Udokozi unawaponza Wabongo kupata ajira

Pundamilia07

JF-Expert Member
Oct 29, 2007
1,439
54
Udokozi unawaponza Wabongo kupata ajira

Na Ramadhan Mbwaduke
20th July 2009

Serikali imesema tatizo la uaminifu kwa vijana walio wengi nchini linachangia kwa kiasi kikubwa tatizo la ajira nchini kwani huwafanya baadhi ya wenye makampuni kulazimika kuja nchini na watu wao walio na moyo safi na kuwaajiri.

Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, amesema hivi sasa, kuna matukio mengi ya aibu yahusianayo na wizi wa pesa, mali na vifaa vya makampuni, ambayo hujikuta yakiingia hasara kubwa.

Kwa sababu hiyo, Waziri Kapuya akasema wahusika wanaoendesha kampuni hizo hulazimika kuajiri watu wa kwao ili kushika nafasi ambazo Watanzania wangeweza kuzitumikia kwa uwezo sawa au hata zaidi ya wageni wanaowaleta.

"Inafikia mahala hata kijisimu tu (cha mkononi) kinaposahauliwa kidogo tu, kinakwapuliwa... Kwa kweli hili ni tatizo ambalo limeanza kuwa kubwa na linasikitisha sana," akasema Waziri Kapuya, huku akitaja sekta mojawapo inayokumbwa zaidi na tatizo hilo kuwa ni ya huduma za hoteli.

Akitolea mfano zaidi, Waziri Kapuya ameema hata Wachina wanaoendelea na ujenzi katika Chuo Kikuu cha Dodoma wamekuwa wakikumbana na matatizo ya kuibiwa mali zao na vifaa vya ujenzi kila kukicha, hali ambayo inawafanya walalamike kila mara kutokana na hasara wanayoipata.

"Nenda pale UDOM (Chuo Kikuu cha Dodoma)... Wachina wanaibiwa stoo kila siku. Je, Mchina Mjenzi akisema anataka meneja anayesimamia vifaa awe Mchina mwenzie kwa sababu waliopo sasa wanamuibia sana, halafu we ukiwa Waziri utasemaje? Ni tatizo kubwa kwa kweli," akasema Waziri Kapuya.

Aidha ameongeza kuwa hivi sasa, Wizara yake imewasiliana na Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi nchini, VETA ili iweze kuongeza somo la uaminifu katika mtaala wake ili walau kupunguza tatizo hilo ambalo linaleta athari kubwa katika sekta ya ajira.

"Nashukuru kwamba baada ya kuzungumza na VETA, hivi sasa suala hilo limekubaliwa na litawekwa katika mitaala yao ili kuondokana na tatizo hili la uaminifu," akasema Waziri Kapuya.
 
Hili ni tatizo kubwa wala sii Udokozi.. Mbongo ukimwachia duka basi akili yake kesho afungue la kwake na mtaji utatoka dukani kwako..Hivyo chimbuko lake limetokana na kuuvamia Ubepari..
 
Hili ni tatizo kubwa wala sii Udokozi.. Mbongo ukimwachia duka basi akili yake kesho afungue la kwake na mtaji utatoka dukani kwako..Hivyo chimbuko lake limetokana na kuuvamia Ubepari..

Mkandara,

Usinikumbushe ndugu hili limenitokea mimi! Na jamaa yangu mmoja alinicheka, na yeye limemtokea siku chache zilizopita.
 
Mzee Mkandara, sio Ubepari bali ni uroho wa watoto wetu. Mbona Kenya ubepari umeanza siku nyingi sana na hakuna visa vingi kama vyetu. Tatizo la Kenya ni kwamba akija TZ ataiba apeleke kwao lakini sisi, duh
 
Mzee Mkandara, sio Ubepari bali ni uroho wa watoto wetu. Mbona Kenya ubepari umeanza siku nyingi sana na hakuna visa vingi kama vyetu. Tatizo la Kenya ni kwamba akija TZ ataiba apeleke kwao lakini sisi, duh
tatizo la tanzania samaki ameoza tokea kichwani (maana viongozi wenyewe ni wezi) hivyo na walio chini wanataka wasiachwe mbali, matokeo yake ndio hayo.
Yeye Kapuya anatakiwa aanze yeye mwenyewe kuwa mwaminifu na wenzake ndipo majority ya watanzania watabadilika.
 
Alhaji Kapuya anajitetea kukwepa lawama ya utoaji holela wa vibali vya kazi chini ya wizara yake.

Atatuambia nini kuhusu wachina waliojazana Kariakoo?

Kwa kadri ya uwelewa wangu,kampuni makini huweka bima dhidi ya majanga ukiwemo wizi na kukosa uaminifu kwa wafanyakazi wake

Tatizo likitokea tu, ni mtuhumiwa kupelekwa kwenye sheria na bima kufidia.

Kampuni za bima siku hizi zinashindana kulipa mapema.

Alhaji Kapuya acha kuumiza watanzania wenzako kwa kisingizio cha wizi
 
Ebwana swala hilo mimi binafsi nakubaliana nalo kwamba kweli vijana wengi wa kibongo wanafanya hivyo wanavyofanya kama short cut ya kupata maisha mazuri, lakini sababu zinazo wafanya wafanye hivyo wanavyofanya zinachangiwa na mambo mengi sana mfano unakuta mtanzania analipwa ujira mdogo sana ukilinganisha na mfanyakazi wa kigeni, kuwepo kwa mazingira mabovu ya kazi mfano mbongo akiumia kazini unakuta anatelekezwa au hata kuachishwa kazi kabisa tu lakini akiumia mgeni yeye anapewa matibabu tena katika hospitali kubwa, kwa hiyo hivi vyote vinachangia kwa namna moja ama nyingine wabongo wawe wanafanya wizi makazini mwao, lakini swala jingine hapa ni la kimfumo zaidi ambapo watu wengi tumeshuhudia wale ambao tumewapa madaraka hawatekelezi majukumu yao bali wamekuwa pale kujineemesha wao wenyewe tumeshuhudia wizi wa epa,mikataba mibovu,ununuzi wa rada na rushwa nyingi tuzilizofanywa na zinazofanywa na viongozi wetu, kwa hiyo utaona kwamba watu wamekosa matumaini kabisa katika maisha yao maana viongozi wanasema maisha bora kwa kila mtanzania wakati kiukweli mtanzania wa kawaida anachokiona ni kinyume chake basi ndio maana wanaaamua na wao kutafuta njia mbadala ya kuyapata hayo maisha bora kwa kufanya chochote,binafsi ninachoona hapa ni kwamba hii nchi yetu kwakweli imeuzwa kabisaaaaaaaaa! Embu angalia kirefu cha hili neno hapa C C M- Chukua Chako Mapema,
 
Hili ni tatizo kubwa wala sii Udokozi.. Mbongo ukimwachia duka basi akili yake kesho afungue la kwake na mtaji utatoka dukani kwako..Hivyo chimbuko lake limetokana na kuuvamia Ubepari..
kaka suala sio kuvamia ubebari ila ni tatizoo tuu la maadili ya kazi kukosekana.. hao vijana wanadokoa ila wenzao sekta ya umma ndo wizi, uvivu, utendaji duni, matumizi mabaya ya muda na vifaa (magari, simu, umeme, maji, samani, nk nk)... kwa pamoja inatoa picha halisi ya watanzania kwamba hatuna ETHICS ZA KAZI (Lack of love working spirit)

Tukijisahihisha kwa hilo hata viongozi wazembe hawatapata nafasi ya KUTUONGOZA...WAJIBU NA HAKI vitaonekana.
 
kaka suala sio kuvamia ubebari ila ni tatizoo tuu la maadili ya kazi kukosekana.. hao vijana wanadokoa ila wenzao sekta ya umma ndo wizi, uvivu, utendaji duni, matumizi mabaya ya muda na vifaa (magari, simu, umeme, maji, samani, nk nk)... kwa pamoja inatoa picha halisi ya watanzania kwamba hatuna ETHICS ZA KAZI (Lack of love working spirit)

Tukijisahihisha kwa hilo hata viongozi wazembe hawatapata nafasi ya KUTUONGOZA...WAJIBU NA HAKI vitaonekana.

Sawa kabisa, tena mtu yoyote aliyewahi kubeba boxi US anaweza akakwambia hili, work ethic ya US na ya bongo ni tofauti kabisa, hata kama mtu anaichukia kazi bado anapiga kikamilifu.
 
Uadilifu na maadili mema huanzia nyumbani. Mtoto akifunzwa vyema tangu utotoni kwamba wizi ama udokozi haufai na kudhibitiwa na kuadhibiwa pale anapofanya vitendo vhiyo, basi atakua akizingatia aliyofunzwa na wazazi. Lakini, ni wazazi wachache sana siku hizi ambao wanajali ama wana muda wa kuangalia mienendo ya watoto wao na kuwafundisha ipasavyo. Mabadiliko ya maisha yamefanya watu wamekuwa hawana muda tena na familia zao. Hata Walimu mashauleni ambao ndio 'wazazi wa pili', kazi ya kuwafunda wanafunzi inakuwa ngumu kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi kiasi cha kushindwa kuwa-control.

Lakini, nakubaliana kwamba sisi Wabongo vijana wetu wamezidi mno udanganyifu, utapeli na wizi bila aibu. Hapa ndipo viongozi wanapaswa ku-play role yao kikamilifu katika kujenga maadili ya Taifa. Kama viongozi wa kisiasa na maofisini wakionyesha mfano wa wao wenyewe kwanza kuwa waadilifu, kukemea na kutoa adhabu kali kwa wale wanaofanya makosa ya wizi na udanganyifu, lazima wanaofanya vitendo hivyo wataogopa. Kinachotokea ni kwamba hata viongozi wenyewe ni washirika wa uhalifu wa aina hiyo.
 
Kapuya amekosa cha kujibu au kujenga hoja kuhusu ajira za wageni hapa kwetu. Ni aina ngapi za kazi watu wanaweza kudokoa? Kuna kazi ngapi ambazo wameajiriwa watu kutoka nje ambapo hakuna hata kitu cha kudokoa. Kama ni udokozi kila mwajiri anatakiwa awe na mechanism ya kumonitor wizi. Mbona wazungu wanakuja kuiba kwenye ATM hapa bongo nani mwizi zaidi? Waziri atafute sababu za msingi na zinazoeleweka.
 
Mkandara,

Usinikumbushe ndugu hili limenitokea mimi! Na jamaa yangu mmoja alinicheka, na yeye limemtokea siku chache zilizopita.


Ahsante jamani.

Naomba tulijadili kwa kina. Hapa nilipo nimesistitisha mradi niliokuwa niuanze kwakuwapatia wadogo zangu mshiko lakini imekuwa ni lawama baada ya kujiondoa.

tatizo la kuiba au ufujaji wa mitaji watu wanayopewa kusimamia ni sugu na siye tulio majuu tunapata lawama eti hatuwapi mikopo ndugu zetu kumbe ndo kabisaa hawafai kwa sababu hata akiula huwezi kunfunga kwani ndugu wanaweza wakaandamana.

Plz any one with idea? Ukweli umaskini uliopo bongo binafsi unaniuma sana.
 
Vijana wetu ni nakala halisi ya sisi wazee wao. Tabia na matendo yao wanaiga toka kwetu. Wanatuona tunavyoitafuna nchi yetu hadi tunawalazimisha kusoma kwa mikopo. Watailipaje mikopo hii? Kapuya anajua alikoifikisha NSSF.
 
Hii Attitude Kubwa Sana Ya Wabongo ...hata Umpe Mshahara kiasi gani yeye atakuibia....Hivi Wadau tuseme ukweli Hivi mtu umpe kiasi gani asiibe...?..ni Attitude Mbaya...Kubwa ni ile Khofu isiyoonekana HAIPO...!!

Mpe leo 1M salary, Safari 100dola au zaid kwa siku...transport costs....bado akirudi safari atakuja na RISITI za Uongo..."

Ikiwe leo brothers zetu wa TRA wanapewa mishahara Minono waache Wizi na wawe Wakweli...atlast yeye ndio atatengeneza Mazingira umpe Rushwa!!!
 
Alhaji Kapuya anajitetea kukwepa lawama ya utoaji holela wa vibali vya kazi chini ya wizara yake.

Atatuambia nini kuhusu wachina waliojazana Kariakoo?

Kwa kadri ya uwelewa wangu,kampuni makini huweka bima dhidi ya majanga ukiwemo wizi na kukosa uaminifu kwa wafanyakazi wake

Tatizo likitokea tu, ni mtuhumiwa kupelekwa kwenye sheria na bima kufidia.

Kampuni za bima siku hizi zinashindana kulipa mapema.

Alhaji Kapuya acha kuumiza watanzania wenzako kwa kisingizio cha wizi

bwana eeh watanzania wizi tu hata huku durban ndo hayoy hayo hatuna ethics za kazi tunataka short cuts tu na sasa unasema kwa kuwa bima ipo tuibe tu!
 
Teh teh teh teh

Kwa hiyo mnakili kuwa tatizo la ufisadi si tatizo la chama fulani bali ni kwa sisi watanzania wote.
 
Hili ni tatizo kubwa wala sii Udokozi.. Mbongo ukimwachia duka basi akili yake kesho afungue la kwake na mtaji utatoka dukani kwako..Hivyo chimbuko lake limetokana na kuuvamia Ubepari..

Kapuya naye kapotoka!! wale wahindi wa TRL ni wabongo?si bora mbongo anawekeza hapahapa kuliko hao wanaopeleka kusiko julikana?
 
Wawekezaji wanatunyima ajira kutokana na udokozi wetu, tumewapa viongozi wetu dhamana ya kuongoza nchi wakaishia kupora rasirimali zetu kwa kuwa ni wadokozi. Tumrejeshe mkoloni kwa kuwa sisi wote ni wadokozi?
 
Tatizo la wizi kazini lina mizizi yake: Nitaorodhesha baadhi kama ifuatavyo

1. Mtu ana utaalamu mzuri sana, na yeye anajua hilo halafu unamlipa mshahara wa laki moja wakati foreigner mbumbumbu anachukua dola 4,000.

2. Kutokuwa na job security kwa wafanyakazi wengi, yaani siku boss akilala na pombe kichwani unasikia anakupa pay-off kazi hakuna, je mtu afanyeje?

3. Gap kati matajiri na masikini limekuwa sana kiasi kwamba kila mtu anahitajia afikie matawi ya juu mapema kabla ya jua halijachwa.

4. Vijana wanaona mfano wa wazee wengi waliolitumikia taifa kwa uadilifu mkubwa na uaminifu ambao wengi baada ya kustaafu wanaishia kuwa omba omba ambao watu huwacheka kwa nafasi walizokuwa nazo kutozitumia kwa kuwekeza kwenye maisha ya baadae (Lack of comprehensive social security programs)

5. Viongozi wetu nao ni sehemu ya sisi kutokuwa waaminifu, kwani wao wana-collude na wawekezaji na kuwashawishi wawalipe vijana mshahara wa chini kutokana na maisha kuwa chini tofauti na nchi watokazo wawekezaji. Pia viongozi hao hao hujilimbizia mali mpaka inakuwa siyo siri tena, ambazo ni mali za umma bila kuwajibishwa. Je vijana wafanyeje?

6. Wawekezaji wengi na hasa wahindi ni wanyanyasaji wakubwa wa watanzania wanaofanya kazi kwenye makampuni yao, na kuwafanya watu hao kutokuwa na imani na biashara hizo na kuona ni kama vile haziwahusu kwani hawaaminiki, japo wengine ni waaminifu. Dawa ya mtu asiyekuamini muibie, maana usipofanya hivyo siku akipoteza kwa uzembe wake atasema umemuibia na itakuuma sana, ila kama ni kweli utakuwa na ahueni kuwa kweli nimeiba.

My take: Ni kweli kabisa kuwa uaminifu kazini ni jambo muhimu sana katika kutengeneza mazingira mazuri ya kujipatia mkate wa kila siku. Lakini pia na viongozi wetu kama kina Kapuya wawe mstari wambele katika kujitakasa na wizi wa mali za umma. Viongozi wakiwa waaminifu wataweza misingi mizuri ya social security na kufanya vijana kutokuwa na wasi katika maisha yao baada ya kulitumikia taifa. Vinginevyo "Cat and mouse" game katika sehemu za kazi haitaisha
 
Back
Top Bottom