Udini waingilia Rasmi kampeni Igunga

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Taarifa ya habari ya ITV saa mbili imeonyesha tamko Rasmi la Bakwata kuwataka waislam wa Igunga wasimpigie kura mgombea wa chadema.Nimepata mshtuko mkubwa na kuona taifa letu sasa linaangamia.Hivi ni halali kwa mujibu wa sheria za uchaguzi dini kutangaza rasmi chama fulani kisipigiwe kura? Watu wote wapenda haki demokrasia na amani walaani tamko hili haramu.
 
Leo katika ibaada ya ijumaa katika msikiti mkuu wa igunga mjini shekhe ama mtoa mawaidha amesema chadema na wakristo ni makafiri. Katika mawaidha hayo shekhe huyo alisikika kupitia spika za mskitini (Public annoucement system) akisema chadema ni chama cha kidi kwa sababu ya kumdharirisha mkuu wa wilaya ambaye ni mwislam. nami ni kiwa eneo ka msikitini nilisikia maneno hayo ya shekhe. Kweli shekhe katugawa wana igunga. Anadai kwa mwislam yeyote atakaye chagua chadema atalaaniwa. Baada ya ibaada wapo baadhi ya waislam wamechukizwa na hotuba ya shekhe huyo. Mbaya yaidi waislam wanashindwa kuelewa kama kuchagua chadema ni dhambi kwa kauli ya shekhe! je wachague chama kipi? Kwani katika vyama venye nguvu hapa ni chadema, ccm na cuf. Wagombea wote kupitia vyama hivyo wote ni wakristo. Kuna mgombea mmoja tu kutoka chama kimoja cha UDPD ambacho hakina mashiko kabisa hapa igunga hata kampeni bado hakijazindua. Sijui huu udini utatupekeka wapi? haya ni ya kweli nimeyackia mwenyewe na kama una dungu yako hapa igunga ambaye anafuatilia siasa kwa ukaribu please jaribu kumuuliza. Tunaomba dua zenu uchaguzi huu umalizike kwa amani.
 
sasa waislam watangaza rasmi kuwa mwislam yeyote atakaye chagua chadema atalaaniwa. Source mskiti mkuu wa igunga
 
MS usilinganishe cuf na CDM! ajenda ya cuf ni ya kidini na maeneo mengi wanayotegemea ni ya waislam so tofauti sana CDM. Kingine waislamu wataiua CCM sababu wanaona ndo chama chao, mimi upande wangu nashauri waislamu wote wachague ccm na cuf na wakristo tuchague CDM tuone kama mtaweza tumesha wachoka.
 
Mbona Waislam Igunga ni wachache saana, hawana effect yeyote. Mbona wanaruka mkojo wanakanyaga mavi? Kafumu wa Yesu, kashindye naye wa Yesu. Mbona hawafikiri hata kidogo?
 
Mama Wille hicho ndiyo nilikuwa nataka kuhoji kwani wagombea wote ni dini gani. sasa napata picha hawa viongozi wetu wa igunga wanataka kutuharibia. waislam naomba tuwakemee hao viongozi wetu wa igunga wasije wakatuharibia ili tuonekane tumeingi
liia kampeni
 
Unachekesha we2
Ht km wakisema OK!CHADEMA ni ya wakristo zen CCM/CUF ni Waislam bac kila mmoja achague tokana na din zao
MA DOG mtakwishne nyie ht robo hamtosh Bongo hii
Bt wenye akil timamu a2fikirii coz sote ni ndugu a2mind udin,WAKRISTO a2jazoea zogo
 
Hayo yalikuwa maoni yake binafsi huyo shekhe.na kila mtu(wananchi wa jimbo la igunga) ana maamuzi yake binafsi juu ya amchague nani mwishoni.
Kuna watu wanaotumiwa kupotosha uma kama huyo shekhe.
 
Mhhhhhhhhhhhh! hayo mambo ya dini mie huwa nayaogopa sana na ukizingatia marafiki wangu wengi ni waislamu huwa naona kuwa siwatendei haki kabisa. Maana mishemishe nyingi niko nao na tunaishi vizuri kweli.

Kuna wakati nilisema waislamu wanahitaji viongozi wenye elimu ahera na elimu dunia kubwa. Nadhani hili linawatatiza sana na ndio maana magamba wamekuwa wanawagonganisha vichwa. Na lingine ni kuwa hata wale wenye elimu kubwa huwa hawako interested sana na kuongoza dini zao, wengi hukurupuka pale tu wanapoona wasomi toka dini nyingine wanapoibana serikali kiitikadi tu, after that wanabaki hamnazo na mambo ya dini. Halii hii imepelekea uislamu kutokuwa na maono, sera na mipango ya muda mrefu. Nadhani wanahitaji waongozwe na watu wenye elimu dunia za viwango vya bachelor, master na PhD degree watafanikiwa sana hawa jamaa na watakomboka kifikra watakapokuja magamba kujaribu kuwatumia kipolitiki.
 
Waislamu mnatakiwa muwe na umoja wa nyuki na sio umoja wa inzi.

Ukilipiga jiwe kundi la inzi kila mmoja ataenda upande wake, hali ni tofauti kwa nyuki ambapo kama ukiwapiga jiwe wote watamtafuta adui na kumtia adabu hali hii ndiyo ipo kwa wakristo amabapo wakisimamia kitu ni mpaka kieleweke tena wanakuja na hoja zenye mashiko. lakini kwa waislamu hali ni tofauti, maulamaa wakisema a dhidi ya serikali, bakwta wanakuja na b matokeo yake ndo kama hivyo tena, wamepigwa mabao na magamba hata kwenye hoja simple kama ya Mahakama ya kadhi. Amkeni, jitengeni na serikali, endesheni mambo yenu kidini zaidi kuliko kisiasa
 
Chokochoko zote hizi bila shaka ni kwa sababu ya yule DC. Mimi nauliza, hivi yule DC alivaa mtandio au Hijab, maana nikimuangalia naona kama ile ilikuwa ni mtandio?
 
Mama Wille km umeskia hayo toka mskitini kiongoz km Sheikh anashabikia co powah!
Jaman!Mbona ht waislam wengine wanakemea,leo nacheck ITV NEWZ wanaongelea hyo cjui HIJABU aliyovuliwa ht maana amna wanaoongea wako very smart na HIJABU kwel imezba ol part except uso na huyo DC kwenye picha hakuwa kw hawa waliokuwa wanaongea na mpk ukatokea kutokuelewana na mareporter haijawaingia akilin Plz!Kuen waangalifu na mnachosema msianze ubaguz wa din badae wengine mjekujua na ze way mko gud kula2mika
M OUT!
 
Ushauri wangu kwa uongozi wa CDM,msimpige magoti mtu/kundi lolote linaloendekeza udini. Heri mkose hizo kura. Kama CCM kupitia kwa huyo DC wao wanapanda mbegu ya udini,waache waichukue igunga kwa kura za udini,lakini siku sinyingi watajutia makosa yao.
 
aise wajemen hali siyo nzur basi kikwete akeme matamko kama hayo ambayo yanaweza kuja kutugawa sisi watanzania kama raisi
 
Nt yet!Kumbe mbunge wa CHADEMA na CCM nahic ht CUF wote ni wakristo afu dis 3 party ndo hot afu ki2 cha SHEIKH pale kat msiwapigie wakristo so wat next
C chadema ndo inawakristo ht Ccm na cuf wapo au umesahau Mbowe na Zitto niwaislam
Msi2fanyie hvyo bwana 2naangalia sera au co wam
a Igunga na co din
M out 4gud
Au maralia sugu unanyongeza coz we ni gamba tahila
 
Waislam bwana yaani matamshi yako utata mtupu .Utadhani Mungu wao hana nguvu hadi wampiganie .Mie nakaa kimya kuangalia mwelekeo na mwisho wao .
 
hata balozi wa marekani alisema msichague cuf ni wadini. Sasa na chadema ndio hao hao

Balozi wa Marekani ana udugu au uchungu na Watanzania kuliko Watanzania wenyewe? Udini ni wimbo wa CCM na washereheshaji wao baadhi ya Masheikh na Waislamu vipofu

Enzi CUF walipokuwa wapinzani kabla ya kuonjeshwa halua Zanzibar, CCM walidai CUF ni chama cha kidini. CDM wamechukua upinzani, CCM, Mashehe na CUF wanaimbisha na kupokezana wimbo ati CDM ni cha kidini, Msajili kimya
 
Back
Top Bottom