Udhalilishaji wa Urais kama taasisi ni lazima ukome, kama tunaitaka Tanzania inayoendelea!!

NewOrder

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
2,119
2,830
Wengi wamegeuza jambo hili kama la Rais dhini ya CDM. Wengi, hata waliomsifu JK kwa kukutana na CDM, sasa wanailaumu CDM na kusema kuwa JK kapata ushindi. Katika hali ya ukweli, CDM na Rais wameshinda na walioshindwa ni sisi wananchi wa kawaida.

CDM imefanikiwa kumwonesha sio Makinda tu, bali hata Rais ni nini kiliwafanya watoke Bungeni. Hata walipokutana nae waliyasema mapungufu yale yale waliyoyataje Bungeni. JK kawaonesha kuwa alichowaahidi wazee wa Dar es Salaam nimetimia licha ya "kelele za wapinzani" ambao kufanya nao mazungumzo hakukuwa na maana yoyote.

Niliandika katika post jana kuwa JK amedhalilisha Urais kama taasisi. Ikiwa Rais anakubaliana na mtu kuboresha muswada na siku moja baadae anausaini katika hali ile ile ya mwanzo, anajionesha ni muongo, mnafiki na mtu asiyeweza kuaminiwa. Bahati mbaya anayoyafanya anadhani ni sahihi kama mtu, anasahau ni taasisi ya Urais ndiyo inaharibiwa.

Haiwezekani tayari JK amekwishaboresha muswada, siku moja baada ya mazungumzo. Na sasa ni sheria na hawezi kuibadilisha sheria, labda ifutwe na kuna taratibu zake pia. JK amelikosesha taifa hili njia ya kumaliza mambo kwa kujadiliana. Akiona sasa njia nyingine zinatumika, asilalamike!! Ametumia mamlaka yake kama Rais na sasa aache wengine watumie mamlaka yao. Na mamlaka hizo zimeainishwa katika Katiba hii ya sasa. Anaendeza utaratibu wa kuamua mambo ya kitaifa kwa mtazamo wa kiCCM.

Ndio maana hata ufisadi unaoliathiri taifa, unaachwa kuendelea au hauadhibiwi kwa sababu CCM itaumizwa!! Akiwa mwenyekiti wa CCM anaona wajibu wa kwanza ni kwa CCM na kwa taifa ni jambo la pili. Binafsi sitapenda kuona chama chochote cha siasa kinapewa umuhimu kuliko maswala ya kitaifa yanayoathiri maisha ya watu wengi wawe ni wanachama au si wanachama wa chama kilicho madarakani. Bila shaka, udhaifu au wa serikali ya CCM au chama hicho, unamwathiri kila mtu isipokuwa viongozi wakuu wa serikali hii na CCM.

JK amelikosea taifa hili kuliko hata Makinda, CCM na CDM!! Yeye ndiye alikuwa na mamlaka ya mwisho au kuleta matatizo au kuyamaliza! Bila shaka ataishi kuona uzuri au ubaya wa maamuzi yake. Nadhani atakuwa tayari kupokea zao lolote la uamuzi wake!!

Huenda sasa ni zamu ya wananchi kusikilizwa!!
 
Nachelea kuchangia, lakini siku zote naamini kwamba "U-Rais si jambo la kukimbilia!"
 
Hata katika hotuba za Baba wa Taifa Mwl. Nyerere alisema kuwa 'Ikulu sio mahali pa kukimbilia, ni mahali pa matatizo makubwa' Ila kwa sasa Ikulu ni mahali pa kwenda kuchukua hazina yako na familia yako basi, sio kwa maslahi ya watanzania.
 
Mzee jakaya huenda ametingwa. Mambo mengi. Huku magamba tena yanajaribu hata kumgusagusa hata yeye. Huku katiba. Huku mfumko wa bei ulioshindikana, huku sarafu, nk, nk. Inahitaji KICHWA hata kukumbuka uliyosema na uliyotenda jana ikifika leo. Ndiyo maana Mwalimu alitahadharisha kuwa ikulu si mahali pa kukimbilia, ikulu ni matatizo matupu!
 
Utaboreshwa kupitia miscellaneous amendments kama inavyofanyika katika sheria zingine. Vile vle hawakukubaliana kwamba muswada usisainiwe (Presidential assent) acheni kupotosha.
 
Alichofanya Kikwete ni kuogopa CCM, wabunge pamoja na mbwembwe zake wakati anahutubia wazee wa ccm pale dar. Ingawa hoja za CDM zilimwingia barabara alikuwa hana jinsi kwani kama asinge sign angepoteza imani na kuonekana amewadharau wabunge wa ccm. Njia pekee iliyobakia ni kupeka marekebisho katika bunge lijalo. ingawa hili nalo linaonyesha udhaifu na uwezo wa watendaji wa serikali
 
Alichofanya Kikwete ni kuogopa CCM, wabunge pamoja na mbwembwe zake wakati anahutubia wazee wa ccm pale dar. Ingawa hoja za CDM zilimwingia barabara alikuwa hana jinsi kwani kama asinge sign angepoteza imani na kuonekana amewadharau wabunge wa ccm. Njia pekee iliyobakia ni kupeka marekebisho katika bunge lijalo. ingawa hili nalo linaonyesha udhaifu na uwezo wa watendaji wa serikali

Yes, kupeleka marekebisho katika Bunge lile lile, Bunge lililojaa wanazi wa CCM, Bunge la Spika Makinda, Bunge la akina Wassira waimba Taarabu na wasinziaji wakuu, Bunge la akina Mrema na Shibuda wafuata Upepo, Bunge la akina Komba na Lusinde wasioelewa nini kimeandikwa kwenye mswaada, we might be kidding kudhani marekebisho yatakuwa na manufaa yoyote kwa Taifa. Nafasi tumeipoteza, tutaijutia na gharama yake sote tutaibeba akiwemo Rais Kikwete.
 
Back
Top Bottom