Uchumi wa Mkapa,Obama uliimarika kwa kasi bila kujibana: Siri,waliruhusu Mijadala mipana ya Kiuchumi.

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Siyo siri, Maraisi hawa walipokabidhiwa nchi zao zikiwa hoi kiuchumi. Lakini kwa kuruhusu mijadala ya wazi nini kifanyike,walishinda majaribu. Hatimaye,uchumi wa nchi na watu wao ukaimarika bila kubanana au kulalamikia watangulizi wao. Mikakati yao ilishirikisha hata watangulizi wao wanaosadikika kuharibu uchumi. Tulishudia Obama na Bush wakija Tanzania katika ndege moja kusaka miradi ya kiuchumi. Tumeshuhudia "Sulivan Summit" wakiwepo kina Comrade Andrew Young wakija Arusha kujadili nasi,namna ya kujiwezesha uchumi wetu sisi weusi ukue. Tumeshuhudia wanaharakati wengi wa masuala ya kijamii na kisiasa katika enzi za maraisi hao zikiwa active kujadili,kushauri na kupingana kwa hoja,hadi muafaka kupatikana katika hali ya amani. Mfano,ni ule mpango kabambe wa kupunguza gharama za afya (Obamacare) kwa watu wa kipato cha chini na kati ambao hata Raisi Trump imebidi aridhie japo hakutaka.
Kwa maoni yangu, na kwa mtizamo wa dunia ya sasa, mijadala,makongamano,ushirikishwaji wa taasisi na wachumi mbalimbali ni jambo zuri katika kuweka mustakabali imara wa ukuzaji uchumi.
 
Yule mwingine uliye mtaja napata kigugumizi, si ndie aliyekuwa akishauriwa kuhusu mikataba ya ovyo katika madini, anatubeza na kutuita tuna wivu na ni wavivu wa kufikiri!! Au siyo yeye?!!
 
Yule mwingine uliye mtaja napata kigugumizi, si ndie aliyekuwa akishauriwa kuhusu mikataba ya ovyo katika madini, anatubeza na kutuita tuna wivu na ni wavivu wa kufikiri!! Au siyo yeye?!!
Inawezekana kwa vile tunakubali kugeuzika kwa kila kitu,hatuna msimamo kama wenzetu. Mfano,unaambiwa usiongee,nisikilize mimi tu,matatizo yako nayajua yote,nitayamaliza. Nawe unakaa kimya,sasa uitweje kwa vile tayari hufikiri tena ?na kuna mtu anafikiria kila kitu kwa niaba yako?
 
Bavicha ni wepesi sana kusahau,enzi za mkapa na yule mtu wake wa kula nyasi nani aliruhusiwa kujadili uchumi?umesahau mpaka Lipumba akaitwa professor uchwara?
Subirini 2020 mkichaguliwa mtafanya mabadiliko mnayoyataka
 
Siyo siri, Maraisi hawa walipokabidhiwa nchi zao zikiwa hoi kiuchumi. Lakini kwa kuruhusu mijadala ya wazi nini kifanyike,walishinda majaribu. Hatimaye,uchumi wa nchi na watu wao ukaimarika bila kubanana au kulalamikia watangulizi wao. Mikakati yao ilishirikisha hata watangulizi wao wanaosadikika kuharibu uchumi. Tulishudia Obama na Bush wakija Tanzania katika ndege moja kusaka miradi ya kiuchumi. Tumeshuhudia "Sulivan Summit" wakiwepo kina Comrade Andrew Young wakija Arusha kujadili nasi,namna ya kujiwezesha uchumi wetu sisi weusi ukue. Tumeshuhudia wanaharakati wengi wa masuala ya kijamii na kisiasa katika enzi za maraisi hao zikiwa active kujadili,kushauri na kupingana kwa hoja,hadi muafaka kupatikana katika hali ya amani. Mfano,ni ule mpango kabambe wa kupunguza gharama za afya (Obamacare) kwa watu wa kipato cha chini na kati ambao hata Raisi Trump imebidi aridhie japo hakutaka.
Kwa maoni yangu, na kwa mtizamo wa dunia ya sasa, mijadala,makongamano,ushirikishwaji wa taasisi na wachumi mbalimbali ni jambo zuri katika kuweka mustakabali imara wa ukuzaji uchumi.
inaelekea huna kumbukumbu sahhivi neno UKAPA chanzo chake kilikua nini??
 
Hivi Mkapa si ndio alikuwa na sera ya ubinafsishaji wa kila mali ya serikali? Angetokea mwingine mwenye kasi kama yake bila shaka Mito, mabonde na milima ingekuwa mali ya mwekezaji kutoka nje.

Kwa kifupi tumekuwa tukiongozwa na chama kimoja toka tupate Uhuru , hao tuliowapa dhamana ya uongozi wamefanya maamuzi mbali mbali mabovu na wamekuwa wakilindwa na wanachama wenzao wanaowaachia kijiti cha kuongoza taifa hili.

Nchi yetu haijawahi kuwa na uwajibikaji halisi kwa upande wa Rais, ndio maana Rais anaweza fanya madudu kwa miaka yake kumi na kupumzika bila ya bugudha yoyote pale kipindi chake kinapoisha.
 
Obama na Bush walikuja kipindi cha Mkapa? Ile Sullivan Summit nayo kipindi cha Mkapa?
 
Hivi Mkapa si ndio alikuwa na sera ya ubinafsishaji wa kila mali ya serikali? Angetokea mwingine mwenye kasi kama yake bila shaka Mito, mabonde na milima ingekuwa mali ya mwekezaji kutoka nje.

Kwa kifupi tumekuwa tukiongozwa na chama kimoja toka tupate Uhuru , hao tuliowapa dhamana ya uongozi wamefanya maamuzi mbali mbali mabovu na wamekuwa wakilindwa na wanachama wenzao wanaowaachia kijiti cha kuongoza taifa hili.

Nchi yetu haijawahi kuwa na uwajibikaji halisi kwa upande wa Rais, ndio maana Rais anaweza fanya madudu kwa miaka yake kumi na kupumzika bila ya bugudha yoyote pale kipindi chake kinapoisha.
Inawezekana tulikuwa tunamshangaa tu bila kushiriki uchumi wa soko huria tukawaachia wengine. Tuna tabia ya kuamini mtu atufanyie sisi tubaki kumshangilia bila kujiongeza. Hata china iliingiza ubinafsishaji na wachina wenyewe wakajitambua haraka na kushiriki bila malalamiko.
 
Back
Top Bottom