Habari zenu wana jamvi,naomba nieleze ambacho nimekuwa nikikifanyia kazi kwa ukaribu zaidi na kupata maoni ya wadau mbalimbali.suala hili la udini limekuwa likiongelewa na kuonesha dalili zote za kutugawa watanzani kwa misingi ya ukristo na uislamu.huu ni mpango kabambe wa mafisadi ambao wanatumia nguvu na pesa nyingi kuhakikisha wanalipandikiza suala hili katika akiri za watanzani.wanajaribu kututumia ili waendelee kufaidika na mipaango yao ya kuiibia nchi.kabla ya kisa cha udini,walitumia neno 'amani' kila mara watu walipotaka kuhoji masula mhimu ya nchi yao,au kuandamana kuhusu mambo machafu ya ufisadi,walionekana kama wanataka kuvunja amani,hivyo jeshi la polisi liliwadhibiti vikali,hata viongozi wetu wa kitaifa walisimama na kukemea waziwazi kwa kudai ni uvunjifu wa amani.kauli hii kwa sasa hainanguvu tena.wamekuja na hili la kutangaza udini ili watu wagawanyike na kushindwa kufanya maamuzi sahihi juu ya mstakabali wa taifa hili.tunaoumia ni sisi wakristo,waislamu na wale wasio na dini.wakati huo wao na familia zao wako salama wanakula bata(kama vijana wasemavyo),suala hili ni hatari sana kwetu hata kwa vuzazi vijavyo,hivyo basi,watanzania wenzangu tuwapuuze na mpango wao ambao hauna maslahi kwetu zaidi ya kutuharibia umoja wetu.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.