UDSM ni chuo dhaifu sana Afrika "Aibu kwa nchi"

hayaland

JF-Expert Member
May 4, 2012
712
399
Chuo kikuu cha DAR ES SALAAM pamoja na kuwa ni chuo chenye kuchukua wanafunzi waliofaulu zaidi mitihani ya kidato cha Sita na baadhi ya wanafunzi kukilaumu chuo hicho kuwa na urasimu na upendeleo wa wazi kwa baadhi ya wanafunzi bado ni chuo kilicho nyuma sana miongoni mwa vyoo vikuu barani Africa.

Baadhi ya viongozi wa kitaifa kupitia chuo hiki kuna haja ya kufanyà kila linawezekana kubadilisha hali hii na kujua chanzo cha kukifanya chuo hiki kubakia kuwa chuo dhaifu kwa utoaji wa elimu miongoni mwa vyoo barani Afrika.

Kama wadau mnafikiri nini chanzo cha chuo chetu kubakia kuwa nyuma barani AFRICA na Africa mashariki na kati?

Ingia mtandaoni utaona tuko nafasi ya ngapi. Tuko nafasi ya 36 kwa mwaka 2018-2019
 
Hoja yako ingekuwa na mashiko kama zamani kilikuwa nafasi za juu, kikashuka, au kwa vile UDSM, kilikuwa chuo kikuu cha kwanza Tanzania, sasa kimepitwa na vyuo vingine vikuu vilivyoanzishwa. Ukisema UDSM imeshika nafasi ya 36, unapaswa kusema kati ya ngapi, mfano hata kwenye football ranking ya Tanzania ni nafasi ya 36, lakini bado tunajivunia, na tumechanga zaidi ya milioni 300 jana kuwamotisha vijana wetu.

Kwenye GDP, Tanzania ni nchi tajiri kwenye top ten barani Africa, tukuchukua the top ten richest, Tanzania ndio ya mwisho.

Hivyo usikisimange chuo chetu, UDSM is still the best in TZ despite all the odds.
P
 
Udsm zamani kidogo miaka ya 2009 ndo kilikuwa tano bora kwenye ranking ya vyuo vikuu vya kusini kwa jangwa la sahara, hapo nakumbuka ilifuata SUA 22, ikafuata Mzumbe 39 na IFM 74,

Lakin tokea 2013 nimekuwa nafuatilia index hizo udsm inacheza 27+ hivi vingine kwenye 200+
 
Kweli kabisa, hata maabara zao zipo hoi, wanafanyiana urasmu kununua vifaa vipya vya ufundishaji. Mechanical dept. Nazi zina mashine nzee kiasi cha kufanya wanafunzi wasiwe wabunifu. Chuo kimebaki na wanahabari na wanasheria kwwnye sayansi wanazidiwa hata arusha tech
 
Chuo kikuu cha DAR ES SALAAM pamoja na kuwa ni chuo chenye kuchukua wanafunzi waliofaulu zaidi mitihani ya kidato cha Sita na baadhi ya wanafunzi kukilaumu chuo hicho kuwa na urasmu na upendeleo wa wazi kwa baadhi ya wanafunzi bado ni chuo kilicho nyuma sana miongoni mwa vyoo vikuu barani Africa.Baadhi ya viongozi wa kitaifa kupitia chuo hiki kuna haja ya kufanyà kila linawezekana kubadilisha hali hii na kujua chanzo cha kukifanya chuo hiki kubakia kuwa chuo dhaifu kwa utoaji wa elimu miongoni mwa vyoo barani Afrika.Kama wadau mnafikiri nini chanzo cha chuo chetu kubakia kuwa nyuma barani AFRICA na Africa mashariki na kati? Ingia mtandaoni utaona tuko nafasi ya ngapi.Tuko nafasi ya 36 kwa mwaka 2018-2019
chanzo ni CCM
 
Udsm zamani kidogo miaka ya 2009 ndo kilikuwa tano bora kwenye ranking ya vyuo vikuu vya kusini kwa jangwa la sahara, hapo nakumbuka ilifuata SUA 22, ikafuata Mzumbe 39 na IFM 74,

Lakin tokea 2013 nimekuwa nafuatilia index hizo udsm inacheza 27+ hivi vingine kwenye 200+
Mkuu tutake radhi wana SUA, hatujawahi toka nje 100.

Halafu mshaurini Mzee Meko aache kuwaondoa wakufunzi vyuoni maana hilo ndio limepelekea chuo kama UDSM kushuka kila mwaka...

Kwa sasa naona UDSM iko nafasi ya 44 na SUA ni 101...
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom