Udhaifu wa Azimio la Arusha na Mapokeo Potofu kuhusu Utajiri na Vipato

Dont'e get me wrong, silaumu Azimio la Arusha kwa Umasikini wa Mtanzania leo, bali nahoji jinsi lilivyopokewa na jinsi lilivyojieleza kama lilileta kitendawili machoni mwa Wananchi na Watekelezaji na katika kufumbua kitendawili, tukafumbua visivyo.


Nimekuelewa vizuri mchungaji; lakini hapo juu umeweka mojawapo ya very conditional statement ambayo inasema "kama Azimio la Arusha lisingepiga vita utajiri... basi tungekuwa.." Kimsingi unasema kuwa Azimio la Arusha ndio libebe lawama ya sisi kutokuendelea. Lakini vile vile uko sahihi kwenye jambo la uelewa wa Azimio na ndio maana nasema Azimio lilikuwa mbele sana ya muda wake.

Leo hii baadhi ya viongozi waliokuwa wakilitekeleza Azimio la Arusha ndio tunaanza kuwasikiliza jinsi wanavyojenga hoja na kutetea misimamo yao. Watu hawa leo hii wanapofungua makanwa yao tunaweza kuona ni jinsi gani hawana uwezo wa uchambuzi, uelewa na hata usimamizi wa jambo zito kama Azimio la Arusha.

Nakubaliana na wewe kabisa kuwa kulikuwa na uelewa potofu wa Azimio la Arusha kwa viongozi wengi lakini naamini si kwa sababu azimio lilikuwa gumu kueleweka bali watendaji walikuwa ni wagumu kuelewa kama wanavyojionesha leo hii.
 
Nimekuelewa vizuri mchungaji; lakini hapo juu umeweka mojawapo ya very conditional statement ambayo inasema "kama Azimio la Arusha lisingepiga vita utajiri... basi tungekuwa.." Kimsingi unasema kuwa Azimio la Arusha ndio libebe lawama ya sisi kutokuendelea. Lakini vile vile uko sahihi kwenye jambo la uelewa wa Azimio na ndio maana nasema Azimio lilikuwa mbele sana ya muda wake.

Leo hii baadhi ya viongozi waliokuwa wakilitekeleza Azimio la Arusha ndio tunaanza kuwasikiliza jinsi wanavyojenga hoja na kutetea misimamo yao. Watu hawa leo hii wanapofungua makanwa yao tunaweza kuona ni jinsi gani hawana uwezo wa uchambuzi, uelewa na hata usimamizi wa jambo zito kama Azimio la Arusha.

Nakubaliana na wewe kabisa kuwa kulikuwa na uelewa potofu wa Azimio la Arusha kwa viongozi wengi lakini naamini si kwa sababu azimio lilikuwa gumu kueleweka bali watendaji walikuwa ni wagumu kuelewa kama wanavyojionesha leo hii.

Mwanakijiji,

Ndiyo nimetoa hukumu kwa kusema kama Azimio lisingepiga vita Utajiri na nitafafanua.

Kunatofauti kati ya Ubepari na Utajiri.

Katika maelezo yangu, nimezungumzia ni jinsi gani tulivyopokea Azimio kwa kuangalia Utajiri na mtu kuwa Tajiri na kuufananisha na Ubepari na Unyonyaji.

Kwa kujipima jinsi tulivyo, ni rahisi sana kuona kasoro ya kauli au kuashirika kuwa Utajiri na mtu kuwa Tajiri ni sumu na dhambi.

Mfano, Mapunda mkulima wa Tumbaku kule Tabora, ikiwa yeye anafanya kazi kwa juhudi kila siku na kufuata ustadi katika kilimo chake na kuwa na mazao bora, anapopata ziada ya mauzo na kujijengea nyumba, kununua trekta na kuendelea kuongeza uzalishaji wake, kwa nini jamii imhukumu kwa kumuona mnyonyaji au kuwa Utajiri wake uliotokana na juhudi zake kuwa sumu na si jambo la kuigwa katika kujenga Ujamaa kamili na kujitegemea?

Kwa nini aundiwe kamati ya kumpeleleza na vikao vya serikali ya kijiji kumbeza na kuhujumu juhudi zake kisa Azimio linasema kuwa Tajiri ni dhambi?

Sasa haoa ndipo ninaposema Azimio lilikosea kutotoa tafsiri kamili ya kauli yake kwa kupimwa Watu na Mazingira. Ama Watendaji na watekelezaji wa Azimio (Viongozi) walitumia ufinyu wa mawazo ama kwa kukusudia kutokana na Azimio kuonekana kuwa ni tata au kutokana na ujingana upumbavu na hivyo kuanza kunyanyasa wle wananchi kama Mapunda ambao kwa juhudi zao, waliweza kujizalishia kwa ziada.

Lakini katika kila Mapunda, kuna Bundala, Masawe, Mwinyimvua ambao wanakaa kando kumshangalia Mapunda na juhudi zake na kumuona kama mnyonyaji!

Ndiyo maana nikatoa hukumu na kufafanua, ingekuwa vema kama tungetoa tafsiri ya maana ya utajiri na tajiri na kubainisha kwa vigezo ni vipi Utajiri na Tajiri vinaweza kuwa ni vyema katika jamii.
 
Mchungaji rejea historia ya kipindi cha Azimio la Arusha. Somaia wa Tanga walitajirika wakati gani? Aga Khan aliwahi kuacha lini kuwa tajiri? Kina Bhoke Munanka walikuwa maskini? Joseph Mungai je? Na Cleopa Msuya? Azimio halikuua uchu wa utajirisho!
 
Mchungaji rejea historia ya kipindi cha Azimio la Arusha. Somaia wa Tanga walitajirika wakati gani? Aga Khan aliwahi kuacha lini kuwa tajiri? Kina Bhoke Munanka walikuwa maskini? Joseph Mungai je? Na Cleopa Msuya? Azimio halikuua uchu wa utajirisho!

Unaongelea watu waliokuwa kwenye Tabaka la kupendelewa na kuneemeka bila kujali Azimio lilisema nini!

Si tulishamuongelea Munanka humu ndani? Na Mungai na Msuya, si wao walikuwa Viongozi? Aga Khan kwani alikuwa anategemea Tanzania pekee kunawiri? Je umesahau ni vipi wote Aga Khan na Somaia walipewa fursa maalum ya kitabaka kuendelea kuneemeka?

Mbona Tiny Rowland tulimfukuza na hatukumpa nafasi sawa na Somaia, Khambaita au waasia na Wanasiasa wengine ambao walifumbiwa macho wakaendelea na kujineemesha kama Andy Chande?

Kuleta kwako majina haya hapo juu, kunafungua lile boksi jingine la mabaya ya Azimio ambayo yalifanyika kwa ubaguzi!
 
Mchungaji tofautisha Utajiri na Unyonyaji. Azimio lilikuwa linapinga Utajiri unaotokana na Unyonyaji. Na kwa mujibu wa Muasisi wa Azimio kulikuwa/kuna mstari mwembamba kati ya Utajiri na Unyonyaji, yaani, ni vigumu sana kupata Utajiri bila kutumia Unyonyaji. Kama unabishana na hili naomba unitajie matajiri 10 tu waliochapa kazi hapa Tanzania na kupata utajiri wao bila kutunyonya sisi Watanzania - je, ni hawa:

1. Reginald Mengi
2. Rostam Aziz
3. Mo Ibrahim
4. Bakhresa
5. Sabodo
6. Iddi Simba
7. Mo Dewji
8. Mrema
9. Mtei
10. Nyoni

?
 
Mwanakijiji,

Ndiyo nimetoa hukumu kwa kusema kama Azimio lisingepiga vita Utajiri na nitafafanua.

Kunatofauti kati ya Ubepari na Utajiri.

Katika maelezo yangu, nimezungumzia ni jinsi gani tulivyopokea Azimio kwa kuangalia Utajiri na mtu kuwa Tajiri na kuufananisha na Ubepari na Unyonyaji.

Kwa kujipima jinsi tulivyo, ni rahisi sana kuona kasoro ya kauli au kuashirika kuwa Utajiri na mtu kuwa Tajiri ni sumu na dhambi.


Hili kwa kweli ukiangalia si kosa "letu" ni kosa la utajiri ulivyoletwa kwetu. Utajiri ulileta kwetu kwa unyonyaji wa mtu mmoja na mwingine. Wakoloni walikuja na kuishi kama matajiri lakini hawakuwa matajiri waliotoka kati yetu bali walikuja na kuchomeka mirija yao yenye ncha ndefu migongoni mwetu na wakapata utajiri wao.

Hata wale "waswahili" wenzetu waliokuwa wakifanya kazi bomani au kwa "mzungu" walipata utajiri wao kwa kuwa karibu na hawa wazungu na kuwatumikia kule kwa DC; wengi wao walianza kupata utajiri wao kwa kuwa vibaraka wa wakoloni. Hivyo, mtu wa kawaida alihusisha utajiri wa mtu mmoja mmoja na ukandamizaji.

Tena ukienda mbali zaidi utaona kuwa utajiri katika eneo letu umehusishwa moja kwa moja na ukandamizaji. Waarabu walioshi maisha ya heri katika mwambao wa Afrika ya Mashariki hao walivuna utajiri wao kwa kupitia biashara ya utumwa na kilimo cha kulazimisha (forced labor). Hadi hivi sasa sijaona bado katika Tanzania ya mkoloni na hata baada ya ukoloni watu waliopata utajiri wao bila ya kuhusishwa na ukandamizaji au unyonyaji wa aina fulani.

Hapa niende mbele zaidi; leo hii katika jamii yetu utajiri bado unahusishwa na ukandamizaji, ufisadi, na uvunjaji wa sheria. Wale ambao tunawaona ni matajiri (sisemi wenye maisha ya ahueni) bali wale wenye majumba, magari, n.k wanahusishwa mara moja na vitendo vya ufisadi au kushukiwa. Watu kama kina Lukaza, na wengine wanapojenga majumba ya kisasa na kifahari watu wanaowaona kuwa ni matajiri (kitu ambacho ni kweli) lakini utajiri wao umetokana na nini?

Ni kwa sababu hiyo basi utaona kuwa Azimio halikuwa linapinga utajiri per se bali namna ya kupata utajiri huo. Na hilo bado ni mgogoro leo hii katika jamii yetu. Watu wetu wanapata vipi utajiri wao na kumudu maisha yao? Je kwa kipato cha kawaida na tumiradi twa hapa na pale mtu anaweza kuwa na maisha ya kitajiri au ahueni?

Utaona kuwa ili mtu aweze kuwa na maisha ya kitajiri (kitu ambacho sidhani kama ni kipimo kizuri) ni lazima kwa namna fulani au nyingine ajihusishe moja kwa moja au kwa athari zake na vitendo vya kifisadi; haijalishi huyo mtu anawadhifa gani.

Azimio la Arusha lilikuwa na lengo la kupunguza pengo kati ya matajiri na maskini kwa kutengeneza tabaka la kati (la middle income) yaani watu wanoishi maisha ya afueni kwa kutegemea vipato vyao. Leo hii watu hawataki kuwa kwenye middle income wanataka watoke kwenye umaskini na kwenda kwenye utajiri uliokubuhu!


Mfano, Mapunda mkulima wa Tumbaku kule Tabora, ikiwa yeye anafanya kazi kwa juhudi kila siku na kufuata ustadi katika kilimo chake na kuwa na mazao bora, anapopata ziada ya mauzo na kujijengea nyumba, kununua trekta na kuendelea kuongeza uzalishaji wake, kwa nini jamii imhukumu kwa kumuona mnyonyaji au kuwa Utajiri wake uliotokana na juhudi zake kuwa sumu na si jambo la kuigwa katika kujenga Ujamaa kamili na kujitegemea?
Hata wakati wa AR kina Mapunda walikuwa wanafanya hivi na hakuna aliyewaingilia kati. Wapo watu waliopata utajiri wao kwa namna hii na jamii haikuwaona ni wanyonyaji kwa sababu wameona walivyojenga maisha yao na kundi hili kubwa hautaliona kwenye miji yetu utaliona zaidi kule vijijini ambako watu wa kawaida walijiingiza katika biashara na shughuli mbalimbali na kuweza kujijengea maisha ya afueni (affluent lifestyle). Ni mijini ndio utaona watu wanaishi maisha ya juu kuliko vipato vyao.

Kwa nini aundiwe kamati ya kumpeleleza na vikao vya serikali ya kijiji kumbeza na kuhujumu juhudi zake kisa Azimio linasema kuwa Tajiri ni dhambi?
Sidhani kama hili limewahi kutokea kule vijijini kwa sababu vijijini watu wanajua nani alipata utajiri vipi na kwa shughuli gani. Vijijini watu hawana matatizo na matajiri wao kwani wanajua wameuchuma vipi. Tatizo letu liko kwa hawa wanaotoka vyuoni kesho na keshokutwa alipoanza kazi tu kamaliza kila kitu.


Sasa haoa ndipo ninaposema Azimio lilikosea kutotoa tafsiri kamili ya kauli yake kwa kupimwa Watu na Mazingira. Ama Watendaji na watekelezaji wa Azimio (Viongozi) walitumia ufinyu wa mawazo ama kwa kukusudia kutokana na Azimio kuonekana kuwa ni tata au kutokana na ujingana upumbavu na hivyo kuanza kunyanyasa wle wananchi kama Mapunda ambao kwa juhudi zao, waliweza kujizalishia kwa ziada.
Wazazi wangu waliishi katika kipindi hiki na kwa kadiri ninavyokupumbuka tuliweza kumiliki mashamba, mifugo, na kuuza pale Makorola ziada pasipo kufatwa na mtu yeyote serikalini. Na nilipokuwa kule boarding school nakumbuka dula la Akonaay ambalo leo naweza kulilinganisha na Mall ya kimarekani maana jamaa alikuwa anauza kuanzia nguo, baskeli, spare parts na pembeni yake alikuwa na mgahawa (food court). Jamaa alikuwa tajiri na hakuna mtu aliyemfikiria kuwa yuko kinyume cha ujamaa! Alianza biashara yake kwa kuleta vitu toka Arusha pole pole na hatimaye kujenga duka lake kubwa na hata baadaye kufungua tawi la duka hilo pale Mbulu mjini.. Hii yote ilikuwa wakati wa Azimio la Arusha.

Ujamaa wa Mwalimu haukuwa na tatizo na utajiri; ulikuwa na tatizo na jinsi watu walivyopata utajiri wao kwa haraka haraka bila kuzalisha mali. Na ukiangalia utaona kuwa ni tatizo hili hili tunahangaika nalo leo hii kama vile nchi za Kibaperi zinavyohangaika na watu kama kina Madoff!
 
Companero,

Unaongeza majina ya wale ambao tayari nimeshawakana na kutamka wazi kuwa wao ni wanyonyaji kwa kuwa Utajiri wao umepatikana kwa hila, hivyo bado unaendelea kukosea unapowaorodhesha watu ambao wanaonekana wazi bila hata kutumia misuli mingi kujua Utajiri wao una walakini!
 
Mwanakijiji,

Kama ulivyoshuhudia upande chanya wa kina Mapunda na Akyoo, pia nami nimewaona hao kina Mapunda na Akyoo na vile vile Masawe na Marwa ambao walihujumiwa na Serikali za vijiji na jamii jirani kutokana na jitihada zao wenyewe za kujizalishia.

Ukisoma mwanzoni mwa thread, nimebainisha kuwa watekelezaji wa Azimio, nikiwa na maana waliopewa dhamana ya kulieneza Azimio n kuhakikisha linafanya kazi, ndio waliosababisha kukawa na upotofu.

Kwenye udhaifu, nauliza kama Azimio lingebainisha wazi kwa lugha nyepesi na kwa kufafanuliwa kwa umakini kwa Watanzania walio wengi kuwa Utajiri wa halali ni kutokana na jasho la mtu na si unyonyaji, je tungeweza kuona ongezeko la kina Mapunda badala ya kuwa mmoja kati ya watu kumi katika eneo, ikawa kuna Mapunda 6 kati ya watu kumi?
 
Azimio la Arusha Jana na Leo
Ni mjadala mzuri kuhusu Azimio, lakini mjadala huu ni vyema ukazingatia kuwa katika kipindi cha utekelezaji wake Mwalimu alikuwa akitoa tasmini mara kwa mara. Alifanya hivyo Mwaka 1977 (baada ya miaka kumi), na alifanya hivyo tena mwaka 1987 (baada ya miaka ishirini) pengine hii ilikuwa ndio mara ya mwisho kufanya hivyo kwani baada ya miaka michache baadae Chama cha Mapinduzi kililiogopa Azimio. Miaka ya awali kabisa baada ya Azimio, Mwalimu alisisitiza kuwa kule kutangaza tu Azimio hakukuwa na maana kuwa Tanzania ilikuwa tayari nchi ya Kijamaa na Inayojitegemea. Bado kulikuwa na mapambano yaliyohitajika kufanyika na bado kulikuwa na upinzani toka hata ndani ya miongoni mwa viongozi na chama na baadhi ya wabenzi na naizesheni ambao Azimio lilitishia sana raha na starehe zao. Hili ni jambo la muhimu sana. Jambo la msingi la kuzingatia ni kuwa Azimio lilikusudia kujenga Tanzania yenye watu sawa, nchi isiyokuwa na unyonyaji wa mtu na mtu au kundi moja kwa kundi jingine. Mfumo wa kinyonyaji unaotamba duniani nyakati za Azimio na sasa ni ule wa kibepari, baada ya ya mifumo ya utumwa na kikabaila kutokomezwa na kushindwa na ubepari. Lakini ubepari katika kuendeleza unyonyaji unatumia njia nyingi, moja ikiwa ile ya kutawala watu na nchi zingine na kuzinyonya - ukoloni, na mbadala wake ni ukoloni mambo leo. Kwa ujumla mifumo hii ya kinyonyaji ya ubepari unaotoka nje ya mipaka yake kwenda kunyonya kwingineko ni kile kinachoitwa Ubeberu. Leo, kwa nguvu ya ubepari unaotamba, umegeuzwa na kuitwa utandawazi. Azimio kwa upande mwingine basi ilikuwa ni jitihada ya kuikomboa nchi na watu wake dhidi ya ubeberu.

Azimio lilitambua kuwa msingi wa unyonyaji ni umiliki wa njia kuu za uchumi, hizi mpaka tunapata uhuru zilikuwa mikononi mwa makampuni ya kigeni. Haya yakataifishwa, na hii kwa upande mmoja pamoja na makosa yalofanyika, ilikuwa ni hatua muhimu katika kuanza kujenga uwezo wa kulimbikiza mtaji wa ndani kwa ajili ya maendeleo yetu. wengi walioongelea Azimio hapa hawajalitendea haki kwa sababu kipindi cha Azimio kilikuwa cha ujenzi wa viwanda, na tofauti na kipindi cha ubinafsishaji ambacho kimekuwa ni kipindi cha kuua uwezo wetu wa ndani wa uzalishaji (Miaka ya Mwishoni mwa Themanini maeneo ya Barabara ya Pugu na Morogoro yalikuwa ni maeneo ya viwanda). Leo hivyo havipo, badala ya kuimarisha palipolegea wavivu wa kufikiri wakaamua kuvifirisha kabisa. Nachojaribu kusema ni kuwa hadithi ya Azimio si nyepesi hivi kama tunavyotaka kuisimulia. Wakubwa wa sasa wangependa sana hadithi mzitoazo, ndio maana hung'ang'ania kuwa hapo zamani tulijipanga kununua unga na sukari, lakini hawaelezi hali hiyo ilianza lini, na hawasemi kuwa leo sukari ni ya kumwaga na pia unga lakini zipo kaya nyingi zisoijua sukari na unga - huutazama kwa macho tu.

Mwisho, napendekeza watu wausome Mwongozo wa CCM wa mwaka 1981, humo kuna uchambuzi wa kujikosoa wa CCM ya Mwalimu Nyerere, mambo ambayo leo hayafanyiki. Katika sehemu moja ya Mwongozo " ... ukweli unaojitokeza wazi ni kuwa baadhi ya matatizo yetu ya uchumi yanatokana na kutoitekeleza kwa dhati siasa ya Ujamaa na Kujitegemea" (uk. 25). Katika kipindi hicho pia CCM kilikuwa kikitafakari kiwe chama cha Makada au cha kila mtu Makada na umma wote. Na mmwongozo unabainisha kuwa "bila ya kikosi cha askari wa mstari wa mbele wa harakati za ujamaa, lengo la kujenga ujamaa haliwezi kufikiwa." (uk 27). Aidha Mwongozo unakili kuwa "Ujenzi wa ujamaa si lelemama bali ni mapambano, mapambano ya kudumu dhidi ya ubepari na unyonyaji, .." (uk. 39). Kwa kifupi tu utaona hali hii ya kujikosoa ndani ya chama hadi wakati huo. Yote haya yalikuja pinduliwa baada ya wabenzi na naizesheni kupata upenyo na kuyapindua mambo. Ukisoma Mwelekeo wa Sera Katika Miaka ya Tisini (wa CCM) utaona jinsi ambavyo Azimio lilivyokuwa likiviziwa kama vile fisi aviziavyo mkono kudondoka.
 
Hili si kweli; mchango wao hauwezo kulinganishwa na juhudi za Watanzania wenyewe; IMF hawakujenga nyumba za matofali ya kuchoma na kuezeka kwa bati kule Mkongo, RUvuma katika operesheni ya "nyumba bora" Watanzania walifanya hivyo; Benki ya Dunia hawakuja kufundisha Elimu ya Watu wazima Watanzania wenyewe walifanya hivyo hadi kufikisha uwezo wa kusoma wa asilimia 90 (leo hii pamoja na misaada ya mashirika hayo hayo literacy level ni asilimia 70!);

Kilimo cha kujitegemea kilifanywa na Watanzania wenyewe; usafi, chakula bora, afya bora, kampeni za kilimo cha kisasa n.k kiliendeshwa na Watanzania wenyewe. Ndio kulikuwa na misaada lakini misaada hiyo haikusababisha Watanzania waamke na kujiletea maendeleo; ingekuwa misaada peke yake inatosha kufanya watu waamke basi Tanzania ya leo ingekuwa mbali sana katika kujitegemea.


Usipuuzie mchango wa azimio la arusha na roho ya kujitegema iliyokuja nayo.



Inabidi urudi na kusoma vizuri jinsi gani misaada ya kigeni iliingia Tanzania na mchango wake; Hili laweza kuwa ni somo la wakati mwingine lakini ukweli unabakia kuwa mwamko wa uhuru ulisababisha Watanzania kushirikiana zaidio na kufanya kazi kwa pamoja na kwa umoja na kujiletea maendeleo wao wenyewe. Nchi gani zilizopokea misaada na kuitumia kwa manufaa ya wananchi wao zilifikia kiwango cha Tanzania? nipe mifano angalau miwili tuilinganishe.




Hili ni rahisi kulisema hivyo lakini bila kuweka mambo ya kihistoria katika historia yake ni rahisi kupotosha. Uchumi wa dunia haukuwa mikononi mwa Tanzania kama vile leo hii tunavyoona kuwa licha ya sera ya kibepari tunayoifuata na misaada tunayopata bado hatuna uamuzi wa mwisho wa mazao ya mashamba, viwanda na juhudi zetu. Azimio la Arusha si la kulaumiwa kwa kutokupiga hatua za haraka za kiuchumi bila kuangalia hali ya kihistoria. Huwezi kuangalia mambo nje ya historia yake.



Hili si kweli; mwanzoni mwa uhuru hadi katikati ya miaka ya sabini hatukupokea misaada per capita kama tunavyopokea leo na kama nilivyoonesha hapo juu hakuna msaada wowote uliowafanya watu waamke na kujiletea maendeleo au kushiriki katika ujenzi wa taifa lao. JKT, Mashamba ya kijiji, hata kushinda njaa ya 1974 kwa kiasi kikubwa ilikuwa ni juhudi za viongozi na Watanzania wenyewe. Misaada yote haielezei mwamko wa kisiasa na kujituma uliokuwepo wakati huo. No sir haiwezi kuelezea.

Mwanakijiji:

Kama watanzania walifanya hivyo kwa juhudi zao wenyewe ni kwanini walishindwa ku-sustain juhudi zao?

Misaada ilipokewa tena mingi sana. Kwa mfano serikali ya Sweden ilikuwa inatoa karatasi za bure za kuchapishia vitabu na kutengeneza madaftari. Misaada ya kifedha mpaka kufikia 1981 ilikuwa 600 millioni USD kwa mwaka.

Njaa ya mwaka 1974, mkombozi mkubwa ulikuwa ugali wa YANGA ambao ulikuja kama msaada. Na njaa hiyo kwa sehemu kubwa ilisababishwa na vijiji vya ujamaa.
 
Azimio la Arusha Jana na Leo
Ni mjadala mzuri kuhusu Azimio, lakini mjadala huu ni vyema ukazingatia kuwa katika kipindi cha utekelezaji wake Mwalimu alikuwa akitoa tasmini mara kwa mara. Alifanya hivyo Mwaka 1977 (baada ya miaka kumi), na alifanya hivyo tena mwaka 1987 (baada ya miaka ishirini) pengine hii ilikuwa ndio mara ya mwisho kufanya hivyo kwani baada ya miaka michache baadae Chama cha Mapinduzi kililiogopa Azimio. Miaka ya awali kabisa baada ya Azimio, Mwalimu alisisitiza kuwa kule kutangaza tu Azimio hakukuwa na maana kuwa Tanzania ilikuwa tayari nchi ya Kijamaa na Inayojitegemea. Bado kulikuwa na mapambano yaliyohitajika kufanyika na bado kulikuwa na upinzani toka hata ndani ya miongoni mwa viongozi na chama na baadhi ya wabenzi na naizesheni ambao Azimio lilitishia sana raha na starehe zao. Hili ni jambo la muhimu sana. Jambo la msingi la kuzingatia ni kuwa Azimio lilikusudia kujenga Tanzania yenye watu sawa, nchi isiyokuwa na unyonyaji wa mtu na mtu au kundi moja kwa kundi jingine. Mfumo wa kinyonyaji unaotamba duniani nyakati za Azimio na sasa ni ule wa kibepari, baada ya ya mifumo ya utumwa na kikabaila kutokomezwa na kushindwa na ubepari. Lakini ubepari katika kuendeleza unyonyaji unatumia njia nyingi, moja ikiwa ile ya kutawala watu na nchi zingine na kuzinyonya - ukoloni, na mbadala wake ni ukoloni mambo leo. Kwa ujumla mifumo hii ya kinyonyaji ya ubepari unaotoka nje ya mipaka yake kwenda kunyonya kwingineko ni kile kinachoitwa Ubeberu. Leo, kwa nguvu ya ubepari unaotamba, umegeuzwa na kuitwa utandawazi. Azimio kwa upande mwingine basi ilikuwa ni jitihada ya kuikomboa nchi na watu wake dhidi ya ubeberu.

Azimio lilitambua kuwa msingi wa unyonyaji ni umiliki wa njia kuu za uchumi, hizi mpaka tunapata uhuru zilikuwa mikononi mwa makampuni ya kigeni. Haya yakataifishwa, na hii kwa upande mmoja pamoja na makosa yalofanyika, ilikuwa ni hatua muhimu katika kuanza kujenga uwezo wa kulimbikiza mtaji wa ndani kwa ajili ya maendeleo yetu. wengi walioongelea Azimio hapa hawajalitendea haki kwa sababu kipindi cha Azimio kilikuwa cha ujenzi wa viwanda, na tofauti na kipindi cha ubinafsishaji ambacho kimekuwa ni kipindi cha kuua uwezo wetu wa ndani wa uzalishaji (Miaka ya Mwishoni mwa Themanini maeneo ya Barabara ya Pugu na Morogoro yalikuwa ni maeneo ya viwanda). Leo hivyo havipo, badala ya kuimarisha palipolegea wavivu wa kufikiri wakaamua kuvifirisha kabisa. Nachojaribu kusema ni kuwa hadithi ya Azimio si nyepesi hivi kama tunavyotaka kuisimulia. Wakubwa wa sasa wangependa sana hadithi mzitoazo, ndio maana hung'ang'ania kuwa hapo zamani tulijipanga kununua unga na sukari, lakini hawaelezi hali hiyo ilianza lini, na hawasemi kuwa leo sukari ni ya kumwaga na pia unga lakini zipo kaya nyingi zisoijua sukari na unga - huutazama kwa macho tu.

Mwisho, napendekeza watu wausome Mwongozo wa CCM wa mwaka 1981, humo kuna uchambuzi wa kujikosoa wa CCM ya Mwalimu Nyerere, mambo ambayo leo hayafanyiki. Katika sehemu moja ya Mwongozo " ... ukweli unaojitokeza wazi ni kuwa baadhi ya matatizo yetu ya uchumi yanatokana na kutoitekeleza kwa dhati siasa ya Ujamaa na Kujitegemea" (uk. 25). Katika kipindi hicho pia CCM kilikuwa kikitafakari kiwe chama cha Makada au cha kila mtu Makada na umma wote. Na mmwongozo unabainisha kuwa "bila ya kikosi cha askari wa mstari wa mbele wa harakati za ujamaa, lengo la kujenga ujamaa haliwezi kufikiwa." (uk 27). Aidha Mwongozo unakili kuwa "Ujenzi wa ujamaa si lelemama bali ni mapambano, mapambano ya kudumu dhidi ya ubepari na unyonyaji, .." (uk. 39). Kwa kifupi tu utaona hali hii ya kujikosoa ndani ya chama hadi wakati huo. Yote haya yalikuja pinduliwa baada ya wabenzi na naizesheni kupata upenyo na kuyapindua mambo. Ukisoma Mwelekeo wa Sera Katika Miaka ya Tisini (wa CCM) utaona jinsi ambavyo Azimio lilivyokuwa likiviziwa kama vile fisi aviziavyo mkono kudondoka.

Mwana-genzi:

Nyerere was in denial. Ujamaa ni kiini cha matatizo. Alichotakiwa ni ku-abandon siasa hizo na kuwapa uhuru watu ku-realize their potentials.

Hayo mambo ya kujikosoa kwa vitu visivyowezekana ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu tu.
 
Mwanakijiji:

Kama watanzania walifanya hivyo kwa juhudi zao wenyewe ni kwanini walishindwa ku-sustain juhudi zao?

Kwa sababu waliacha misingi iliyounda taifa lao.

Misaada ilipokewa tena mingi sana. Kwa mfano serikali ya Sweden ilikuwa inatoa karatasi za bure za kuchapishia vitabu na kutengeneza madaftari.

kwa kiasi gani cha mahitaji ya Taifa?


Misaada ya kifedha mpaka kufikia 1981 ilikuwa 600 millioni USD kwa mwaka.

Ilikuwa inaenda kwenye sekta gani? Na wakati huo Taifa lilikuwa lina mahitaji ya kiasi gani na kiasi gani cha hiyo misaada kilienda kwenye sekta husika? Hiyo misaada ilikuwa ni sehemu gani ya bajeti ya taifa?


Njaa ya mwaka 1974, mkombozi mkubwa ulikuwa ugali wa YANGA ambao ulikuja kama msaada. Na njaa hiyo kwa sehemu kubwa ilisababishwa na vijiji vya ujamaa.

si kweli; vijiji vya ujamaa havikusababisha njaa. Rudia tena usome hali ya dunia wakati ule maana tukikubali hoja yako hiyo tunajiuliza njaa ya leo inasababishwa na vijiji vya ujamaa au ni kitu gani kimekuwa kikisababisha njaa maana njaa ilikuwepo hata 1960!
 
Mwana-genzi:

Nyerere was in denial. Ujamaa ni kiini cha matatizo. Alichotakiwa ni ku-abandon siasa hizo na kuwapa uhuru watu ku-realize their potentials.

Hayo mambo ya kujikosoa kwa vitu visivyowezekana ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu tu.

si kweli ujamaa si kiini cha tatizo kwa sababu kama hilo lingekuwa kweli tungeweza kuelezea vipi matatizo ya nchi nyingine za kiafrika zilizopata uhuru wakati sawa na sisi na zenye mazingira kama ya kwetu lakini hazikuwa zinazojaribu kuwa za kijamaa. As a matter of fact an argument can be made that Ujamaa was the most single factor that established Tanzania as it is today; It was the fabric that united the nation after independence and through which we attempted to build a modern nation where individuals were all equal and deserved all their dignity as human beings.
 
Azimio la Arusha halina udhaifu wowote ule. Udhaifu uko kwa viongozi ambao walikuwa wanabanwa na hilo azimio, walichofanya ni kulizika na kutafuna pesa ya walipa kodi bila kuulizwa maswali. Matokeo yake ndiyo hayo ya kashfa za mafisadi kila kukicha wakati walipa kodi wanaendelea kuwa na maisha duni.

Hakuna sababu yoyote ile ya msingi kuwaachia wahujumu wakubwa kabisa wa uchumi kutafuna kile walichoiba. Tena viongozi ndio wako mstari wa mbele kuwalinda kwa hali na mali.
 
nimefuatilia kwa karibu michango yenu hapo juu..mingine imenigusa sana. mi nadhani tujaribu kuona kwa nini azimio la Arusha lilikuja? lilikusudia kufanya nini? wakoloni hawakuondoka 9 december bali waliendelea kuwepo kwa stahili nyingine, ya kiuchumi. hivyo nyerere na wenzake wakaona matunda ya kisiasa,kiuchumi na kijamii hayatapatikana kirahisi kwa mfumo ule na ukisoma msahafu wa azimio hapo juu utaona kutoka sura ya kwanza hadi ya mwisho msisitizo ni kuwaonjesha wazalendo matunda ya uhuru,hivyo adui wa wakati huo alikuwa ni mfumo wa kiuchumi wa kikoloni against ujenzi wa jamii mpya ya kitanzania yenye uhuru na haki!!!!Sasa hilo lina ubaya gani? tatizo lilikuja kwa wale waliopewa dhamana ya kuongoza hii vita mpya! Hivyo azimio la arusha halikutimiza malengo yake,Lilipaswa kujenga misingi ya uzalishaji inayotokana na science kwa embrace education na sio (UPE) hivyo leo tungekuwa nchi ya africa yenye uwezo wa ku-innovate na kuwa na utalii bora,agricultural produce bora n.k Hivyo azimio la Zenji lingerekebisha na kuimarisha mifumo kama ya marketing kwa kuruhusu watu kuuza mazao aggressively popote duniani bila urasimu, Kwani dunia nzima wakati huo ilikuwa inaingia kwenye kipindi kingine chenye changamoto mpya za kiuchumi na hasa sisi tuliokuwa na maneno ya socialism kwenye vitabu vyetu. hivyo baada ya azimio la zenji watu wakatumia udhaifu ule kufanya hayo tunayoyaona leo na hakika mafisadi wengi ni vijana wa azimio la zanzibar!!!
 
Kwa sababu waliacha misingi iliyounda taifa lao.

kwa kiasi gani cha mahitaji ya Taifa?

Ilikuwa inaenda kwenye sekta gani? Na wakati huo Taifa lilikuwa lina mahitaji ya kiasi gani na kiasi gani cha hiyo misaada kilienda kwenye sekta husika? Hiyo misaada ilikuwa ni sehemu gani ya bajeti ya taifa?


si kweli; vijiji vya ujamaa havikusababisha njaa. Rudia tena usome hali ya dunia wakati ule maana tukikubali hoja yako hiyo tunajiuliza njaa ya leo inasababishwa na vijiji vya ujamaa au ni kitu gani kimekuwa kikisababisha njaa maana njaa ilikuwepo hata 1960!

Mwanakijiji:

Mkuu ukipenda chongo utaita makengeza. Unasema waliacha misingi iliyounda taifa. Ni misingi gani iliyoachwa? Ujamaa na Azimio la Arusha ilikuwa misingi ya chama tawala na sio misingi ya taifa. Na hata kama ilikuwa ni misingi ya taifa mambo yalianza kwenda mlama wakati the architect bado akiwa madarakani. Hivyo ni yeye alioacha misingi hiyo. Na kuna watu walitaka awe rais wa maisha. Angechukua tu urais wa maisha na kuhakikisha anafanikiwa.

Misaada ilikwenda kwenye sekta ya elimu. Bila misaada kutoka Sweden kulikuwa hakuna kitu kinachoitwa elimu ya watu wazima.

Mkuu kuhusu njaa ya 1974, get you facts right. Mipango ya vijiji vya Ujamaa vilisababisha upungufu mkubwa wa chakula. Na bila mabepari hari ingekuwa mbaya sana. Najua unga wa YANGA ulitoka Marekani na sio URUSI.
 
si kweli ujamaa si kiini cha tatizo kwa sababu kama hilo lingekuwa kweli tungeweza kuelezea vipi matatizo ya nchi nyingine za kiafrika zilizopata uhuru wakati sawa na sisi na zenye mazingira kama ya kwetu lakini hazikuwa zinazojaribu kuwa za kijamaa. As a matter of fact an argument can be made that Ujamaa was the most single factor that established Tanzania as it is today; It was the fabric that united the nation after independence and through which we attempted to build a modern nation where individuals were all equal and deserved all their dignity as human beings.

Ukweli wa mambo Tanzania hiko ilivyo sasa kwa sababu waTanzania ndivyo walivyo.

Watanzania wanamsikiliza mtu aliye madarakani hata kama anaboronga. Hiyo ndio fabric yetu. Kwa mfano, ungekuwa na madaraka kijarida chako cha CHECHE kingekuwa ni must read na kingekuwa kwenye mitaala ya somo la uraia. Lakini kwa sababu huna madaraka yoyote, juhudi zako zinahatarisha amani.
 
nimefuatilia kwa karibu michango yenu hapo juu..mingine imenigusa sana. mi nadhani tujaribu kuona kwa nini azimio la Arusha lilikuja? lilikusudia kufanya nini? wakoloni hawakuondoka 9 december bali waliendelea kuwepo kwa stahili nyingine, ya kiuchumi. hivyo nyerere na wenzake wakaona matunda ya kisiasa,kiuchumi na kijamii hayatapatikana kirahisi kwa mfumo ule na ukisoma msahafu wa azimio hapo juu utaona kutoka sura ya kwanza hadi ya mwisho msisitizo ni kuwaonjesha wazalendo matunda ya uhuru,hivyo adui wa wakati huo alikuwa ni mfumo wa kiuchumi wa kikoloni against ujenzi wa jamii mpya ya kitanzania yenye uhuru na haki!!!!Sasa hilo lina ubaya gani? tatizo lilikuja kwa wale waliopewa dhamana ya kuongoza hii vita mpya! Hivyo azimio la arusha halikutimiza malengo yake,Lilipaswa kujenga misingi ya uzalishaji inayotokana na science kwa embrace education na sio (UPE) hivyo leo tungekuwa nchi ya africa yenye uwezo wa ku-innovate na kuwa na utalii bora,agricultural produce bora n.k Hivyo azimio la Zenji lingerekebisha na kuimarisha mifumo kama ya marketing kwa kuruhusu watu kuuza mazao aggressively popote duniani bila urasimu, Kwani dunia nzima wakati huo ilikuwa inaingia kwenye kipindi kingine chenye changamoto mpya za kiuchumi na hasa sisi tuliokuwa na maneno ya socialism kwenye vitabu vyetu. hivyo baada ya azimio la zenji watu wakatumia udhaifu ule kufanya hayo tunayoyaona leo na hakika mafisadi wengi ni vijana wa azimio la zanzibar!!!


Blah blah blah. Mambo ni free-market tu.
 
Mwanakijiji:

Mkuu ukipenda chongo utaita makengeza. Unasema waliacha misingi iliyounda taifa. Ni misingi gani iliyoachwa? Ujamaa na Azimio la Arusha ilikuwa misingi ya chama tawala na sio misingi ya taifa. Na hata kama ilikuwa ni misingi ya taifa mambo yalianza kwenda mlama wakati the architect bado akiwa madarakani. Hivyo ni yeye alioacha misingi hiyo. Na kuna watu walitaka awe rais wa maisha. Angechukua tu urais wa maisha na kuhakikisha anafanikiwa.

Ni wazi hujafanya utafiti wa kujua misingi iliyounda Taifa la Tanzania ni nini. Kumbuka kuwa AR lilikuja mwaka 1967.. hii ni baada ya uhuru wa Tanganyika na baada ya Muungano na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Maana yake ni kuwa misingi iliyounda taifa ilitangulia Azimio la Arusha!


Misaada ilikwenda kwenye sekta ya elimu. Bila misaada kutoka Sweden kulikuwa hakuna kitu kinachoitwa elimu ya watu wazima.

Hii si kweli; rudia historia yako. Walimu waliokuwa wanafundisha kisomo cha watu wazima walikuwa wanafanya kwa kujitolea na siyo kwa kulipwa na serikali au NGO yoyote ile! Vitabu vilivyotumika vilifadhiliwa kwa asilimia kubwa na fedha zetu sisi wenyewe. Misaada ya wafadhili ilikuwa ni kidogo sana kulinganisha na mahitaji ya nchi na mchango wetu sisi wenyewe.


Mkuu kuhusu njaa ya 1974, get you facts right. Mipango ya vijiji vya Ujamaa vilisababisha upungufu mkubwa wa chakula. Na bila mabepari hari ingekuwa mbaya sana. Najua unga wa YANGA ulitoka Marekani na sio URUSI.

Si kweli; tatizo la njaa la mwaka 1974 lilichangiwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya hali ya hewa na hali ya kiuchumi ya mwanzoni mwa miaka ya sabini (bei ya mafuta n.k). Vijiji vya ujamaa as a matter of fact ilikuwa ni juhudi kubwa ya taifa kuokoa watu wengi zaidi kwa kuwaleta pamoja ili kuweza kuwafikishia huduma mbalimbali na misaada ya chakula badala ya kiila mtu kuishi umbali mkubwa kutoka mwingine wakati wa ukame. Hivyo, mipango ya vijiji vya ujamaa iliokoa maisha ya watu wetu wengi na ushahidi ni kuwa leo hii vijiji hivyo hivyo vimefanya rahisi zaidi kufikisha huduma mbalimbali na kuwasogeza watu pamoja na hivyo kuwa ni vya mafanikio kwa asilimia 100!

Waliopinga vijiji vya ujamaa hawakuamini kuwa kataifa kachanga kama ka kwetu kangeweza kufanikisha operesheni kubwa na delicate kama hii. Ndio operesheni yenyewe mara ya pili ilikabiliwa na matatizo ya hapa na pale lakini hiyo ndiyo gharama ya maendeleo. Ingekuwa vichekesho kama operesheni kubwa kama ile ingeenda kwa ulaini bila ya matatizo yoyote.

Leo hii tumeona mataifa makubwa kama Marekani wakati wa Katrina ilivyoshindwa kuorganize watu wake kukabiliana na majanga; imagine Tanzania miaka ya sabini!
 
Back
Top Bottom