UFAFANUZI: Kisandu sio Ukoo wangu na halikuwa jina Langu kiukoo na ndio maana Ukoo wa Kisandu haufanani kisura nami DJ. Don Nalimison

Hueleweki kabisa,yaani unajikanyaga na kujirudisha wewe mwenyewe
Mwaka 2017 uliandikaje?
Kuwa baba ako ni msukuma na alikuwa Dj Arusha,au unadhani tumesahau?
Huyu anaekataa kuwa jina kisandu sio lake ni yupu maana namfahamu kama ni huyo baba yake alikuwa DJ kisandu anaitwa mashaka kisandu uandishi wa habari kasoma na alikuwa anaishi kigamboni dar kwa mama kadete ambae sasa ni marehemu pia bibi huyo ni mama yake mdogo na baba yake mzee kisandu

DJ pia huyu kijana juzi tu alikuwa kivule dar kwa shangazi yake na kama anasema yuko dar kama ni yeye lazima atakuwa huko kivule nakama sio huko atakuwa mbezi kwa dada yake au kibaha naomba anibishie na ameshawahi kuwa mwalimu wa sekondari huko mwanza akapata mgogoro wa kisiasa akafutwa kazi sasa anaimba bongo freva
 
Huyu anaekataa kuwa jina kisandu sio lake ni yupu maana namfahamu kama ni huyo baba yake alikuwa DJ kisandu anaitwa mashaka kisandu uandishi wa habari kasoma na alikuwa anaishi kigamboni dar kwa mama kadete ambae sasa ni marehemu pia bibi huyo ni mama yake mdogo na baba yake mzee kisandu DJ pia huyu kijana juzi tu alikuwa kivule dar kwa shangazi yake na kama anasema yuko dar kama ni yeye lazima atakuwa huko kivule nakama sio huko atakuwa mbezi kwa dada yake au kibaha naomba anibishie na ameshawahi kuwa mwalimu wa sekondari huko mwanza akapata mgogoro wa kisiasa akafutwa kazi sasa anaimba bongo freva

Kumbe ni ndugu yenu keshakua mwehu tayari
 
Huyu anaekataa kuwa jina kisandu sio lake ni yupu maana namfahamu kama ni huyo baba yake alikuwa DJ kisandu anaitwa mashaka kisandu uandishi wa habari...
Mkuu kama unamfahamu kiasi hicho basi chukua hatua kufuatilia kwa ndugu zake huyu mtu apelekwe mirembe. Kila siku zinavyoenda anazidi kudata.
 
Mkuu kama unamfahamu kiasi hicho basi chukua hatua kufuatilia kwa ndugu zake huyu mtu apelekwe mirembe. Kila siku zinavyoenda anazidi kudata.
TANZANIANS Citizens are too much insane. If you present True fact they ignore fact and they appreciate False Fact.
 
Salaam wapendwa katika Malaika wa Mungu na Mungu Mkuu mwenye nguvu.

Wengi wamekuwa wakiniuliza Sana kuhusu ubini wa KISANDU inbox, naomba leo ni jibu.

Baba yangu Mzazi alipoondoka kurudi kwao Marekani alinikabidhi kwa rafiki yake Abdalah Kisandu pale Kahama, SHINYANGA na hivyo Ukoo wa Abdalah Kisandu wakamshauri mama yangu na NDugu zake kuniwekea ubini wa KISANDU kwakuwa wamepewa jukumu la kunilea DJ. DON NALIMISON maana baba yangu hayupo Tena Nchini.

Hivyo tukawa NDugu na Ukoo wa KISANDU pale KAHAMA. Abdalah yeye alikuwa fundi radio tu. Iliibuka mgogoro mwaka 1988 Bwana Abdalah akilaumuwa kupokea mtoto wa mnegro bila IDHINI ya Ukoo wa KISANDU. Kutokana na Hilo nilihamishiwa kijijini kwa baba wa mama yangu na huko nikaanza shule ya msingi 1990 huku nikitumua jina la ubini wa Ukoo wa KISANDU.

Hata hivyo baada ya kumaliza elimu ya msingi jina(Mashaka Kisandu) nililokuwa natumia shule ya msingi akapewa NDugu wa Ukoo wa KISANDU. Nanikazuiwa kulitumia kwa kuwa Mimi sio Ukoo wao. Ndipo nikaanza kutumia jina la ubatizo(DEOGRATIUS, yaani DEOGRATIUS Kisandu) nikiwa Magu Secondary 1997 Walimu wakanizuia kabisa kutumia jina la Kisandu, niliwaambia Ni jina Langu wao wakaniambia tumia jina la baba yako Mzazi achana na Ukoo wa watu watakutaifisha Hilo jina. Nilimwambia Mkuu wa shule baba yangu ndio Ni Raia wa Marekani akija nitamwambia.

Mwaka 1998 baba yangu alirudi TANZANIA nikamweleza kuhusu navyo pata shida ya Ukoo alioniacha. Wakati huo baba yangu nilimjua kwa jina moja tu Curtis. Mzee aliniambia kwakuwa umeandikishwa shule kwa ubini wao wa KISANDU hamna shida hivyo endelea na asikutishe mtu Ila jina Langu liko kwenye Cheti chako Cha Clinic siku yako ya kuzaliwa.

Ukimaliza sekondari takuja nikuchukue uhamie nyumbani(Marekani USA) na nitakuapisha mahakamani na utaanza kutumia jina la Ukoo wako Sasa. Nilipotoka kwa Padre Ricardo Morogoro April 1999 ambako niliishi utawani kwa takribani miezi 8tu nikaingia Kishimba Secondary school KAHAMA SHINYANGA. Ndipo nikaweka jina "Pio" katikati yaani DEOGRATIUS PIO KISANDU nikiwa na lengo baadae nije niwaachie majina yao Ukoo wa KISANDU na Mimi kuwa Pio iliniepuke mgogoro wa majina. Bahati nzuri Padre mmoja alikuwa Mzee Sana (Padre Manoja) akaniambia tumia jina la baba yako akimanisha "NALIMI" ili uachane na hiyo Kisandu yao pia hiyo Pio, mapadre wa fransisikani watakuvurugia maana Ni jina la mtakatifu wao wa Italia (Padre Pio).

Niligoma kabisa. Nilimaliza shule mpaka vyuo kwa jina Hilo. Kumbe Ukoo wa wenye jina la Kisandu wakaunda NDugu yao wakamwita DEOGRATIUS Kisandu hasa kipindi nilipotangaza kugombea Urais wa Tanzania Aug-sept 2012. Nikiwa Katibu wa Bavicha(CHADEMA) mkoa wa Tanga. Lengo ikiwa nikunizima nisitumie ubini wao huo. Tanga nilikuwa mgeni na walipojua huo mgogoro nao wakaona ndio njia yakujipatia vyeo.

Niliwasiliana na Mzee wangu nikamwambia nikaape mahakamani akanikubalia kuondoa Kisandu tu. Sasa nikawa najiuliza jina nimelipromoti halafu nimesomea then niwaachie? Baba yangu aliniambia nisijali. Mimi nikaapa nikaondoa Pio nikaweka jina la baba "NALIMI", (DEOGRATIUS NALIMI KISANDU),Mzee nilipomueleza aliniambia toa kabisa hiyo Kisandu maana ameshajua Kuna mchezo mchafu unachezwa na Ukoo wa KISANDU ili kuniharibia kwa kuwa naonesha njia ya kwenda pa zuri. Mimi sikusikia.

Mwaka feb 2017 baada ya kutoka lokapu ya Polisi Mwanza nilipokamatwa kwa tuhuma ya kuzusha ushoga. Nilipotoka nilimpigia baba kwa laini maalum isiyo trakiwa. Akaniambia achana na jina lao kata passport ya kusafiria njoo nyumbani USA uungane na wenzako na ukifika takupeleka kwa Wanasheria kuapa. Nilimwambia sawa.

Bahati mbaya nikafungwa mwaka 2018 na nilipotoka gerezani Juni 2020 nilibadili jina Mara moja na kuachana kabisa na jina linaloitwa Kisandu. Ndipo nikajibatiza mwenyewe " NALIMISON" nikitohoa kutoka jina la baba yangu la NALIMI. Hivyo nikaua jina utotoni(Mashaka) na nikaua jina la ubatizo (DEOGRATIUS) na Mimi nikatengeneza jina moja(DON NALIMISON). NDugu zangu USA nilipowapa taarifa walifurahi Sana hasa walipoipata Deed Poli ya wakili nilipofanyia marekebisho.

Walinipongeza na kusema Sasa "simamia hapohapo na wakikuvurugia tutatumia CIA kukuokoa maana Hilo ndilo jina lako rasmi". Ukifika Marekani utaendelea hivyo hivyo. Niliwafahamisha NDugu upande wa mama yangu hapa Kahama SHINYANGA, wengine waliunga mkono na wengine walipinga. Mama aliambiwa anipinge lakini NDugu zangu Nchini Marekani waliniambia niwapuuze wote wanaonipinga.

Kwa kifupi kila Jambo Langu nalotumia Ni hili jina Langu DJ. DON NALIMISON. Hivyo, NALIMISON sio baba yangu Bali Mimi ndio jina Langu. Don niongezeko la kunyambulisha jina Langu na kuliboresha kuwa na hadhi ya Kimataifa. Baba yangu Ana baki kuwa "NALIMI" Kazi yangu Ni Mwanamuziki. Sitegemei kupokea baba wa kubumba TANZANIA Wala kutumia Tena majina ya Kitanzania kwani yamenidharirishia utu wangu.

DJ. DON NALIMISON
14 OKT, 2021.

Aksante kwa kunielewa

View attachment 1973973
Mental state assessment:
-Flight of ideas
-Delusions of grandiosity
-Loosening of associations
-Tangential speech
-Persecutory delusions

Hivi huyu jamaa hana ndugu au marafiki wa karibu wamsaidie?
 
Kipindi hicho kahama wanamfagilia balsa mwanamziki mtoto WA Dandu maana anko yake aliyekuwa WA jina Hilo alikuwa akiishi Kahama

Jamaa mmoja mrefu mpenda miwani

Mwana AICT

UKAME WA MAJI MNAAMKA USIKU KICHOTA MAJI. NYIE HAYA MAISHA HAYA
Daah we jamaa hapa naamini huenda tunafahamiana, huyo Dandu nimefanya nae sana biashara za vifaa vya umeme miaka hiyo.

Sent from my M2006C3LI using JamiiForums mobile app
 
Hueleweki kabisa,yaani unajikanyaga na kujirudisha wewe mwenyewe.

Mwaka 2017 uliandikaje?

Kuwa baba ako ni msukuma na alikuwa Dj Arusha,au unadhani tumesahau?
nasikia amewahi ku advocate haki yake ya kutifuliwa suez canal ndipo polisi wakamdaka,
 
Back
Top Bottom