UDSM chapinga kudahili vilaza, NACTE pia waipinga TCU

Hata hivyo UDSM hakuna vilaza, ndio maana wao tu ndio wamenyoosha mkono na kupinga. vyuo vyenye vilaza vimeinamisha nyuso zao chini kwa aibu na woga.
unakanusha kwa maneno au kwa kukupeleka vyeti vihakikiwe,, tuliwahi siku nyingi humu kusema kuhusu udahili wa hovyo unaofanywa hapo udsm tukatukanwa leo ukwel uko adharani ..waache maneno wapeleke vyeti & then wakishahakikiwa watoke hadharani waseme .
 
hii ni aibu mpya kwa udsm sasa inashukiwa kuwa na w2 wengi wasiokua na sifa kuliko hata vyuo walivyoviita vya kata.
 
Kuna washona cherehani hapo eti textile engineering nakumbuka mwaka 2014 walichukuliwa hadi wenye daraja la nne,jamaa yangu alipoomba chaguo la kwanza alitemwa kwenye vyuo kama DIT,MUST na vingine akaomba hapo akapata na four yake, mimi huwa namuita kilaza kila siku japo yeye ananiambia kuna four wenzake wapo nao.
Labda sijui tafsiri ya kilaza naomba unieleweshe pia uje uwasafishe hao washona cherehani.
ulishasema ni fundi sherehani, sasa unataka achukuliwe mwenye division one kwenda kusomea ufundi cherehani!
Tatizo lake huyo dogo alijiona kipanga akaomba kozi tofauti na ufundi chelehani hapo DIT. kama angeomba ufundi cherehani, asingekosa. ufaulu wake ulikua ni wakusomea ufundi cherehani au kwenda upolisi.
JIULIZE
kwanini UDSM hawakumchagua ktk kozi ya maana kama CIVIL ENG. badala yake wakamchagua ktk kozi ya UFUNDI UCHEREHANI?
 
unakanusha kwa maneno au kwa kukupeleka vyeti vihakikiwe,, tuliwahi siku nyingi humu kusema kuhusu udahili wa hovyo unaofanywa hapo udsm tukatukanwa leo ukwel uko adharani ..waache maneno wapeleke vyeti & then wakishahakikiwa watoke hadharani waseme .
Cha kwanza ni kukanusha uzushi na kuomba umma upuuze uzushi huo wa TCU. Hatua kali zitachukuliwa dhidi ya hao wazushi
 
mtu akiwa mwaka wa tatu, kafaulu semester zote, huyo sio kilaza. tena wanamkosea heshima kusema hana sifa. wasio na sifa ni wale waliodisco.

kosa lilishafanyika na kwasasa busara itumike kwa hili. kama ni kilaza, basi angalia matokeo yake ya chuo, kilaza haana uwezo ya kumudu madesa yaa chuo.


Siku hizi kila mtu anatamani kuonekana amebuni kitu kipya ili aonekane anampendeza baba mwenye nyumba.Bahati mbaya sana kila wanalokuja nalo daah mpaka aibu.Kaja mtu na madawa ya kulevya,mara mashoga nk.Hata wa wale wa bodi ya mkopo wamekuja na asilimia 15,bila kujali take home ya mtu.Kuna jamaa alijikuta anarudi na 90,000 tu katika mshahara wake.Nikweli bodi watakuwa wamepata hela yao,familia kilio,je ufanisi kazini itakuwaje? atafanya kazi huyo? yaani ni shida tupu.
Mimi naangalia hata wabunge wetu nao sijui.
 
Siku hizi kila mtu anatamani kuonekana amebuni kitu kipya ili aonekane anampendeza baba mwenye nyumba.Bahati mbaya sana kila wanalokuja nalo daah mpaka aibu.Kaja mtu na madawa ya kulevya,mara mashoga nk.Hata wa wale wa bodi ya mkopo wamekuja na asilimia 15,bila kujali take home ya mtu.Kuna jamaa alijikuta anarudi na 90,000 tu katika mshahara wake.Nikweli bodi watakuwa wamepata hela yao,familia kilio,je ufanisi kazini itakuwaje? atafanya kazi huyo? yaani ni shida tupu.
Mimi naangalia hata wabunge wetu nao sijui.
inauma sana, hizi namba tunazosomeshwa zimeanza kukera
 
ulishasema ni fundi sherehani, sasa unataka achukuliwe mwenye division one kwenda kusomea ufundi cherehani!
Tatizo lake huyo dogo alijiona kipanga akaomba kozi tofauti na ufundi chelehani hapo DIT. kama angeomba ufundi cherehani, asingekosa. ufaulu wake ulikua ni wakusomea ufundi cherehani au kwenda upolisi.
JIULIZE
kwanini UDSM hawakumchagua ktk kozi ya maana kama CIVIL ENG. badala yake wakamchagua ktk kozi ya UFUNDI UCHEREHANI?
Kama umekiri kuwa mafundi cherehani ni vilaza basi kubali kuwa UDSM vilaza wapo mana wanafunzi wa textile engineering ni sehemu ya UDSM over.
 
:’Kuchezea elimu ya Tanzania ni hatari zaidi ya dawa za kulevya’ -Bashe

Moja ya habari kubwa hivi sasa Tanzania ni pamoja na hatua ya Serikali kupitia TCU kutoa orodha ya majina ya baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu wasio na sifa za kuwa wanafunzi wa vyuo.

Badhi ya watu na taasisi mbalimbali kikiwemo chuo kuku Dar es salaam UDSM kilichoikataa orodha hiyo. Kwenye Exclusive interview ya Ayo TV na millardayo.com tunaye Mbunge wa Nzega mjini Hussein Bashe ambaye na yeye ametoa ya moyoni baada ya kuiona taarifa hiyo huku akisisitiza kuwa Serikali imefanya makosa.

Bashe amesema…>>>’Tunatatizo kubwa la mfumo wa elimu kwenye nchi yetu, toka nimekuwa na ufahamu na kufuatilia mambo nimeona kila Waziri amekuwa akija na movie yake, ukijiuliza swali nani aliwadahili hawa wanafunzi jibu ni TCU‘ –Hussein Bashe

‘Leo mwanafunzi amekaa chuoni na katumia gharama nyingi achilia mbali matarajio yake aliyojiwekea na familia yake alafu unaenda kuzima mshumaa wake, tujiulize mara ya kwanza wakati wanadahiliwa walikuwa na sifa alafu sasa hawana sifa?‘ –Hussein Bashe

‘Hii inatafsiri kwamba mfumo wetu wa elimu unatatizo kubwa lakini la pili wakati unawaadhibu wanafunzi hao kwa kuwaita hawana sifa aliyewadahili umewachukulia hatua gani? leo chuo kikuu Dar es salaam wametofautiana na TCU na umeona‘ –Hussein Bashe

‘Mimi nasema kama Mbunge kwamba hili jambo la kuchezea elimu ya nchi hii ni hatari mno kuliko hata dawa za kulevya, kuifanya elimu hii kama ni sehemu ya kuifanyia majaribio ni hatari‘ –Hussein Bashe

‘Tumekuwa ni watu wa kusukumwa na matukio, Moja kati ya mtu aliyekuwa nilikuwa na matarajio makubwa sana kwenye nchi hii ni Profesa Joyce Ndalichako lakini siku zinavyokwenda naona kama anashusha viwango vya elimu ya Tanzania huyu ni mama ninayemuheshimu lakini kwa hili hatuwezi kucheza na elimu ya nchi hii‘ –Hussein Bashe

‘Mimi nataka nitumie fursa hii kumweleza Rais Magufuli kwamba anakila sababu ya kuwatazama watendaji wake aliyowaamini, anaweza kuwa na nia njema pamoja lakini chakutazama ni je, amewapa watu sahihi kwenye hizo nafasi?‘ –Hussein Bashe

Vipi kuhusu TCU kudaiwa kutaja majina ya wanafunzi ambao hawapo vyuoni? Bashe amesema>>’Hii inaleta tafsiri kwamba ukurupukaji uliopo ndani ya Serikali, hakuna lugha nyingine unaweza tumia na suala la kudahili ni kazi ya vyuo na TCU wao wanafanya kazi ya udalali na ni mambo ya kukurupuka‘ –Hussein Bashe
 
Kama umekiri kuwa mafundi cherehani ni vilaza basi kubali kuwa UDSM vilaza wapo mana wanafunzi wa textile engineering ni sehemu ya UDSM over.
UDSM hawajawahi kua na vilaza hata mwaka mmoja. kama wagekua wanapokea vilaza, basi Jesca Kilaza (yule mtoto wa dakitari) asingekimbilia shamba la bibi, wakati baba, mama na familia yake kwa ujumla walikua wanaishi Dar. Angejiunga UDSM.
mwaka 2014 ulioutaja wewe, aliepata alama D mbili ambapo alama D ilianzia Makasi 30, alikua na sifa ya kwenda chuo kikuu kwa mujibu wa TCU, japo kwa mujibu wa NECTA alikua na division 4. NECTA walisema principal pass ni kuanzia alama C iliyokua inaanzia maski 40,TCU wao wakashusha mpaka alama D ili wapate wanafunzi. hivyo basi, hao mafundi cherehani waliokwenda UDSM mwaka huo kwakua walikua na vigezo vya kwenda chuo kikuu. hata hivyo, pamoja na kua walikua na vigezo, vigezo vyao havikufua dafu ktk kushindania programs za maana, ndio maana wakajikuta wanaangukia kwenye ufundi cherehani.
 
:’Kuchezea elimu ya Tanzania ni hatari zaidi ya dawa za kulevya’ -Bashe

Moja ya habari kubwa hivi sasa Tanzania ni pamoja na hatua ya Serikali kupitia TCU kutoa orodha ya majina ya baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu wasio na sifa za kuwa wanafunzi wa vyuo.

Badhi ya watu na taasisi mbalimbali kikiwemo chuo kuku Dar es salaam UDSM kilichoikataa orodha hiyo. Kwenye Exclusive interview ya Ayo TV na millardayo.com tunaye Mbunge wa Nzega mjini Hussein Bashe ambaye na yeye ametoa ya moyoni baada ya kuiona taarifa hiyo huku akisisitiza kuwa Serikali imefanya makosa.

Bashe amesema…>>>’Tunatatizo kubwa la mfumo wa elimu kwenye nchi yetu, toka nimekuwa na ufahamu na kufuatilia mambo nimeona kila Waziri amekuwa akija na movie yake, ukijiuliza swali nani aliwadahili hawa wanafunzi jibu ni TCU‘ –Hussein Bashe

‘Leo mwanafunzi amekaa chuoni na katumia gharama nyingi achilia mbali matarajio yake aliyojiwekea na familia yake alafu unaenda kuzima mshumaa wake, tujiulize mara ya kwanza wakati wanadahiliwa walikuwa na sifa alafu sasa hawana sifa?‘ –Hussein Bashe

‘Hii inatafsiri kwamba mfumo wetu wa elimu unatatizo kubwa lakini la pili wakati unawaadhibu wanafunzi hao kwa kuwaita hawana sifa aliyewadahili umewachukulia hatua gani? leo chuo kikuu Dar es salaam wametofautiana na TCU na umeona‘ –Hussein Bashe

‘Mimi nasema kama Mbunge kwamba hili jambo la kuchezea elimu ya nchi hii ni hatari mno kuliko hata dawa za kulevya, kuifanya elimu hii kama ni sehemu ya kuifanyia majaribio ni hatari‘ –Hussein Bashe

‘Tumekuwa ni watu wa kusukumwa na matukio, Moja kati ya mtu aliyekuwa nilikuwa na matarajio makubwa sana kwenye nchi hii ni Profesa Joyce Ndalichako lakini siku zinavyokwenda naona kama anashusha viwango vya elimu ya Tanzania huyu ni mama ninayemuheshimu lakini kwa hili hatuwezi kucheza na elimu ya nchi hii‘ –Hussein Bashe

‘Mimi nataka nitumie fursa hii kumweleza Rais Magufuli kwamba anakila sababu ya kuwatazama watendaji wake aliyowaamini, anaweza kuwa na nia njema pamoja lakini chakutazama ni je, amewapa watu sahihi kwenye hizo nafasi?‘ –Hussein Bashe

Vipi kuhusu TCU kudaiwa kutaja majina ya wanafunzi ambao hawapo vyuoni? Bashe amesema>>’Hii inaleta tafsiri kwamba ukurupukaji uliopo ndani ya Serikali, hakuna lugha nyingine unaweza tumia na suala la kudahili ni kazi ya vyuo na TCU wao wanafanya kazi ya udalali na ni mambo ya kukurupuka‘ –Hussein Bashe
huyu jamaa hakawiagi. napenda sana alivyo mkweli. hana ile hali ya kukurembaremba na kusifia pumba.
kosoa mheshimiwa ili wajirekebishe, sio kupiga meza na kusema ndiooooooo_O
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Huyu ndiye mbunge pekee ndani ya MACCM aliyebaki na heshima kwenye jamii ya Watanzania wanaojitambua wengine wote ni wapiga madili tu.

huyu jamaa hakawiagi. napenda sana alivyo mkweli. hana ile hali ya kukurembaremba na kusifia pumba.
kosoa mheshimiwa ili wajirekebishe, sio kupiga meza na kusema ndiooooooo_O
 
Kuna washona cherehani hapo eti textile engineering nakumbuka mwaka 2014 walichukuliwa hadi wenye daraja la nne,jamaa yangu alipoomba chaguo la kwanza alitemwa kwenye vyuo kama DIT,MUST na vingine akaomba hapo akapata na four yake, mimi huwa namuita kilaza kila siku japo yeye ananiambia kuna four wenzake wapo nao.
Labda sijui tafsiri ya kilaza naomba unieleweshe pia uje uwasafishe hao washona cherehani.
We jamaa sio mzima kichwani, textile engineering wachukue div 4 hebu punguza chumvi mkuu.

Kozi yoyote inayoitwa engineering ukitaka kuisoma lazima unywe maji kwanza
 
muda ni shaidi mzuri tusubiri tutapeana mrejesho.
Hakuna lolote, katika awamu tuliyowahi kua na watu wakurupukaji ni awamu hii peke yake, hasa huyu Ndalichako sijui PhD yake kama ni halali.

Nakupa mfano: Mimi kuna jamaa yangu wakati nasoma UD alikua roommate wangu, jamaa yuko vizuri upstairs alikua anasoma geology engineering na vyeti vyake viko clean kabisa cha ajabu TCU wanamtoa kwenye majina kwamba hana sifa, kufatilia wanasema alionekana kua kuna kipindi alipata admission chuo cha nje.
Sasa hivi sio vituko yaani TCU ilishindwa kujua hili hata kwa kupitia chuo ili wajue kama jamaa yuko UDSM au yuko nje?

Mfano mwingine; watu wengi waliotajwa ni foreigners kutoka Rwanda, Burundi, Mozambique etc
Hawa wametajwa kisa kwenye system ya Necta matokeo yao ya form 4 hayaonekani, yaani TCU wanashindwa kujua kama UDSM imedahili wanafunzi kutoka nje ya Tanzania eti wanafikiria kila mtu ni lazima apatikane kwenye database ya Necta, huu sio upuuzi?
Hawa watu wakati wanaomba vyuo walileta documents zao kibao na TCU wakaridhika nazo sasa leo imekuaje wakose sifa tena wengi wao wamehitimu mwaka jana
 
16836687_1367829649954050_2152111161348238515_o.jpg
SIKU moja baada ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kutangaza utata wa udahili wa wanafunzi wa vyuo vikuu, wadau wakubwa wa elimu, wamejitokeza kupinga hatua hiyo. Wadau hao ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Baraza la Vyuo vya Ufundi Tanzania (NACTE).

Taarifa ya UDSM Kwa upande wake, UDSM kimeeleza kwamba hakuna mwanafunzi hata mmoja aliyedahiliwa chuoni hapo, ambaye hana sifa za kujiunga na chuo hicho.

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Florens Luoga aliliambia gazeti hili jana kuwa chuo hicho kimeweka utaratibu ambao unaweza mwanafunzi yeyote anayedahiliwa chuoni hapo, awe na sifa zinazohitajika kwa kuwa hawafanyi biashara.

“Sisi hapa ni wakali kuhusu jambo hilo, tukibaini kuwepo kwa mwanafunzi ambaye hana sifa tunamfukuza. Hatusubiri TCU iseme...hata tukibaini kuwa mtu alifanya udanganyifu na alishamaliza chuo, lakini hakuwa na sifa, tunamnyang’anya digrii tulivyompa,” alisema Profesa Luoga na kuongeza:

“Hiki ni chuo, hatufanyi biashara, sisi kazi yetu hapa ni kuandaa wataalamu na ndio maana tunakuwa wakali na makini kuhakikisha wanafunzi tunaowachukua, wote wanakuwa na sifa stahiki”, alisema Profesa Luoga alisema uhakiki ambao umefanywa na TCU na kutoa idadi ya wanafunzi 224 wanaosoma chuoni hapo, kuhakikisha wanawasilisha ushahidi wa nyaraka zao, wanaufanyia kazi, kwani kuna uwezekano tume hiyo haina taarifa kuhusu programu zinazoendeshwa na chuo hicho.

Alifafanua kuwa kuna baadhi ya programu maalumu, ambazo Serikali ya Tanzania imeingia na nchi nyingine kwa ajili ya kuendesha programu maalum.

Alisema kozi hizo zimekuwepo chuoni hapo kwa muda wa miaka 40 sasa na zinafanywa kutokana na makubalino ya Serikali ya Tanzania na nchi husika.

Alisema chuo hicho kikongwe Tanzania, kutokana na kuwepo makubaliano hayo kimekuwa kinapokea baadhi ya wanafunzi ambao wanatoka nje ya nchi na akasisitiza kuwa yawezekana ndio hao ambao TCU imeshindwa kupata nyaraka zao.

“Yawezekana kuna taarifa ambazo hazijakaa sawa, tumepokea taarifa ya TCU sisi kama chuo ni jukumu letu kuitekeleza,” alieleza Profesa Luoga

Chanzo: Habari Leo
Kwani hajapata listi?
 
Sisi hapa ni wakali kuhusu jambo hilo, tukibaini kuwepo kwa mwanafunzi ambaye hana sifa tunamfukuza. Hatusubiri TCU iseme...hata tukibaini kuwa mtu alifanya udanganyifu na alishamaliza chuo, lakini hakuwa na sifa, tunamnyang’anya digrii tulivyompa,” alisema Profesa Luoga

Hapa atueleze vizuri.
 
We jamaa sio mzima kichwani, textile engineering wachukue div 4 hebu punguza chumvi mkuu.

Kozi yoyote inayoitwa engineering ukitaka kuisoma lazima unywe maji kwanza
Mwaka 2014 ilikuwa ata mtu mwenye four anakuwa amekidhi vigezo vya kuingia University mana mfumo uliotumika ni wa tofauti kipindi kile three iliishia point 13.
Uzuri wa UDSM wanapotoa list ya waliochaguliwa pale lazima waweke matokeo ya kidato cha sita na cha nne, kwaiyo waliochaguliwa UDSM kwa textile engineering mwenye ufaulu mkubwa alikuwa na two point nine yani two ya mwisho kwa mwaka ule 2014,Mkuu nipo makini sana kabla sijatoa taarifa pia sio UDSM pekee kuna vyuo vingine walichukua four za engineering ile ilikuwa inaitwa BRN.
Unakuja kubisha kumbe hata huelewi mambo, ukitaka nikutumie namba ya mtu wa textile engineering wa third year ntakutumia umuulize, watu hatukurupuki kuongea tuna evidence.
 
Back
Top Bottom