Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
he he heheeeeeeeeeeee, habari za jikoni zina facts. Kuliko mleta ndoto za mchana, sijui ulikuwa hujala maskini ya mungu Mdaku!

ha ha ha ha,

umepatikana tena masikini kwa kuleta habari za kidaku za jikoni na sasa umeanza kuziita facts. ha ha ha ha, hapa sina mbavu.
 
mdaku kama vile mdaku mwenzake alivyokimbilia kuja kujadili mjadala wa kidaku

Mdaku uliyeleta habari ya UDAKU ukashindwa kuleta facts, ulidhani umepata kumbe umepatikana. Siku ingine ukifungua thrad hakikisha una DATAZ za kutosha.
 
ha ha ha ha,

umepatikana tena masikini kwa kuleta habari za kidaku za jikoni na sasa umeanza kuziita facts. ha ha ha ha, hapa sina mbavu.

kwi kwi kwi, UDAKU huo mwanaume mzima aibu jamani aibu, kwa kufungua thread ya udaku.
 
MDAKU; Kama haya ndio unayoyaita majadiliano basi CHADEMA huku wamekwisha, ndio mnavyojadiliana hivi? no wonder mnafukuzana.


ha ha ha ha.

mafisadi wa ccm mtapata magonjwa ya moyo mwaka huu.
mkuki kwa nguruwe, mliita CUF chama cha kidini mkadhani hakuna mtu anayejua siri ya udini ulivyojaa ccm. Hapa mama mmepatikana, mtabanwa mbavu kwenye mambo ya EPA na buzwagi, na mkileta mambo ya udini na ukabila, mtaanikwa tu.

Ha ha ha, ninapenda sana ccm wakibwana mbavu vile wanavyohangaika.
 
kwi kwi kwi, UDAKU huo mwanaume mzima aibu jamani aibu, kwa kufungua thread ya udaku.

kwi kwi kwi,

bana mbavu mpaka wachukie na kuanza kuleta habari za jikoni huku wakiziita facts. ha ha hah,
 
Mdaku uliyeleta habari ya UDAKU ukashindwa kuleta facts, ulidhani umepata kumbe umepatikana. Siku ingine ukifungua thrad hakikisha una DATAZ za kutosha.

Ninakuwekea tena hii habari ya udini ndani ya ccm ili uisome vizuri na ukimaliza urudi kuendeleza udaku:


1. Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete - Mwenyekiti - Muslim
2. Ndugu Pius Msekwa - Makamu Mwenyekiti (Bara) -
3. Ndugu Amani Abeid Amani Karume - Makamu Mwenyekiti(Zanzibar) - Muslim
4. Ndugu Yussuf R. Makamba - Katibu Mkuu - Muslim
5. Capt. (mst) George Huruma Mkuchika - Naibu Katibu Mkuu (Bara)
6. Ndugu Salehe Ramadhan Ferouz - Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar)- Muslim
7. Dr. Ali Mohamed Shein - Mjumbe - Muslim
8. Ndugu Mizengo Kayanza Peter Pinda - Mjumbe
9. Ndugu Shamsi Vuai Nahodha - Mjumbe - Muslim
10. Alhaj Ali Hassan Mwinyi - Mjumbe - Muslim
11. Ndugu Benjamin William Mkapa - Mjumbe
12. Mzee Rashid Mfaume Kawawa - Mjumbe - Muslim
13. Dr. Salmin Amour - Mjumbe - Muslim
14. Ndugu John Samwel Malecela - Mjumbe
15. Capt. (mst) John Zefania Chiligati - Mjumbe
16. Ndugu Amos Gabriel Makala - Mjumbe
17. Ndugu Bernard Kamilius Membe - Mjumbe
18. Ndugu Kidawa Hamid Saleh - Mjumbe - Muslim
19. Ndugu Samwel John Sitta - Mjumbe
20. Ndugu Pandu Ameir Kificho - Mjumbe - Muslim
21. Ndugu Anna Abdallah - Mjumbe
22. Ndugu Rostum Aziz - Mjumbe - Muslim
23. Dr. Mohamed Gharib Bilal - Mjumbe - Muslim
24. Ndugu Pindi Hazara Chana - Mjumbe
25. Ndugu Andrew Chenge - Mjumbe
26. Dr. Maua Abeid Daftari - Mjumbe - Muslim
27. Ndugu Samia Suluhu Hassan - Mjumbe - Muslim
28. Ndugu Mohamed Seif Khatib - Mjumbe - Muslim
29. Ndugu Haji Omar Kheri - Mjumbe - Muslim
30. Dr. Abdallah Omari Kigoda - Mjumbe - Muslim
31. Ndugu Abdurahman Kinana - Mjumbe - Muslim
32. Ndugu Anne Semamba Makinda - Mjumbe -
33. Ndugu Fatuma Said Ali Mchumo - Mjumbe - Muslim
34. Ndugu Zakia Hamdan Meghji - Mjumbe - Muslim
35. Ndugu Omar Yussuf Mzee - Mjumbe - Muslim
36. Ndugu Emmanuel John Nchimbi - Mjumbe
37. Ndugu Ali Ameir Mohamed - Mjumbe - Muslim
38. Ndugu Yussuf Moh’d Yussuf - Mjumbe - Muslim
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amethibitisha kuwa alikikopesha chama chake sh. milioni 500 kwa ajili ya kampeni na pia amekuwa akikikopesha chama hicho mara kwa mara mahitaji yakijitokeza. Huyu ndio Mbowe anayedaiwa na taifa la Tanzania na ameshindwa kulipa deni hilo kwa taifa kwa madai ya kushindwa kufanya hivyo! kwa hili Mbowe amedhihirisha kuwa kwake yeye chama na maslahi yake binafsi ni muhimu kuliko maslahi ya taifa.

Mbowe hafai kuongoza nchi yetu.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amethibitisha kuwa alikikopesha chama chake sh. milioni 500 kwa ajili ya kampeni na pia amekuwa akikikopesha chama hicho mara kwa mara mahitaji yakijitokeza. Huyu ndio Mbowe anayedaiwa na taifa la Tanzania na ameshindwa kulipa deni hilo kwa taifa kwa madai ya kushindwa kufanya hivyo! kwa hili Mbowe amedhihirisha kuwa kwake yeye chama na maslahi yake binafsi ni muhimu kuliko maslahi ya taifa.

Mbowe hafai kuongoza nchi yetu.

Kwi kwi kwi,

yaani sasa umeanza flooding, unaweka kila thread. Au unatafuta sababu ya kufungiwa kwa flooding kisha uanze malalamiko? Ukisikia kuishiwa hoja ndiko huku. Unatia huruma sasa na hii obsession yako na Mbowe.

Ngoja nikupe break kidogo sasa maana umeanza kuonyesha frustrutions. Usinilaumu mimi, muliyaanza haya huko ccm kwa kuita vyama vingine vya kidini na kikabila. Mnavuna tu kile mlichopanda.

Kuwa na siku njema, jaribu kuchukua breki kidogo upunge upepo maana unakoelekea sasa siko.
 
kwi kwi kwi,

bana mbavu mpaka wachukie na kuanza kuleta habari za jikoni huku wakiziita facts. ha ha hah,

mdaku utamjua tu, kesha dakia habari ambayo haijaulizwa, aliyoulizwa hana facts nayo! Mdaku original wengine wote photocopy
 
MDAKU Mgaya, afadhali umekimbia maana umejua, ukichimbwa huna facts wala figures, unadakia tu, ukisikia mwenzio kajamba nawe wajamba, akipiga mwayo nawe wapiga kwi kwi kwiiii, kazi ipo mwaka huu.

Tena kwa akili yako ilivyokaa kidaku basi ukiona mtu hasupport CHADEMA basi yeye sisiemu, kwi kwi kwi yaani kiumbe mzito kweli wewe.
 
Huu Nimuda Wa Kuangalia Maendeleo Ya Nchi, Tumo Kwenye Ushndani Wa Viama Vingi Tukianza Kuleta Udini Kwenye Chama Tawala Tutajigawa Utakuwa Mwanya Kwa Wapinzani. Muhimu Wenye Cheo Anaweza Kutuletea Maendeleo Na Tumpe Support Kwa Nguvu Zote Tusiangalie Dini Wala Kabila Lake.
wakati Wa Utawala Wa Rais Mkapa Ukiristo Ulitawala Sehemu Zote Waislamu Hawakusema Kitu Iweje Leo Yamekuwa Hayo?tukiangalia Hayo Amani Itatoweka Nchi.
 
Ukweli ni kuwa Kabla ya mtu kuwa mzalendo kwa nchi yake anakuwa mzalendo kwa Mungu wake. Nadhani hoja hii ina mantiki kubwa ambayo contributors wengi wanajaribu kuifunika kwa kuwa wanajua si tu repurcations zake lakini pia wanaelewa vizuri agenda iliyo nyuma. Sio siri kuwa Uislamu ni zaidi ya dini, ni mfumo wa utawala unaoamini kuwa ndiyo bora kuliko mifumo yote including democracy. Na kwa kweli hatimaye uislamu una strive to take over the whole world and especially the western world.

Hapo mzee umegonga mahali! Na ninajua reactions zitakuwa nyingi za kukuita mdini n.k Lakini je ni nani mdini anayetaka kulazimisha matakwa ya imani kwa wengine au vipi? Wakristo nao imewapasa kufunguka macho katika nafasi za uongozi wenzetu hamasa wanapatia msikitini! Na issue ya kidini watu kugombea na kupigiana kura je lengo hatimaye ni lipi? Misikiti ina interest gani ktk kuhimiza waislamu wagombee na kupigiana kura? Nafikiri tusipoamka sasa iko siku tutakuta ya Somalia yamefika bongo.
 
Kati ya hao walio-orodheshwa na dogo Mgaya, sijaona muislam wala mkristo. wote ni Caesarian!!!!!!!
 
Naomba kuwauliza wote mliochangia hii mada kwa upande wa kimagharibi au kimashariki: -

Hivi Wakristo wangekuwa Viongozi wengi CCM kuliko Waislam kama ilivyo kwa Waislam kuwa wengi kuliko Wakristo, SI WAISLAM WANGEKUWA WAMESHA ANDAMANA?

Mkweli yeyote wa JF analijua hili.
 
Kama mnapost kwa ushabiki wa dini, angalieni makala ya Ndesanjo Macha.

Ukristo unafundisha upendo, Uislamu amani: Lakini mbona bado twauana?
na ndesanjo macha

Kwenye lile gumzo la Mtu ni Utu sio Dini nilizungumzia jinsi ambavyo dini inaweza kuwa chanzo cha mfarakano na mgongano katika jamii. Na kuwa utu wetu waweza kuwa na uzito kuliko dini zetu. Nikasema kuwa ukitaka watu wauane kikatili bila huruma basi jenga chuki juu ya misingi ya dini. Nikasema sababu moja kubwa ni kuwa masuala ya dini ni masuala ya kuamini. Ni masuala ya hisia zaidi.

Sasa tumeona yaliyotokea kule Nigeria. Watu zaidi ya 200 wameuawa sio katika vita vya mitutu ya bunduki na maguruneti bali fujo za waumini wa dini mitaani. Hii ni idadi kubwa mno. Roho 200 zimeteketezwa. Ingekuwa wamekufa baada ya mabomu ya kisasa kudodoshwa tungekuwa na mtazamo tofauti. Watu 200 wameuawa kutokana na fujo za waumini wa Mungu ambaye huitwa Mugu wa amani. Mungu wa Upendo.

Makanisa yamechomwa moto. Misikiti imechomwa moto. Wakristo wameuawa. Waislamu wameuawa. Ukristo ni dini ya upendo. Unafundisha sio tu kumpenda jirani yako bali pia adui yako. Uislamu ni dini ya amani. Unafundisha unyenyekevu.

Kwa msingi huu ungedhani kuwa nchi inapokuwa na waislamu au wakristo basi amani,upendo na unyenyekevu vitatawala. Lakini kumbe mambo ni kinyume. Tumeona unyama usio na mfano. Watu wanamwaga damu kama vile wamepoteza akili na ubinadamu wao kabisa.

Dini pamoja kuwa zinahubiri amani na upendo hatuwezi kukataa kuwa ni dhana hatari sana. Katika dini kuna unafiki mkubwa sana. Wakati Saddam Hussein anapigwa vita kwa kuwa na silaha za maangamizi. Dini zaweza kuwa na unafiki na jazba za maangamizi.

Maafa haya ya Nigeria yalianza pale ilipoandikwa makala ikisema kuwa Mtume Muhammad angekuwa hai leo hii angependa kuchukua mmoja wa wanawake wanaoshindania taji la Miss World kama mke wake. Hawa watu 200 waliouawa hawakuandika hiyo makala. Wengi wao hata magazeti huwa hawasomi. Hawana fedha za kununulia magazeti. Hawana hata muda wa kusoma. Wanatumia magazeti kufungia maandazi, chumvi na bidhaa nyingine sio kuyasoma. Uandishi wa habari wala hawajui ni kitu gani.

Lakini wameuawa. Hakuna mtu mwenye haki yoyote ya kuondoa uhai wa mtu mwingine, awe amekashifu imani yako au la. Ndio maana dini hizi zinaamini juu ya siku ya hukumu. Kwanza ukichunguza kwa undani mahubiri ya dini moja utagundua kuwa ni kashfa kwa dini au imani nyingine. Hii ni kwa maana ya kashfa inayochukuliwa na waumini wengi.Tungekuwa hatutumii busara na maelewano tungekuwa tunauana kila kukicha.

Ninaposikia watu wanahubiri kuwa kuna siku ya mwisho na hiyo siku kuna watu watakaochomwa moto ninaweza kuja juu na kudai kuwa unanikashifu maana Mungu ninayemjua mimi (ambaye ndiye wa kweli...kumbuka kila mtu huamini Mungu wake ndio wa kweli!) hawezi kuoka baadhi ya watu na huku wengine wakiimba na kustarehe!

Kama wote tutakubaliana kuwa Mungu ni upendo. Na kuwa dini ziko duniani kwa ajili ya kufanya binadamu tuishi kwa wema, upendo na amani. Basi lazima tukubali pia kuwa kuna tatizo kama dini hizi hizi zinatufanya tuishi kwa chuki na unyama usio na mfano. Kuna tatizo kubwa sana.

Tatizo liko wapi? Liko kwenye vitabu vya dini hizi au kwa manabii walioleta ujumbe toka kwa Mungu (kama inavyodaiwa) au kwa walimu wanaotufundisha dini zenyewe au kwa binadamu tunaofuata hizi dini? Au hii ni silika yetu binadamu kupata furaha kwa kuleta majonzi na machungu kwa wengine? Au binadamu ni kiumbe ambaye kamwe hawezi kuwa mwema? Wema ni dhana tu ya kufikirika?

Inaelekea Mungu katuma manabii chungu nzima na vitabu vingi tu vimeandikwa na wahubiri wanakemea maovu kila siku lakini binadamu bado habadiliki. Ndivyo tulivyo? Hatuambiliki?

Kuna maswali mengi sana ya kujiuliza. Yuko mwanamuziki aliyewahi kuimba kuwa dunia hii ina maswali mengi kuliko majibu. Ni kweli lakini haitatuzuia kuuliza maswali. Sasa kama binadamu tukiwa na dini tunakuwa wauaji, wanafiki na maharamia huenda basi tusingekuwa na dini tungekuwa wema! Pengine unaweza kuona kuwa hii hoja ni ya kijinga. Sio.

Tazama kule Somalia kwa mfano. Wale Wasomalia wana dini moja, Uislamu, lakini tazama wanavyotwangana. Kule Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Rwanda na Burundi wengi ni Wakristo lakini tazama wanavyomalizana. Hawapigani kwasababu za kidini ila swali hapa ni kuwa iweje dini zao haziwasaidii kumaliza mifarakano hii?

Kule Mashariki ya Kati kuna vita visivyo na mwisho. Wapalestina na Waisraeli wote wana dini hawa. Tena kule ndiko zilikozaliwa hizi dini mbili za kuja. Kule ndiko manabii wa dini hizi walikoishi na kuhubiri lakini ndiko kuliko na machafuko yasiyo na mbele wala nyuma.

Inaweza kuwa vigumu kwa baadhi yetu kuelewa hoja hii ya kuwa huenda hatuhitaji dini kutokana na dhana potofu kuwa ukiwa huna dini unakuwa humwamini Mungu. Kuna watu, tena wengi tu, wanaodhani kuwa ili umwamini Mungu lazima uwe na dini. Kumbe wakati mwingine dini huzuia binadamu kumfahamu Mungu! Yaani dini inaweza kujenga ukuta wa chuma kati yako na Mungu.

Kila ninayemweleza hili huwa anamaka, " Haiwezekani kumwamini Mungu bila kuwa na dini. Yaani usiwe na dini kabisa? Sasa Mungu utamwaminije?" Tena wanaongeza, "Sasa kama huna dini ukifa utaenda wapi?" Wengi wetu kumbe basi huwa wana dini kwakuwa wana hofu ya kifo. Hawajui wakifa wanakwenda wapi hivyo basi wanakuwa na dini kwakuwa inawapa imani kuwa wakifa watakwenda mahali kuitwako mbinguni ambako kuna raha ya milele! Tafuta mbingu yako leo hii. Sio mpaka ufe!

Watu hawa huwa ninawaelewa kabisa. Unajua tumekuzwa na dhana fulani ambazo hatuthubutu kuzihoji na kuzipa changamoto. Dhana mojawapo ndiyo hii ya kuwa bila dini hakuna Mungu. Nyingine ni kuwa imani yako lazima iwe inaungwa mkono na mistari ya vitabu kadhaa vinavyoaminiwa kuwa vimeandikwa na watu waliotumwa na Mungu. Kama unayoamini hayako kwenye hivi vitabu basi wewe subiri moto tu siku ya mwisho.

Unaweza kuwa na imani ya Mungu bila kuwa dini na wala bila kuwa na kitabu chochote. Nenda kule Namibia au Botswana ukakutane na watu wa kabila la San. Ukikutana nao wauliza kama wana dini. Watakwambia hawana dini. Hii haimaanishi kuwa hawana imani ya kuwa kuna nguvu yenye uweza zaidi yetu ambayo wewe ndio unaiita Mungu. Wana imani tena nzito kweli ingawa hawana dini. Utamaduni wao unajumuisha mambo mbalimbali ya maisha mojawapo ni masuala ya kiroho. Kwahiyo kitendo cha mtu kuwa wa kabila hili tayari utamaduni wake unampa mtazamo fulani juu ya masuala ya imani na kiroho. Lakini hana dini. Wala hahitaji.

Mfano mwingine wa karibu ni Wamasai. Wao nao kama makabila yote Afrika wana imani nzito sana juu ya uwepo wa Mola lakini hawana dini. Hii ni kabla ya kuja kwa watu weupe na waarabu. Wana manabii kama akina Lenana na Phariti. Wana maelezo mazito tu juu ya kuumbwa kwa dunia. Wamisionari waliowaingilia na kuwaingiza kwenye ukristo walishindwa kabisa kuelewa mtazamo wao wa kiimani wakadhani eti kwa kuwa hawana dini basi wamepotea kabisa na dawa ni kuwaingiza katika ukristo ili kuwaokoa!

Juu ya hoja kuwa lazima imani iwe inaungwa mkono na maandishi, nitapenda kusema kuwa wako watu walioshika mistari yote ya vitabu vyao vya dini. Wakianza kuhubiri au kushusha aya utakoma. Lakini jaribu kuwauliza, " Hivi lakini Mungu ni nani au ni nini?" Watabaki wanatoa aya juu ya aya bila kutoa jibu. Kumbe unaweza kuwa mistari yote kichwani lakini bado usimjue Mungu. Na unaweza pia ukawa na dini lakini ukashindwa kuwa mtu mwema. Tena tujue kuwa imani juu ya Mungu zilikuwepo kabla ya binadamu kugundua maandishi.

Kwenye gumzo lile la Binadamu ni Utu nilisema kuwa dini imetumiwa mara nyingi sana katika kuhalalisha mambo ya ajabu. Labda kwa wasiofahamu, makaburu kule Afrika Kusini kwa mfano walitumia kanisa la Reformed kuhalalisha ubaguzi. Kwa mujibu wa imani yao, Mungu amewaumba wao kuwa bora kuliko watu weusi na hivyo ni jukumu lao kutawala nchi hiyo.

Hapa Marekani nako wako watu weupe wanaoamini kuwa Mungu kawapa hii nchi. Ni mali yao na hakuna watu wengine wenye haki ya kuishi hapa. Wanataka nchi hii itamkwe kuwa ni nchi ya kikristo. Wanataka amri kumi zitundikwe katika ofisi zote za serikali. Kule Mashariki ya Kati Waisraeli wanadai kuwa wamepewa nchi ile na Yehova hivyo Wapalestina hawana lao. Wana mistari chungu nzima ya kutetea hoja hii. Wapalestina nao wanadai nchi ni ya kwao. Tena kwa mujibu wa imani yao mji wa Yerusalem ni moja ya sehemu takatifu. Basi ubishi huu watu wasio na hatia wanakufa miaka nenda rudi.

Swali letu kuu bado hatujalijibu. Ni kitu gani kinafanya watu wamwage damu na kujenga chuki kwa sababu za kidini? Dini kazi yake si ndio kumaliza hizi chuki? Mbona sasa ndio inazikuza?

Hatutaweza kujibu maswali haya kama tutaogopa kuleta uwiano wa hisia na mantiki katika imani zetu. Tukiacha mantiki tupu itutawale tutakuwa tumekosea. Tukiacha pia hisia zitutawale tujue tumekwisha. Kutokana na hisia wakati mwingine tunaamini masuala ambayo katika hali ya kawaida huwezi hata kuthubutu kuyafikiria. Ni hisia tu ambazo zinaweza kwa mfano kutufanya tuamini kuwa eti mtoto mchanga aliyezaliwa leo hii tayari ana dhambi na asipomwagiwa maji kichwani akifa atakwenda motoni! Ni mtoto huyu huyu tunayeambiwa kuwa ufalme wa mbinguni ni kwa ajili yake.

Au kuamini kuwa kumpiga binadamu mwingine kwa mawe (tena sio mawe makubwa bali madogomadogo ili asife haraka) sio unyama kwa kuwa imeandikwa mahali fulani.

Kama dini imeshindwa kumkomboa binadamu tunahitaji dhana nyingine ya kumkomboa binadamu toka kwenye ulevi wa dini. Imetulevya. Tumeweka dini mbele ya ubinadamu wetu. Sio ndio? Hii dhana mpya itatoka wapi?... Kwenye vitabu? Historia? Utamaduni? Akilini? Nyoyoni?

Nitarudia tena: Ukristo unafundisha upendo, uislamu amani... uharamia huu wa nini sasa?

Ndio maana nalisema, hao wanasiasa wa bongo wenye majina ya kiislam/kikiristo sijaona muumini wa dini hizo, wote ni makaisaria!!!!!!
 
Kama mnapost kwa ushabiki wa dini, angalieni makala ya Ndesanjo Macha.



Ndio maana nalisema, hao wanasiasa wa bongo wenye majina ya kiislam/kikiristo sijaona muumini wa dini hizo, wote ni makaisaria!!!!!!

Ukiangalia TREND YOTE ya jinsi pesa za ufisadi zilivyogawanya...Utangundua kuwa ulikuwa ni mpango maalum kwani pesa zilikuwa nyingi kupindukia!

Waliojimilikisha migodi...Wakaanzisha na EPA na msururu wake ndio kama virusi!

Halafu kila mahali wakaweka wachagga na kuwaingiza humo kwenye ufisadi wao!Wengi tu!Tena pesa zenyewe zilianzia huko kwa wasilamu...Kina Iddi Simba na wamiliki wa BORA APTS,NDOVU SOAP NK!

Pesa hizo wakazi channel kwa watu ambao kisa ni wachaga tu maana hata walikuwa si watu wa ma connection kihivyo!Walizitapakaza kila mahali hadi marekani na kwingineko ulaya!

Sasa mpango wao unakuwa wazi...UDINI NA UKABILA!

Wale waliokuwa wakijuwa kuwa ccm itadaiwa kuwa ni mafisadi na huku ccm yenyewe ikiwa wazi kuwa ni chama cha waislam...Wakazipenyeza pesa za EPA kwa style ya kuchafuana na sasa ni PROPAGANDA TIME!

Tatizo bado narudia...Ni jf!

Trend ya pesa za ufisadi pamoja na kinachohubiriwa na ccm hapa unajuwa kuwa wizi wote ilikuwa ni wa kisiasa uliopangwa kimafia ili hata wale wapinzani wanaoelekea kushinda kwa hoja basi wachafuliwe!

Mfano mwingine ni hata jinsi wamekuwa wakijaribu kumchafua hata MWAKYEMBE!

Pesa walizochukuwa ni nyingi sana!Haziwezi kwisha...Na ni wazi serikali yetu inazitumia tena ili kuwaghilibu wananchi!Sidhani kama ni possible this time.

Ripoti ya EPA iko hapa...Tumeshazisoma na tunajuwa everything na ni nani wanahusika!

Wananchi naomba muelewe hili...Kwamba RIPOTI ZOTE ZIKISHAKUSOMWA...HAPO TUTAKUTA MAFISADI WENGI TU KUANZIA WAKRISTO,WAISLAM,WAHINDI,WACHAGGA,WASUKUMA,
WAMASAI NK!

Wote hao ni MAFISADI NA KAMWE WASILICHAFUE KABILA LOLOTE WALA DINI YOYOTE!

Watanzania DAINI UHURU WENU NA MTAONA MATUNDA YAKE!

TANZANIA NI NCHI TAJIRI INAYOMILIKIWA NA MAFISADI WACHACHE WA DINI TOFAUTI NA MAKABILA TOFAUTI WAKISHIRIKIANA NA MKOLONI WALIYENWUZIA NCHI!

Tunawaomba watanzania muwashurutishe wabunge wenu wadai ripoti za EPA NA MADINI NA ISSUES NYINGINE ZOTE HADI TUERUDISHIWE NCHI YETU!
 
Ukiangalia TREND YOTE ya jinsi pesa za ufisadi zilivyogawanya...Utangundua kuwa ulikuwa ni mpango maalum kwani pesa zilikuwa nyingi kupindukia!

Waliojimilikisha migodi...Wakaanzisha na EPA na msururu wake ndio kama virusi!

Halafu kila mahali wakaweka wachagga na kuwaingiza humo kwenye ufisadi wao!Wengi tu!Tena pesa zenyewe zilianzia huko kwa wasilamu...Kina Iddi Simba na wamiliki wa BORA APTS,NDOVU SOAP NK!

Pesa hizo wakazi channel kwa watu ambao kisa ni wachaga tu maana hata walikuwa si watu wa ma connection kihivyo!Walizitapakaza kila mahali hadi marekani na kwingineko ulaya!

Sasa mpango wao unakuwa wazi...UDINI NA UKABILA!

Wale waliokuwa wakijuwa kuwa ccm itadaiwa kuwa ni mafisadi na huku ccm yenyewe ikiwa wazi kuwa ni chama cha waislam...Wakazipenyeza pesa za EPA kwa style ya kuchafuana na sasa ni PROPAGANDA TIME!

Tatizo bado narudia...Ni jf!

Trend ya pesa za ufisadi pamoja na kinachohubiriwa na ccm hapa unajuwa kuwa wizi wote ilikuwa ni wa kisiasa uliopangwa kimafia ili hata wale wapinzani wanaoelekea kushinda kwa hoja basi wachafuliwe!

Mfano mwingine ni hata jinsi wamekuwa wakijaribu kumchafua hata MWAKYEMBE!

Pesa walizochukuwa ni nyingi sana!Haziwezi kwisha...Na ni wazi serikali yetu inazitumia tena ili kuwaghilibu wananchi!Sidhani kama ni possible this time.

Ripoti ya EPA iko hapa...Tumeshazisoma na tunajuwa everything na ni nani wanahusika!

Wananchi naomba muelewe hili...Kwamba RIPOTI ZOTE ZIKISHAKUSOMWA...HAPO TUTAKUTA MAFISADI WENGI TU KUANZIA WAKRISTO,WAISLAM,WAHINDI,WACHAGGA,WASUKUMA,
WAMASAI NK!

Wote hao ni MAFISADI NA KAMWE WASILICHAFUE KABILA LOLOTE WALA DINI YOYOTE!

Watanzania DAINI UHURU WENU NA MTAONA MATUNDA YAKE!

TANZANIA NI NCHI TAJIRI INAYOMILIKIWA NA MAFISADI WACHACHE WA DINI TOFAUTI NA MAKABILA TOFAUTI WAKISHIRIKIANA NA MKOLONI WALIYENWUZIA NCHI!

Tunawaomba watanzania muwashurutishe wabunge wenu wadai ripoti za EPA NA MADINI NA ISSUES NYINGINE ZOTE HADI TUERUDISHIWE NCHI YETU!
__________________
 
Hakuna udini Raisi aondoe udini gani?CCM haiteuwi wajumbe bali wanapigiwa kura!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom