PNC AKIMWOMBA MSAMAHA USTAZ JUMA - YouTube
Mimi kama mdau wa muziki wa kizazi kipya napinga na kulaani huu udhalilishaji wanaofanyiwa wasanii wetu.
Nimestushwa kuona hii video inayosambaa kwenye social network ambayo member wa zamani wa kundi la Watanashati PNC akiwa amempigia magoti don wa kundi hilo Ostaz Juma Namusoma huku akimwomba msamaha.
Hakika hii video inaondoa thamani ya wasanii wetu na kuonesha kuwa bila hao wanyonyaji wanaojiita mameneja wa wasanii basi muziki sio kitu.
Na nyie wasanii muwe na msimamo thabiti na sio kuhama hama makundi kama malaya na ndiyo maana mnaishia kudhalilishwa kwa ujinga wenu.
Na ninyi madon wa muziki acheni kudhalilisha wasanii,kwa kuwanyonya inatosha tu na sio kuanza kuwaanika kwenye mitandao mambo wanayofanya.Mimi sijafurahishwa kabisa na hii video.
Narudia tena; Nalaani vikali huu udhalilishaji kwa wasanii.
mhh mhh mhhAsije akamuomba *148*00# tu
eh... kumbe hawa wadogo wanamilikiwa, huku ni sawa na kuolewa tu.....Mkuu, Ostaz Juma Namusoma ni mdau wa muziki hapa nchi na ndo anawamiliki wasanii walio chini ya lebo ya watanashati.Anapenda kuimbwa sana na wasanii.