Mtokambali
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 216
- 91
Hebu tuwe wawazi wana jamvi wenzangu. Je kuna tabia gani au kasoro yoyote aliyonayo mwenzio wa ndoa uliyenae ambayo kama ungegundua kabla hamjaoana basi usingekubali kufunga pingu na kwa sasa unavumilia tu kwa vile ni mke/mme. Mfano mimi naanza,wa kwangu huyu ni muongo. Yaani anapenda kuongea lile ambalo anahisi mtu au watu alionao muda huo wangependa kusikia. Atamplease mtu kwa uongo hata ule wa hatari wenye madhara. Na akiongea na wewe 50% ni uongo!