Uchunguzi BOT: Tunatwanga Maji Kwenye Kinu

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,503
19,341
Nimerudi mjini ila naona jamaa waliniachia maboksi yangu ya kubeba mengi sana. Kwa hiyo nimekuwa mtoro sana hapa kijiweni siku hizi ili niyapunguze kidogo. Hata hivyo nimeona nitoe duku duku langu kuhusu uchunguzi unaofanywa pale BOT na 'independent company.' Inasemekana kuwa uchunguzi huu unafanywa na kampuni ya kimarekani inayoitwa Ernst Young, lakini ukweli ni kuwa kazi hiyo inafanywa na jamaa mmoja ambaye ni ndugu wa aliyekuwa aliyekuwa waziri wa fedha wakati wa Mkapa. Waziri huyu ndiye aliyemsaidia ndugu yake huyo kupata franchise ya Ernst Young kwa vile alikuwa akipewa tenda nyingi sana za kukagua mahesbau ya serikali. Nina wasiwasi kuwa mtu kama huyo katika mazingira ya utata uliopo kweli atafanya uchunguzi independent. Ndiyo maana nadhani kuwa tunatwanga maji kwenye kinu, jamaa watayeya tukiwa tunawaona hivi hivi tu.

Uchunguzi mzito kama huu unatakiwa kweli ufanywe na kampuni credible, wala siyo hizi kampuni zetu kanyabwoya za mishen town.
 
It's an open secret on this... Franchisee wa Ernst & Young hapa ni jamaa anaitwa ERNEST MASSAWE (akiwa ndo boss wa franchise hiyo). Office zake ni pale ubalozi wa Marekani wa zamani (uliolipuliwa), alihamia hapo kutoka IPS (Samora na Azikiwe).

Amepata kuwa RECEIVER MANAGER wa TANZANAIR kukusanya madeni ambayo TANZANIAR ilikuwa hairudishi mkopo wa benki.

Kuwa karibu na wakubwa inasemekana ndiye 'finacial consultant' kwa hawa jamaa wanao reap what they didn't saw!

KESI YA NYANI KAPELEKEWA NGEDERE
 
...yaani angle zote mafisadi wana mkono wao sijui tutatokea wapi jamani? hawa guilty verdict yao ni kwa wananchi tuu wakati wa uchaguzi kwingine huku wataendelea kula pesa yetu tuu kama walivyoanza ziara za kujibu wapinzani na hotuba za budget mikoani wakitumia pesa zetu kipumbavu tuu kwa ajiri ya propaganda zao,sasa angalia hilo changa la macho with our own money kumpa huyo mchaga (Massawe) to seal the deal na kuambiwa report kanyaboya na Slaa ni mzushi tuu na kuishia kuburuzwa mahakamani for the next five yrs,dawa yao ni kushambulia kila report wanayotoa na kuitoboa toboa mpaka ionekane Buzwagi nyingine
 
Nimerudi mjini ila naona jamaa waliniachia maboksi yangu ya kubeba mengi sana. Kwa hiyo nimekuwa mtoro sana hapa kijiweni siku hizi ili niyapunguze kidogo. Hata hivyo nimeona nitoe duku duku langu kuhusu uchunguzi unaofanywa pale BOT na 'independent company.' Inasemekana kuwa uchunguzi huu unafanywa na kampuni ya kimarekani inayoitwa Ernst Young, lakini ukweli ni kuwa kazi hiyo inafanywa na jamaa mmoja ambaye ni ndugu wa aliyekuwa aliyekuwa waziri wa fedha wakati wa Mkapa. Waziri huyu ndiye aliyemsaidia ndugu yake huyo kupata franchise ya Ernst Young kwa vile alikuwa akipewa tenda nyingi sana za kukagua mahesbau ya serikali. Nina wasiwasi kuwa mtu kama huyo katika mazingira ya utata uliopo kweli atafanya uchunguzi independent. Ndiyo maana nadhani kuwa tunatwanga maji kwenye kinu, jamaa watayeya tukiwa tunawaona hivi hivi tu.

Uchunguzi mzito kama huu unatakiwa kweli ufanywe na kampuni credible, wala siyo hizi kampuni zetu kanyabwoya za mishen town.

Labda tuweke matumaini yetu katika kuamini kuwa "MacDonald Burgers" ni hayo hayo popote pale, iwe ni Moscow, Beijing, au Gaborone!

Vinginevyo hao Ernst & Young wakikubali kuchafuliwa jina kwa kulegeza 'standard' na kutupilia mbali 'standard operating procedures' zao, biashara waisahau. Nadhani kuna 'oversite' ya namna fulani. Ngoja tusubiri, maanake sio sisi (WaTanzania) pekee tunaosubiri hiyo ripoti. Wakoloni wetu nao wanaisubiri kwa hamu.
 
Hivi haiwezekani kuwapa message kwa njia yoyote hawa Ernst n young HQ kwamba we expect that job to be clean coz macho yetu yote yapo hapo, wakicheza wanapoteza umaarufu wao duniani coz itawekwa bayana.Nyie huko mbele wakuu mnaonaje? It will hurt if these mafisadi will get away with this. What can we do to make them pay?
 
mtu mwenye details za deals za zamani za hao ernest and young tunaziomba hapa tafadhali, ili tuweze kuonyesha ni vipi hii kampuni ipo upande wa serikali
 
Nilishasema awali:

Waziri wa fedha mtuhumiwa - Mrombo;
Mkaguzi mkuu wa serikali - Mrombo;
Ernest & Young - (Partner wao)- Mrombo.

Expectations?
 
huyo Mrombo cannot defend the indefensible,la sivyo naye kitanzi chake kinakuja
 
Nilishasema awali:

Waziri wa fedha mtuhumiwa - Mrombo;
Mkaguzi mkuu wa serikali - Mrombo;
Ernest & Young - (Partner wao)- Mrombo.

Expectations?

Zero

Serikali inafanya mchezo na pesa ya walipa kodi, kwa hili litawatokea puani.
 
WaTZ sasa tumekwisha, huwa nikiangalia salary slip yangu nakuaona hela ninayokatwa kodi inaniuma sana, sasa leo unaniongezea maumivu mengine kwa kuniambia kodi yangu hiyo inatumika kuficha ufisadi wa mafisadi walioiba hela zetu, doesnt pass in my mind.

Why this people wantuchezea, ndo maana wanazunguka huku na kule wakijigamba wapinzani ni waongo wana jibu tayari la ripoti na hiyo ukaguzi ni deal nyingine ya kuwaingizia pesa.

Dawa ya hawa watu ni nguvu ya umma, tutakufa maskini wa kutupwa waTZ. Tuamke kupigania nchi yetu maana hii ni vita ya mafisadi na wananchi.

Tunakoelekea sasa ni watoto wa viongozi wale wale ndo watakuwa wakiachiwa madaraka ili kulinda maslahi ya baba zao na mafisadi wengine.
 
Hivi haiwezekani kuwapa message kwa njia yoyote hawa Ernst n young HQ kwamba we expect that job to be clean coz macho yetu yote yapo hapo, wakicheza wanapoteza umaarufu wao duniani coz itawekwa bayana.Nyie huko mbele wakuu mnaonaje? It will hurt if these mafisadi will get away with this. What can we do to make them pay?

Naona Judy kasema kitu ambacho kikifanyiwa kazi ya umakini kitawafanya hawa jamaa wa ernst & young wa TZ wasituletee za kuletwa. Hata kama wakileta za kuletwa basi ndio itakua the end of them.

Ninafikiri (kama alivosema Judy) ni bora kupeleka taarifa hii kwa President wa dunia wa ernst & young kumweleza kwamba sisi wadanganyika wenye uchungu na nchi yetu tunafahamu fika kwamba kinachoendelea kwenye ukaguzi wa benki kuu ni kiini macho tu; na kwamba tunafahamu kwamba serikali yetu imewachagua wawakilishi wa ernst & young waliopo TZ (Masawe et al) ili kuficha ufisadi wake na kwamba tunaelewa wazi kwamba kuna conflict of interest iliyo wazi kabisa kati ya warombo waliotajwa kwenye thread hii (hivi ni akina nani hawa?) na serikali yetu inaelewa hilo na mpaka sasa tunaweza kutabiri the outcome of their investigation, kwamba itakuwa on the side of mafisadi. Kama kuna data zozote kuhusiana na hao warombo nazo ziwekwe kwenye hiyo taarifa. I tell you, hakuna president yoyote wa organisation ya kuaminika duniani ambaye atakubali kupandikizwa upuuzi na mrombo yoyote (sorry warombo - usemi wa samaki mmoja akioza basi wameoza wote hau-apply hapa). This might be the end of ernst & young Tanzania. Ikumbukwe kwamba hawa E & Y wana mioto mingine ambayo bado hawajaizima. I don't think wako ready kupata scandal nyingine.

Ma-presidents wa organisations kama ernst & young global hawaendeshi mambo yao kwa kiini macho kama tunavyofanyiwa na waheshimiwa wetu wa kibongo.. I tell you, president huyu lazima ata-take action haraka kurekebisha ujinga huu. Anaweza hata kutuma watu kutoka headquarters kuja kuanza kazi upya... Can you predict the reaction ya wanasiasa wetu kama president wa E & Y global akituma watu wake kutoka HQ? .....Waheshimiwa watawakatalia kufanya kazi hiyo maana watajua kwamba sasa janja yao itajulikana...

Hivi hamna watu wenye data zozote za kupandikizwa kwenye huo ujumbe? (kama vile uhusiano wa hao warombo). Hivi walipewa siku ngapi wamalize kiini macho chao?
 
Hawa jamaa wamekalia moto tu nina uhakika kuwa watanzania kuanzia Mtwara mpaka kule Ziwani-mara wameisha kuwa macho.

Wakileta ripoti yenye longolongo wale watani wangu BuKOBA huwa uanasema MWAFA. Hakuna jinsi zaidi ya kujimaliza wenyewe na ripoti yao.

Na pili kuna haja kupata data za kampuni hiyo vizuri, ili ikigundulika kweli kuna ukaribu sana na watuhumiwa ripoti iweze kukataliwa kabla hata haijakuwa presented.

Hii ishue lazima tukubali bila kuunda kamati ambayo iko neutral (kama vile ya Bunge) kampuni moja kama tunayoiona sasa haina ubavu.

Majina ya waliotajwa na pesa inayotajwa(iliyofisadiwa) ni kubwa sana kushinda ukubwa wa kampuni Inayochunguza.

Hata siku moja Swala(pamoja na umahiri wake wa kukimbia) hawezi kumchunguza Simba.
 
Judy & Nikifufukammekwisha,

Yes pamoja nakuwasiliana na president wao, pia tusubir ripoti yenyewe, tuichambue, kama kuna kasoro zozote za kuficha uozo makala tutaandika ktk magazeti ya kimataifa
 
One thing i can guarantee is Enerst & Young cant afford what arthur Andersen get. Big four firm are so sensitive about corruption and unethical acts. Mr. Massawe, anaweza kufanya upuuzi anaotaka lakini nakuaidi endepo itajulikana then ataloose franchise.
Mr Massawe is oldschool accountant, i believe he works under international standard, so lets wait and see what he will say, before we make final decisions.
 
ripoti mtapewa?mtaambiwa tu kama Hosea alivyomsafisha ndanda kossovo na suala la Richmond
 
Ninachofahamu mie ni kuwa Ernest & Young hawezi kufanya kazi na Co. ambayo haikidhi international standards, tusipayuke sana na kuhukumu kwa kuwa tu amepewa mweusi mwenzetu. Ila mngeona ni mzungu japo hata shule yake hovyo mnepiga makofi. Acheni wivu wa kike tena wa wanawake wa Tandale ! ebo! na hawa jamaa hawakurupuki kama wewe!
 
One thing i can guarantee is Enerst & Young cant afford what arthur Andersen get. Big four firm are so sensitive about corruption and unethical acts. Mr. Massawe, anaweza kufanya upuuzi anaotaka lakini nakuaidi endepo itajulikana then ataloose franchise.
Mr Massawe is oldschool accountant, i believe he works under international standard, so lets wait and see what he will say, before we make final decisions.
JF ni kiboko, huu mwaka wa 10 sasa
 
Nimerudi mjini ila naona jamaa waliniachia maboksi yangu ya kubeba mengi sana. Kwa hiyo nimekuwa mtoro sana hapa kijiweni siku hizi ili niyapunguze kidogo. Hata hivyo nimeona nitoe duku duku langu kuhusu uchunguzi unaofanywa pale BOT na 'independent company.' Inasemekana kuwa uchunguzi huu unafanywa na kampuni ya kimarekani inayoitwa Ernst Young, lakini ukweli ni kuwa kazi hiyo inafanywa na jamaa mmoja ambaye ni ndugu wa aliyekuwa aliyekuwa waziri wa fedha wakati wa Mkapa. Waziri huyu ndiye aliyemsaidia ndugu yake huyo kupata franchise ya Ernst Young kwa vile alikuwa akipewa tenda nyingi sana za kukagua mahesbau ya serikali. Nina wasiwasi kuwa mtu kama huyo katika mazingira ya utata uliopo kweli atafanya uchunguzi independent. Ndiyo maana nadhani kuwa tunatwanga maji kwenye kinu, jamaa watayeya tukiwa tunawaona hivi hivi tu.

Uchunguzi mzito kama huu unatakiwa kweli ufanywe na kampuni credible, wala siyo hizi kampuni zetu kanyabwoya za mishen town.

Mambo yalishaharibiwa siku nyingi
 
Back
Top Bottom