Uchunguzi MwanaHalisi usivunje utawala bora

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
Uchunguzi MwanaHalisi usivunje utawala bora


TUMEPOKEA kwa masikitiko makubwa habari ya kuchunguzwa kwa ofisi za gazeti la kila wiki la MwanaHalisi na nyumbani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Hali Halisi Publisher, Bw. Saed Kubenea.

Tunatahadharisha uchunguzi unaofanywa na Jeshi la Polisi usitumiwe vibaya na kuingilia uhuru wa wananchi kutoa na kupata habari ambao ni haki yao ya kidemokrasia.

Tunasema hivyo kwakuwa kwa namna moja au nyingine kitendo hicho kinaweza kuwafunga mdomo Watanzania wenye nia njema na nchi yao kutoa taarifa za vitendo wanavyoona vinalengo baya kwa nchi yao.

Vyombo vya habari ndio sehemu pekee ambayo Watanzania wanaweza kuitumia kutoa dukuduku lao kwa uwazi au kwa siri kwa nia ya kubadilisha mwelekeo wa nchi wanaodhani siyo sahihi.

Kama taarifa zao za siri kwa wananchi wenzao zitakuwa zikipekuliwa na polisi kama walivyofanya, Watanzania wenye taarifa zinazoweza kuiokoa nchi isipotee, watakosa sehemu ya kukimbilia.

Kama vyombo vya habari vitafungwa mdomo kutakuwa na doa kubwa sana katika demokrasia ya Tanzania na utawala bora ambao unasisitiza umuhimu wa uwazi wa Serikali kwa wananchi wanaoichagua na kuipa kodi.

Wananchi ndio walioiweka Serikali madarakani na wanastahili kupata taarifa juu utendaji wake na hasa zama hizi ambazo hali ya maisha inazidi kuwa ngumu huku viongozi waliochaguliwa wakionekana kuneemeka.

Aidha kwa Rais Jakaya Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kitendo hicho kinaweza kumuharibia na kumfanya ashindwe kuhimiza utawala bora katika nchi nyingine.

Tunatambua umuhimu wa usiri kwa kila mtu lakini pia tunatahadharisha umuhimu huo usitumike vibaya kuvifunga mdomo vyombo vya habari na kuigeuza nchi kichaka cha wahalifu.

Pia wanahabari wenzetu tusitishwe na kilichofanyika kwa Bw. Kubenea bali iwe changamoto ya utendaji wetu wa kazi na tunatetea nchi yetu kwa kutumia nafasi tuliyonayo.
 
Uchunguzi MwanaHalisi usivunje utawala bora


TUMEPOKEA kwa masikitiko makubwa habari ya kuchunguzwa kwa ofisi za gazeti la kila wiki la MwanaHalisi na nyumbani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Hali Halisi Publisher, Bw. Saed Kubenea.

Tunatahadharisha uchunguzi unaofanywa na Jeshi la Polisi usitumiwe vibaya na kuingilia uhuru wa wananchi kutoa na kupata habari ambao ni haki yao ya kidemokrasia.

Tunasema hivyo kwakuwa kwa namna moja au nyingine kitendo hicho kinaweza kuwafunga mdomo Watanzania wenye nia njema na nchi yao kutoa taarifa za vitendo wanavyoona vinalengo baya kwa nchi yao.

Vyombo vya habari ndio sehemu pekee ambayo Watanzania wanaweza kuitumia kutoa dukuduku lao kwa uwazi au kwa siri kwa nia ya kubadilisha mwelekeo wa nchi wanaodhani siyo sahihi.

Kama taarifa zao za siri kwa wananchi wenzao zitakuwa zikipekuliwa na polisi kama walivyofanya, Watanzania wenye taarifa zinazoweza kuiokoa nchi isipotee, watakosa sehemu ya kukimbilia.

Kama vyombo vya habari vitafungwa mdomo kutakuwa na doa kubwa sana katika demokrasia ya Tanzania na utawala bora ambao unasisitiza umuhimu wa uwazi wa Serikali kwa wananchi wanaoichagua na kuipa kodi.

Wananchi ndio walioiweka Serikali madarakani na wanastahili kupata taarifa juu utendaji wake na hasa zama hizi ambazo hali ya maisha inazidi kuwa ngumu huku viongozi waliochaguliwa wakionekana kuneemeka.

Aidha kwa Rais Jakaya Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kitendo hicho kinaweza kumuharibia na kumfanya ashindwe kuhimiza utawala bora katika nchi nyingine.

Tunatambua umuhimu wa usiri kwa kila mtu lakini pia tunatahadharisha umuhimu huo usitumike vibaya kuvifunga mdomo vyombo vya habari na kuigeuza nchi kichaka cha wahalifu.

Pia wanahabari wenzetu tusitishwe na kilichofanyika kwa Bw. Kubenea bali iwe changamoto ya utendaji wetu wa kazi na tunatetea nchi yetu kwa kutumia nafasi tuliyonayo.

Mwanahalisi,

Hii imekaa kama press release ya IKULU a.k.a CCM
unaweza kutuambia nani kaitoa hiyo statement??????

Je Tanzania kuna utawala Bora kweli??????????? Tanzania Kuna bora utawala hata kama ni kilaza. Huo uwazi unaozungumziwa hapa ni upi???? wa kuwaficha mafisadiiii?

Haki ya mwanamchi mpiga kura anaezungumziwa hapa ni nani????

Kama serikali inawasikiliza wapiga kura wake mbona
 
Nchi hii walishaiteka na tunatakiwa kukaza buti ili tuwanyang'anye hawa manyang'au. Tukiogopa vitisho kamwe hatutaikomboa na ole wetu wanetu na wajukuu zetu watatoa lawama kwetu. Maana twaanza kuwa watumwa katika nchi yetu wenyewe.
 
Back
Top Bottom