Kubwajinga
JF-Expert Member
- Jan 23, 2008
- 2,194
- 297
Viongozi wakuu wa Chadema hawapo ila Mbowe peke anaonekana kubanana na Lowasa
Wimbi la kuanzishwa chama cha ACT kulikuwa na mengi yaliuyoongelewa kuhusu udikteta ndani ya Chadema unaofanywa na Mbowe, pia kwamba kuna msuguano kati ya Mbowe na Slaa, ingawa ilikanushwa lakini ufa huo unaonekana kujitokeza sasa.
Kilichoendelea ni CHADEMA kuonekana kumwandaa Slaa kuwa mgombea wa Urais. Pia Slaa kuonekana kukubalika kimataifa hata kualikwa na mataifa makubwa au jumuia za kimataifa duniani kama Marekani, Ujerumani na Umoja wa nchi za Ulaya.
UKAWA ilionekana NCCR wako radhi Dr Slaa awe mgombea, ila upade wa CUF Lipumba hakuridhika na alitaka yeye agombee. Mbowe alipoonekana kumilikiwa na kisha kummiliki Lowassa kuwa mgombea, Lipumba akapoa kwa vile wote yeye na Slaa wamekosa, huko alikokuwa mafichoni akajifichua na kuanza kuonekana katika vikao vya UKAWA.
Mgawanyiko Kamati Kuu CHADEMA kutokana na Lowassa
Katibu Mkuu Slaa, makamu wake bara John Mnyika na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu hawakushiriki mapokezi ya Lowassa wakati walionekana wako na moyo kwa mapokezi ya Lembeli na wengineo. Dalili kwamba Lowassa ni chaguo la Mbowe na kushinikiza kamati kuu waridhie matakwa yake.
Mbowe amkumbatia Lowasa anayewawakilisha Rostam na Chenge
CHADEMA ilijipambanua na kueleweka kwa umma kwamba wako kinyume kabisa na ufisadi na katu hawatakaa sahani moja na mafisadi, lakini leo Freeman Mbowe anakula sahani moja na fisadi Lowasa anayewakilisha mafisadi wenzake akina Rostam Aziz na Chenge.
LOWASA AKWEPA MASWALI YA WAANDISHI KUHUSU KUWAKUMBATIA MAFISADI WENZAKE
Katika tukio la kukabidhiwa kadi za Chadema, Lowasa alipoulizwa na waandishi kuhusu yasemwayo na watu kwamba akiwa Rais atawakaribisha mafisadi wenzake Chenge na Rostam, hakujibu akakwepa na kusema tu anachukia ufukara na anataka watanzania wengi wawe matajiri. Hapo kuna jambo ambalo dhahiri analikwepa kuliweka wazi kuhusu uhusika wake kugombea urais nyuma yake wakiwamo mafisadi Chenge na Rostam. Akishakalia kiti cha magogoni ni mfalme nani wa kumnyoshea kidole?
Muono mzuri lakini mengi hayatajulikana mpaka uchaguzi utakpoisha. CHADEMA = Mbowe LLC, mjinga tu ndiye hatalielewa hilo. Kwa hiyo CDM kumkumbatia Lowassa mla rushwa ni kwa manufaa ya Mbowe LLC na sio kwa ajili ya kuwasaidia watanzania.