UDA imebinafsishwa ili iingie Biashara na DART - Siri ya kuuzwa Bei Chee

ni hatari zaidi ya hatari yenyewe, hiyo ni UDA tu inayoonekana kwenye macho ya watanzania hawa maskini, ni mangapi mazito zaidi ya hayo yaliyojificha kwenye mashirika ya umma na mikataba mingine yenye utata ambayo maskini hawa walipa kodi hawaijui?

SAKATA LA UUZAJI WA UDA: Hakuna atakayesalimika




Na Jacob Daffi - Imechapwa 12 October 2011




KAMATI ya baraza la madiwani iliyoundwa na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Ma------ kuchunguza ubinafsishaji wa shirila la usafiri jijini (UDA), kuvunjwa kwa bodi ya shirika hilo na kuuzwa kwa mali zake, imeagiza kufikishwa kwenye mkono wa sheria aliyekuwa meneja wa shirika hilo, Victor Millanzi.


Katika ripoti ambayo ----------- imeipata, kamati imeagiza meneja huyo achunguzwe na vyombo vya dola kutokana na ushiriki wake katika kulihujumu shirika hilo.


Aidha, ripoti imesema hatua ya Ma------ kukabidhi UDA mikononi mwa muwekezaji – kampuni ya Simon Group Ltd., - ni "kinyume cha utaratibu."


Dk. Ma------ aliunda kamati hiyo Juni mwaka huu. Ripoti inatuhumu Millanzi kuuza kinyume cha taratibu rasilimali za UDA zinazohamishika na zile zisizohamishika kama sehemu ya mkakati wake wa kukabiliana na hasara.


Hata hivyo, Millanzi katika taarifa yake mbele ya wajumbe wa Kamati amekana madai yote dhidi yake na kusema, "Nilichokiteleza nilikifanya kwa mujibu wa sheria na taratibu za kuendesha UDA."


Meya hakupata ridhaa (Resolution) ya mkutano wa madiwani. Yumkini mwanahisa wa pili mkubwa, Hazina naye hakuridhia maamuzi ya kikao hicho wala wakurugenzi wa bodi ya UDA."


Kamati ya Ma------ imeeleza, "uuzaji wa rasilimali za UDA haukufuta sheria za manunuzi ya umma (PPRA) ya mwaka 2004; wala hakukufanyika tathimini ya mali zake kabla ya kuuzwa."


Hadi kufikia 30 Juni 2010, shirika hilo la umma lilikuwa likiendeshwa kwa hasara ya Sh. 1.4 bilioni.


Kamati hiyo imebaini mali zisizohamishika za shirika hilo zilizouzwa kwa kile inachoita kiholela kwa nyakati tofauti kuanzia mwaka 1997 hadi mwaka 2010, ni pamoja na nyumba iliyoko kiwanja Na. 10 eneo la Jangwani Beach. Nyumba hiyo imeuzwa mwaka 1997 kwa Harold John kwa thamani ya Sh. 40 milioni.


Nyumba nyingine ni ile iliyopo Na. 60 iliyoko katika eneo la Oysterbay, ambayo imeuzwa kwa Sh. 120 milioni (1997) na ile iliyoko kitalu Na. 354, eneo la Masaki, Kinondoni, ambayo imeuzwa mwaka 2001 kwa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kwa thamani ya Sh. 600 milioni.


Katika uza uza hiyo, kimo kiwanja kilichoko kitalu Na. 261 eneo la Ubungo kilichouzwa mwaka 1998 kwa Shirila la Maendeleo la Dar es Salaam (DCC) kwa Sh. 800 milioni, viwanja Na. 1-21 vilivyoko block V, katika Manispaa ya Ilala, vilivyouzwa mwaka 2003 kwa DCC kwa Sh. 350 milioni, kiwanja Na. 38 kilichoko Oysterbay kilichouzwa mwaka 2005 kwa kampuni ya Century Properties Ltd kwa Sh. 516.2 milioni na nyumba Na. 54 iliyoko Ilala iliyouzwa 2009 kwa Trans Ocean Supplies Ltd kwa Sh 180 milioni.


Aidha, Kamati hiyo imebaini kuwapo kwa mikataba kadhaa yenye utata ya pango ya majengo na maeneo ya wazi yanayomilikiwa na UDA. Katika maeneo mengi, hata bei hicho kinachoitwa "bei ya pango," haikuzingatia ukubwa wa eneo. Vitega uchumi vingi vimeuzwa kwa bei ya kutupa.


Kwa mfano, menejimenti ya UDA, chini ya Millanzi na Bodi ya Wakurugenzi iliyokuwa chini ya Idd Simba, ilipangisha watu mbalimbali kuanzia kwenye jengo la utawala yalipo makao makuu ya UDA, Kurasini, Dar es Salaam hadi maeneo ya wazi yaliyoko katika karakana zake.


Wapangaji hao wanaiolipa kodi ya kutupwa, ni pamoja na Nagla General Shipping Services Ltd., aliyepangishwa kwenye jengo la utawala eneo lenye ukubwa mita za mraba 19 kwa Sh. 7,500 kwa mwezi.


Wengine ni F.A.Agencies (T) Ltd., anayelipa Sh 7,200 kwa mwezi, Rafad Complex Ltd (kituo cha basi kati), anayelipa Sh. 8,400 kwa mwezi na Lake Corridor Petroleum Ltd anayeendesha kantini ya UDA kwa malipo ya Sh. 7,429 kwa mwezi. Kampuni ya Lake Corridor Petroleum Ltd imekodishwa eneo lingine la ufundi lenye ukubwa wa mita za mraba 140 ambapo inalipa Sh. 3,000 kwa mwezi.


Nyingine ni kampuni ya Mupingwa Petroleum Ltd iliyokodishiwa ofisi za UDA zilizoko bandarini kwa Sh. 4,800 kwa mwezi, Koru Freght Ltd iliyokodisha ghala la UDA kwa malipo ya Sh 2,457 kwa mwezi, huku kampuni hiyo ikiwa imepangishwa eneo la wazi katika viwanja vya makao makuu ya UDA lenye ukubwa wa mita za mraba 370 kwa Sh. 2,485 kwa mwezi.


Wapangaji wengine na kiasi wanacholipa kwa mwezi kikiwa katika mabano, ni pamoja na Seleman Keraba (Sh. 850 kwa mwezi), Mak Consult Engineering (Sh. 4,312), Macbean Sea Trading (Sh 7,200), Koru Freight Ltd (Sh. 6,000), Koru Freight pia imepanga eneo la mita za mraba 164.52 kwa Sh. 3000, Shibat Enterprises Ltd (Sh. 7,000) na Exaud Epiana aliyepewa karakana kwa kodi ya Sh. 6,000 kwa mwezi.


Kwa mujibu wa ripoti ya kamati hiyo, viwango vya soko kwa sasa vya kukodi katika maeneo ya mijini, na hasa jijini Dar es Salaam, ni kati ya dola 7 hadi 12, sawa na karibu Sh. 10,500 hadi Sh. 18,000 kwa kila mita moja ya mraba kutegemeana na eneo lilipo jengo husika linalopangishwa.


Ripoti hiyo imebainisha wazi kwamba baadhi ya wapangaji hao wa maeneo ya UDA wameyapangisha kwa makampuni mengine ambayo wao wanawatoza bei kubwa zaidi na hivyo makampuni hayo kujinufaisha zaidi kupitia mgogo wa shirika hilo.


Kampuni ya Lake Corridor Petroleum Ltd imetajwa kama mfano wa makampuni ambayo yameingia mikataba ya kukodishwa ofisi au maeneo ya wazi, lakini wakaamua kupangisha kwa watu wengine bila kupata idhini wala kibali cha UDA.


Wakati kampuni ya Koru Freight imepanga eneo la wazi lenye ukubwa wa mita za mraba 1,916, kamati imebaini kwamba kampuni hiyo imekuwa ikilipia eneo la mita za mraba 370 tu.


"UDA iliingia ubia na Africarriers tarehe 13/10/2009kuendeleza kiwanja Na 437/129 kilichopo Mtaa wa Sokoine (kilipo kituo cha mabasi cha Stesheni). Makubaliano hayo yamebainika kuwa na mapungufu kadhaa, ikiwa ni pamoja na kutokuwapo nyaraka zozote zinazoonyesha jinsi mwekezaji huyu alivyopatikana, hivyo kutia shaka iwapo sheria ya manunuzi ya mwaka 2004 na kanuni zake za mwaka 2005 zilizingatiwa," inasema sehemu ya ripoti hiyo.


Upungufu mwingine uliotajwa na ripoti hiyo katika mkataba wa ubia huo wa UDA na Africarriers, ni kampuni hiyo kutaka kwamba baada ya mradi wa ujenzi wa ghorofa ndani ya kiwanja hicho cha kituo cha Stesheni kukamilika, mwekezaji huyo atatakiwa kumiliki hisa asilimia 75 na UDA ibakiwe na hisa 25 tu.


Aliyekuwa Meneja huyo wa UDA, Millanzi, ambaye alitimuliwa na Ma------ Juni mwaka huu, kabla ya kuivunja pia Bodi ya UDA iliyokuwa chini ya Idd Simba, anadaiwa kujichotea Sh. 40,622,651.80 kama malipo ya kiinua mgongo chake hata kabla ya kumaliza mkataba wake wa kuliongoza shirika hilo.


Kwa mujibu wa ripoti ya kamati hiyo ya Ma------, mkataba wa utumishi wa meneja huyo ulipaswa kufikia ukomo 30 Juni 2011, lakini hata kabla ya kufikia mwisho wa mkataba huo yeye alikwishajilipa tayari kiinua mgogo chake.


Malipo hayo yanaelezwa kulipwa kwa awamu tatu. Tarehe 19 Mei 2011 kupitia vocha Na 21, alijilipa Sh. 25,000,000, tarehe 25 Mei 2011, akajilipa Sh. 5,800,000 na 30 Mei 2011, ambapo amejilipa Sh. 9,822,651.80 kupitia hundi Na. 930322.


Katika utetezi wake wa maandishi mbele ya kamati kuhusu tuhuma za kujilipa mafao kabla ya mkataba kumalizika, Milanzi alisema, "Siyo kweli. Mimi niliajiriwa UDA mwaka 2006, tarehe 1 Juni. Hivyo mkataba wangu uliisha 30 Mei 2011."


Anasema, "Nilitoa notisi ya mwezi mmoja na taratibu zetu (UDA) malipo yanafanywa kwenye mwezi wa mwisho uliotoa notisi."


Hata hivyo, nyaraka zilizopo zinaonyesha Milanzi alisaini mkataba wa ajira tarehe 29 Juni 2006, wenye Kumb. Na UDA/A.1/6. Ulipaswa kumalizika 30 Juni 2011.


Mgogoro kuhusu menejimenti nzima ya UDA uliibuka mapema Juni mwaka huu baada ya Meya Ma------ kuamuru kumfuta kazi Millanzi, pamoja na kuivunja Bodi ya UDA iliyokuwa chini ya Idd Simba kukabiliwa na tuhuma za ufujaji wa fedha zilizokuwa zimewekezwa na mwekezaji mpya ndani ya shirika hilo
 
Ninashangaa wabunge na mawaziri wanalumbana.
Rais wa JMT aliapa kwa kutumia katiba kulinda mali na watu wa JMT.

UDA ni mali ya watu. Kuna vitu viwili, mali na watu. Hivi inakuwaje mali ya taifa hili inauzwa Rais wa nchi akiwa hajui.
Shirika kama UDA kwa nchi masikini kama yetu limekula kodi za watu sana.
Ndiyo mali ya masikini, leo tunaambiwa mawaziri na wabunge wananyosheana vidole Rais akiwa kimya kana kwamba hakuna kinachotokea.

Acheni kulumbana, huu ni muda wa kumuuliza aliyeapa kulinda mali zetu Mh Rais, UDA imeuzwaje, kwa utaratibu gani, nani walihusika na kwasababu zipi.

Itakuwa ni kituko Ofisi ya Rais ikisema haikuhusika. Itakuwa haikuhusika vipi wakati ndiyo inayolinda mali zetu.
Nani mwenyekiti wa cabinet, na kwanini wabunge na mawaziri walumbane wakati mwenyekiti wa baraza la mawaziri yupo kimya.

Hivi kesi ile serikali iliyoshindwa, haikutosha kumwambia mwenyekiti wa baraza la mawaziri kuwa kuna tatizo.
Leo, Takukukuru, Polisi na intelligence ya nchi zinafanya kazi kulinda watu na si mali za watu. Nani mkubwa wa vyombo hivyo. Kwanini mlumbane wakati mwenye ngoma kakaa kimya ! mnacheza ngoma gani ikiwa manju hataki kupiga fiilimbi.
 
Ukweli huwa unasimama wenyewe; hauitaji kusimamishwa; unahitaji kuoneshwa tu. Wabunge na wote wanaozungumzia suala la UDA kwa kiasi kikubwa wanakwepa kusema ule ukweli... wanazunguka mbuyu..
 
Ukweli huwa unasimama wenyewe; hauitaji kusimamishwa; unahitaji kuoneshwa tu. Wabunge na wote wanaozungumzia suala la UDA kwa kiasi kikubwa wanakwepa kusema ule ukweli... wanazunguka mbuyu..
Ndio maana hapo juu nimesema, hakuna sababu za mawaziri na wabunge kulumbana.
Wanachokifanya ni kucheza ngoma, kitu cha ajabu mpiga ngoma ambaye pia ni mpiga zumari kakaa kimyaa, sijui wanacheza mirindimo gani. Unachezaje ngoma isiyopigwa!

Hili ni suala la Rais kueleza umma, mali aliyoahidi kuilinda kwa katiba, tena akisema na watu wake imekuwaje?
Wabunge hawana chombo chochote cha dola, kikubwa wanachokifanya ni kusotana madole ya macho.
Ni sawa na akina dada pale mtaani wakiwa wamefunga vibwebwe wanatishiana, utaona! utaona!

Mwenye ngoma ni Rais Kikwete, kakaa kimya mnaulizana wenyewe kwa wenyewe.
Watu wanataka kuuziwa mafuta ya gari kutoka wodi ya Mwaisela, wakijua fika kituo cha mafuta wamekiacha faya
 
Rekodi yangu juu ya utawala wa kifisadi bado inasimama. Tuliandika hili miaka minne iliyopita. Yametimia.
Unajua Mzee Mwanakijiji, msimamo wangu toka siku ile nilipojiunga rasmi na JF, haujayumba...nilidhani naungana na watu wenye uchungu wa kweli na taifa hili na wanakerwa haswa na tunakoelekea. How wrong I was! Siku hizi kuna posts humu nikizisoma natokwa na machozi ingawa hizo ni posts tu kwenye mtandao. Lakini linalofunga mwaka ni kwamba nimebahatika kukutana uso kwa uso na baadhi ya wachangiaji...oh my God, huwezi kuamini wanayoyatetea kuhusu hatma yetu kitaifa! We are but zombies, the walking dead I see in movies. We Tanzanians are not real, just a fake specie that ought to be extinct!
 
Last edited by a moderator:
Unajua Mzee Mwanakijiji, msimamo wangu toka siku ile nilipojiunga rasmi na JF, haujayumba...nilidhani naungana na watu wenye uchungu wa kweli na taifa hili na wanakerwa haswa na tunakoelekea. How wrong I was! Siku hizi kuna posts humu nikizisoma natokwa na machozi ingawa hizo ni posts tu kwenye mtandao. Lakini linalofunga mwaka ni kwamba nimebahatika kukutana uso kwa uso na baadhi ya wachangiaji...oh my God, huwezi kuamini wanayoyatetea kuhusu hatma yetu kitaifa! We are but zombies, the walking dead I see in movies. We Tanzanians are not real, just a fake specie that ought to be extinct!

Mzee mwenzangu; bila ya shaka naweza kuwahesabu watu wachache tu humu ambao hawaatetereka katika mapambano haya. Ukijua ni jinsi gani angalia jinsi gani watu wanazungumzia CCM na wagombea wake as if wana legitimacy ya kupewa hata siku moja ya ziada kuongoza. Yaani watu wameona madudu yote na wanaua ni nani kaliingiza taifa hapa lakini bado tunazungumza kana kwamba labda tujaribu tena.. miaka hamsini na ushee hatujachoka tu...
 
Mzee mwenzangu; bila ya shaka naweza kuwahesabu watu wachache tu humu ambao hawaatetereka katika mapambano haya. Ukijua ni jinsi gani angalia jinsi gani watu wanazungumzia CCM na wagombea wake as if wana legitimacy ya kupewa hata siku moja ya ziada kuongoza. Yaani watu wameona madudu yote na wanaua ni nani kaliingiza taifa hapa lakini bado tunazungumza kana kwamba labda tujaribu tena.. miaka hamsini na ushee hatujachoka tu...
Niliwahi kufikiri kama nikichaguliwa kuongoza Tanzania nitaweza? Nilikuwa nawaangalia watu wa zama hizo. Siku hizi ndoto hizo hazipo maana najua ninaweza, tatizo kubwa linalonisumbua ni pale ninapofikiri aina ya suti zitakazonipendeza

Watanzania ni watu wasahaulifu, wanaongelea matukio na wanaoshangilia hata jogoo kuchi wakipigana.

Leo wanasema fulani anafaa kuwa Rais, kesho wanasema shilingi inaanguka thamani.

Yaani wanadhani shilingi inapanda thamani kama kishada, na kuanguka kama tunda damu.

Leo unawaibia kesho wanakuita mjasirilia mali tena wanakualika katika harambee

Leo wanasema wanapigika kicuhumi, kesho wanakwambi 'huyu' anafaa ataleta lile kontena la ubuyu a.k.a maendeleo

Hawajishughulishi kabisa kufikiri tatizo ni kitu gani
 
Niliwahi kufikiri kama nikichaguliwa kuongoza Tanzania nitaweza? Nilikuwa nawaangalia watu wa zama hizo. Siku hizi ndoto hizo hazipo maana najua ninaweza, tatizo kubwa linalonisumbua ni pale ninapofikiri aina ya suti zitakazonipendeza

Watanzania ni watu wasahaulifu, wanaongelea matukio na wanaoshangilia hata jogoo kuchi wakipigana.

Leo wanasema fulani anafaa kuwa Rais, kesho wanasema shilingi inaanguka thamani.

Yaani wanadhani shilingi inapanda thamani kama kishada, na kuanguka kama tunda damu.

Leo unawaibia kesho wanakuita mjasirilia mali tena wanakualika katika harambee

Leo wanasema wanapigika kicuhumi, kesho wanakwambi 'huyu' anafaa ataleta lile kontena la ubuyu a.k.a maendeleo

Hawajishughulishi kabisa kufikiri tatizo ni kitu gani

Oh Nguruvi; you couldn't have said it better. Ni watu hawa hawa ambao wanalia umaskini na ndio hao hao wanashangilia kuwaingiza wale wale waliowafikisha kwenye umaskini huo. Angalia mikoa inayoitwa "iko nyuma kiuchumi" utaona ndio hiyo hiyo inayochagua kwa wingi CCM. Go figure.
 
Oh Nguruvi; you couldn't have said it better. Ni watu hawa hawa ambao wanalia umaskini na ndio hao hao wanashangilia kuwaingiza wale wale waliowafikisha kwenye umaskini huo. Angalia mikoa inayoitwa "iko nyuma kiuchumi" utaona ndio hiyo hiyo inayochagua kwa wingi CCM. Go figure.
Jenerali alilisema hili vizuri sana katika toleo moja la Raia Mwema, nanukuu;
Jenerali Ulimwengu said:
Tunachagua kama vipofu, kisha tunalalama kama vichaa. Sasa tuamue: ama tuchague viongozi wetu kwa makini, au tukae kimya wakati wakitunyanyasa. Wachagua hovyo wasiwe wasema hovyo wakitendewa hovyo.
 
Hivi hawa viongozi wetu kuna kitu wanafanya kwa manufaa ya taifa lao kweli?? Yaani inchi imekuwa kama haina watu wa kuingoza kila sehemu ni ufisadi, ufisadi. Hakuna tunachoweza kujivunia si shule tumeshindwa, si hopital tumeshindwa, viwanda tumeshinda, barabara tumeshindwa. umeme ni kero tu.. yaani kila sekta sisi ni zero.. Halafu kuna watu wanatafuta ndani mwa watu wale wale waliofeli kila kitu kupata kiongozi bora..

Hivi sisi watanzania tumelogwa? mtu yuko serikali miaka 20, 30 hakuna alilolifanya la maana halafu leo huyu mtu ndo tumpe uongozi na kutegemea miujiza!!.. Hivi kweli kweli kwa akili za kawaida tunaweza kupata kitu kipya kwa watu wale wale, wenye mitizamo ile ile na mawazo yale yale?
 
Hivi hawa viongozi wetu kuna kitu wanafanya kwa manufaa ya taifa lao kweli?? Yaani inchi imekuwa kama haina watu wa kuingoza kila sehemu ni ufisadi, ufisadi. Hakuna tunachoweza kujivunia si shule tumeshindwa, si hopital tumeshindwa, viwanda tumeshinda, barabara tumeshindwa. umeme ni kero tu.. yaani kila sekta sisi ni zero.. Halafu kuna watu wanatafuta ndani mwa watu wale wale waliofeli kila kitu kupata kiongozi bora..

Hivi sisi watanzania tumelogwa? mtu yuko serikali miaka 20, 30 hakuna alilolifanya la maana halafu leo huyu mtu ndo tumpe uongozi na kutegemea miujiza!!.. Hivi kweli kweli kwa akili za kawaida tunaweza kupata kitu kipya kwa watu wale wale, wenye mitizamo ile ile na mawazo yale yale?
Alinda, naomba nitofautiane nawe kuhusu viwanda.
Viwanda hatujashindwa, tumegawa zawadi na vingine kugeuza maghala ya chumvi.

Kuna kiongozi kasema nchi hii ipo katika auto-pilot, nadhani ni kweli.
Sidhani kama Tanzania inahitaji viongozi, inaweza kwenda kwa solar energy

Watanzania ni watu wa ajabu sana. Wanafanya jambo lile lile kwa miaka 50 bila matokeo tofauti na wanategemea kufanya namna ile ile kwa mara nyingine wapate matokeo tofauti.

Watanzania wanaamini kwa dhati kabisa '' unaweza kupata malaika kutoka miongoni genge la wahalifu''

Tena watanzania wapo busy wakiwakatasa majambazi kwa ''kuwavisha nguo nyeupe na mabawa ili wawe malaika''
 
Ripoti ifuatayo inatudokeza mambo mbalimbali kuhusiana na mpango wa DART - Dar Rapid Transit - yaani Mradi wa Mabasi ya Abiria yaendayo kasi. Bila ya shaka watu wengi wamekuwa wakifiria kwua hiyo DART itakuja na mabasi yake n.k Kama inavyoonekana kwenye ripoti hii DART itahusisha makampuni binafsi katika kusafirisha abiria ambayo yata "qualify". Kwa mujibu wa ripoti hii ambayo "ka-nzi" kalidokeza kuwa imepitiwa hata na WB ni kampuni ya UDA ambayo ina mfumo, uzoefu na hata uwezo wa kuweza kushiriki vizuri kwenye DART.

Kwenye ile mada nyingine wengine tulikuwa tunajiuliza kwanini magenius wetu hawakufikiria kuibadili UDA na kuifanya iwe DARTA (Dar Rapid Transit Agency/Authority)? hasa ukizingatia kuwa ina uzoefu, miundo mbinu, na raslimali watu ya kutosha? Ni mpaka kuisoma ripoti hii ndio kwa upande wangu nimeelewa kuwa UDA imeuzwa kwa watu binafsi ili hao watu binafsi waje kuingia ubia na DART kufanya kitu ambacho kingeweza kufanywa bila UDA kuuzwa bali kuwezeshwa!

Baada ya ya kupitia ripoti hii ikabidi nikimbilia kusoma Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kuhusu Shirika la Usafiri Dar (UDA) niweze kuona alikuwa na maoni gani na kama yamezingatiwa. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu (CAG) alisema hivi kwenye ripoti yake ya mashirika ya umma ya mwaka wa 2009/2010:


Ni katika ripoti hiyo CAG anatudokeza kuwa iko kwenye mpango wa kuuza hisa asilimia 51 zinazomilikiwa na serikali. Wakati huo huo Jiji la Dar lilikuwa na hisa asilimia 49 na hivyo kufanya UDA kuwa shirika linalomiliwa kwa asilimia 100 na watu wa Tanzania. Lakini CAG anatudokeza:


Sasa, tukiangalia ripoti hii na ripoti hizi nyingine tunabakia na swali moja; kwanini Jiji na au kwa kushirikiana na Serikali Kuu isiendeshe exclusively suala la usafiri wa umma baada ya kuleta Rapid Mass Transit System hasa kwenye Jiji kubwa kama la Dar? Na kutoka hapo kuboresha mfumo wa magari ya Taxi's na usafiri wa tour (vijigari vidogo maalum)? Lengo likiwa kuondokana na daladala? Kwanini suala la Mass Transit kwenye majiji yetu makubwa lisifanywe na Local Cities na Halmashauri za Miji?
Miaka nane nyuma.. haki inaweza kuchelewa lakini inaweza kufika
 
Mzee mwenzangu; bila ya shaka naweza kuwahesabu watu wachache tu humu ambao hawajatetereka katika mapambano haya. Ukijua ni jinsi gani angalia jinsi gani watu wanazungumzia CCM na wagombea wake as if wana legitimacy ya kupewa hata siku moja ya ziada kuongoza. Yaani watu wameona madudu yote na wanajua ni nani kaliingiza taifa hapa lakini bado tunazungumza kana kwamba labda tujaribu tena.. miaka hamsini na ushee hatujachoka tu...
How times change, how time flies fast, how time and tide waits for no man...kweli hujafa hujaumbika!
 
Miaka nane nyuma.. haki inaweza kuchelewa lakini inaweza kufika
Exactly tulichosema ndicho kinachoonekana

Kuna somo hapa, si yale yaliyosemwa bali waliosema. Waliolieleza hili kwa uchungu kwa bahati nzuri hawakuitwa wasaliti! Walipuuzwa tu pengine kwa kuitwa wapuuzi

Watu hao hao wakisema yale yale siku hizi wanaitwa wasaliti

Somo la pili, uzalendo si tukio la msimu na wala haupandikizwi. Uzalendo ni kitu 'intrinsic'
 
Back
Top Bottom