Udhalilishaji: Video ya PNC akimuomba msamaha Ostaz Juma na Musoma

Hi ni misaada au biashara maana misaaada mingi ya masharti ndio inawataka watu waruhusu ushoga .yaani ukikubali kusaidiwa ni sawa na kukubali kupoteza utu wako.Angalia huyo jamaa jinsi anavyodhalilika hapo
 
Huku ni kudhalilika kipaji chako lakini mpaka umnyenyekee mtu ndo uone faida ya kipaji chako Wasanii badilikeni....
 
inauma. ndo wanaanzaga hv usishangae ukasikia msanii kachezwa mchezo mchafu
 

PNC AKIMWOMBA MSAMAHA USTAZ JUMA - YouTube

Mimi kama mdau wa muziki wa kizazi kipya napinga na kulaani huu udhalilishaji wanaofanyiwa wasanii wetu.

Nimestushwa kuona hii video inayosambaa kwenye social network ambayo member wa zamani wa kundi la Watanashati PNC akiwa amempigia magoti don wa kundi hilo Ostaz Juma Namusoma huku akimwomba msamaha.

Hakika hii video inaondoa thamani ya wasanii wetu na kuonesha kuwa bila hao wanyonyaji wanaojiita mameneja wa wasanii basi muziki sio kitu.

Na nyie wasanii muwe na msimamo thabiti na sio kuhama hama makundi kama malaya na ndiyo maana mnaishia kudhalilishwa kwa ujinga wenu.

Na ninyi madon wa muziki acheni kudhalilisha wasanii,kwa kuwanyonya inatosha tu na sio kuanza kuwaanika kwenye mitandao mambo wanayofanya.Mimi sijafurahishwa kabisa na hii video.

Narudia tena; Nalaani vikali huu udhalilishaji kwa wasanii.

attachment.php

Dogo nadhani hujajitambua kwamba una kitu ambacho hata huyo unayemwomba msamaha hana.Kuwa na meneja ni vzr ila angalia usiwe mtumwa.Hayo ni mambo ya mwaka 47 upo kwenye game long time hebu jiamini YOU CAN DO ALONE.
Kuomba radhi ni sawa hata mbele za Mungu but not in that way aaaaah.So chochote asemacho utafanya?Hebu sometime kuwa mbishi kama dada yetu JIDE kagoma nyimbo zisipigwe radio flani na kaweza na anasonga mbele.POLE DOGO
 
Last edited by a moderator:
Nadhani hio video ingeendelea kdg P.N.C atakuwa alipewa mic ahitubie taifa....kuimba niimbe mm halafu magoti nkupigie ww?...nani atakuthamini tena kwa video kama hii.
 
Mkuu, Ostaz Juma Namusoma ni mdau wa muziki hapa nchi na ndo anawamiliki wasanii walio chini ya lebo ya watanashati.Anapenda kuimbwa sana na wasanii.
eh... kumbe hawa wadogo wanamilikiwa, huku ni sawa na kuolewa tu.....
 
Nakumbuka kuna kipindi pale clouds walikuwa wanahojiwa PNC na ostadh Juma, Adam akawa anawaongelesha ngeli, mungu wangu hayo majibu ya PNC nilichoka bora ostadh alikubali kabisa yeye mburula wa hyo lugha
 
Na sasa iwe uthibitisho kwa wasanii na mashabiki kwamba kipaji bila elimu bongo ni unsecured business.Ndio utapiga pesa kwa muda na mara zote wewe sio mwamuzi,ni wengine.Kipaji chako wamiliki wengine.kuwepo kwa njia mjabadala (elimu) kunakufanya ujimiliki mwenyewe. KWA WALIOKARIBU NA HUYO JUMA MWAMBIE NA AWEKE MIKATABA YA WASANII WAKE KTK SOCIAL MEDIA.

kweli ukubwa wa mwili na umri sio uwingi wa akili.
 
Hawa wasanii pesa pesa wanazokamata wangekuwa smart kuwekeza kwenye miradi mbalimbali wala wasingezalilika hivo.

Tatizo wakipata pesa ni anasa tu watadhalilishwa sana.

Angekuwa ana miradi mingi asingekubali kudhalilishwa hivi.wajenge utaratibu wa kujisomea vitabu kuongeza maarifa
 
Hivi mtu akikukosea halafu akuombe radhi kweli kama ni kumsamehe ni mpaka akupigie goti?????!!!!!!

Kazzzzziiiiiii kweli
 
NAPITA tafadhali tutambulishe tusiofahamu. Aliyepigiwa magoti ni nani na anayepiga magoti ni nani? Wana mahusiano gani?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom