PEA
Member
- Dec 31, 2010
- 77
- 33
Wakati macho na masikio ya Watanzania yakielekezwa Igunga kwenye uchaguzi wa Ubunge, mjini Njombe Wabunge watatu wa Chadema watahudhuria uzinduzi wa Kampeni za kiti cha Udiwani kata ya Mjimwema, siku ya Ijumaa tarehe 09/09/2011. Wabunge hao ni Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), Chiku Abwao (Viti Maalum-Iringa) na David Silinde (Mbozi Magharibi).
Uchaguzi wa diwani wa kata hiyo utafanyika kama ilivyo kwa kata zingine 22 nchi nzima tarehe 2/10/2011 kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo kupitia CCM Marehemu Augustino Mbanga.
Ni matumaini yetu kuwa ujio wa Wabunge hawa na uhakika kwamba Mh Silinde atakuwepo Njombe kwa siku 4 utasaidia sana kupambana na njama za CCM waliozoea kujishindia kiulaini kila mara kunapokuwa na uchaguzi katika Wilaya ya Njombe
Uchaguzi wa diwani wa kata hiyo utafanyika kama ilivyo kwa kata zingine 22 nchi nzima tarehe 2/10/2011 kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo kupitia CCM Marehemu Augustino Mbanga.
Ni matumaini yetu kuwa ujio wa Wabunge hawa na uhakika kwamba Mh Silinde atakuwepo Njombe kwa siku 4 utasaidia sana kupambana na njama za CCM waliozoea kujishindia kiulaini kila mara kunapokuwa na uchaguzi katika Wilaya ya Njombe