manaibu mawaziri nishati mukanda
*jaji mkuu mukanda
*reli ya kisasa kuelekea mukanda wakati reli ya kaskazini imekufa kabisa
*hospitali ya kwanza ya rufaa kajenga mukanda
*uwanja wa ndege wa kwanza kajenga mukanda
*ziara nyingi mukanda
*teuzi yeye mwenyewe
ENDELEENI KULALA maana kupata akili ndani ya CCM ni sawa na tanzania kutoa manabii wasiwe wa uwongo !
 
Tumeshawazoea wazee wa short cut.
Mkizidiwa mnapita chocho, mnaibukia mbele.

Mradi kufika, wacheni waende, kwani kuna shida gani? Bora wao wabunge, wengine walipata mgombea urais kwa kusema ndiooooooo! Shamba la bwana heri, mbuzi wa bwana heri
 
Back
Top Bottom