VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Huku Chuo Kikuu cha Dodoma-UDOM kikiandamwa na kashfa ya wanafunzi wake wa kike kujiuza kwa ajili ya kujikimu,hali ndani ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam-UDSM si shwari. Wanafunzi wa UDSM sasa wapo kwenye hali mbaya kiuchumi.Wameishiwa. Sasa wanafunzi hao wapo kwenye juma la nane tangu wafungue chuo. Walipofika walipewa fedha za kujikimu kwa ajili ya miezi miwili ya mwanzo ambayo tayari imeshakwisha.Sasa kula na kunywa ni mbinde.
Jana,kulikuwa na rabsha za hapa na pale UDSM wakati wanafunzi walipojaribu kushinikiza kupewa 'boom' lao lililobakia. Hali hii haiwezi kusababisha kashfa kama ya UDOM? Kwanini Bodi ya Mikopo inapiga danadana huku mafisadi yakiendelea kuiba tu? Wanachuo msikubali.Pambaneni mpate haki yenu.Nina wasiwasi mkuu...
Jana,kulikuwa na rabsha za hapa na pale UDSM wakati wanafunzi walipojaribu kushinikiza kupewa 'boom' lao lililobakia. Hali hii haiwezi kusababisha kashfa kama ya UDOM? Kwanini Bodi ya Mikopo inapiga danadana huku mafisadi yakiendelea kuiba tu? Wanachuo msikubali.Pambaneni mpate haki yenu.Nina wasiwasi mkuu...