MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Leo nimepata habari za kusikitisha. Kuna shemeji yangu, anasomea Masters yake huko UDSM, zahama anazozikabili, kwa kweli, kama angekuwa mtu mwenye "munkari" wala asingemaliza masomo yake...
Taarifa nilizonazo ni kwamba, baada ya kumaliza Bachelors yake hapo UD alifanya kazi kama Graduate Teaching Assistant (wengine wanasema Assistant Lecturer-Trainee). Aliifanya kazi yake hiyo kwa ufanisi mkubwa, na kwa kuwa aligraduate top of his class, basi, kupata full academic scholarship (international) haikuwa ngumu sana kwake na wenzake. Siwezi kutaja yuko idara gani, kwa kuhofia yeye kufikwa na madhara ambayo yanaweza kuhatarisha mustakabali wake hapo UD.
Kimsingi ni kwamba, masurufu yake na wenzake, shemeji yangu huyu, yanatoka nje... siwezi kutaja nchi gani pia... lakini yanapitia mkono wa UD... na kumbukeni, hapo kuna "watu". Pesa ni shetani, ukiipitishia mkononi mwa mtu itapigwa panga.... na kweli, panga linapita hapo, mpaka fungu linapowafikia wanazuoni hao, linakuwa dogo kiasi cha kukatisha tamaa.
Wenyewe hawawezi kusema ukweli - kwa kuwa wahadhiri, wanaomega fungu hilo ndio wenye kushika mpini, wakati wanazuoni wameshika makali - kwani wakithubutu kulalamika, habari zitarudi UD, na wao watakuwa wamejiweka kwenye tafrani ya kunyimwa hata vyeti vyao, kwa kufelishwa mitihani MAKUSUDI!
Ninachouliza, hawa wahadhiri wanataka nini? Maisha yenyewe haya ni ya shida. Wanazuoni wamesoma, kwa shida, wamefaulu, wanastahili kupewa mafungu yao kwa asilimia 100! Wahadhiri wanalipwa mishahara lukuki, lakini wana tamaa kupita kiasi. Fedha za ufadhili zinatumwa kwa matumizi ya wanazuoni, hususan wanapofanya utafiti kwa ajili ya Shahada zao za Uzamili (Masters).
Je, hili, pamoja na lile za "maksi za chupi" yatakwisha lini?
Jamani, huu si ufisadi huu?
Kazi kwenu!
./Mwana wa Haki
NA BADO, ntasema zaidi.... vitisho havintishi.... kwani kufa si WAJIBU tu? Niogope? Nyoooooooooooo!
Taarifa nilizonazo ni kwamba, baada ya kumaliza Bachelors yake hapo UD alifanya kazi kama Graduate Teaching Assistant (wengine wanasema Assistant Lecturer-Trainee). Aliifanya kazi yake hiyo kwa ufanisi mkubwa, na kwa kuwa aligraduate top of his class, basi, kupata full academic scholarship (international) haikuwa ngumu sana kwake na wenzake. Siwezi kutaja yuko idara gani, kwa kuhofia yeye kufikwa na madhara ambayo yanaweza kuhatarisha mustakabali wake hapo UD.
Kimsingi ni kwamba, masurufu yake na wenzake, shemeji yangu huyu, yanatoka nje... siwezi kutaja nchi gani pia... lakini yanapitia mkono wa UD... na kumbukeni, hapo kuna "watu". Pesa ni shetani, ukiipitishia mkononi mwa mtu itapigwa panga.... na kweli, panga linapita hapo, mpaka fungu linapowafikia wanazuoni hao, linakuwa dogo kiasi cha kukatisha tamaa.
Wenyewe hawawezi kusema ukweli - kwa kuwa wahadhiri, wanaomega fungu hilo ndio wenye kushika mpini, wakati wanazuoni wameshika makali - kwani wakithubutu kulalamika, habari zitarudi UD, na wao watakuwa wamejiweka kwenye tafrani ya kunyimwa hata vyeti vyao, kwa kufelishwa mitihani MAKUSUDI!
Ninachouliza, hawa wahadhiri wanataka nini? Maisha yenyewe haya ni ya shida. Wanazuoni wamesoma, kwa shida, wamefaulu, wanastahili kupewa mafungu yao kwa asilimia 100! Wahadhiri wanalipwa mishahara lukuki, lakini wana tamaa kupita kiasi. Fedha za ufadhili zinatumwa kwa matumizi ya wanazuoni, hususan wanapofanya utafiti kwa ajili ya Shahada zao za Uzamili (Masters).
Je, hili, pamoja na lile za "maksi za chupi" yatakwisha lini?
Jamani, huu si ufisadi huu?
Kazi kwenu!
./Mwana wa Haki
NA BADO, ntasema zaidi.... vitisho havintishi.... kwani kufa si WAJIBU tu? Niogope? Nyoooooooooooo!