Mkwawe
JF-Expert Member
- Jun 10, 2016
- 2,344
- 4,167
Katika makuzi yangu naweza kusema wanaume wanapokuwa katika rika dogo hutilia maanani sana mahusiano yao na huweka malengo ya muda mrefu na wenzi wao kwa kuwa fikra ya mwanaume ndiyo huanza kuchanua na kujiona ni mtu anayeweza kutimiza majukumu yoyote yatakayomkabili. Na jambo la kufahamu mienendo ya mwanaume katika rika hilo huchagizwa sana na ukaribu wa mwanamke ampendaye kwake, kama mwanamke aliye naye atampa chachu na pia maendeleo ya mwanaume huonekana ila ikiwa kinyume chake mwanaume hukata tamaa na haamini kama kuna mbadala wa mwanamke aliyekuwa naye utatokea. Hapa sasa akili ya mwanaume ikishavurugwa ule utayari na uthubutu wote hupungua na maisha atakayoishi ni ya mazoea
Mtoto wa kike ni kama bamia, linapokuwa teke thamani yake huwa kubwa kuliko maelezo na hapa ndipo wasichana wengine wanapokosa utimamu binafsi wa akili kwa kudhani nyakati wanazozishuhudia kipindi hicho hudumu. Kuna kipindi msichana anaweza shuhudia hadi wanaume watatu wanaoweza kumwaga machozi mbele yake kwa ajili yake lakini yeye anaamini thamani yake ni ya milele jambo linalopelekea kutoangalia ya mbele, kadri muda unavyokwenda ndio bamia hupoteza ubora wake na kila mlaji hupoteza uhitaji nalo, ndivyo kwa wadada wanapokuwa rika kubwa huanza kuwa serious kwa kurejea kumbukumbu za nyakati za nyuma.
Migongano iko hapa, kipindi mtoto wa kiume anapokuwa serious mtoto wa kike hajali na haelewi (Under 25) ila kipindi ambacho mwanamke anapokuwa serious mwanaume alishakata tamaa na wengi huwa wachafuzi (Over 30) na hapa ndo wadada hupata tabu sana na zile kauli za "Wanaume wote mbwa tu" huwa nyingi sana
Mtoto wa kike ni kama bamia, linapokuwa teke thamani yake huwa kubwa kuliko maelezo na hapa ndipo wasichana wengine wanapokosa utimamu binafsi wa akili kwa kudhani nyakati wanazozishuhudia kipindi hicho hudumu. Kuna kipindi msichana anaweza shuhudia hadi wanaume watatu wanaoweza kumwaga machozi mbele yake kwa ajili yake lakini yeye anaamini thamani yake ni ya milele jambo linalopelekea kutoangalia ya mbele, kadri muda unavyokwenda ndio bamia hupoteza ubora wake na kila mlaji hupoteza uhitaji nalo, ndivyo kwa wadada wanapokuwa rika kubwa huanza kuwa serious kwa kurejea kumbukumbu za nyakati za nyuma.
Migongano iko hapa, kipindi mtoto wa kiume anapokuwa serious mtoto wa kike hajali na haelewi (Under 25) ila kipindi ambacho mwanamke anapokuwa serious mwanaume alishakata tamaa na wengi huwa wachafuzi (Over 30) na hapa ndo wadada hupata tabu sana na zile kauli za "Wanaume wote mbwa tu" huwa nyingi sana