Uchunguzi: Ngono zembe inaharibu bahati na future

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,327
51,831
Anaandika, Robert Heriel,
Kuhani katika Hekalu Jeusi.

Ukitaka bahati yako na mkondo wako wa pesa uanze kuyumba basi itakupasa uanze uzinzi au uasherati. Yaani hiyo ndiyo mbinu namba moja kabambe ya kujitia matatizoni.

Nafsi ya mtu huchafuliwa na uzinzi, yaani ili mtu awe mchafu basi itampasa awe mzinzi.
Uzinzi siyo tuu ni hatari kwa magonjwa hatari ya zinaa, bali pia ni hatari kwa magonjwa ya kuondoa kinga za kiroho.

Kikawaida binadamu akishaanza kufanya uzinzi ataanza kupoteza uwezo wake wa asili. Moja ya uwezo wa asili wa binadamu ni kuota ndoto zenye mantiki nyakati za usiku.

Binadamu kabla hajaanza ngono huota ndoto na anakuwa na uwezo wa kuzikumbuka kama siyo kuzitafsiri kabisa. Lakini akishaanza uzinzi ndoto hizo huanza kupungua na kupotea kabisa.

Huwezi ukawa mzinzi alafu ukaomba bahati au misaada ya kiroho kivyovyote vile. Hapo itakupasa ujitakase walau kwa siku zisizopungua tano ili uwe safi, kisha ndiyo ufanye mawasiliano na falme za rohoni.

Hata ukienda kwa waganga wa kienyeji kuna dawa ambazo ukipewa utaambiwa usikutane na mwanamke kwa siku kadhaa ili dawa zifanye kazi.

Au utaambiwa utembee na binti mdogo tena ikiwezekana ambaye ni bikra. Hapo ndipo kesi nyingi za ubakaji kwa watoto wadogo hujitokeza.

Vijana mnaoanza biashara, hasa hizi biashara za mitaji midogo chin ya milioni tano. Ukitaka biashara yako iende bila shida basi cha kwanza itakupasa ukae mbali na wanawake, acha ngono zembe.

Kama utashindwa ni akheri uoe kabisa, tena uoe mwanamke msafi mwenye maadili. Siyo uoe tena limalaya ambao litakuwa linafanya zinaa huko na kukuletea wewe mikosi.

Tunaposema mwanamke malaya au muasherati hafai kwa ndoa, na ikiwezekana kama umemuoa ukamfumania, basi itakupasa usijiulize mara mbilimbili, fukuza! Siyo kwa sababu tuu ya wivu wa kimapenzi. No! Bali ni pamoja na mambo ya kimaendeleo.

Hakuna familia zenye kufanya umalaya zikaendelea. Umalaya na umasikini vinapelekana bega kwa bega.

Mwanamke aliyefanya uzinzi au ngono anakuwa mchafu Kwa siku 14 wakati mwanaume anakuwa mchafu kwa siku 7.

Kama unamchongo unaousikilizia basi itakupasa ukae mbali na ngono zembe mpaka utiki. Lakini kama utajiingiza huko siyo ajabu pesa zako zikawa zinakuja lakini kila zikikaribia kuingia zinapeperuka. Yaani ni kama unanyang'anywa tonge mdomoni.

Umalaya ndiyo dhambi pekee ambayo mtu anaufanyia mwili wake. Dhambi zingine mtu hufanya nje ya mwili wake, yaani huwafanyia wengine. Ndiyo dhambi inayodhuru mwili na roho kwa haraka sana.

Ngono zinavuta mikosi, yaani unaweza pata pesa sasa hivi alafu hapohapo likatokea tatizo la kuitumia pesa uliyoipata nje ya mipango yako.

Namna pekee ambayo wazinzi wanaweza kuwa na bahati katika mambo yao ni kujiingiza kwenye ushirikina na ulozi. Ambapo itawapasa wagharamike kwa namna moja ama nyingine kusafisha nyota zao kwa kipindi cha muda fulani, huku wakiendelea na uchafu wao.

Sio rahisi umuone mtu anafanya uzinzi halafu mambo yake yanaenda bila ya kuwa mshirikina. Hiyo haiwezekaniki.

Biashara inahitaji usafi siyo tuu wa kimwili, bali pia usafi wa kiroho (mvuto) na kitu pekee kinachochafua mvuto wa kiroho ni zinaa.

Huwezi kuwa mzinzi halafu ukaenda kwenye project zako, mfano unamashamba ya mpunga au nyanya halafu uende ukiwa unafanya uchafu, lazima mambo yaharibike, au ufugaji. Kila kitu kina siri zake, aidha utumie madawa ya jadi ndiyo ufanikiwe lakini kumuomba Mungu asaidie miradi yao ilhali roho yako imechafuka huo ni uongo.

Kuna baadhi ya watu wanatabia ya kuingiza wanawake au malaya kwenye nyumba zao wanazoishi, ndugu zangu hivi kama umekosa akili kwa kiwango hicho, umeona haitoshi ulete wanawake waitie mikosi nyumba yako. Unafikiri guest house zilijengwa kwaajili gani.

Kama utashindwa kabisa ni bora mkafanyie kwenye vichaka, huko mbona fresh tuu kuliko kuingiza uchafu nyumbani kwako. Huo ni ukosefu wa maarifa.

Vijana kama unahitaji njia yako isiwe ngumu sana, yaani pesa zako zisije kwa mbinde basi unashauriwa acha ngono zembe. Na uliyenaye awe mwaminifu, na kamwe mtu asiyemwaminifu usijisumbue kumfundisha uaminifu au kumbembeleza, unabembeleza mtu anayeharibu mifumo ya maisha yako.

Usiponielewa, utanielewa katika mambo unayoyafanya, yaani kila ukifanyacho hakiendi, unafeli. Wakati wenzako chochote tunachogusa kitaenda kitake kisitake.

Ni yule kuhani

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es salaam.
 
20220920_092101.jpg
 
Mkuu Taikon tupe muda kidogo tuvute pumzi maana kila siku ni mawe magumu kumeza

😀😀😀

Sasa mtu anakamtaji kamilioni tano alafu hakohako anajiingize kwenye Uzinzi au uasherati hata akisema aende Kwa mganga wa kienyeji bado pesa yake haitanunua uganga wa maana zaidi ya kuliwa pesa zake tu.
 
Kiukweli siwezi sema umesema ukweli ila tayari sisi waislamu Allah amesema uzinzi ni uchafu

Kwahiyo nikama umedadafua zaidi.

Niseme NAUNGA MKONO HOJA 100%

Huwa na washangaa vijana wenzangu wengi wanapoona maumbo ya wanawake makalio /rangi nyeupe ambayo hata kwa macho tu unatambua hii sio rangi ya mwanadamu. Sasa wao vijana huwa haelewi hapo. Anachotaka ni pale kati.

Lakini nisema waziwazi uzinzi ni kitu kama utashikamana nacho "basi hasara yake huwa inadumu hata ukifanya toba "

MWANAMKE ni mzuri ukimmiliki kisheria nae akawa ameshikamana na hofu ya mungu.

ILA PIA MWANAMKE pia ni mchafu kiuhalisia tu.Na hasa pale asipo pata maarifa ya kujitakasa .

Mwanamke ndo kiumbe anaye weza ku fanya ngono na akapata ladha ya ngono kwa asilimia 80% kuliko wee mwaname ulo sex nae. Yaan utaambulia asilimia 20% kwenye hilo tendo. Na ndo maana mawanamme anapo maliza huwanza kutafakari hivi "nilicho kifuata kwa huyu mtu ni nini"

Lakini mwanamke yee huwa anawaza kuridhishwa TU. Na endapo katika hesabu yake ,ume kuwa bora kwenye kumridhisha basi atakuganda mpaka wee utashangaa.

Ndomaana wake za watu hutembea mapaka na shamba boy na vijana wasio na pesa coz wao hufuata ladha TU.

*************************************************


mwanamke anaweza kutembea na wanaume zaid ya 3 kwa siku na nyote msigundue. Sasa tafakari hapo.

Huyo ni MWANNADAM aliye vaa uwezo wa ajabu. Na anaweza kuwaangamiza ulimwengu. Kirahisi.


Kuna baadhi ya makabila ya miiko hasa kwa hawa viumbe.

Me ni mkulima. Nimeshudia mimea ikiharibika kisa tu mwanamke amepandamo mtini .
 
Does rhis only apply to africans? Mbona wazungu wanazini sana na uasherati kuoitiliza na bado wao ndio wenye mihela hapa duniani? Mwengine juzi juzi tuu hapa kawa mfalme pamoja na roho mbaya ya mama yake lakini wapi....jamaa kaula
Hujui usemalo unadanganywa video vya ngono.
Wazungu wengi waaminifu mno.
Hasa us ukishikwa uzinzi utapata tabu mnoo
 
Hujui usemalo unadanganywa video vya ngono.
Wazungu wengi waaminifu mno.
Hasa us ukishikwa uzinzi utapata tabu mnoo
Acha story wewe ile kitu vijana wanapataka wazee wanapataka haijalishi kabila wa nchi.
 
Back
Top Bottom