Uchumi wa Zanzibar

Fundi Mchundo

Platinum Member
Nov 9, 2007
8,935
6,844
Zanzibar exports climb to USD 9.6m

2008-03-26 09:12:37
By Beatrice Philemon


Zanzibar total export revenues for January rose to USD 9.6m up from USD 5.6m registered in December last year, mainly driven by cloves.

Bank of Tanzania Monthly Economic Review of February this year indicates that clove exports increased in both volume and price to the tune of USD 5.3m from USD 1.0m posted in December 2007.

Furthermore services receipts from tourism related activities decreased slightly to USD 4.3m from USD 4.6m realised in the previous month due to low tourism season.

On annual basis, total export proceeds amounted to USD 92.7m down from USD 102.6m registered in the corresponding period in 2007, mainly on account of decrease in receipts from services receipts.

On the other hand, cloves exports declined dramatically to USD 4.0m from 9.0m, recorded in the same period in 2006 and represented 4.3 percent of total exports receipts.

Seaweeds exports are equally becoming important export commodity as it fetched USD 2.2m or 2.4 percent of total receipts and manufactured goods exports amounted to USD 3.7m, constituting 4.0 percent of total exports receipts .

Fish and fish produce exports stood at USD 0.2m while earnings from other exports amounted to USD 4.3m or 4.6 percent of total export receipts.

Zanzibar imports performance decreased to USD 6.3m from USD 7.2m recorded in the preceding month, responding to slow down in import of capital goods particularly transport equipment and machinery and this was also mainly associated with completion of some major projects.

At the same time, capital goods imports amounted to USD 2.6m down from USD 3.7m registered in December 2007. And intermediate goods imports which are driven by oil rose to USD 2.6m from USD 2.4m registered in the previous month, it indicates.

The report also indicates consumer goods importation increased to USD 1.2m from USD 1.1m mainly as a result of increase in imports of (clothes and foot wear.

Also on annual basis, goods imports went up to USD 93.1m from USD 80.7m recorded in the corresponding period in 2007 largely due to increase in capital goods imports, especially building and construction materials and transport equipment.

The increase corresponds with boom in construction sector and expanding transit cars business with Tanzania Mainland.

Also food and food stuffs imports remained at USD 6.3m, same as the previous corresponding period in 2007

Hivi kweli nchi yenye watu zaidi ya milioni moja( sawasawa na Mauritius) inaweza kujisifia kuongeza export kutoka dola milioni tatu kwa mwezi hadi milioni tisa na nusu? Na hii ikafanywa kichwa cha habari! Tutafika kweli?
 
Zenj hawajajisifia, hiyo ni taarifa kwa wananchi na wadau wengine. Hata kama ongezeko lingekuwa ni la senti hamsini, lakini taarifa ikatolewa ni jambo la msingi na busara kuliko kukaa gizani kama Bara...
 
Zenj hawajajisifia, hiyo ni taarifa kwa wananchi na wadau wengine. Hata kama ongezeko lingekuwa ni la senti hamsini, lakini taarifa ikatolewa ni jambo la msingi na busara kuliko kukaa gizani kama Bara...

Haujanielewa Mkuu!

Ninachosema ni kuwa hatuwezi kutoka hapa tulipo, sisi wabara na nyie wazanzibari, kama tutaendelea kuona vitu kama hivi kuwa ni mafanikio. Takwimu kama hizi huwa zinatolewa sana hata na Bara ambako wakati mwingine ili kuzijazia jazia wanajumuisha za miaka kadhaa. Wenzetu walikuwa kila kukicha wakijipima na wenzao waliowapita na kupanga mikakati ya namna gani kuwafikia.

Mapato ya export ya nchi ya watu milioni 35 hayajagusa $ bilioni moja kwa mwaka ambapo kanchi ka watu milioni moja kamauritius wanaexport mabilioni ya dola! na hawana mafuta.

Ni lazima tuchukie umaskini wetu ndio tutaweza kujinasua. Si suala la Bara na Zanzibar. Ni letu wote.
 
Hivi kweli nchi yenye watu zaidi ya milioni moja( sawasawa na Mauritius) inaweza kujisifia kuongeza export kutoka dola milioni tatu kwa mwezi hadi milioni tisa na nusu? Na hii ikafanywa kichwa cha habari! Tutafika kweli?

Fundi uko pessimistic sana. Hapa umekurupuka tu kuuona umasikini wetu lakini hukufanya uchambuzi wa hiyo habari. Ukaangalia background information kuhusu exports revenues na imports za Zanzibar kwa angalau mwaka (miezi) iliyopita. Hiyo habari inaeleza hapo kuwa kumekuwepo na juhudi inayofanyika kukuza mapato na kupunguza matumizi na hivyo huko ndio kunakoitwa kukua kwa uchumi. Hasa kwa vile huko Zanzibar kwa muda mrefu kumekuwepo na trend iliyokuwa ikionyesha kuwa kinachotolewa kwa kununua kutoka nje (import) ni kikubwa kuliko kinachopatikana kutokana na mauzo (exports). Ukuaji kama huu ndio utakaotuwezesha siku moja nasi ku export kwa Mamilioni kama wafanyavyo wenzetu wa Mauritius. Hawakufanya kwa siku moja hao. Usiwavuje moyo Wazenj wacha tuombe kusikia katika habari ijayo kuwa wameuzxa vinavyofikia Milioni angalau 12 badala ya tisa za hivi sasa.
 
Fundi uko pessimistic sana. Hapa umekurupuka tu kuuona umasikini wetu lakini hukufanya uchambuzi wa hiyo habari. Ukaangalia background information kuhusu exports revenues na imports za Zanzibar kwa angalau mwaka (miezi) iliyopita. Hiyo habari inaeleza hapo kuwa kumekuwepo na juhudi inayofanyika kukuza mapato na kupunguza matumizi na hivyo huko ndio kunakoitwa kukua kwa uchumi. Hasa kwa vile huko Zanzibar kwa muda mrefu kumekuwepo na trend iliyokuwa ikionyesha kuwa kinachotolewa kwa kununua kutoka nje (import) ni kikubwa kuliko kinachopatikana kutokana na mauzo (exports). Ukuaji kama huu ndio utakaotuwezesha siku moja nasi ku export kwa Mamilioni kama wafanyavyo wenzetu wa Mauritius. Hawakufanya kwa siku moja hao. Usiwavuje moyo Wazenj wacha tuombe kusikia katika habari ijayo kuwa wameuzxa vinavyofikia Milioni angalau 12 badala ya tisa za hivi sasa.

Ingawa sina kawaida ya kukurupuka lakini kila kitu kina mwanzo. Mimi siko pessimistic. Kwa nini kila siku tunapenda kujiweka chini? Mauritius wanaingiza zaidi ya $millioni 900 kutokana na utalii. Wamewekeza kwenye Information technology, financial services na huduma nyingine zitakazoendeleza uchumi wao. Hawa walikuwa masikini kama sisi wakitegemea miwa tu! Singapore ilipopata uhuru ilikuwa maskini kuliko nchi nyingi za kiafrika leo iko wapi? Hapana Mkuu, hii kuridhika na hali yetu ndiyo inayotuweka hapa. Tumebaki kutegemea windfalls kama mafuta na misaada kutoka kwa wenye kutuonea huruma badala ya kupanga mikakati ya namna gani tutawafikia.

With all due respect, kwa mwendo huo unategemea lini serikali ya Zanziba itapata surplus?Hayo mapato hata yakiongezeka mara dufu hayatatutoa hapa tulipo, nchi ya nne masikini duniani. Hizo gains zimetokana na mabadiliko ya bei ya karafuu, zao la asilia. Kwingine kote the situation is dire. Consumer goods importation increase ni kwenye nguo na viatu, vitu ambavyo ni basic! Mapato jumla ni chini ya dola millioni mia moja! Utalii unaingiza chini ya dola milioni tano kwa mwezi ambapo wenetu wanaingiza on average milioni 80! Bado tusikasirike?

Tunahitaji kufanya kazi ya ziada, Mkuu. Kama alivyosema Mwalimu R.I.P, inabidi tukimbie wakati wenzetu wanatembea. Tupongezane, ndio, lakini tukumbushane kuwa bado safari ni ndefu! Hakuna njia ya mkato.
 
Ingawa sina kawaida ya kukurupuka lakini kila kitu kina mwanzo. Mimi siko pessimistic. Kwa nini kila siku tunapenda kujiweka chini? Mauritius wanaingiza zaidi ya $millioni 900 kutokana na utalii. Wamewekeza kwenye Information technology, financial services na huduma nyingine zitakazoendeleza uchumi wao. Hawa walikuwa masikini kama sisi wakitegemea miwa tu! Singapore ilipopata uhuru ilikuwa maskini kuliko nchi nyingi za kiafrika leo iko wapi? Hapana Mkuu, hii kuridhika na hali yetu ndiyo inayotuweka hapa. Tumebaki kutegemea windfalls kama mafuta na misaada kutoka kwa wenye kutuonea huruma badala ya kupanga mikakati ya namna gani tutawafikia.

With all due respect, kwa mwendo huo unategemea lini serikali ya Zanziba itapata surplus?Hayo mapato hata yakiongezeka mara dufu hayatatutoa hapa tulipo, nchi ya nne masikini duniani. Hizo gains zimetokana na mabadiliko ya bei ya karafuu, zao la asilia. Kwingine kote the situation is dire. Consumer goods importation increase ni kwenye nguo na viatu, vitu ambavyo ni basic! Mapato jumla ni chini ya dola millioni mia moja! Utalii unaingiza chini ya dola milioni tano kwa mwezi ambapo wenetu wanaingiza on average milioni 80! Bado tusikasirike?

Tunahitaji kufanya kazi ya ziada, Mkuu. Kama alivyosema Mwalimu R.I.P, inabidi tukimbie wakati wenzetu wanatembea. Tupongezane, ndio, lakini tukumbushane kuwa bado safari ni ndefu! Hakuna njia ya mkato.

maneno ya wenzetu kule bara nimekusoma, ama kikwetu nimekuelewa vilivyo.

tuombe mungu baada ya muafaka na kuja na serikali ya kitaifa iwe na lengo la makusudi kutafuta njia za kunyanyua kiwango cha uchumi wetu.

uchumi wetu kuwa unadorora tusitafute mchawi hatujajituma bali tumeweka siasa mbele, kuna vitu tuone aibu jamani na tuukubali ukweli.

kama tuko darasani tuna haki kuambiwa tunacheza hatutaki kusoma
 

Tunahitaji kufanya kazi ya ziada, Mkuu. Kama alivyosema Mwalimu R.I.P, inabidi tukimbie wakati wenzetu wanatembea. Tupongezane, ndio, lakini tukumbushane kuwa bado safari ni ndefu! Hakuna njia ya mkato.

Sadakta Fundi. Nimekuelewa. Na kumradhi kwa kusema umekurupuka. Nakubabaliana na vision yako, hasa katika kuimarisha utalii, na kuacha kutumia fedha nyingi kununua nguo, viatu au mchele ambavyo vinaweza, tukiimarisha uzalishaji, kupatikana hapa hapa TZ. Tatizo la Zenj siasa na ubishani wa kugombania madaraka vimetawala sana, na ndiyo maana kuna kulegalega. Watu wote (hata wataalamu wetu wa kilimo na uchumi), kule, wanachapa siasa tu. Tunahitaji watu wenye mtizamo kama wako kuwasaidia wenzetu wa Zenj. Endelea kuwahamasisha, Fundi, kila upatapo nafasi.
 
Mapato ya Zanzibar kwa mwezi hayazidi pesa anazolipa Rostam Aziz kwenye kodi!

Aziz ameripoti kulipa zaidi ya USD 100 m, Zaznibar inacheza kwenye single digits!

And then watu wanataka kuja na excuses.
 
Back
Top Bottom