Udhaifu wa JK ulikuwa wapi? Je ni kuruhusu demokrasia kwa kufuata katiba? Au ni baada ya ufisadi kufichuliwa?

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Wanajamvi,

Kumekuwepo na maneno kutoka kila pande za siasa! Maneno yenye kuzungumzia kauli aliyowahi kuitoa John Mnyika pamoja na Dr Slaa!

Sasa hayo maneno ambayo ni kama “tafsiri” zenye kuelezea au kudokeza, kuhusu udhaifu huo!

Spika wa Bunge Ndugai, amesema kuwa serikali ya sasa siyo dhaifu kwasababu kuna watu wako Segerea. Hapa naona spika mwenyewe pengine haelewi hata anachoongea! Kama anazungumzia kina Mbowe kuwepo segerea kwamba ndo kuonyesha uimara wa Maghufuli, basi hajaonyesha werevu wala weledi kwenye mambo yenye kuhitaji sifa hizo.

Kiukweli Mnyika alitaja jina kabisa! Hakusema “serikali ni dhaifu”! Pia tukumbuke kuwa serikali ina mihimili mitatu.

Kama anazungumzia kuwepo ndani kwa viongozi wa chadema kuwa ni uimara wa Maghufuli, basi hapo inaonyesha wazi kabisa kuwa hakuna uhuru kwenye mihimili!

Na ndiyo maana hakuna checks and balances! Hata yaliyotokea juzi dhidi ya CAG, yana akisi hilo la uelewa mdogo miongoni mwetu especially viongozi Mfano wa Ndugai!

Labda angesema “muhimili wa mahakama siyo dhaifu”!, Lakini alichokisema Mnyika? Siyo sawa na anachokisema huyu Spika!

Mambo yaliyokuwa yakitokea hadi JK kuitwa dhaifu na Mnyika pamoja na Dr Slaa, siyo kwasababu aliacha kuwafunga wapinzani, kuminya demokrasia nk. Ila ni kutokuwachukulia hatua wale ambao ni “wenye ccm”, na haya yalichagizwa na ile kauli ya Waziri Mkuu wa wakati ule Mizengo Kayanza Pinda, ambaye alisema wazi kabisa “kuna watu hawagusiki” na kwamba wakiguswa, “uchumi utayumba”, kiukweli, hilo ndilo lilikuwa msingi mkuu wa kuitwa dhaifu! Na siyo vinginevyo kama wengi wetu wanavyotaka kutuaminisha!

Watu wa ccm walitengeneza kitu kinaitwa “spin”, ambapo ni njia ya kuugaragaza ukweli na kupindisha maana halisi ili kuweza kukidhi haja ama mahitaji yao!

Wengine wanasema “JK aliwapa demokrasia mkamuita dhaifu”, kauli ambazo zinaonyesha kuwa hatuko serious hata kiodogo. Tuko kama zecomedy!

Kusema eti “JK aliwapa demokrasia”, maneno ya jingalao , inaonyesha jinsi ambavyo tuko kwenye “different paradigms” kwenye mustakabali wa Taifa hili, yani kumbe demokrasia wao wanachukulia kama ni privileged au kama favor flani hivi wanayotupatia, na wala siyo haki inayolindwa na katiba yetu! Katiba hiyo hiyo anayoitumia mkuu wa nchi kuapa!

Hadi usawa huu! Wale wa ccm wana mentality flani hivi kuona kwamba wapinzani ni kama favor tu wanapewa, mentality hii, ni mbaya sana, maana ni kama wengine wana haki milki ya nchi yetu na wengine wanategemea huruma zao! Haya yote kwa maoni yangu, yanasababishwa na katiba iliyopo.

Ni katiba hii hii, ambayo anaweza akaja rais akawa dhaifu ama akawa dikteta!

Sasa spika wa Bunge hajui hata maana halisi inayozungumziwa! Na ndiyo maana hata CAG aliposema Bunge ni dhaifu, yeye akakimbilia mambo ya polisi na pingu! Hapo utafahamu kuwa kichwani ni mtupu kabisa! Sijui hata hawa watu huwa wanafikaje kwenye hizo nafasi? Ama ndo udhaifu wenyewe huo?

Kwasababu bunge likiacha kuburuzwa kwasababu ya udhaifu na uelewa wa spika, hapo ndipo tutakuwa na taasisi ama mihimili imara! Kama mahakama inafuata matakwa ya rais, haina maana kwamba hakuna udhaifu. Hapo serikali ni dhaifu kwani muhimili wa mahakama unaburuzwa!

Wana ccm wengi, Maghufuli akiwa mmojawapo, walitafsiri udhaifu wa ccm kuwa ni pamoja na ku “leak” kwa zile kashfa Mfano EPA, KAGODA, MEREMETA, BUZWAGI, RICHMOND, Rada, mapanki nk, vyote kujulikana kwake, ndivyo walivyochukulia kuwa ni udhaifu.

Yani kuficha ufisadi Mfano ile trillion 1.5, ndo kuwa “strong “... Mfano angekuwa upande wa CAG, basi asingekuwa dhaifu kwa maoni yangu, zaidi ya hapo ni dhaifu kuliko JK!
 
Mlimuona JK hachukui hatua angali alikuwa anachukua!
Mlimuona mpole sasa amekuja mkali...anayechukua hatua kiasi mnasema ananyanyasa mafisadi sielewi mnasimamia nini.
Demokrasia mnayoitaka haipo duniani wala hata kwenye chama chenu.
 
Mlimuona JK hachukui hatua angali alikuwa anachukua!
Mlimuona mpole sasa amekuja mkali...anayechukua hatua kiasi mnasema ananyanyasa mafisadi sielewi mnasimamia nini.
Anayechukuwa hatua gani? Kwani upole au ukali ni sifa inayotakiwa kuchaguliwa kati katiba mbovu na nzuri?

Wapi nimesema ananyanyasa mafisadi? Mbona hii JF ambayo ilisaidia kufichua ufisadi Mfano RICHMOND na EPA, yeye anaichukia? Kama una nia nzuri, kwanini uchukie wanaofichua maovu? Maghufuli namshangaa sana hapo kusema ukweli. Wapi uwajibikaji? Ni nadhani yeye ndo ameonyesha udhaifu!
 
CCM wana tafsiri udhaifu wa JK ni baada ya serikali yake kupelekeshwa na kashfa za ufisadi! Kuzuia kashfa zisijulikane ndo udhaifu wenyewe! Tena ule mbaya utakaolimaliza taifa!
 
Mlimuona JK hachukui hatua angali alikuwa anachukua!
Mlimuona mpole sasa amekuja mkali...anayechukua hatua kiasi mnasema ananyanyasa mafisadi sielewi mnasimamia nini.
Demokrasia mnayoitaka haipo duniani wala hata kwenye chama chenu.
Katiba, kanuni na sheria zetu hazimruhusu Rais kuwa dikteta, rais bora ni yule anayetekeleza matakwa ya sheria hata kama sheria hiyo ni mbaya. Ndiyo maana JK aliridhia katiba iandikwe upya ili wananchi tuamue tunataka rais wa namna gani pia.
 
Wanajamvi,

Kumekuwepo na maneno kutoka kila pande za siasa! Maneno yenye kuzungumzia kauli aliyowahi kuitoa John Mnyika pamoja na Dr Slaa!

Sasa hayo maneno ambayo ni kama “tafsiri” zenye kuelezea au kudokeza, kuhusu udhaifu huo!

Spika wa Bunge Ndugai, amesema kuwa serikali ya sasa siyo dhaifu kwasababu kuna watu wako Segerea. Hapa naona spika mwenyewe pengine haelewi hata anachoongea! Kama anazungumzia kina Mbowe kuwepo segerea kwamba ndo kuonyesha uimara wa Maghufuli, basi hajaonyesha werevu wala weledi kwenye mambo yenye kuhitaji sifa hizo.

Kiukweli Mnyika alitaja jina kabisa! Ha kusema “serikali ni dhaifu”, na tukumbuke kuwa serikali ina mihimili mitatu. Kama anazungumzia kuwepo ndani kwa viongozi wa chadema kuwa ni uimara wa Maghufuli, basi hapo inaonyesha wazi kabisa kuwa hakuna uhuru kwenye mihimili! Na ndiyo maana hakuna checks and balances! Hata yaliyotokea juzi dhidi ya CAG, yana akisi hilo la kuelewa mdogo miongoni mwetu especially viongozi Mfano wa Ndugai!

Labda angesema muhimili wa mahakama siyo dhaifu! Lakini alichokisema Mnyika? Siyo sawa na anachokisema huyu Spika!

Mambo yaliyokuwa yakotokea hadi JK kuitwa dhaifu na Mnyika pamoja na Dr Slaa, siyo kwasababu aliacha kuwafunga wapinzani, kuminya demokrasia nk. Ila ni kutokuwachukulia hatua wale ambao ni “wenye ccm”, na haya yalichagizwa na ile kauli ya Waziri Mkuu wa wakati ule Mizengo Kayanza Pinda, ambaye alisema wazi kabisa “kuna watu hawagusiki” na kwamba wakiguswa, “uchumi utayumba”, kiukweli, hilo ndilo lilikuwa msingi mkuu wa kuitwa dhaifu! Na siyo vinginevyo kama wengi wetu wanavyotaka kutuaminisha! Watu wa ccm walitengeneza kitu kinaitwa “spin”, ambapo ni njia ya kuugaragaza ukweli na kupindisha maana halisi ili kukidhi haja ama mahitaji yao! Wengine wanasema “JK aliwapa demokrasia mkamuita dhaifu”, kauli ambazo zinaonyesha kuwa hatuko serious hata kiodogo. Tuko kama zecomedy!

Kusema eti “JK aliwapa demokrasia”, maneno ya jingalao , inaonyesha jinsi ambavyo tuko kwenye “different paradigms”, yani kumbe demokrasia wao wanachukulia kama ni privileged wanayotupatia, na wala siyo haki inayolindwa na katiba yetu! Katiba hiyo hiyo anayoitumia mkuu wa nchi kuapa!

Hadi usawa huu! Wale wa ccm wana mentality flani hivi kuona kwamba wapinzani ni kama favor tu wanapewa, mentality Hii ni mbaya sana, maana ni kama wengine wana haki milki ya nchi yetu na wengine wanategemea huruma zao! Haya yote kwa maoni yangu, yanasababishwa na katiba iliyopo.

Ni katina hii hii, ambayo anaweza akaja rais akawa dhaifu ama akawa dikteta!

Sasa spika wa Bunge hajui hata maana halisi inayozungumziwa! Na ndiyo maana hata CAG aliposema Bunge ni dhaifu, yeye akakimbilia mambo ya polisi na pingu! Hapo utafahamu kuwa kichwani ni mtupu kabisa! Sijui hata hawa watu huwa wanafikaje kwenye hizo nafasi? Ama ndo udhaifu wenyewe huo?

Kwasababu bunge likiacha kuburuzwa kwasababu ya udhaifu na uelewa wa spika, hapo ndipo tutakuwa na taasisi ama mihimili imara! Kama mahakama inafuata matakwa ya rais, haina maana kwamba hakuna udhaifu. Hapo serikali ni dhaifu kwani muhimili wa mahakama unaburuzwa!

Wana ccm wengi, Maghufuli akiwa mmojawapo, walitafsiri udhaifu wa ccm kuwa ni pamoja na ku “leak” kwa zile kashfa Mfano EPA, KAGODA, MEREMETA, BUZWAGI, Rada, mapanki nk, vyote kujulikana kwake, ndivyo walivyochukulia kuwa ni udhaifu.

Yani kuficha ufisadi Mfano ile trillion 1.5, ndo kuwa “strong “.. Mfano angekuwa upande wa CAG, basi asingekuwa dhaifu, zaidi ya hapo ni dhaifu kuliko JK!

Monoko Mushi,

CCM ni chama cha kinafiki... wanarukaruka kama panzi... kazi kutafuta maslahi! they will never admit mapungufu yao wala kuyachukulia hatua thabiti za kisheria iwe ndani ya chama au kwenye sheria za nchi.

10 years from today we will be discussing mapungufu ya Uongozi wa Magufuli na jinsi vita dhidi ya mafisadi na kuondoa umasikini ilivyoshindwa... then kama kawaida Wapambe na mashabiki maandazi watashangilia slogan mpya za Mgombea na Mwenyekiti wa CCM Taifa!

Think about it: Nyerere alikuwa na Uhur na kazi, Ujamaa na Kujitegemea Kilimo ni uti wa mgongo, wakashangilia sana... akaja Mwinyi na Ruksa na fagio la chuma... wakapanda miti kama tumbili kupiga mayowe ya furaha... akaja Mkapa na uwazi na kuuza mashirika yaliyotaifishwa kutokana na Azimo la Arusha na siasa ya Ujamaa na kujitegemea... wakatunisha vifua mbele kusema sasas Uchumi ni dhahiri utakuwa... akatinga Kikwete na Ari, Kasi na Nguvu Mpya.. then Kilimo Kwanza.. wakasadifu mpaka Ilani na mapambio kemkem kusifia fikra za Mwenyekiti..

Now they areall hyped up with HapaKaziTu na MATAGA... lakini ukiuliza Ujamaa na Kujitegemea kwa mujibu wa Katiba Ya CCM ( na ya nchi) wako wapi kujenga jamii yenye kujitegemea, kuishi kijamaa ili kushinda Ujinga Umasikini na maradhi.. watakupa talalila nyingi za kusifia flyover na ndege za ATCL kuwa ni maendeleo...
Ask them asilimia ngapi ya Wananchi sasa wana uwezo wa kujitegemea na kuchangia huduma za elimu an afya bila kutegemea bure ya serikali....watadai wewe ni kuwadi wa mabeberu wasioitakia tanzania mema!

CCM ni mufilis! Wanadandia slogan za Wagombea na Wenyekiti wa Chama lakini kufanya kazi kufuta umasikini, ujinga na maradhi hawataki!
 
Wanajamvi,

Kumekuwepo na maneno kutoka kila pande za siasa! Maneno yenye kuzungumzia kauli aliyowahi kuitoa John Mnyika pamoja na Dr Slaa!

Sasa hayo maneno ambayo ni kama “tafsiri” zenye kuelezea au kudokeza, kuhusu udhaifu huo!

Spika wa Bunge Ndugai, amesema kuwa serikali ya sasa siyo dhaifu kwasababu kuna watu wako Segerea. Hapa naona spika mwenyewe pengine haelewi hata anachoongea! Kama anazungumzia kina Mbowe kuwepo segerea kwamba ndo kuonyesha uimara wa Maghufuli, basi hajaonyesha werevu wala weledi kwenye mambo yenye kuhitaji sifa hizo.

Kiukweli Mnyika alitaja jina kabisa! Hakusema “serikali ni dhaifu”! Pia tukumbuke kuwa serikali ina mihimili mitatu.

Kama anazungumzia kuwepo ndani kwa viongozi wa chadema kuwa ni uimara wa Maghufuli, basi hapo inaonyesha wazi kabisa kuwa hakuna uhuru kwenye mihimili!

Na ndiyo maana hakuna checks and balances! Hata yaliyotokea juzi dhidi ya CAG, yana akisi hilo la kuelewa mdogo miongoni mwetu especially viongozi Mfano wa Ndugai!

Labda angesema “muhimili wa mahakama siyo dhaifu”!, Lakini alichokisema Mnyika? Siyo sawa na anachokisema huyu Spika!

Mambo yaliyokuwa yakotokea hadi JK kuitwa dhaifu na Mnyika pamoja na Dr Slaa, siyo kwasababu aliacha kuwafunga wapinzani, kuminya demokrasia nk. Ila ni kutokuwachukulia hatua wale ambao ni “wenye ccm”, na haya yalichagizwa na ile kauli ya Waziri Mkuu wa wakati ule Mizengo Kayanza Pinda, ambaye alisema wazi kabisa “kuna watu hawagusiki” na kwamba wakiguswa, “uchumi utayumba”, kiukweli, hilo ndilo lilikuwa msingi mkuu wa kuitwa dhaifu! Na siyo vinginevyo kama wengi wetu wanavyotaka kutuaminisha!

Watu wa ccm walitengeneza kitu kinaitwa “spin”, ambapo ni njia ya kuugaragaza ukweli na kupindisha maana halisi ili kuweza kukidhi haja ama mahitaji yao!

Wengine wanasema “JK aliwapa demokrasia mkamuita dhaifu”, kauli ambazo zinaonyesha kuwa hatuko serious hata kiodogo. Tuko kama zecomedy!

Kusema eti “JK aliwapa demokrasia”, maneno ya jingalao , inaonyesha jinsi ambavyo tuko kwenye “different paradigms” kwenye mustakabali wa Taifa hili, yani kumbe demokrasia wao wanachukulia kama ni privileged au kama Gabor flani hivi wanayotupatia, na wala siyo haki inayolindwa na katiba yetu! Katiba hiyo hiyo anayoitumia mkuu wa nchi kuapa!

Hadi usawa huu! Wale wa ccm wana mentality flani hivi kuona kwamba wapinzani ni kama favor tu wanapewa, mentality hii, ni mbaya sana, maana ni kama wengine wana haki milki ya nchi yetu na wengine wanategemea huruma zao! Haya yote kwa maoni yangu, yanasababishwa na katiba iliyopo.

Ni katiba hii hii, ambayo anaweza akaja rais akawa dhaifu ama akawa dikteta!

Sasa spika wa Bunge hajui hata maana halisi inayozungumziwa! Na ndiyo maana hata CAG aliposema Bunge ni dhaifu, yeye akakimbilia mambo ya polisi na pingu! Hapo utafahamu kuwa kichwani ni mtupu kabisa! Sijui hata hawa watu huwa wanafikaje kwenye hizo nafasi? Ama ndo udhaifu wenyewe huo?

Kwasababu bunge likiacha kuburuzwa kwasababu ya udhaifu na uelewa wa spika, hapo ndipo tutakuwa na taasisi ama mihimili imara! Kama mahakama inafuata matakwa ya rais, haina maana kwamba hakuna udhaifu. Hapo serikali ni dhaifu kwani muhimili wa mahakama unaburuzwa!

Wana ccm wengi, Maghufuli akiwa mmojawapo, walitafsiri udhaifu wa ccm kuwa ni pamoja na ku “leak” kwa zile kashfa Mfano EPA, KAGODA, MEREMETA, BUZWAGI, RICHMOND, Rada, mapanki nk, vyote kujulikana kwake, ndivyo walivyochukulia kuwa ni udhaifu.

Yani kuficha ufisadi Mfano ile trillion 1.5, ndo kuwa “strong “... Mfano angekuwa upande wa CAG, basi asingekuwa dhaifu kwa maoni yangu, zaidi ya hapo ni dhaifu kuliko JK!
Sina la kuongeza, umeandika vizuri, sidhani kama kuna mtu wa CCM anaweza ku comprehend hii! Bravo!

Spika Ndugai: Si mlisema serikali iliyopita ilikuwa dhaifu, sasa mnaona, serikali hii, wengine wako Segerea - JamiiForums
 
Shida ya Bavicha ni kukariri na Sio kuelewa.Unapozungumzia Udhaifu au uimara wa Uongozi flani unaangalia nyanja nyingi.Serikali dhaifu haiwez kukusanya kodi, Inawachekea mafisadi, wazembe makazini, wanasiasa uchwara nk.Wakati wa Jk kulikua na mapungufu mengi mno kuliko mazuri. Wapinzani walikua wanaburuzwa mahakaman lkn Wanaachiwa,Ushawahi jiuliza kwanini kesi zao zilikua zinayeyukia juu kwa juu?Kwamba walikua wanashinda kesi huko mahakaman?Swala ni maagizo kutoka juu tu,bwana hao jamaa waachieni waendelee na mambo yao. Muhimili wa Mahakama haujaanza kuingiliwa leo hata huu wa Bunge pia. Angalia kesi zilizokuwa zinawakabili akina Yona,Mramba,Mahayu, Zombe nk jinsi zilivyokuwa zinaisha. Mafisadi wanaishia kupewa adhabu ya kufagia na wengine Walikua hawafanyi chochote. Haya yote ni UTASHI wa Serikali na sio Mahakama.

Alichoongea ni speaker ni moja tu ya uimara wa Serikali.Swala la kushughulika na wanasiasa uchwara enzi za Jk lilikua dhaifu mno. Kwamba utamuona mwanasiasa anaongea anachojisikia na kufanya yyt yale.Mfano Enzi za Jk mikutano na maandamano ilikua inapigwa vita pia, tunaona yaliyotokea Iringa 2012 mwandishi Aliuawa, Arusha 2011,watu 3 waliuawa, Morogoro mtu mmoja aliuawa, mabomu huko Arusha, Kipigo cha mbwa koko kwa lipumba huko Dar nk.Huku serikali ilishindwa kuzuia mambo haya ya kijinga kiasi kila mkutano wa Upinzan lzm jambo baya litokee. Kwa jpm ukileta siasa UCHWARA za enzi za Jk ye hasubir uandamane,watu wauawe ndio ashughulike nawe,Ye ni juu kwa juu anakudaka. Ukidakwa na kupelekwa mahakaman hakuna cha kimemo kuwa hao watu waachie kama enzi za Jk,Huko ni wewe ukapambane na Vyombo vya SHERIA.

Sasa watu wakipelekwa mahakaman badala ya kupambana na vifungu vya SHERIA wao wanahamisha mjadala kumwangalia Rais anasemaje.Ingikuwa enzi za Jk akina Mbowe wangekua nje na sio kwamba hawana Hatia, la hasha Jk hakuwa anapenda Hawa watu wakae huko na kwa style hii wakampanda hadi kichwani kuwa ni DHAIFU. Walisahau udhaifu huo ndio unaowafanya wao wasiwe na kesi yyt polisi na hata wakifanya fujo dk kesi imeisha. Na ndio maana saiz watu wanakwambia wapinzani walikua wanamchezea jk lkn kwa jpm akili zinawakaa sawa.Kwa jpm ukivunja sheria jiandae kwenda kupambana na mawakili wa Serikali huko mahakaman na kutoboa kwake ni ujipange sana.

Speaker kaongelea ktk angle hii tu lkn kama ungetaka aongelee yote kuhusu uimara wa Serikali hii basi ni mengi sana na angeyaongea tu.Kwahiyo wewe kukarr angle moja aliyoiongelea na kufanya ndio mada kuu,Hili naona ni mwendelezo wa siasa uchwara pamoja na propaganda za kisiasa. Na hii pia inachangiwa na kutokuwa na Hoja za mcng za kujadili na sasa ni kudandia speech za viongoz tu.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
 
Monoko Mushi,

CCM ni chama cha kinafiki... wanarukaruka kama panzi... kazi kutafuta maslahi! they will never admit mapungufu yao wala kuyachukulia hatua thabiti za kisheria iwe ndani ya chama au kwenye sheria za nchi.

10 years from today we will be discussing mapungufu ya Uongozi wa Magufuli na jinsi vita dhidi ya mafisadi na kuondoa umasikini ilivyoshindwa... then kama kawaida Wapambe na mashabiki maandazi watashangilia slogan mpya za Mgombea na Mwenyekiti wa CCM Taifa!

Think about it: Nyerere alikuwa na Uhur na kazi, Ujamaa na Kujitegemea Kilimo ni uti wa mgongo, wakashangilia sana... akaja Mwinyi na Ruksa na fagio la chuma... wakapanda miti kama tumbili kupiga mayowe ya furaha... akaja Mkapa na uwazi na kuuza mashirika yaliyotaifishwa kutokana na Azimo la Arusha na siasa ya Ujamaa na kujitegemea... wakatunisha vifua mbele kusema sasas Uchumi ni dhahiri utakuwa... akatinga Kikwete na Ari, Kasi na Nguvu Mpya.. then Kilimo Kwanza.. wakasadifu mpaka Ilani na mapambio kemkem kusifia fikra za Mwenyekiti..

Now they areall hyped up with HapaKaziTu na MATAGA... lakini ukiuliza Ujamaa na Kujitegemea kwa mujibu wa Katiba Ya CCM ( na ya nchi) wako wapi kujenga jamii yenye kujitegemea, kuishi kijamaa ili kushinda Ujinga Umasikini na maradhi.. watakupa talalila nyingi za kusifia flyover na ndege za ATCL kuwa ni maendeleo...
Ask them asilimia ngapi ya Wananchi sasa wana uwezo wa kujitegemea na kuchangia huduma za elimu an afya bila kutegemea bure ya serikali....watadai wewe ni kuwadi wa mabeberu wasioitakia tanzania mema!

CCM ni mufilis! Wanadandia slogan za Wagombea na Wenyekiti wa Chama lakini kufanya kazi kufuta umasikini, ujinga na maradhi hawataki!
It is my honor to hear from you again! Sir!🙏🏾
 
Shida ya Bavicha ni kukariri na Sio kuelewa.Unapozungumzia Udhaifu au uimara wa Uongozi flani unaangalia nyanja nyingi.Serikali dhaifu haiwez kukusanya kodi, Inawachekea mafisadi, wazembe makazini, wanasiasa uchwara nk.Wakati wa Jk kulikua na mapungufu mengi mno kuliko mazuri. Wapinzani walikua wanaburuzwa mahakaman lkn Wanaachiwa,Ushawahi jiuliza kwanini kesi zao zilikua zinayeyukia juu kwa juu?Kwamba walikua wanashinda kesi huko mahakaman?Swala ni maagizo kutoka juu tu,bwana hao jamaa waachieni waendelee na mambo yao. Muhimili wa Mahakama haujaanza kuingiliwa leo hata huu wa Bunge pia. Angalia kesi zilizokuwa zinawakabili akina Yona,Mramba,Mahayu, Zombe nk jinsi zilivyokuwa zinaisha. Mafisadi wanaishia kupewa adhabu ya kufagia na wengine Walikua hawafanyi chochote. Haya yote ni UTASHI wa Serikali na sio Mahakama.

Alichoongea ni speaker ni moja tu ya uimara wa Serikali.Swala la kushughulika na wanasiasa uchwara enzi za Jk lilikua dhaifu mno. Kwamba utamuona mwanasiasa anaongea anachojisikia na kufanya yyt yale.Mfano Enzi za Jk mikutano na maandamano ilikua inapigwa vita pia, tunaona yaliyotokea Iringa 2012 mwandishi Aliuawa, Arusha 2011,watu 3 waliuawa, Morogoro mtu mmoja aliuawa, mabomu huko Arusha, Kipigo cha mbwa koko kwa lipumba huko Dar nk.Huku serikali ilishindwa kuzuia mambo haya ya kijinga kiasi kila mkutano wa Upinzan lzm jambo baya litokee. Kwa jpm ukileta siasa UCHWARA za enzi za Jk ye hasubir uandamane,watu wauawe ndio ashughulike nawe,Ye ni juu kwa juu anakudaka. Ukidakwa na kupelekwa mahakaman hakuna cha kimemo kuwa hao watu waachie kama enzi za Jk,Huko ni wewe ukapambane na Vyombo vya SHERIA.

Sasa watu wakipelekwa mahakaman badala ya kupambana na vifungu vya SHERIA wao wanahamisha mjadala kumwangalia Rais anasemaje.Ingikuwa enzi za Jk akina Mbowe wangekua nje na sio kwamba hawana Hatia, la hasha Jk hakuwa anapenda Hawa watu wakae huko na kwa style hii wakampanda hadi kichwani kuwa ni DHAIFU. Walisahau udhaifu huo ndio unaowafanya wao wasiwe na kesi yyt polisi na hata wakifanya fujo dk kesi imeisha. Na ndio maana saiz watu wanakwambia wapinzani walikua wanamchezea jk lkn kwa jpm akili zinawakaa sawa.Kwa jpm ukivunja sheria jiandae kwenda kupambana na mawakili wa Serikali huko mahakaman na kutoboa kwake ni ujipange sana.

Speaker kaongelea ktk angle hii tu lkn kama ungetaka aongelee yote kuhusu uimara wa Serikali hii basi ni mengi sana na angeyaongea tu.Kwahiyo wewe kukarr angle moja aliyoiongelea na kufanya ndio mada kuu,Hili naona ni mwendelezo wa siasa uchwara pamoja na propaganda za kisiasa. Na hii pia inachangiwa na kutokuwa na Hoja za mcng za kujadili na sasa ni kudandia speech za viongoz tu.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
Kama unataka nijibu bandiko lako, ondoa hayo maneno “shida ya bavicha ni kukariri”

Do not rely on politics of “groupies”
 
Kama unataka nijibu bandiko lako, ondoa hayo maneno “shida ya bavicha ni kukariri”

Do not rely on politics of “groupies”
Sifuti hayo maneno mkuu.Kama liko juu ya uwezo wako pita kimya.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
 
Sifuti hayo maneno mkuu.Kama liko juu ya uwezo wako pita kimya.

Nokia ya kitochi yuzingi jamii foramu
Siwezi kupita kimya na wakati ni thread niliyoanzisha mimi. Ukitaka mjadala wa kistaarabu, ondoa hayo maneno. Otherwise I cannot respond to it. You will take me down to your level and defeat me!
 
Katiba, kanuni na sheria zetu hazimruhusu Rais kuwa dikteta, rais bora ni yule anayetekeleza matakwa ya sheria hata kama sheria hiyo ni mbaya. Ndiyo maana JK aliridhia katiba iandikwe upya ili wananchi tuamue tunataka rais wa namna gani pia.
Basi kama majibu ya uimara wa serikali au kiongozi ndio huu (kusimamia sheria hata kama mbaya) naona mfano wa spika yupo sahihi.
Kitendo cha Mbowe kuwa jela ni ktk kusimamia sheria inayotaka mtu akiandamana bila kibali achukuliwe hatua, kubwa zaidi akivunja mashariti ya dhamana afutiwe hiyo dhamana.
 
Kama unataka nijibu bandiko lako, ondoa hayo maneno “shida ya bavicha ni kukariri”

Do not rely on politics of “groupies”
jmushi1 jibu hoja usikwepe kujibu sababu ya hayo maneno machache ambayo sio matusi.

Usipojibu naona jamaa kakupiga na kitu kizito (kwa hoja) kichwani umepoteza fahamu (mwelekeo wa mjadala).
 
jmushi1 jibu hoja usikwepe kujibu sababu ya hayo maneno machache ambayo sio matusi.

Usipojibu naona jamaa kakupiga na kitu kizito (kwa hoja) kichwani umepoteza fahamu (mwelekeo wa mjadala).
Afute aone kama sijajibu, vijembe naviweza sana mkuu, tukienda huko hata Page ya pili haijafika tutaharibu mjadala kwa maoni yangu.
 
Afute aone kama sijajibu, vijembe naviweza sana mkuu, tukienda huko hata Page ya pili haijafika tutaharibu mjadala kwa maoni yangu.
Mbona hayo sio matusi mkuu?
Mjibu tu wajifunze wengi kupitia hoja zako.

Siku hizi kutambulishwa kama BAVICHA imekuwa kejeli?!! Kweli maisha yanaenda kasi sana.
 
Mbona hayo sio matusi mkuu?
Mjibu tu wajifunze wengi kupitia hoja zako.

Siku hizi kutambulishwa kama BAVICHA imekuwa kejeli?!! Kweli maisha yanaenda kasi sana.
Aondoe nitamjibu, mbona hoja nyepesi sana? Ni msimamo tu kwasasa kama Trump vs Pelosi kwenye issue ya ukuta mzuri😀. Haiwezi kuita watu majina halafu useme ni mjadala. Ninaweza kufanya the same, halafu akachukia. Hapo itamfaidisha nani?
 
Back
Top Bottom